< Yoshua 18 >
1 Kisha kusanyiko lote la watu wa Israeli walikusanyika pamoja hapo Shilo. Walilijenga hema la kukutania hapo na waliishinda nchi mbele yao.
Og al Israels Børns Menighed samledes i Silo og satte der Forsamlingens Paulun, og Landet var dem underlagt.
2 Kulikuwa na makabila saba miongoni mwa watu wa Israeli ambayo yalikuwa bado hayajapewa urithi wao.
Og der var endnu syv Stammer tilovers af Israels Børn, som ikke havde delt deres Arv.
3 Yoshua aliwaambia watu wa Israeli, “Je mtaacha mpaka lini katika kuingia nchi ambayo Yahweh, Mungu wa baba zenu, amewapeni ninyi?
Og Josva sagde til Israels Børn: Hvor længe ere I saa efterladne med at komme til at eje Landet, som Herren, eders Fædres Gud, har givet eder?
4 Chagueni ninyi wenyewe watu watatu kutoka katika kila kabila, na nitawatuma. Wataenda na kuipeleleza nchi juu na chini. Wataandika maelezo pamoja na maelekezo kuhusu urithi wao, na kisha watarudi kwangu.
Vælger eder tre Mænd for hver Stamme, saa vil jeg udsende dem, at de kunne gøre sig rede og gaa igennem Landet og beskrive det for at kunne bestemme deres Arv, og de skulle komme til mig igen.
5 Wataigawanya nchi katika sehemu saba. Yuda itasalia katika eneo lao upande wa kusini, na nyumba ya Yusufu itaendelea katika himaya yao katika upande wa kaskazini.
Og de skulle dele det i syv Dele; Juda skal blive i sit Landemærke mod Sønden; og Josefs Hus, de skulle blive i deres Landemærke mod Norden.
6 Mtaigawanya nchi katika sehemu saba na kisha mtaniletea maelezo hayo hapa kwangu. Nami nitapiga kura kwa ajili yenu hapa mbele za Yahweh Mungu wetu.
Men I skulle beskrive Landet og dele det i syv Dele og føre Beskrivelsen herhid til mig; saa vil jeg her kaste Lod for eder, for Herrens vor Guds Ansigt.
7 Walawi hana sehemu miongoni mwenu, kwa kuwa ukuhani wa Yahweh ni urithi wao. Makabila ya Gadi, Rubeni na nusu ya kabila la Manase wameshapokea urithi wao ng'ambo ya Yordani. Huu ni urithi ambao Musa mtumishi wa Yahweh aliwapa wao.
Thi Leviterne have ingen Del midt iblandt eder, men Herrens Præstedømme er deres Arv; og Gad og Ruben og den halve Manasse Stamme have taget deres Arv paa hin Side Jordanen mod Østen, som Mose, Herrens Tjener, gav dem.
8 Hivyo, watu waliinuka na wakaenda. Yoshua akawaamuru wale walioenda kuandika maelezo ya nchi, akisema, “Pandeni juu na mshuke chini katika nchi na andikeni maelezo kuhusu nchi na kisha mrejee kwangu. Nitapiga kura kwa ajili yenu hapa mbele za Yahweh huko Shilo.
Da gjorde Mændene sig rede og gik; og Josva befalede dem, som gik hen at beskrive Landet, og sagde: Gaar og vandrer om i Landet og beskriver det og kommer tilbage til mig, saa vil jeg her kaste Lod for eder, for Herrens Ansigt, i Silo.
9 Watu walienda na walitembea juu na chini katika nchi na wakaandika maelezo kuihusu nchi hiyo juu ya gombo kwa miji yake katika sehemu saba, kwa kutaja miji, kila mmoja katika sehemu moja. Kisha wakarudi kwa Yoshua katika kambi huko Shilo.
Saa gik Mændene hen og gik igennem Landet og beskreve det i en Bog efter Stæderne og delte det i syv Dele; og de kom tilbage til Josva til Lejren i Silo.
10 Kisha Yoshua akapiga kura kwa ajili yao huko Shilo mbele za Yahweh. Na hapo Yoshua akaigawa nchi kwa watu wa Israeli, kila kabila lilipewa sehemu ya nchi.
Saa kastede Josva Lod for dem i Silo, for Herrens Ansigt; og Josva delte der Landet for Israels Børn, efter deres Afdelinger.
11 Katika kabila la Benyamini, ugawanaji wa nchi ulifanyika kwa kupewa kwa koo zao. Eneo la nchi waliyopewa lilikuwa kati ya wazawa wa Yuda na wazawa wa Yusufu.
Og Benjamins Børns Stammes Lod kom ud efter deres Slægter, og Landemærket for deres Lod gik ud imellem Judas Børn og imellem Josefs Børn.
12 Katika upande wa kusini, mpaka wao ulianzia katika Yordani. Mpaka ulipanda hata sehemu ya juu kaskazini mwa Yeriko, na kisha ukapita katikati ya nchi ya milima upande wa magharibi. Huko ukafika hadi nyika ya Bethi Aveni.
Og deres Landemærke paa den nordre Side var fra Jordanen; Landemærket gaar op til Nordsiden af Jeriko og gaar op til Bjerget imod Vesten, og Udgangene derpaa vare mod Ørken ved Beth-Aven.
13 Kutoka hapo mpaka ulipita upande wa kusini katika mwelekeo wa Luzi (sehemu ile ile inayoitwa Betheli). Kisha mpaka ukashuka chini hata Atarothi Adda, karibu na mlima uliolekea kusini mwa Bethi Horoni.
Og Landemærket gaar derfra over til Lus, til den søndre Side af Lus, det er Bethel; og Landemærket gaar ned til Atharoth-Addar over Bjerget, som ligger Sønden for det nedre Beth-Horon.
14 Kisha mpaka ukaendelea upande mwingine: katika upande wa magharibi uligeukia upande wa kusini, ulienda mbele kuukabili mlima ulio ng'ambo ya Bethi Horoni. Mpaka huu ulikomea huko Kiriathi Baali ( ambao ndio Kiriathi Yearimu), mji ambao ulikuwa ni wa kabila la Yuda. Na huu ndio ulikuwa ni mpaka katika upande wa magharibi.
Og Landemærket gaar videre og bøjer sig om den venstre Side mod Sønden, fra Bjerget, som ligger tværs over for Beth-Horon mod Sønden, og Udgangen derpaa er til Kirjath-Baal, det er Kirjath-Jearim, Judas Børns Stad; dette er den vestre Side.
15 Katika upande wa kusini, mpaka ulianzia nje tu ya Kiriathi Yearimu. Mpaka uliendelea kutoka Efroni hata chemichemi ya maji ya Neftoa.
Men Sydsiden er fra det yderste af Kirjath-Jearim; og Landemærket gaar ud fra Vesten, og det gaar ud til Nefthoas Vandkilde.
16 Kisha mpaka ulishuka chini hadi mpaka wa mlima ambao ulikuwa mkabala ya bonde la Beni Hinomu, ambalo lililokuwa katika upande wa kaskazini mwishoni mwa bonde la Refaimu. Kisha ulishuka chini kuelekea bonde la Hinomu, sehemu ya kusini mwa mteremko wa Wayebusi, na uliendelea kushuka chini hadi Eni Rogeli.
Og Landemærket gaar ned til Enden af Bjerget, som ligger tværs over for Hinnoms Søns Dal, og som er i Refaims Dal mod Norden; og det gaar ned til Hinnoms Dal, mod den søndre Side af Jebus, og gaar ned til En-Rogel.
17 Ulizunguka upande wa kaskazini, kuelekea mwelekeo wa Eni Shemeshi, na kutoka hapa ulienda hadi Gelilothi, ambao ulikuwa mkabala na mwinuko wa Adumimu. Kisha ulishuka chini kuelekea Jiwe la Bohani mwana wa Rubeni.
Og det bøjer sig fra Norden og gaar ud til En-Semes og gaar ud til Geliloth, som ligger tværs over for Opgangen til Adummim, og gaar ned til Bohans, Rubens Søns, Sten.
18 Ulipita kuelekea upande wa kaskazini wa bega la Bethi Araba na chini kuelekea Araba.
Og det gaar om til Siden tværs over for Araba, mod Norden; og det gaar ned til Araba.
19 Mpaka ulipita hadi upande wa bega la kaskazini la Bethi Hogla. Mpaka ulikome katika ghuba ya kaskazini mwa Bahari ya Chumvi, katika upande wa kusini mwishoni mwa Yordani. Huu ulikuwa ni mpaka wa upande wa kusini.
Og Landemærket gaar om til Nordsiden af Beth-Hogla, og Landemærkets Udgang er ved den nordlige Odde af Salthavet, ved Jordanens Udløb mod Sønden; dette er det søndre Landemærke.
20 Yordani ulikuwa mpaka wake katika upande wa mashariki. Na huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Benyamini, na walipewa kwa kila ukoo wao, mpaka baada ya mpaka, kwa kuizunguka nchi yote.
Men Jordanen sætter Grænse derfor mod den østre Side; dette er Benjamins Børns Arv i deres Landemærker rundt omkring efter deres Slægter.
21 Kwa hiyo sasa miji ya kabila la Benyamini kufuatana na koo zao ilikuwa ni Yeriko,
Og Benjamins Børns Stammes Stæder efter deres Slægter, vare: Jeriko og Beth-Hogla og Emek-Keziz
22 Bethi Hogla, Emeki Kezizi, Bethi Araba, Zemaraimu, Betheli,
og Beth-Araba og Zemarajim og Bethel
24 Kefari Amoni, Ofini, na Geba. Ilikuwa ni miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake.
og Kefar-Ammonai og Ofnai og Geba; tolv Stæder og deres Landsbyer.
25 Kulikuwa pia na miji ya Gibeoni, Rama, Beerothi,
Gibeon og Rama og Beeroth
og Mizpe og Kefira og Moza
27 Rekemu, Iripeeli, Tarala,
og Rekem og Jirpeel og Tharala
28 Zela, Haelefu, Yebusi (ambao ndio Yerusalemu), Gibea, na Kiriathi. Kulikuwa na miji kumi na nne, pamoja na vijiji vyake. Huu ulikuwa ni urithi wa Benyamini kufuatana na koo zao.
og Zela, Elef og Jebusi, det er Jerusalem, Gibeath, Kirjath; fjorten Stæder og deres Landsbyer; dette er Benjamins Børns Arv, efter deres Slægter.