< Yoshua 16 >
1 Nchi waliyopewa kabila la Yusufu ilianzia katika Yordani huko Yeriko, mashariki mwa chemichemi za Yeriko, kupitia nyikani, kupanda kutoka Yeriko kupitia nchi ya milima ya Betheli.
A los synów Józefa przypadł od Jordanu przy Jerychu do wód Jerycha na wschodzie, do pustyni, która rozciąga się od Jerycha przez górę Betel;
2 Kisha uliendelea kutoka Betheli hadi Luzi na kupita hata Atarothi, iliyo miliki ya Waarkiti.
Od Betel biegnie do Luz i dalej do granic Archy, do Atarot.
3 Kisha ilishuka chini upande wa magharibi kuelekea himaya ya Wayafuleti, hadi kufika miliki ya Loweri Bethi Horoni, na kisha iliendelea hadi Gezeri; na ilikomea katika bahari.
Potem ciągnie się ku zachodowi do granicy Jaflety, aż do granicy dolnego Bet-Choron i aż do Gezer, i kończy się przy morzu.
4 Ilikuwa ni kwa njia hii makabila ya Yusufu, yaani Manase na Efraimu yalipata urithi wao.
Tak więc synowie Józefa, Manasses i Efraim, wzięli dziedzictwo.
5 Eneo la kabila la Efraimu ambalo lilikuwa limegawanya kwa koo zao lilikuwa kama ifuatavyo: mpaka wa urithi wao katika upande wa mashariki ulikuwa Atarothi Ada uliopanda kuelekea Bethi Horoni ya juu,
A granica synów Efraima według ich rodzin – granica ich dziedzictwa na wschodzie – była [od] Atarot-Addar aż do górnego Bet-Choron.
6 na kutoka pale uliendelea hadi katika bahari. Kutoka Mikimethathi katika upande wa Kasikazini ulipinda upande wa mashariki kuelkea Taanathi Shilo na kupita ng'ambo yake katika upande wa mashariki kukabili Yanoa.
I ta granica biegła w kierunku morza do Mikmetat na północy, potem skręcała na wschód do Taanat-Szilo i przechodziła obok jej wschodniej strony aż do Janocha;
7 Kisha ulishuka kutoka Yanoa hadi Atarothi na hata Naara, na kisha ukafika Yeriko, na kuishia katika Yordani.
I ciągnęła się od Janocha do Atarot i Naarat, i dochodziła do Jerycha, a kończyła się przy Jordanie.
8 Kutoka Tapua, mpaka uliendelea katika upande wa magharibi hata kijito cha Kana na ulikomea katika bahari. Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Efraimu, uliogawanywa katika koo zao,
Od Tappuach granica biegła na zachód do potoku Kana, a kończyła się przy morzu. Takie było dziedzictwo pokolenia synów Efraima według ich rodzin.
9 pamoja na miji yao iliyochaguliwa kwa ajili ya kabila la Efraimu iliyokuwa ndani ya urithi wa kabila la Manase - miji yote pamoja na vijiji vyao.
Synowie Efraima [mieli] też wydzielone miasta pośrodku dziedzictwa synów Manassesa – wszystkie te miasta wraz z przyległymi do nich wioskami.
10 Lakini hawakuwafukuza Wakanaani walioishi katika Gezeri, hivyo basi Wakanaani wanaishi ndani ya Efraimu hadi leo, lakini watu hawa walifanywa kuwa watumwa.
I nie wygnali Kananejczyków, mieszkających w Gezer. I mieszkają Kananejczycy pośród Efraimitów aż do dziś, i stali się sługami składającymi daninę.