< Yoshua 15 >

1 Ugawanaji wa nchi kwa kabila la watu wa Yuda, walipewa kwa kufuatana na koo zao, kutoka upande wa kusini hadi mpaka wa Edomu, pamoja na nyika ya Sini iliyokuwa mbali sana kuelekea kusini.
And the lot for the tribe of the children of Judah according to their families was unto the border of Edom, even to the wilderness of Zin southward, at the uttermost part of the south.
2 Mpaka wao wa upande wa kusini ulianzia mwisho wa Bahari ya Chumvi, kutoka ghuba iliyokabili upande wa kusini.
And their south border was from the uttermost part of the Salt Sea, from the bay that looked southward:
3 Mpaka wao mwingine ulielekea upande wa kusini wa mlima wa Akrabimu na kupita kuelekea Sini, na kupanda upande wa Kadeshi Barnea, karibu na Hezroni, hadi Addari mahali ambapo ulipinda kuelekea Karika.
and it went out southward of the ascent of Akrabbim, and passed along to Zin, and went up by the south of Kadesh-barnea, and passed along by Hezron, and went up to Addar, and turned about to Karka:
4 Ulipita katika Azimoni, kuelekea kijito cha Misri, na mwisho ulikuwa katika bahari. Huu ulikuwa ni mpaka wa kusini.
and it passed along to Azmon, and went out at the brook of Egypt; and the goings out of the border were at the sea: this shall be your south border.
5 Mpaka wa mashariki ulikuwa ni Bahari ya Chumvi, katika mdomo wa Yordani. Mpaka wa upande wa kasikazini ulianzia katika ghuba ya bahari katika mdomo wa Yordani.
And the east border was the Salt Sea, even unto the end of Jordan. And the border of the north quarter was from the bay of the sea at the end of Jordan:
6 Ulielekea mpaka Bethi Hogla na ulipita kaskazini mwa Bethi Araba. Kisha ulipanda hata JIwe la Bohani mwana wa Rubeni.
and the border went up to Beth-hoglah, and passed along by the north of Beth-arabah; and the border went up to the stone of Bohan the son of Reuben:
7 Basi mpaka ule ulienda hadi Debiri kutoka katika bonde la Akori, kuelekea upande wa kasikazini, kuendelea hadi Giligali, ambayo iko mkabala na mlima Adumimu, iliyo upande wa kusini wa bonde. Kisha mpaka uliendelea hata katika chemichemi za Eni Shemeshi na kufika Eni Rogeli.
and the border went up to Debir from the valley of Achor, and so northward, looking toward Gilgal, that is over against the ascent of Adummim, which is on the south side of the river: and the border passed along to the waters of En-shemesh, and the goings out thereof were at En-rogel:
8 kisha mpaka ulishuka hadi bonde la Beni Hinomu kuelekea upande wa kusini wa mji wa Wayebusi ( ambao ni Yerusalemu). Kisha ulipanda hata katika mlima ulio juu ya bonde la Hinomu, katika upande wa magharibi, ulio mwishoni mwa bonde la Refaimu katika upande wa kasikazini.
and the border went up by the valley of the son of Hinnom unto the side of the Jebusite southward (the same is Jerusalem): and the border went up to the top of the mountain that lieth before the valley of Hinnom westward, which is at the uttermost part of the vale of Rephaim northward:
9 Kisha mpaka ulitanuka kutoka katika kilele cha milima hata chemichemi ya Nefutoa, na ulipanda kutoka hapo kuelekea miji ya Mlima Efroni. Kisha mpaka ulipiga kona kuelekea Baala ( ambao ndio Kiriathi Yearimu).
and the border was drawn from the top of the mountain unto the fountain of the waters of Nephtoah, and went out to the cities of mount Ephron; and the border was drawn to Baalah (the same is Kiriath-jearim):
10 Baadaye mpaka ulizunguka kuelekea magharibi mwa Baala kukabili Mlima Seiri, na kupita kufuata upande wa Mlima wa Yearimu katika upande wa kasikazini (ambao ndio Kesaloni), ulienda chini hadi Bethi Shemeshi na kuvuka hata ng'ambo ya Timna.
and the border turned about from Baalah westward unto mount Seir, and passed along unto the side of mount Jearim on the north (the same is Chesalon), and went down to Beth-shemesh, and passed along by Timnah:
11 Mpaka uliendelea karibu na mlima wa kasikazini mwa mlima wa Ekroni, na kisha ukakata kona kuzunguka Shikeroni na kupita kuelekea sambasamba na Mlima Baala, kutoka hapo uliendelea hadi Yabneeli. Mpaka ule ulikomea katika bahari.
and the border went out unto the side of Ekron northward: and the border was drawn to Shikkeron, and passed along to mount Baalah, and went out at Jabneel; and the goings out of the border were at the sea.
12 Mpaka wa magharibi ulikuwa Bahari Kuu na katika ukanda wa pwani yake. Huu ndio mpaka uliozunguka kabila la Yuda, ukoo kwa ukoo.
And the west border was to the great sea, and the border [thereof]. This is the border of the children of Judah round about according to their families.
13 Katika kulitunza agizo la Yahweh kwa Yoshua, Yoshua alimpa Kalebu mwana wa Yefune mgao wa nchi ya. miongoni mwa kabila la Yuda, alimgawia nchi Kiriathi Arba, ambayo ndio Hebroni (Arba alikuwa ni baba wa Anaki).
And unto Caleb the son of Jephunneh he gave a portion among the children of Judah, according to the commandment of the LORD to Joshua, even Kirjath-arba, [which Arba was] the father of Anak (the same is Hebron).
14 Kalebu aliwafukuzia mbali wana watatu wa Anaki: Sheshai, Ahimani na Talmai, wazawa wa Anaki.
And Caleb drove out thence the three sons of Anak, Sheshai, and Ahiman, and Talmai, the children of Anak.
15 Alipanda kutoka pale kinyume cha wenyeji wa Debiri (Debiri hapo mwanzo iliitwa Kiriathi Seferi).
And he went up thence against the inhabitants of Debir: now the name of Debir beforetime was Kiriath-sepher.
16 Kalebu akasema, “Mtu atakayeishambulia Kiriathi Seferi na kuiteka, nitampa binti yangau, Akisa, awe mke wake.
And Caleb said, He that smiteth Kiriath-sepher, and taketh it, to him will I give Achsah my daughter to wife.
17 Wakati huo Othinieli mwana wa Kenazi, kaka yake na Kalebu, aliuteka mji, na Kalebu alimpatia Akisa, binti yake awe mke wake.
And Othniel the son of Kenaz, the brother of Caleb, took it: and he gave him Achsah his daughter to wife.
18 Mara baada ya hayo, Akisa alienda kwa Othinieli na alimsihi amwombe baba yake shamba. Na mara aliposhuka kutoka katika punda wake, Kalebu alimwambia Akisa, “Unataka nini?”
And it came to pass, when she came [unto him], that she moved him to ask of her father a field: and she lighted down from off her ass; and Caleb said unto her, What wouldest thou?
19 Akisa akamjibu, “Nifanyie neema. Kwa kuwa umeshanipa nchi ya Negevu, nipe pia baadhi ya chemichemi za maji.” Na Kalebu alimpa chemichemi ya juu na chemichemi ya chini.
And she said, Give me a blessing; for that thou hast set me in the land of the South, give me also springs of water. And he gave her the upper springs and the nether springs.
20 Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Yuda, waliopewa kufuatana na koo zao.
This is the inheritance of the tribe of the children of Judah according to their families.
21 Miji iliyo mali ya kabila la Yuda katika upande wa kusini, kuelekea mpaka wa Edomu, ilikuwa ni Kabzeeli, Eda, Yaguri,
And the uttermost cities of the tribe of the children of Judah toward the border of Edom in the South were Kabzeel and Eder, and Jagur;
22 Kina, Dimona, Adada,
and Kinah, and Dimonah, and Adadah;
23 Kadeshi, Hazor, Ithinani,
and Kedesh, and Hazor, and Ithnan;
24 Zifu, Telemu, Bealothi.
Ziph, and Telem, and Bealoth;
25 Hazori Hadata, Keriothi Hezroni (mji huu ulijulikana kama Hazori),
and Hazor-hadattah, and Kerioth-hezron (the same is Hazor);
26 Amamu, shema, Molada,
Amam, and Shema, and Moladah;
27 Hazari Gada, Heshimoni, Bethi Peleti,
and Hasar-gaddah, and Heshmon, and Beth-pelet;
28 Hazari Shuali, Beerisheba, Biziothia.
and Hazar-shual, and Beer-sheba, and Biziothiah;
29 Baala, Limu, Ezemu,
Baalah, and Iim, and Ezem;
30 Eltoladi, Kesili, Horma,
and Eltolad, and Chesil, and Hormah;
31 Ziklagi, Madimana, Sansana,
and Ziklag, and Madmannah, and Sansannah;
32 Lebaothi, Shilihimu, Aini, na Rimoni. Miji hii ilikuwa ishirini na tisa kwa ujumla, kujumlisha na vijiji vyake.
and Lebaoth, and Shilhim, and Ain, and Rimmon: all the cities are twenty and nine, with their villages.
33 Katika nchi iliyo chini ya mlima upande wa magharibi, kulikuwa na miji ya Eshtaoli, Zora, Ashina,
In the lowland, Eshtaol, and Zorah, and Ashnah;
34 Zanaoa, Eni Ganimu, Tapua, Enamu,
and Zanoah, and En-gannim, Tappuah, and Enam;
35 Yarmuthi, Adulamu, Soko, Azeka,
Jarmuth, and Adullam, Socoh, and Azekah;
36 Shaaraimu, Adithaimu, na Gedera ( ambayo ndio Gederothaimu). Hesabu ya miji hii ilikuwa ni kumi na nne, pamoja na vijiji vyao.
and Shaaraim, and Adithaim, and Gederah, and Gederothaim; fourteen cities with their villages.
37 Zena, Hadasha, Migidagadi,
Zenan, and Hadashah, and Migdal-gad;
38 Dileani, Mizipa, Yokitheeli,
and Dilan, and Mizpeh, and Joktheel;
39 Lakishi, Bozikathi, Egloni.
Lachish, and Bozkath, and Eglon;
40 Kaboni, Lahmamu, Kitilishi,
and Cabbon, and Lahmam, and Chithlish;
41 Gederothi, Bethi Dagoni, Naama, Makeda. Hesabu ya miji hii ilikuwa kumi na sita, kujumlisha na vijiji vyao.
and Gederoth, Beth-dagon, and Naamah, and Makkedah; sixteen cities with their villages.
42 Libna, Etheri, Ashani,
Libnah, and Ether, and Ashan;
43 Ifuta, Ashina, Nezibu,
and Iphtah, and Ashnah, and Nezib;
44 Keila, Akizibu, na Maresha. Hii ilikuwa ni miji tisa, kujumlisha na vijiji vyao.
and Keilah, and Achzib, and Mareshah; nine cities with their villages.
45 Ekroni, pamoja na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka;
Ekron, with her towns and her villages:
46 kutoka Ekroni kuelekea Bahari Kuu, makazi yote ambayo yalikuwa karibu na Ashidodi, pamoja na vijiji vyake.
from Ekron even unto the sea, all that were by the side of Ashdod, with their villages.
47 Ashidodi, na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka; Gaza na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka; hata kufika kijito cha Misri, na kuelekea Bahari Kuu pamoja na ukanda wake wa pwani.
Ashdod, her towns and her villages; Gaza, her towns and her villages; unto the brook of Egypt, and the great sea, and the border [thereof].
48 Katika nchi ya milima, kuna miji ya Shamiri, Yatiri, Soko,
And in the hill country, Shamir, and Jattir, and Socoh;
49 Dana, Kiriathi Sana (ambayo ndio Debiri),
and Dannah, and Kiriath-sannah (the same is Debir);
50 Anabu, Eshitemo, Animu,
and Anab, and Eshtemoh, and Anim;
51 Gosheni, Holoni, na Gilo. Hii ilikuwa ni miji kumi na moja, kujumuisha na vijiji vyake.
and Goshen, and Holon, and Giloh; eleven cities with their villages.
52 Arabu, Duma, Ehani,
Arab, and Dumah, and Eshan;
53 Yanimu, Bethi Tapua, Afeka,
and Janim, and Bath-tappuah, and Aphekah;
54 Humta, Kiriathi Arba (ambayo ndio Hebroni), na Ziori. Hii ilikuwa miji tisa, pamoja na vijiji vyake.
and Humtah, and Kiriath-arba (the same is Hebron), and Zior; nine cities with their villages.
55 Maoni, Karmeli, Zifu, Yuta,
Maon, Carmel, and Ziph, and Jutah;
56 Yezreeli, Yokdeamu, Zanoa,
and Jezreel, and Jokdeam, and Zanoah;
57 Kaini, Gibea, na Timna. Hii ilikuwa ni miji kumi, kujumuisha na vijiji vyake.
Kain, Gibeah, and Timnah; ten cities with their villages.
58 Halhuli, Bethi Zuri, Gedori,
Halhul, Beth-zur, and Gedor;
59 Maarathi, Bethi Anothi, na Elitekoni. Hii ilikuwa miji sita, pamoja na vijiji vyake.
and Maarath, and Beth-anoth, and Eltekon; six cities with their villages.
60 Kiriathi Baali (ambayo ndio Kiriathi Yearimu), na Raba. Hii ilikuwa ni miji miwili, pamoja na vijiji vyake.
Kirjath-baal (the same is Kirjath-jearim), and Rabbah; two cities with their villages.
61 Katika nyika, kulikuwa na miji ya Bethi Araba, Midini, Sekaka,
In the wilderness, Beth-arabah, Middin, and Secacah;
62 Nibushani, mji wa chumvi, na Eni Gedi. Hii ilikuwa miji, pamoja na vijiji vyao.
and Nibshan, and the City of Salt, and En-gedi; six cities with their villages.
63 Lakini kwa Wayebusi, wenyeji wa Yerusalemu, kabila la Yuda halikuweza kuwafukuza, na hivyo, Wayebusi wanaishi pamoja na kabila la Yuda hadi leo hii.
And as for the Jebusites, the inhabitants of Jerusalem, the children of Judah could not drive them out: but the Jebusites dwelt with the children of Judah at Jerusalem, unto this day.

< Yoshua 15 >