< Yoshua 14 >

1 Maeneo haya ya nchi ambayo watu wa Israeli waliyapokea kama urithi wao katika nchi ya Kanaani. Urith huu uligawanywa kwao na Eliazeri kuhani, na Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa makabila ya mababu wa familia zao kati ya watu wa Israeli.
These also are the places which the children of Israel inherited in the land of Canaan, which Eleazar the Priest, and Ioshua the sonne of Nun and the chiefe fathers of the tribes of the children of Israel, distributed to them,
2 Urithi wao ulichaguliwa kwa kupiga kura kwa makabila tisa na nusu, kama vile Yahweh alivyoagiza kwa mkono wa Musa.
By the lot of their inheritance, as the Lord had commanded by the hande of Moses, to giue to the nine tribes, and the halfe tribe.
3 Kwa kuwa Musa alikuwa amewapa urithi makabila mawili na nusu ng'ambo ya Yordani, lakini Walawi hawakupewa urithi wowote.
For Moses had giuen inheritance vnto two tribes and an halfe tribe, beyond Iorde: but vnto the Leuites he gaue none inheritance among them.
4 Kabila la Yusufu kwa uhalisia yalikuwa makabila mawili, Manase na Efraimu. Na hakuna sehemu yoyote ya urithi waliyopewa Walawi katika nchi, lakini walipewa miji ya kuishi ndani yake pamoja na sehemu ya malisho ya mifugo yao na kwa ajili ya riziki zao.
For the childre of Ioseph were two tribes, Manasseh and Ephraim: therefore they gaue no part vnto the Leuites in the lande, saue cities to dwell in, with the suburbes of the same for their beastes and their substance.
5 Watu wa Israeli walifanya hivyo kama vile Yahweh alivyomwagiza Musa, basi waliiganywa nchi.
As the Lord had commanded Moses, so the children of Israel did when they deuided the land.
6 Kisha kabila la Yuda lilikuja kwa Yoshua huko Giligali. Kalebu mwana wa Yefune Mkenizi, akamwambia,”Unajua kile Yahweh alichomwambia Musa mtu wa Mungu juu yako na mimi huko Barnea.
Then the children of Iudah came vnto Ioshua in Gilgal: and Caleb the sonne of Iephunneh the Kenezite saide vnto him, Thou knowest what the Lord saide vnto Moses the man of God, concerning me and thee in Kadesh-barnea.
7 Nilikuwa na umri wa miaka arobani wakati Musa mtumishi wa Yahweh aliponituma kutoka Kadeshi Barnea kuipeleleza nchi. Nilimletea taarifa tena kama nilivyotakiwa kufanya katika moyo wangu.
Fourtie yeere olde was I, when Moses the seruant of the Lord sent me from Kadesh-barnea to espie the land, and I brought him word againe, as I thought in mine heart.
8 Lakini ndugu zangu walioenda pamoja nami waliifanya mioyo ya watu iyeyuke kwa woga. Lakini mimi nilimfuata Yahweh kabisa.
But my brethren that went vp with me, discouraged the heart of the people: yet I followed still the Lord my God.
9 Musa aliapa katika siku hiyo akisema, “Hakika nchi ambayo miguu yako imetembea juu yake itakuwa urithi wako na kwa watoto wako milele, kwasababu umemfuata kabisa Yahweh Mungu wangu.
Wherefore Moses sware the same day, saying, Certainely the land whereon thy feete haue troden, shalbe thine inheritance, and thy childrens for euer, because thou hast followed constantly the Lord my God.
10 Tazama! sasa, Yahweh amenihifadhi hai kwa miaka hii arobaini na tano, kama alivyosema - tangu kipindi kile Yahweh alivyomwambia Musa neno hili, wakati huo Waisraeli walikuwa wakitembea jangwani. Tazama! sasa katika siku hii ya leo nina miaka themanini na mitano.
Therefore beholde nowe, the Lord hath kept me aliue, as he promised: this is the fourtie and fift yeere since the Lord spake this thing vnto Moses, while the children of Israel wandered in the wildernes: and nowe loe, I am this day foure score and fiue yeere olde:
11 Bado hata siku hii ya leo nina nguvu kama nilivyokuwa katika siku ile ambayo Musa alinituma. Nguvu zangu za sasa ni sawa na nguvu zangu za kipindi kile, kwa ajili ya vita na kwa kwenda na kwa kuja.
And yet am as strong at this time, as I was when Moses sent me: as strong as I was then, so strong am I nowe, either for warre, or for gouernment.
12 Sasa basi, nipe nchi hii ya milima, ambayo Yahweh aliniahidi katika siku hiyo. Kwa kuwa ulisikia katika siku hiyo kuwa Wanakimu walikuwa huko katika miji yenye ngome. Itakuwa kwamba Yahweh atakuwa pamoja nami na ya kwamba nitawafukuzia mbali, kama vile Yahweh alivyosema.”
Nowe therefore giue me this mountaine whereof ye Lord spake in that day (for thou heardest in that day, how the Anakims were there, and the cities great and walled) if so be the Lord will be with me, that I may driue them out, as the Lord said.
13 Kisha Yoshua alimbariki Kalebu mwana wa Yefune na alimpa Hebroni kama urithi wake.
Then Ioshua blessed him, and gaue vnto Caleb the sonne of Iephunneh, Hebron for an inheritance.
14 Hivyo Hebroni ikawa urithi wa Kalebu mwana wa Yefune Mkenizi hata leo, kwasababu alimfuata kabisa Yahweh, Mungu wa Israeli.
Hebron therefore became the inheritance of Caleb the sonne of Iephunneh the Kenezite, vnto this day: because he followed constantly the Lord God of Israel.
15 Basi, jina la Hebroni hapo mwanzo lilikuwa ni Kiriathi Arba ( Arba ambaye alikuwa ni mtu mkuu miongoni mwa Wanakim). Kisha nchi ikawa na raha bila vita.
And the name of Hebron was before time, Kiriath-arba: which Arba was a great man amog the Anakims: thus the land ceassed from warre.

< Yoshua 14 >