< Yoshua 12 >
1 Basi hawa ndio wafalme wa nchi, ambao watu wa Israeli walishindwa. Waisraeli walichukua miliki ya nchi katika upande wa mashariki mwa Yordani sehemu ambako jua huchomoza, kutoka bonde la Mto Arnoni hadi Mlima Hermoni, na nchi yote ya Araba kuelekea kusini.
hii sunt reges quos percusserunt filii Israhel et possederunt terram eorum trans Iordanem ad solis ortum a torrente Arnon usque ad montem Hermon et omnem orientalem plagam quae respicit solitudinem
2 Sihoni, mfalme wa Waamori, aliishi katika Heshiboni. Alitawala kutoka Aroeri, ambayo iko juu ya bonde la Arnoni kutoka katikati ya bonde, na nusu ya Geleadi kushuka mpaka Mto Yaboki katika mpaka wa Waamori.
Seon rex Amorreorum qui habitavit in Esebon dominatus est ab Aroer quae sita est super ripam torrentis Arnon et mediae partis in valle dimidiique Galaad usque ad torrentem Iaboc qui est terminus filiorum Ammon
3 Sihoni pia alitawala juu ya Araba mpaka Bahari ya Kinerethi, kwenda mashariki, kuelekea Bahari ya Araba (Bahari ya Chumvi) upande wa mashariki, hadi huko Bethi Yeshimothi na upande wa kusini, kuelekea chini ya miteremko wa Mlima Pisiga.
et a solitudine usque ad mare Cheneroth contra orientem et usque ad mare Deserti quod est mare Salsissimum ad orientalem plagam per viam quae ducit Bethesimoth et ab australi parte quae subiacent Asedothphasga
4 Ogu, mfalme wa Bashani, mmoja kati ya mabaki ya Rephaimu, aliyeishi huko Shatarothi na Edrei.
terminus Og regis Basan de reliquiis Rafaim qui habitavit in Astharoth et in Edrain et dominatus est in monte Hermon et in Salacha atque in universa Basan usque ad terminos
5 Alitawala juu ya Mlima Hermoni, Saleka, na Bahani yote, hadi mpaka wa watu wa Geshuri na Wamakathi, na nusu ya Gleadi, hadi kufika mpaka wa Sihohi, mfalme wa Heshboni.
Gesuri et Machathi et dimidiae partis Galaad terminos Seon regis Esebon
6 Musa mtumishi wa Yahweh, na watu wa Israeli walikuwa wamewashinda, na Musa mtumishi wa Yahweh aliwapa nchi kama mali ya Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase.
Moses famulus Domini et filii Israhel percusserunt eos tradiditque terram eorum Moses in possessionem Rubenitis et Gadditis et dimidiae tribui Manasse
7 Hawa ndio wafalme wa nchi ambayo Yoshua na watu wa Israeli waliwashinda katika upande wa magharibi mwa mto Yordani, kutoka Baali Gadi katika bonde karibu na Lebanoni hadi Mlima Halaki karibu na Edom. Yoshua aliyapa nchi makabila ya Israeli ili yaimiliki.
hii sunt reges terrae quos percussit Iosue et filii Israhel trans Iordanem ad occidentalem plagam a Baalgad in campo Libani usque ad montem cuius pars ascendit in Seir tradiditque eam Iosue in possessionem tribubus Israhel singulis partes suas
8 Aliwapa nchi ya milima, tambarare, Araba, sehemu za milima, nyika na Negevu, nchi ya Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi.
tam in montanis quam in planis atque campestribus in Aseroth et solitudine ac meridie Hettheus fuit et Amorreus Chananeus et Ferezeus Eveus et Iebuseus
9 Wafalme hawa walikuwa ni mfalme wa Yeriko, mfalme wa Ai iliyo karibu na Betheli,
rex Hiericho unus rex Ahi quae est ex latere Bethel unus
10 mfalme wa Yerusalemu, mfalme wa Enaimu,
rex Hierusalem unus rex Hebron unus
11 mfalme wa Yarmuthi, mfalme wa Lakishi,
rex Hierimoth unus rex Lachis unus
12 mfalme wa Egloni, mfalme wa Gezeri,
rex Eglon unus rex Gazer unus
13 mfalme wa Debiri, mfalme wa Gederi,
rex Dabir unus rex Gader unus
14 mfalme wa Horima, mfalme wa Aradi,
rex Herma unus rex Hered unus
15 mfalme wa Libna, mfalme wa Adula,
rex Lebna unus rex Odollam unus
16 mfalme wa Makeda, mfalme wa Betheli,
rex Maceda unus rex Bethel unus
17 mfalme wa Tapua, mfalme wa Heferi,
rex Thaffua unus rex Afer unus
18 mfalme wa Afeki, mfalme wa Lasharoni,
rex Afec unus rex Saron unus
19 mfalme wa Madoni, mfalme wa Hazori,
rex Madon unus rex Asor unus
20 mfalme wa Shimroni - Meroni, mfalme wa Akshafu.
rex Someron unus rex Acsaph unus
21 mfalme wa Taanaki, mfalme wa Megido,
rex Thenach unus rex Mageddo unus
22 mfalme wa Kedeshi, mfalme wa Jokineamu katika Karmeli,
rex Cades unus rex Iachanaem Chermeli unus
23 mfalme wa Dori katika Nafutali Dori, mfalme Goyimu katika Giligali, na
rex Dor et provinciae Dor unus rex gentium Galgal unus
24 mfalme Tiriza. Hesabu ya wafalme ilikuwa ni thelathini na moja kwa ujumla wake.
rex Thersa unus omnes reges triginta et unus