< Yoshua 12 >

1 Basi hawa ndio wafalme wa nchi, ambao watu wa Israeli walishindwa. Waisraeli walichukua miliki ya nchi katika upande wa mashariki mwa Yordani sehemu ambako jua huchomoza, kutoka bonde la Mto Arnoni hadi Mlima Hermoni, na nchi yote ya Araba kuelekea kusini.
ואלה מלכי הארץ אשר הכו בני ישראל וירשו את ארצם בעבר הירדן מזרחה השמש מנחל ארנון עד הר חרמון וכל הערבה מזרחה׃
2 Sihoni, mfalme wa Waamori, aliishi katika Heshiboni. Alitawala kutoka Aroeri, ambayo iko juu ya bonde la Arnoni kutoka katikati ya bonde, na nusu ya Geleadi kushuka mpaka Mto Yaboki katika mpaka wa Waamori.
סיחון מלך האמרי היושב בחשבון משל מערוער אשר על שפת נחל ארנון ותוך הנחל וחצי הגלעד ועד יבק הנחל גבול בני עמון׃
3 Sihoni pia alitawala juu ya Araba mpaka Bahari ya Kinerethi, kwenda mashariki, kuelekea Bahari ya Araba (Bahari ya Chumvi) upande wa mashariki, hadi huko Bethi Yeshimothi na upande wa kusini, kuelekea chini ya miteremko wa Mlima Pisiga.
והערבה עד ים כנרות מזרחה ועד ים הערבה ים המלח מזרחה דרך בית הישמות ומתימן תחת אשדות הפסגה׃
4 Ogu, mfalme wa Bashani, mmoja kati ya mabaki ya Rephaimu, aliyeishi huko Shatarothi na Edrei.
וגבול עוג מלך הבשן מיתר הרפאים היושב בעשתרות ובאדרעי׃
5 Alitawala juu ya Mlima Hermoni, Saleka, na Bahani yote, hadi mpaka wa watu wa Geshuri na Wamakathi, na nusu ya Gleadi, hadi kufika mpaka wa Sihohi, mfalme wa Heshboni.
ומשל בהר חרמון ובסלכה ובכל הבשן עד גבול הגשורי והמעכתי וחצי הגלעד גבול סיחון מלך חשבון׃
6 Musa mtumishi wa Yahweh, na watu wa Israeli walikuwa wamewashinda, na Musa mtumishi wa Yahweh aliwapa nchi kama mali ya Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase.
משה עבד יהוה ובני ישראל הכום ויתנה משה עבד יהוה ירשה לראובני ולגדי ולחצי שבט המנשה׃
7 Hawa ndio wafalme wa nchi ambayo Yoshua na watu wa Israeli waliwashinda katika upande wa magharibi mwa mto Yordani, kutoka Baali Gadi katika bonde karibu na Lebanoni hadi Mlima Halaki karibu na Edom. Yoshua aliyapa nchi makabila ya Israeli ili yaimiliki.
ואלה מלכי הארץ אשר הכה יהושע ובני ישראל בעבר הירדן ימה מבעל גד בבקעת הלבנון ועד ההר החלק העלה שעירה ויתנה יהושע לשבטי ישראל ירשה כמחלקתם׃
8 Aliwapa nchi ya milima, tambarare, Araba, sehemu za milima, nyika na Negevu, nchi ya Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi.
בהר ובשפלה ובערבה ובאשדות ובמדבר ובנגב החתי האמרי והכנעני הפרזי החוי והיבוסי׃
9 Wafalme hawa walikuwa ni mfalme wa Yeriko, mfalme wa Ai iliyo karibu na Betheli,
מלך יריחו אחד מלך העי אשר מצד בית אל אחד׃
10 mfalme wa Yerusalemu, mfalme wa Enaimu,
מלך ירושלם אחד מלך חברון אחד׃
11 mfalme wa Yarmuthi, mfalme wa Lakishi,
מלך ירמות אחד מלך לכיש אחד׃
12 mfalme wa Egloni, mfalme wa Gezeri,
מלך עגלון אחד מלך גזר אחד׃
13 mfalme wa Debiri, mfalme wa Gederi,
מלך דבר אחד מלך גדר אחד׃
14 mfalme wa Horima, mfalme wa Aradi,
מלך חרמה אחד מלך ערד אחד׃
15 mfalme wa Libna, mfalme wa Adula,
מלך לבנה אחד מלך עדלם אחד׃
16 mfalme wa Makeda, mfalme wa Betheli,
מלך מקדה אחד מלך בית אל אחד׃
17 mfalme wa Tapua, mfalme wa Heferi,
מלך תפוח אחד מלך חפר אחד׃
18 mfalme wa Afeki, mfalme wa Lasharoni,
מלך אפק אחד מלך לשרון אחד׃
19 mfalme wa Madoni, mfalme wa Hazori,
מלך מדון אחד מלך חצור אחד׃
20 mfalme wa Shimroni - Meroni, mfalme wa Akshafu.
מלך שמרון מראון אחד מלך אכשף אחד׃
21 mfalme wa Taanaki, mfalme wa Megido,
מלך תענך אחד מלך מגדו אחד׃
22 mfalme wa Kedeshi, mfalme wa Jokineamu katika Karmeli,
מלך קדש אחד מלך יקנעם לכרמל אחד׃
23 mfalme wa Dori katika Nafutali Dori, mfalme Goyimu katika Giligali, na
מלך דור לנפת דור אחד מלך גוים לגלגל אחד׃
24 mfalme Tiriza. Hesabu ya wafalme ilikuwa ni thelathini na moja kwa ujumla wake.
מלך תרצה אחד כל מלכים שלשים ואחד׃

< Yoshua 12 >