< Yona 2 >

1 Kisha Yona akamwomba Bwana Mungu wake kutoka katika tumbo la samaki.
Then Jonah prayed unto the LORD his God out of the fish’s belly.
2 Akasema, Nimemwita Bwana juu ya shida yangu naye akanijibu; kutoka tumbo la Kuzimu nililia kwa msaada! Uliisikia sauti yangu. (Sheol h7585)
And he said, I called by reason of mine affliction unto the LORD, and he answered me; out of the belly of hell cried I, [and] thou heardest my voice. (Sheol h7585)
3 Ulikuwa umenitupa ndani ya kina, ndani ya moyo wa bahari, na maji yaliyonizunguka; mawimbi yako yote na gharika yalipita juu yangu.
For thou didst cast me into the depth, in the heart of the seas, and the flood was round about me; all thy waves and thy billows passed over me.
4 Nikasema, 'Nimefukuzwa mbele ya macho yako; lakini nitaangalia tena juu ya hekalu lako takatifu. '
And I said, am cast out from before thine eyes; yet I will look again toward thy holy temple.
5 Maji yalifunika kunizunguka karibu na shingo yangu; kina kilinizunguka; mwani ukakizinga kichwa changu.
The waters compassed me about, even to the soul; the deep was round about me; the weeds were wrapped about my head.
6 Nilikwenda chini ya milima; nchi na baa zake zimefungwa juu yangu milele. Lakini wewe umeinua uhai wangu shimoni, Bwana, Mungu wangu!
I went down to the bottoms of the mountains; the earth with her bars [closed] upon me for ever: yet hast thou brought up my life from the pit, O LORD my God.
7 Wakati nafsi yangu ilipozimia ndani yangu, nikamwita Bwana; basi sala yangu ilikujia, katika hekalu lako takatifu.
When my soul fainted within me, I remembered the LORD: and my prayer came in unto thee, into thine holy temple.
8 Wote ambao huzingatia miungu isiyofaa hukataa uaminifu wako wao wenyewe.
They that regard lying vanities forsake their own mercy.
9 Lakini mimi, nitakuchinjia kwa sauti ya shukrani; Nitayatimiza yale niliyoapa. Wokovu hutoka kwa Bwana!
But I will sacrifice unto thee with the voice of thanksgiving; I will pay that which I have vowed. Salvation is of the LORD.
10 Kisha Bwana akanena na samaki, akamtapika Yona juu ya nchi kavu.
And the LORD spake unto the fish, and it vomited out Jonah upon the dry land.

< Yona 2 >