< Yona 1 >

1 Ndipo neno la Bwana lilimjia Yona mwana wa Amittai, kusema,
And it came [the] word of Yahweh to Jonah [the] son of Amittai saying.
2 “Simama uende Ninawi, mji kuu, na ukapaze sauti dhidi yake, kwa sababu uovu wao umeinuka mbele yangu.”
Arise go to Nineveh the city great and call out on it for it has come up wickedness their before me.
3 Lakini Yona akaondoka kukimbia kutoka mbele ya Bwana na kwenda Tarshishi. Akatelemka mpaka Yafa na akaona melikebu inayokwenda Tarshishi. Kwa hiyo alilipa nauli na akapanda melikebu kwenda nayo Tarishishi, mbali na uwepo wa Yahweh.
And he arose Jonah to flee Tarshish towards from to before Yahweh and he went down Joppa and he found a ship - [which was] about to go Tarshish and he gave fare its and he went down in it to go with them Tarshish towards from to before Yahweh.
4 Lakini Bwana akatuma upepo mkubwa juu ya bahari, ikawa tufani juu ya bahari. Hivi karibuni ikaonekana kwamba meli ilikuwa inataka kuvunjika.
And Yahweh he threw a wind great to the sea and it was a storm great on the sea and the ship it thought to be broken.
5 Wale baharia waliogopa sana na kila mtu alilia kwa mungu wake mwenyewe. Wakatupa mizigo bahari iliyokuwa merikebuni ili kuifungua. Yona alikuwa ameshuka hapa pande za ndani ya melikebu, naye alikuwa amelala huko usingizi.
And they were afraid the sailors and they cried for help everyone to gods his and they threw the vessels which [were] in the ship into the sea to lighten from on them and Jonah he had gone down into [the] innermost parts of the ship and he had lain down and he had fallen fast asleep.
6 Basi nahoza akamwendea akamwambia, “kwa nini unalala? Amka! ukamwombe mungu wako! Labda mungu wako atatutambua na hatutapotea.”
And he drew near to him [the] chief of the sailor[s] and he said to him what? [is] to you sleeping arise call to god your perhaps he will give thought the god to us and not we will perish.
7 Wote wakaambiana, 'Njoni, tupige kura, ili tujue ni nani ndiye sababu ya mabaya haya yanayotupata.' Basi wakapiga kura, na kura ikaangukia kwa Yona.
And they said each to neighbor his come so let us cast lots so we may know by which of whom? the evil this [belongs] to us and they cast lots and it fell the lot on Jonah.
8 Kisha wakamwambia Yona, “Tafadhali tuambie ni nani ndiye sababu ya mabaya haya yanayotupata. Unafanya kazi gani, na umetoka wapi? Nchi yako ni ipi, na kutoka kwa watu wa kabila gani?”
And they said to him tell! please to us because of whom? the evil this [belongs] to us what? [is] occupation your and from where? do you come what? [is] land your and where? from this people [are] you.
9 Yona akawaambia, Mimi ni Mhebrania; Nami namuogopa Bwana, Mungu wa mbinguni, aliyeifanya bahari na nchi kavu.
And he said to them [am] a Hebrew I and Yahweh [the] God of the heavens I [am] fearing who he made the sea and the dry land.
10 Ndipo watu hao waliogopa zaidi, wakamwambia Yona, Ni jambo gani hili ulilolifanya? Kwa maana hao watu walijua kwamba alikuwa akikimbia mbele ya Bwana, kwa sababu alikuwa amewaambia.
And they feared the men a fear great and they said to him what? this have you done for they knew the men that from to before Yahweh he [was] fleeing for he had told to them.
11 Ndipo wakamwambia Yona, Tukufanyie nini ili bahari iweze kutulia? Kwa maana bahari ilikuwa imechafuka zaidi na zaidi.
And they said to him what? will we do to you so it may be calm the sea from on us for the sea [was] going and storming.
12 Yona akawaambia, “Nikamateni na nitupeni baharini. Kisha bahari itatulia kwa ajili yenu, kwa maana najua kwamba ni kwa sababu yangu kwamba tufani hii kubwa iwapate.”
And he said to them pick up me and throw me into the sea so it may be calm the sea from on you for [am] knowing I that by which to me the storm great this [is] on you.
13 Hata hivyo, watu hao wavuta makasia kwa bidii ili kurudi nchi kavu, lakini hawakuweza kufanya hivyo kwa sababu bahari ilikuwa imechafuka zaidi dhidi yao.
And they rowed the men to return to the dry land and not they were able for the sea [was] going and storming on them.
14 Basi wakamwomba Bwana, wakasema, Tunakuomba, Bwana, tunakuomba, usiache tuangamize kwa sababu ya maisha ya mtu huyu; wala usituwekee hatia ya kufa kwake, kwa kuwa wewe, Bwana, umefanya kama ulivyopenda.
And they called out to Yahweh and they said we beg you O Yahweh do not please let us perish by [the] life of the man this and may not you put on us blood innocent for you O Yahweh just as you pleased you have done.
15 Basi wakamchukua Yona wakamtupa baharini, nayo bahari ikaacha kuchafuka.
And they picked up Jonah and they threw him into the sea and it stopped the sea from storming its.
16 Ndipo watu wale wakamuogopa Bwana sana. Wakamtolea dhabihu Bwana na kuweka nadhiri.
And they feared the men a fear great Yahweh and they sacrificed a sacrifice to Yahweh and they vowed vows.
17 Bwana alikuwa ameandaa samaki mkubwa kummeza Yona, na Yona alikuwa ndani ya tumbo lasamaki siku tatu na usiku wa tatu.
And he appointed Yahweh a fish great to swallow Jonah and he was Jonah in [the] inward parts of the fish three days and three nights.

< Yona 1 >