< Yona 1 >

1 Ndipo neno la Bwana lilimjia Yona mwana wa Amittai, kusema,
And there is a word of YHWH to Jonah son of Amittai, saying,
2 “Simama uende Ninawi, mji kuu, na ukapaze sauti dhidi yake, kwa sababu uovu wao umeinuka mbele yangu.”
“Rise, go to Nineveh, the great city, and proclaim against it that their wickedness has come up before Me.”
3 Lakini Yona akaondoka kukimbia kutoka mbele ya Bwana na kwenda Tarshishi. Akatelemka mpaka Yafa na akaona melikebu inayokwenda Tarshishi. Kwa hiyo alilipa nauli na akapanda melikebu kwenda nayo Tarishishi, mbali na uwepo wa Yahweh.
And Jonah rises to flee to Tarshish from the face of YHWH, and goes down [to] Joppa, and finds a ship going [to] Tarshish, and he gives its fare, and goes down into it, to go with them to Tarshish from the face of YHWH.
4 Lakini Bwana akatuma upepo mkubwa juu ya bahari, ikawa tufani juu ya bahari. Hivi karibuni ikaonekana kwamba meli ilikuwa inataka kuvunjika.
And YHWH has cast a great wind on the sea, and there is a great storm in the sea, and the ship has reckoned to be broken;
5 Wale baharia waliogopa sana na kila mtu alilia kwa mungu wake mwenyewe. Wakatupa mizigo bahari iliyokuwa merikebuni ili kuifungua. Yona alikuwa ameshuka hapa pande za ndani ya melikebu, naye alikuwa amelala huko usingizi.
and the mariners are afraid, and they each cry to his god, and cast the goods that [are] in the ship into the sea, to make [it] light of them; and Jonah has gone down to the sides of the vessel, and he lies down, and is fast asleep.
6 Basi nahoza akamwendea akamwambia, “kwa nini unalala? Amka! ukamwombe mungu wako! Labda mungu wako atatutambua na hatutapotea.”
And the chief of the company draws near to him and says to him, “What are you [doing], O sleeper? Rise, call to your God, it may be God considers Himself of us, and we do not perish.”
7 Wote wakaambiana, 'Njoni, tupige kura, ili tujue ni nani ndiye sababu ya mabaya haya yanayotupata.' Basi wakapiga kura, na kura ikaangukia kwa Yona.
And they each say to his neighbor, “Come, and we cast lots, and we know on whose account this evil [is] on us.” And they cast lots, and the lot falls on Jonah.
8 Kisha wakamwambia Yona, “Tafadhali tuambie ni nani ndiye sababu ya mabaya haya yanayotupata. Unafanya kazi gani, na umetoka wapi? Nchi yako ni ipi, na kutoka kwa watu wa kabila gani?”
And they say to him, “Now declare to us, on whose account [is] this evil on us? What [is] your occupation, and where do you come from? What [is] your country, seeing you are not of this people?”
9 Yona akawaambia, Mimi ni Mhebrania; Nami namuogopa Bwana, Mungu wa mbinguni, aliyeifanya bahari na nchi kavu.
And he says to them, “I—a Hebrew, and I fear YHWH, God of the heavens, who made the sea and the dry land.”
10 Ndipo watu hao waliogopa zaidi, wakamwambia Yona, Ni jambo gani hili ulilolifanya? Kwa maana hao watu walijua kwamba alikuwa akikimbia mbele ya Bwana, kwa sababu alikuwa amewaambia.
And the men fear a great fear, and say to him, “What [is] this you have done!” For the men have known that he is fleeing from the face of YHWH, for he has told them.
11 Ndipo wakamwambia Yona, Tukufanyie nini ili bahari iweze kutulia? Kwa maana bahari ilikuwa imechafuka zaidi na zaidi.
And they say to him, “What do we do to you that the sea may cease from us, for the sea is more and more turbulent?”
12 Yona akawaambia, “Nikamateni na nitupeni baharini. Kisha bahari itatulia kwa ajili yenu, kwa maana najua kwamba ni kwa sababu yangu kwamba tufani hii kubwa iwapate.”
And he says to them, “Lift me up, and cast me into the sea, and the sea ceases from you; for I know that on my account this great storm [is] on you.”
13 Hata hivyo, watu hao wavuta makasia kwa bidii ili kurudi nchi kavu, lakini hawakuweza kufanya hivyo kwa sababu bahari ilikuwa imechafuka zaidi dhidi yao.
And the men row to turn back to the dry land, and are not able, for the sea is more and more turbulent against them.
14 Basi wakamwomba Bwana, wakasema, Tunakuomba, Bwana, tunakuomba, usiache tuangamize kwa sababu ya maisha ya mtu huyu; wala usituwekee hatia ya kufa kwake, kwa kuwa wewe, Bwana, umefanya kama ulivyopenda.
And they cry to YHWH, and say, “Ah, now, O YHWH, please do not let us perish for this man’s life, and do not lay innocent blood on us! For You, YHWH, as You have pleased, You have done.”
15 Basi wakamchukua Yona wakamtupa baharini, nayo bahari ikaacha kuchafuka.
And they lift up Jonah, and cast him into the sea, and the sea ceases from its raging;
16 Ndipo watu wale wakamuogopa Bwana sana. Wakamtolea dhabihu Bwana na kuweka nadhiri.
and the men fear YHWH [with] a great fear, and sacrifice a sacrifice to YHWH, and vow vows.
17 Bwana alikuwa ameandaa samaki mkubwa kummeza Yona, na Yona alikuwa ndani ya tumbo lasamaki siku tatu na usiku wa tatu.
And YHWH appoints a great fish to swallow up Jonah, and Jonah is in the bowels of the fish three days and three nights.

< Yona 1 >