< Yohana 1 >

1 Mwanzoni kulikuwako Neno, na Neno alikuwa pamoja na Mungu, na Neno alikuwa Mungu.
Au commencement était la Parole, et la Parole était avec Dieu, et la Parole était Dieu.
2 Huyu, Neno, Mwanzoni alikuwa pamoja na Mungu.
Elle était au commencement avec Dieu.
3 Vitu vyote vilifanyika kupitia yeye, na pasipo yeye hakuna hata kitu kimoja kilichokuwa kimefanyika.
Toutes choses ont été faites par elle, et rien de ce qui a été fait n'a été fait sans elle.
4 Ndani yake kulikuwa uzima, na huo uzima ulikuwa nuru ya wanadamu wote.
En elle était la vie, et la vie était la lumière des hommes.
5 Nuru yang'aa gizani, wala giza halikuizimisha.
La lumière brille dans les ténèbres, et les ténèbres ne l'ont point reçue.
6 Palikuwa na mtu aliyetumwa kutoka kwa Mungu, ambaye jina lake alikuwa Yohana.
Il y eut un homme, envoyé de Dieu, dont le nom était Jean.
7 Alikuja kama shahidi kushuhudia kuhusu ile nuru, ili kwamba wote waweze kuamini kupitia yeye.
Il vint pour être témoin, pour rendre témoignage à la lumière, afin que, par lui, tous fussent amenés à la foi.
8 Yohana hakuwa ile nuru, bali alikuja ili ashuhudie kuhusu ile nuru
Il n'était pas lui-même la Lumière, mais il devait rendre témoignage à la Lumière.
9 Hiyo ilikuwa nuru ya kweli ambayo ilikuwa inakuja katika dunia nayo humtia nuru kila mmoja
Celle-ci était la véritable Lumière, qui éclaire tout homme en venant dans le monde.
10 Alikuwa katika dunia, na dunia iliumbwa kupitia yeye, na dunia haikumjua.
La Parole était dans le monde, et le monde a été fait par elle; mais le monde ne l'a pas connue.
11 Alikuja kwa vitu vyake, na watu wake hawakumpokea.
Elle est venue chez les siens, et les siens ne l'ont point reçue.
12 Bali kwa wale wengi waliompokea, ambao waliamini jina lake, kwa hao aliwapa haki ya kuwa wana wa Mungu,
Mais à tous ceux qui l'ont reçue, elle a donné le pouvoir de devenir enfants de Dieu, à tous ceux qui croient en son nom,
13 Ambao walizaliwa, sio kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili, wala kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu mwenyewe.
qui ne sont pas nés du sang, ni de la volonté de la chair, ni de la volonté de l'homme, mais qui sont nés de Dieu.
14 Naye Neno alifanyika mwili na akaishi miongoni mwetu, tumeuona utukufu wake, utukufu kama wa mtu pekee wa kipekee aliyekuja kutoka kwa Baba, amejaa neema na kweli.
La Parole a été faite chair; elle a habité parmi nous, pleine de grâce et de vérité, et nous avons contemplé sa gloire, une gloire telle qu'est celle du Fils unique venu d'auprès du Père.
15 Yohana alishuhudia kuhusu yeye, na alipaza sauti akisema, “Huyu ndiye ambaye nilisema habari zake nikisema, “Yule ajaye baada yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa sababu amekuwako kabla yangu.”
Jean lui rendait témoignage lorsqu'il s'écriait: C'est de lui que je disais: Celui qui vient après moi m'a devancé, parce qu'il était avant moi.
16 Kwa kuwa kutoka katika utimilifu wake, sisi sote tumepokea bure kipawa baada ya kipawa.
En effet, c'est de sa plénitude que nous avons tous reçu grâce sur grâce.
17 Kwa kuwa sheria ililetwa kupitia Musa. Neema na kweli vilikuja kupitia Yesu Kristo.
Car la loi a été donnée par Moïse; la grâce et la vérité sont venues par Jésus-Christ.
18 Hakuna mwanadamu aliyemwona Mungu wakati wowote. Mtu pekee ambaye ni Mungu, aliye katika kifua cha Baba, amemfanya yeye ajulikane.
Personne n'a jamais vu Dieu; le Fils unique, qui est dans le sein du Père, est celui qui nous l'a fait connaître.
19 Na huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati makuhani na walawi waliotumwa kwake na Wayahudi kumwuliza, “Wewe ni nani?”
Voici quel fut le témoignage de Jean, lorsque les Juifs envoyèrent de Jérusalem des sacrificateurs et des lévites pour lui demander: Qui es-tu? Il fit cette déclaration, et il la confirma sans réserves:
20 Bila kusitasita na hakukana, bali alijibu, “Mimi sio Kristo.”
Moi, déclara-t-il, je ne suis pas le Christ.
21 Hivyo wakamuuliza, “kwa hiyo wewe ni nani sasa?” Wewe ni Eliya? Akasema, “Mimi siye.” Wakasema, Wewe ni nabii? Akajibu,” Hapana.”
Qui es-tu donc? lui demandèrent-ils, — es-tu Élie? Et il dit: Je ne le suis pas. Es-tu le prophète? Il répondit: Non.
22 Kisha wakamwambia, “Wewe ni nani, ili kwamba tuwape jibu waliotutuma”? Wajishuhudiaje wewe mwenyewe?”
Ils reprirent: Dis-nous donc qui tu es, afin que nous puissions donner une réponse à ceux qui nous ont envoyés. Que dis-tu au sujet de toi-même?
23 Akasema, “Mimi ni sauti yake aliaye nyikani: 'Inyosheni njia ya Bwana,' kama nabii Isaya alivyosema.”
Il répondit: Je suis la voix de celui qui crie dans le désert: «Aplanissez le chemin du Seigneur», comme l'a dit le prophète Ésaïe.
24 Basi kulikuwa na watu wametumwa pale kutoka kwa Mafarisayo. Wakamuuliza na kusema,
Ceux qui avaient été envoyés vers lui étaient des pharisiens.
25 “Kwa nini unabatiza basi kama wewe sio Kristo wala Eliya wala nabii?”
Ils lui demandèrent encore: Pourquoi donc baptises-tu, si tu n'es pas le Christ, ni Elie, ni le prophète?
26 Yohana aliwajibu akisema, “Ninabatiza kwa maji. Hata hivyo, miongoni mwenu anasimama mtu msiyemtambua.
Jean leur répondit: Pour moi, je baptise d'eau; mais il en est un au milieu de vous, que vous ne connaissez pas.
27 Huyu ndiye ajaye baada yangu. Mimi sisitahili kulegeza kamba za viatu vyake.”
C'est celui qui vient après moi, et je ne suis pas digne de délier la courroie de sa chaussure.
28 Mambo haya yalitendeka huko Bethania, ng'ambo ya Yordani, mahali ambapo Yohana alikuwa akibatiza.
Ces choses se passèrent à Béthanie au delà du Jourdain, où Jean baptisait.
29 Siku iliyofuata Yohana alimwona Yesu akija kwake akasema, “Tazama mwanakondoo wa Mungu aichukuae dhambi ya ulimwengu!
Le lendemain, Jean vit Jésus qui venait à lui, et il dit: Voici l'agneau de Dieu, qui ôte le péché du monde.
30 huyu ndiye niliyesema habari zake nikisema, “Yeye ajaye nyuma yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa kuwa alikuwa kabla yangu.'
C'est celui dont je disais: Il vient après moi un homme qui m'a devancé, parce qu'il était avant moi.
31 Sikumtambua yeye, lakini ilifanyika hivyo ili kwamba afunuliwe katika Israeli, kwamba nilikuja nikibatiza kwa maji.”
Pour moi, je ne le connaissais pas; mais je suis venu baptiser d'eau, afin qu'il fût manifesté à Israël.
32 Yohana alishuhudia, “Niliona Roho akishuka kutoka mbinguni mfano wa hua, na ilibaki juu yake.
Jean rendit encore ce témoignage: J'ai vu l'Esprit descendre du ciel comme une colombe, et il s'est arrêté sur lui.
33 Mimi sikumtambua lakini yeye aliyenituma ili nibatize kwa maji aliniambia, 'yule ambaye utaona Roho akishuka na kukaa juu yake, Huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu.'
Pour moi, je ne le connaissais pas; mais celui qui m'a envoyé baptiser d'eau m'a dit: Celui sur qui tu verras l'Esprit descendre et s'arrêter, c'est celui qui baptise d'Esprit saint.
34 Nimeona na nimeshuhudia kwamba huyu ni Mwana wa Mungu.”
Je l'ai vu, et j'ai rendu ce témoignage: C'est lui qui est le Fils de Dieu.
35 Tena siku iliyofuata Yohana alikuwa amesimama pamoja na wanafunzi wake wawili,
Le lendemain, Jean se trouvait là de nouveau avec deux de ses disciples;
36 walimwona Yesu akitembea na Yohana akasema, “Tazama, Mwana kondoo wa Mungu!”
et, regardant Jésus qui passait, il dit: Voici l'agneau de Dieu!
37 Wanafunzi wawili walimsikia Yohana akisema haya wakamfuata Yesu.
Les deux disciples entendirent cette parole, et ils suivirent Jésus.
38 Tena Yesu aligeuka na kuwaona wanafunzi wale wakimfuata, na akawambia, “Mnataka nini?” Wakajibu, “Rabbi, (maana yake 'mwalimu,' unaishi wapi?”
Jésus, s'étant retourné et voyant qu'ils le suivaient, leur dit: Que cherchez-vous? Ils lui répondirent: Rabbi, — c'est-à-dire Maître, — où demeures-tu?
39 Akawambia, “Njooni na mwone.”Kisha walikwenda na kuona mahali alipokuwa akiishi; walikaa pamoja naye siku hiyo, kwa kuwa ilikuwa yapata kama saa kumi hivi.
Il leur dit: Venez et voyez. Ils allèrent donc et virent où il demeurait, et ils restèrent auprès de lui ce jour-là. C'était environ la dixième heure.
40 Mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana akiongea na kisha kumfuata Yesu alikuwa ni Andrea, ndugu yake Simoni Petro.
André, frère de Simon Pierre, était l'un des deux qui avaient entendu ce que Jean disait, et qui avaient suivi Jésus.
41 Akamwona ndugu yake Simoni na akamwambia, “Tumempata Masihi” (ambayo inatafsiriwa Kristo).
Il trouva d'abord son frère Simon, et il lui dit: Nous avons trouvé le Messie — c'est-à-dire le Christ —.
42 Akamleta kwa Yesu. Yesu akamtazama na akasema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana” utaitwa Kefa,” (maana yake 'Petro').
Et il l'amena à Jésus. Jésus, l'ayant regardé, lui dit: Tu es Simon, fils de Jona; tu seras appelé Céphas — c'est-à-dire Pierre —.
43 Siku iliyofuata wakati Yesu alipotaka kuondoka kwenda Galilaya, alimpata Filipo na akamwambia, “Nifuate mimi.”
Le lendemain, Jésus voulut se rendre en Galilée. Il rencontra Philippe et lui dit: Suis-moi.
44 Filipo alikuwa ni mwenyeji wa Bethsaida, mji wa Andrea na Petro.
Or, Philippe était de Bethsaïda, la ville d'André et de Pierre.
45 Filipo alimpata Nathanaeli na kumwambia, Tumempata yule ambaye Musa aliandika habari zake katika sheria na Manabii. Yesu mwana wa Yusufu, kutoka Nazareti.
Philippe rencontra Nathanaël, et il lui dit: Nous avons trouvé celui dont Moïse a parlé dans la loi et dont les prophètes aussi ont parlé; c'est Jésus de Nazareth, le fils de Joseph.
46 Nathanaeli akamwambia, “Je kitu chema chaweza kutokea Nazareti?” Filipo akamwambia, Njoo na uone.”
Nathanaël lui dit: Peut-il venir quelque chose de bon de Nazareth? Philippe lui répondit: Viens et vois!
47 Yesu akamwona Nathanaeli akija kwake na akasema, “Tazama, Mwisraeli kweli kweli asiye na udanganyifu ndani yake!”
Jésus, voyant venir à lui Nathanaël, dit de lui: Voici un véritable Israélite, dans lequel il n'y a point de fraude. Nathanaël lui dit:
48 Nathanaeli akamwambia, “Umenifahamuje mimi?” Yesu akajibu na akamwambia, “Kabla Filipo hajakuita ulipokuwa chini ya mtini, nalikuona.”
D'où me connais-tu? Jésus lui répondit: Avant que Philippe t'appelât, je t'ai vu, quand tu étais sous le figuier.
49 Nathanaeli akajibu, “Rabi wewe u Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli”!
Nathanaël reprit: Maître, tu es le Fils de Dieu, tu es le roi d'Israël!
50 Yesu akajibu akamwambia, Kwa sababu nilikuambia 'nilikuona chini ya mtini' je waamini? utaona matendo makubwa kuliko haya.”
Jésus répondit: Parce que je t'ai dit que je t'avais vu sous le figuier, tu crois; tu verras de plus grandes choses que celles-ci!
51 Yesu akasema, “Amini amini nawambieni mtaziona mbingu zikifunguka, na kuwaona malaika wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”
Et il ajouta: En vérité, en vérité, je vous le déclare, vous verrez le ciel ouvert, et les anges de Dieu montant et descendant sur le Fils de l'homme.

< Yohana 1 >