< Yohana 9 >

1 Wakati, kama Yesu alipokuwa akipita, alimwona mtu kipofu tangu kuzaliwa kwake.
Comme il passait, il vit un homme aveugle de naissance,
2 Wanafunzi wake wakamwuliza, “Rabi, nani aliyetenda dhambi, mtu huyu au wazazi wake, hata azaliwe kipofu?”
et ses disciples lui demandèrent: «Maître, qui est-ce qui a péché, de cet homme, ou de ses parents, pour qu'il soit né aveugle?»
3 Yesu akawajibu, “Siyo huyu mtu wala wazazi wake waliotenda dhambi, bali kazi za Mungu zipate kufunuliwa kupitia kwake.
Jésus répondit: «Ce n'est pas qu'il ait péché, ni lui, ni ses parents, mais c'est afin que les oeuvres de Dieu éclatent en lui.
4 Tunapaswa kufanya kazi zake yeye aliyenituma wakati bado ni mchana. Usiku waja wakati ambapo hakuna atakayeweza kufanya kazi.
Il nous faut faire les oeuvres de celui qui m'a envoyé, pendant qu'il est jour; la nuit vient, où l'on ne peut travailler.
5 Wakati niwapo ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu.”
Pendant que je suis dans le monde, je suis la lumière du monde.»
6 Baada ya Yesu kusema maneno haya, alitema kwenye ardhi, alifanya tope kwa mate, na akampaka yule mtu machoni na lile tope.
Ayant ainsi parlé, il cracha à terre, fit de la boue avec sa salive, enduisit de cette boue les yeux de l'aveugle,
7 Akamwambia, nenda kaoge katika kisima cha Siloam (Inayotafsiriwa kama 'aliyetumwa').” Kwa hiyo huyo mtu alienda, akanawa, na akarudi, anaona.
et lui dit: «Va, lave-toi au réservoir de Siloé» (nom qui signifie Envoyé). Il s'en alla donc, se lava, et revint clairvoyant.
8 Majirani wa yule mtu na wale waliomuona mwanzo kama mwombaji walisema, Je! huyu siye yule mtu aliyekuwa akikaa na kuomba?” wengine walisema, “Ni yeye.”
Ses voisins et ceux qui auparavant l'avaient vu mendier, disaient: «N'est-ce pas là celui qui était assis et qui mendiait?»
9 Na wengine walisema, “Hapana, bali anafanana naye.” Lakini alikuwa akisema, “Ni mimi.”
Les uns disaient: «C'est lui.» — «Non, disaient d'autres, mais il lui ressemble.» Lui disait: «C'est moi.»
10 Wakamwambia, “Sasa macho yako yalifunguliwaje?”
Sur quoi ils lui dirent: «Comment tes yeux ont-ils été ouverts?»
11 Alijibu, mtu aitwaye Yesu alifanya tope na kupaka macho yangu na kuniambia, 'Nenda Siloam ukanawe.' Kwa hiyo nilienda, na nikanawa, na nikapata kuona tena.”
Il répondit: «Un homme appelé Jésus a fait de la boue, il m'en a enduit les yeux, et m'a dit: «Va à Siloé, et te lave.» J'y suis allé, et, m'étant lavé, j'ai recouvré la vue.»
12 Wakamwambia, “Yuko wapi?” Alijibu, “Sijui.”
Ils lui dirent: «où est cet homme?» — «Je ne sais pas, » répondit-il.
13 Wakampeleka yule mtu aliyewahi kuwa kipofu kwa Mafarisayo.
Ils menèrent vers les pharisiens celui qui naguère était aveugle.
14 Nayo ilikuwa siku ya Sabato wakati Yesu alipotengeneza tope na kuyafumbua macho yake.
Or, c'était un jour de sabbat que Jésus avait fait de la boue, et lui avait ouvert les yeux.
15 Ndipo tena Mafarisayo wakamwuliza alipataje kuona. Aliwaambia, “Aliweka tope katika macho yangu, nikanawa, na sasa naweza kuona.”
Les pharisiens à leur tour, lui demandèrent aussi comment il avait recouvré la vue; et il leur dit: «Il m'a mis de la boue sur les yeux; je me suis lavé, et je vois.»
16 Baadhi ya Mafarisayo wakasema, “Mtu huyu hajatoka kwa Mungu kwa sababu haishiki Sabato.” Wengine walisema, “Inawezekanaje mtu mwenye dhambi kufanya ishara kama hizo?” Kwa hiyo kukawa na mgawanyiko kati yao.
Là-dessus, quelques-uns des pharisiens dirent: «Cet homme n'est pas envoyé de Dieu, puisqu'il n'observe pas le sabbat.» Mais d'autres disaient: «Comment un méchant pourrait-il faire de tels miracles?» Et ils étaient divisés entre eux.
17 Ndipo walipomwuliza yule kipofu tena, “Unasemaje juu yake kwa sababu aliyafungua macho yako?” Kipofu akasema, “Ni nabii.”
Ils dirent donc de nouveau à l'aveugle: » Et toi, que dis-tu de cet homme qui t'a ouvert les yeux?» — «C'est un prophète, » dit-il.
18 Hata wakati huu Wayahudi hawakumwamini kwamba alikuwa kipofu naye amepata kuona mpaka walipowaita wazazi wake yeye aliyepata kuona.
Les Juifs ne voulurent point croire que cet homme eût été aveugle et qu'il eût recouvré la vue, jusqu’à ce qu'ils eussent fait venir son père et sa mère.
19 Waliwauliza wazazi, Je, huyu ni mtoto wenu mnayesema alizaliwa kipofu? amewezaje sasa kuona?”
Et ils les interrogèrent: «Est-ce là, demandèrent-ils, votre fils, que vous dites être né aveugle? Comment donc voit-il à cette heure?»
20 Hivyo wazazi wake wakamjibu, “Tunajua kuwa huyu ni mtoto wetu na kwamba alizaliwa kipofu.
Les parents répondirent: «Nous savons que c'est bien là notre fils, et qu'il est né aveugle;
21 Jinsi gani sasa anaona, hatujui, na yeye aliyemfumbua macho yake, hatumjui. Mwulizeni yeye. Ni mtu mzima. Anaweza kujieleza mwenyewe.”
mais comment il se fait qu'il voie maintenant, nous l'ignorons; qui lui a ouvert les yeux, nous ne le savons pas. Interrogez-le, il a de l'âge, il s'expliquera lui-même.»
22 Wazazi wake walisema mambo haya, kwa sababu waliwaogopa Wayahudi. Kwa vile Wayahudi walikuwa wamekubaliana tayari kuwa, ikiwa yeyote atakiri kuwa Yesu ni Kristo, atatengwa na Sinagogi.
Ses parents dirent cela, parce qu'ils craignaient les Juifs; car ceux-ci s'étaient déjà concertés pour faire chasser de la synagogue quiconque reconnaîtrait Jésus pour le Messie.
23 Kwa sababu hii, wazazi wake walisema, “Ni mtu mzima, mwulizeni yeye.”
C'est pour cela que ses parents dirent: «Il a de l'âge, interrogez-le.»
24 Kwa hiyo kwa mara ya pili, walimwita yule mtu aliyewahi kuwa kipofu na kumwambia, “Mpe Mungu utukufu. Tunajua kwamba mtu huyu ni mwenye dhambi.”
Les pharisiens tirent venir une seconde fois l'homme qui avait été aveugle, et lui dirent: «Donne gloire à Dieu: nous savons que cet homme est un méchant.»
25 Ndipo yule mtu alijibu, “Awe ni mwenye dhambi, mimi sijui. Kitu kimoja ninachokijua: nilikuwa kipofu, na sasa ninaona.”
Il répondit: «Si c'est un méchant, je l'ignore; je ne sais qu'une chose, c'est que j'étais aveugle et qu'à cette heure je vois.»
26 Ndipo walipomwambia, “Amekufanyia nini? Aliyafumbuaje macho yako?”
Ils lui dirent: «Que t'a-t-il fait? Comment t'a-t-il ouvert les yeux?»
27 Alijibu, “Nimekwishawaambia tayari, na nyinyi hamkusikiliza! Kwa nini mnataka kusikia tena? Nanyi hamtaki kuwa wanafunzi wake pia, sivyo?
— «Je vous l'ai déjà dit, leur répliqua-t-il, et vous n'avez pas écouté; pourquoi voulez-vous l'entendre encore une fois? Est-ce que vous voulez devenir aussi ses disciples?»
28 Walimtukana na kusema, “Wewe ni mwanafunzi wake, lakini sisi ni wanafunzi wa Musa.
Ils l'injurièrent et lui dirent: «C'est toi qui es disciple de cet homme; pour nous, nous sommes disciples de Moïse.
29 Tunajua kwamba Mungu alizungumza na Musa, lakini kwa huyu mtu, hatujui kule atokako.”
Nous savons que Dieu a parlé à Moïse; mais pour celui-ci, nous ne savons d'où il est.»
30 Yule mtu akajibu na kuwaambia, “Kwa nini, hili ni jambo la kushangaza, kwamba hamjui anakotoka, na bado ameyafumbua macho yangu.
Cet homme répondit et leur dit: «C'est une chose étrange que vous ne sachiez d'où il est; et pourtant il m'a ouvert les yeux.
31 Tunajua kuwa Mungu hawasikilizi wenye dhambi, lakini ikiwa mtu yeyote anamwabudu Mungu na hufanya mapenzi yake, Mungu humsikiliza.
Nous savons que Dieu n'exauce point les méchants; mais si quelqu'un est pieux et fait sa volonté, c'est celui-là qu'il exauce.
32 Tangu kuanza kwa Ulimwengu haijawahi kamwe kusikiwa kwamba yeyote ameyafumbua macho ya mtu aliyezaliwa kipofu. (aiōn g165)
Jamais on n'a entendu dire que quelqu'un ait ouvert les yeux d'un aveugle-né; (aiōn g165)
33 Ikiwa mtu huyu hakutoka kwa Mungu, asingelifanya chochote.”
si cet homme ne venait pas de Dieu, il ne pourrait rien faire de pareil.»
34 Walijibu na kumwambia, “Ulizaliwa katika dhambi kabisa, na wewe unatufundisha sisi?” Ndipo walipomfukuza kutoka katika sinagogi.
Ils lui dirent: «Tu es né tout entier dans le péché, et tu te mêles de nous faire des leçons!» Et ils le chassèrent.
35 Yesu alisikia kwamba wamemwondoa kwenye sinagogi. Alimpata na kumwambia, “Unamwamini Mwana wa Mtu?”
Jésus apprit qu'on l'avait chassé, et, l'ayant rencontré, il lui dit: «Tu crois, toi, au Fils de Dieu?»
36 Alijibu na kusema, “Ni nani, Bwana, ili nami nipate kumwamini?”
Cet homme répondit: «Et qui est-il, Seigneur, afin que je croie en lui?»
37 Yesu akamwambia, “Umeshamuona, naye unayezungumza naye ndiye.”
— «Tu le vois, lui dit Jésus, et c'est lui-même qui te parle.»
38 Yule mtu akasema, “Bwana, Naamini.” Ndipo akamsujudia.
— «Je crois, Seigneur, » dit-il alors, et il se prosterna devant lui.
39 Yesu akasema, “Kwa hukumu nimekuja katika Ulimwengu huu ili kwamba wale wasioona wapate kuona na wale wanaoona wawe vipofu.”
Jésus ajouta: «Je suis venu dans ce monde pour un jugement, pour que ceux qui ne voient pas, voient, et que ceux qui voient deviennent aveugles.»
40 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa pamoja naye wakasikia maneno hayo na kumwuliza, “Na sisi pia ni vipofu?”
Les pharisiens qui étaient auprès de lui, entendirent cette parole, et lui dirent: «Et nous, sommes- nous aussi aveugles?»
41 Yesu akawaambia, “Kama mngelikuwa vipofu, msingelikuwa na dhambi. Hata hivyo, sasa mnasema, 'Tunaona,' dhambi yenu inakaa.”
Jésus leur dit: «Si vous étiez aveugles, vous seriez sans péché; mais puisque vous dites, «nous voyons, » votre péché subsiste.»

< Yohana 9 >