< Yohana 9 >

1 Wakati, kama Yesu alipokuwa akipita, alimwona mtu kipofu tangu kuzaliwa kwake.
And passing along, He saw a man blind from his birth.
2 Wanafunzi wake wakamwuliza, “Rabi, nani aliyetenda dhambi, mtu huyu au wazazi wake, hata azaliwe kipofu?”
And His disciples asked Him, saying, Master, who sinned, this one, or his parents, that he was born blind?
3 Yesu akawajibu, “Siyo huyu mtu wala wazazi wake waliotenda dhambi, bali kazi za Mungu zipate kufunuliwa kupitia kwake.
Jesus responded, Neither did he nor his parents sin; but that the works of God may be made manifest in him.
4 Tunapaswa kufanya kazi zake yeye aliyenituma wakati bado ni mchana. Usiku waja wakati ambapo hakuna atakayeweza kufanya kazi.
It behooveth us to work the works of Him that sent us, while it is day: the night comes, when no one is able to work.
5 Wakati niwapo ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu.”
While I am in the world, I am the light of the world.
6 Baada ya Yesu kusema maneno haya, alitema kwenye ardhi, alifanya tope kwa mate, na akampaka yule mtu machoni na lile tope.
Saying these words, He spat on the ground, and made mortar out of the spittle, and besmeared the mortar on his eyes,
7 Akamwambia, nenda kaoge katika kisima cha Siloam (Inayotafsiriwa kama 'aliyetumwa').” Kwa hiyo huyo mtu alienda, akanawa, na akarudi, anaona.
and He said to him; Go, wash in the pool of Siloam, (which is interpreted, Sent). Then he went away, and washed, and came seeing.
8 Majirani wa yule mtu na wale waliomuona mwanzo kama mwombaji walisema, Je! huyu siye yule mtu aliyekuwa akikaa na kuomba?” wengine walisema, “Ni yeye.”
Then the neighbors, and those seeing him previously, because he was a beggar, continued to say, Is not this the one sitting and begging?
9 Na wengine walisema, “Hapana, bali anafanana naye.” Lakini alikuwa akisema, “Ni mimi.”
Some said, That he is: others said, No, but he is like him: he said, I am he.
10 Wakamwambia, “Sasa macho yako yalifunguliwaje?”
Then they said to him, How then were your eyes opened?
11 Alijibu, mtu aitwaye Yesu alifanya tope na kupaka macho yangu na kuniambia, 'Nenda Siloam ukanawe.' Kwa hiyo nilienda, na nikanawa, na nikapata kuona tena.”
He responded, a man called Jesus made mortar and besmeared my eyes, and said, Go to Siloam, and wash. Then having gone away and washed, I looked up.
12 Wakamwambia, “Yuko wapi?” Alijibu, “Sijui.”
They said to him, Where is He? He says, I know not.
13 Wakampeleka yule mtu aliyewahi kuwa kipofu kwa Mafarisayo.
They lead him to the Pharisees, him formerly blind.
14 Nayo ilikuwa siku ya Sabato wakati Yesu alipotengeneza tope na kuyafumbua macho yake.
And it was the Sabbath on the day on which Jesus made mortar, and opened his eyes.
15 Ndipo tena Mafarisayo wakamwuliza alipataje kuona. Aliwaambia, “Aliweka tope katika macho yangu, nikanawa, na sasa naweza kuona.”
Then again the Pharisees also asked him how he looked up. And he said to them, He placed the mortar on my eyes, and I washed, and see.
16 Baadhi ya Mafarisayo wakasema, “Mtu huyu hajatoka kwa Mungu kwa sababu haishiki Sabato.” Wengine walisema, “Inawezekanaje mtu mwenye dhambi kufanya ishara kama hizo?” Kwa hiyo kukawa na mgawanyiko kati yao.
Then certain ones of the Pharisees said, This man is not with God, because He does not keep the Sabbath. Others said, How is a wicked man able to do such miracles? And there was a division among them.
17 Ndipo walipomwuliza yule kipofu tena, “Unasemaje juu yake kwa sababu aliyafungua macho yako?” Kipofu akasema, “Ni nabii.”
Then they again say to the blind man, What do you say concerning Him, because He opened your eyes? And he said that, He is a prophet.
18 Hata wakati huu Wayahudi hawakumwamini kwamba alikuwa kipofu naye amepata kuona mpaka walipowaita wazazi wake yeye aliyepata kuona.
Then the Jews did not believe concerning him, that he was blind, and looked up, until they called the parents of him that looked up,
19 Waliwauliza wazazi, Je, huyu ni mtoto wenu mnayesema alizaliwa kipofu? amewezaje sasa kuona?”
and asked them, saying, Is this your son, who you say was born blind? how then does he now see?
20 Hivyo wazazi wake wakamjibu, “Tunajua kuwa huyu ni mtoto wetu na kwamba alizaliwa kipofu.
Then his parents responded and said; We know that he is our son, and that he was born blind:
21 Jinsi gani sasa anaona, hatujui, na yeye aliyemfumbua macho yake, hatumjui. Mwulizeni yeye. Ni mtu mzima. Anaweza kujieleza mwenyewe.”
but how he now sees, we know not; nor who opened his eyes, we know not: ask him; he has majority; he will speak for himself.
22 Wazazi wake walisema mambo haya, kwa sababu waliwaogopa Wayahudi. Kwa vile Wayahudi walikuwa wamekubaliana tayari kuwa, ikiwa yeyote atakiri kuwa Yesu ni Kristo, atatengwa na Sinagogi.
And his parents said these things, because they feared the Jews: for the Jews had already stipulated, that if any one should confess Him to be Christ, he should be put out of the synagogue.
23 Kwa sababu hii, wazazi wake walisema, “Ni mtu mzima, mwulizeni yeye.”
Therefore his parents said that, He has majority, ask him.
24 Kwa hiyo kwa mara ya pili, walimwita yule mtu aliyewahi kuwa kipofu na kumwambia, “Mpe Mungu utukufu. Tunajua kwamba mtu huyu ni mwenye dhambi.”
Then they asked the man the second time who was blind, and said to him, Give God the glory: we know that this man is a sinner.
25 Ndipo yule mtu alijibu, “Awe ni mwenye dhambi, mimi sijui. Kitu kimoja ninachokijua: nilikuwa kipofu, na sasa ninaona.”
Then he responded, If He is a sinner, I know not: one thing I do know, that being blind I now see.
26 Ndipo walipomwambia, “Amekufanyia nini? Aliyafumbuaje macho yako?”
Then they said to him, What did He to you? how did He open your eyes?
27 Alijibu, “Nimekwishawaambia tayari, na nyinyi hamkusikiliza! Kwa nini mnataka kusikia tena? Nanyi hamtaki kuwa wanafunzi wake pia, sivyo?
He responded to them, I told you already, and you did not hearken: why do you wish to hear again? whether do you wish to become His disciples?
28 Walimtukana na kusema, “Wewe ni mwanafunzi wake, lakini sisi ni wanafunzi wa Musa.
They railed on him, and said, You are His disciple; but we are the disciples of Moses:
29 Tunajua kwamba Mungu alizungumza na Musa, lakini kwa huyu mtu, hatujui kule atokako.”
we know that God spoke to Moses: but we do not know this One, whence He is.
30 Yule mtu akajibu na kuwaambia, “Kwa nini, hili ni jambo la kushangaza, kwamba hamjui anakotoka, na bado ameyafumbua macho yangu.
The man responded and said to them; For in this it is wonderful, that you do not know whence He is, He truly opened my eyes.
31 Tunajua kuwa Mungu hawasikilizi wenye dhambi, lakini ikiwa mtu yeyote anamwabudu Mungu na hufanya mapenzi yake, Mungu humsikiliza.
We know that God hears not sinners: but if any one may be a worshiper of God, and do His will, He hears him.
32 Tangu kuanza kwa Ulimwengu haijawahi kamwe kusikiwa kwamba yeyote ameyafumbua macho ya mtu aliyezaliwa kipofu. (aiōn g165)
It was never heard of from the beginning that any one opened the eyes of a man who was born blind: (aiōn g165)
33 Ikiwa mtu huyu hakutoka kwa Mungu, asingelifanya chochote.”
if He were not with God, He would not be able to do anything.
34 Walijibu na kumwambia, “Ulizaliwa katika dhambi kabisa, na wewe unatufundisha sisi?” Ndipo walipomfukuza kutoka katika sinagogi.
They responded and said to him, Thou art altogether born in sins, and dost thou teach us? And they cast him out.
35 Yesu alisikia kwamba wamemwondoa kwenye sinagogi. Alimpata na kumwambia, “Unamwamini Mwana wa Mtu?”
Jesus heard that they cast him out; and having found him, said, Do you believe on the Son of man?
36 Alijibu na kusema, “Ni nani, Bwana, ili nami nipate kumwamini?”
He responded and said, Who is He, Lord, that I may believe on, Him?
37 Yesu akamwambia, “Umeshamuona, naye unayezungumza naye ndiye.”
Jesus said to him, Indeed you have seen Him, and the One speaking with you is He.
38 Yule mtu akasema, “Bwana, Naamini.” Ndipo akamsujudia.
And He said, I believe, Lord: and he worshiped Him.
39 Yesu akasema, “Kwa hukumu nimekuja katika Ulimwengu huu ili kwamba wale wasioona wapate kuona na wale wanaoona wawe vipofu.”
And Jesus said, For judgment I came into this world, that those not seeing may see; and those seeing may be made blind.
40 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa pamoja naye wakasikia maneno hayo na kumwuliza, “Na sisi pia ni vipofu?”
And those of the Pharisees being with Him heard, and said to Him, Whether are we also blind?
41 Yesu akawaambia, “Kama mngelikuwa vipofu, msingelikuwa na dhambi. Hata hivyo, sasa mnasema, 'Tunaona,' dhambi yenu inakaa.”
Jesus said to them, If you were blind you would not have sin: but now you say that, We see: your sin remaineth.

< Yohana 9 >