< Yohana 8 >
1 (Zingatia: Angalia ufafanuzi wa Yohana 7: 53 - 8: 11 hapo juu). Yesu alienda mlima wa Mizeituni.
but Jesus went unto the mount of Olives.
2 Mapema asubuhi akaja tena hekaluni, na watu wote wakamwendea; akakaa na kuwafundisha.
And early in the morning he came again into the temple, and all the people came unto him; and he sat down, and taught them.
3 Waandishi na Mafarisayo wakamletea mwanamke aliyekamatwa katika kitendo cha kuzini. Wakamweka katikati.
And the scribes and the Pharisees bring a woman taken in adultery; and having set her in the midst,
4 (Zingatia: Angalia ufafanuzi wa Yohana 7: 53 - 8: 11 hapo juu). Ndipo wakamwambia Yesu, “Mwalimu, mwanamke huyu amekamatwa katika uzinzi, katika kitendo kabisa.
they say unto him, Master, this woman hath been taken in adultery, in the very act.
5 Sasa, katika sheria, Musa ametuamuru kuwaponda mawe watu kama hawa, unasemaje juu yake?
Now in the law Moses commanded us to stone such: what then sayest thou of her?
6 Walisema haya ili kumtega ili kwamba wapate jambo la kumshitaki, lakini Yesu akainama chini akaandika katika ardhi kwa kidole chake.
And this they said, tempting him, that they might have [whereof] to accuse him. But Jesus stooped down, and with his finger wrote on the ground.
7 (Zingatia: Angalia ufafanuzi wa Yohana 7: 53 - 8: 11 hapo juu). Walipoendelea kumwuliza, alisimama na kuwaambia, “Yeye asiyekuwa na dhambi miongoni mwenu, awe wa kwanza kumponda mawe.”
But when they continued asking him, he lifted up himself, and said unto them, He that is without sin among you, let him first cast a stone at her.
8 Akainama tena chini, akaandika katika ardhi kwa kidole chake.
And again he stooped down, and with his finger wrote on the ground.
9 (Zingatia: Angalia ufafanuzi wa Yohana 7: 53 - 8: 11 hapo juu). Waliposikia hayo, waliondoka mmoja baada ya mwingine, kuanzia aliye mzee. Mwishowe Yesu aliachwa peke yake, pamoja na mwanamke aliyekuwa katikati yao.
And they, when they heard it, went out one by one, beginning from the eldest, [even] unto the last: and Jesus was left alone, and the woman, where she was, in the midst.
10 Yesu alisimama na kumwambia, “Mwanamke, waliokushitaki wako wapi? Hakuna hata mmoja aliyekuhukumu?”
And Jesus lifted up himself, and said unto her, Woman, where are they? did no man condemn thee?
11 Akasema, “Hakuna hata mmoja Bwana.” Yesu akasema, “Hata mimi sikuhukumu. Nenda njia yako; kuanzia sasa na kuendelea usitende dhambi tena.”
And she said, No man, Lord. And Jesus said, Neither do I condemn thee: go thy way; from henceforth sin no more.]
12 Tena Yesu akazungumza na watu akisema, “Mimi ni nuru ya ulimwengu; yeye anifuataye hatatembea gizani bali atakuwa na nuru ya uzima.”
Again therefore Jesus spake unto them, saying, I am the light of the world: he that followeth me shall not walk in the darkness, but shall have the light of life.
13 Mafarisayo wakamwambia, “Unajishuhudia mwenyewe; ushuhuda wako siyo wa kweli.”
The Pharisees therefore said unto him, Thou bearest witness of thyself; thy witness is not true.
14 Yesu alijibu akawaambia, “Hata kama nitajishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ni kweli. Ninajua mahali nilikotoka na kule ninakoenda, lakini ninyi hamjui mahali ninapotoka au kule ninakoenda.
Jesus answered and said unto them, Even if I bear witness of myself, my witness is true; for I know whence I came, and whither I go; but ye know not whence I come, or whither I go.
15 Nyinyi mnahukumu kimwili; mimi simhukumu yeyote.
Ye judge after the flesh; I judge no man.
16 Mimi hata nikihukumu, hukumu yangu ni kweli kwa sababu siko peke yangu, bali niko pamoja na baba aliyenituma.
Yea and if I judge, my judgment is true; for I am not alone, but I and the Father that sent me.
17 Ndiyo, na katika sheria yenu imeandikwa kwamba ushuhuda wa watu wawili ni kweli.
Yea and in your law it is written, that the witness of two men is true.
18 Mimi ndiye ninayejishuhudia, na Baba aliyenituma ananishuhudia.”
I am he that beareth witness of myself, and the Father that sent me beareth witness of me.
19 Wakamwambia, “Baba yako yuko wapi?” Yesu akajibu, “mimi hamnijui wala Baba yangu hammjui; mngelikuwa mnanijua mimi, mngemjua na Baba yangu pia.”
They said therefore unto him, Where is thy Father? Jesus answered, Ye know neither me, nor my Father: if ye knew me, ye would know my Father also.
20 Alisema maneno haya akiwa karibu na hazina alipokuwa akifundisha hekaluni, na hakuna hata mmoja aliyemkamata kwa sababu saa yake ilikuwa bado haijafika.
These words spake he in the treasury, as he taught in the temple: and no man took him; because his hour was not yet come.
21 Basi akawaambia tena, “Ninaenda zangu; mtanitafuta na mtakufa katika dhambi zenu. Kule niendako, hamuwezi kuja.”
He said therefore again unto them, I go away, and ye shall seek me, and shall die in your sin: whither I go, ye cannot come.
22 Wayahudi wakasema, “Atajiua mwenyewe, yeye ambaye alisema, 'kule niendako hamuwezi kuja'?”
The Jews therefore said, Will he kill himself, that he saith, Whither I go, ye cannot come?
23 Yesu akawaambia, “Mnatoka chini; mimi natoka juu. Ninyi ni wa Ulimwengu huu; mimi si wa ulimwengu huu.
And he said unto them, Ye are from beneath; I am from above: ye are of this world; I am not of this world.
24 Kwa hiyo, naliwaambieni kuwa mtakufa katika dhambi zenu. Vinginevyo muamini kuwa MIMI NDIYE, mtakufa katika dhambi zenu”.
I said therefore unto you, that ye shall die in your sins: for except ye believe that I am [he], ye shall die in your sins.
25 Kwa hiyo wakamwambia, “Wewe ni nani?” Yesu akawaambia, Yale niliyowaambia tangu mwanzo.
They said therefore unto him, Who art thou? Jesus said unto them, Even that which I have also spoken unto you from the beginning.
26 Ninayo mambo mengi ya kuzungumza na kuhukumu juu yenu. Hata hivyo, yeye aliyenituma ni wa kweli; na mambo niliyoyasikia kutoka kwake, mambo haya nayasema kwa Ulimwengu.”
I have many things to speak and to judge concerning you: howbeit he that sent me is true; and the things which I heard from him, these speak I unto the world.
27 Hawakumuelewa kwamba alikuwa akiongea nao kuhusu Baba.
They perceived not that he spake to them of the Father.
28 Yesu akasema, “Mtakapomwinua juu Mwana wa Mtu, ndipo mtakapojua kuwa MIMI NDIYE, na kwamba sifanyi lolote kwa nafsi yangu. Kama Baba alivyonifundisha, ninazungumza mambo haya.
Jesus therefore said, When ye have lifted up the Son of man, then shall ye know that I am [he], and [that] I do nothing of myself, but as the Father taught me, I speak these things.
29 Yeye aliyenituma yuko pamoja nami, na yeye hajaniacha peke yangu, kwani kila mara nafanya yale yanayompendeza.”
And he that sent me is with me; he hath not left me alone; for I do always the things that are pleasing to him.
30 Wakati Yesu akisema mambo haya, wengi walimwamini.
As he spake these things, many believed on him.
31 Yesu akasema kwa wale Wayahudi waliomwamini, “Ikiwa mtakaa katika neno langu, ndipo mtakuwa wanafunzi wangu kweli,
Jesus therefore said to those Jews which had believed him, If ye abide in my word, [then] are ye truly my disciples;
32 nanyi mtaijua kweli, na kweli itawaweka huru.”
and ye shall know the truth, and the truth shall make you free.
33 Walimjibu, “Sisi ni uzao wa Ibrahimu na kamwe hatujawahi kwa chini ya utumwa wa yeyote; utasemaje, “Tutawekwa huru?”
They answered unto him, We be Abraham’s seed, and have never yet been in bondage to any man: how sayest thou, Ye shall be made free?
34 Yesu aliwajibu, “Amini, amini, nawaambia, kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.
Jesus answered them, Verily, verily, I say unto you, Every one that committeth sin is the bondservant of sin.
35 Mtumwa hakai nyumbani wakati wote; mwana hudumu siku zote. (aiōn )
And the bondservant abideth not in the house for ever: the son abideth for ever. (aiōn )
36 Kwa hiyo, ikiwa Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kabisa.”
If therefore the Son shall make you free, ye shall be free indeed.
37 Ninajua kwamba ninyi ni uzao wa Ibrahimu; mnatafuta kuniua kwa sababu neno langu halina nafasi ndani yenu.
I know that ye are Abraham’s seed; yet ye seek to kill me, because my word hath not free course in you.
38 Ninasema mambo ambayo nimeyaona pamoja na Baba yangu, na ninyi vile vile mnafanya mambo ambayo mliyasikia kutoka kwa baba yenu.”
I speak the things which I have seen with [my] Father: and ye also do the things which ye heard from [your] father.
39 Walijibu na kumwambia, “Baba yetu ni Abrahamu.” Yesu akawaambia, Kama mngelikuwa watoto wa Ibrahimu, mngefanya kazi za Ibrahimu.
They answered and said unto him, Our father is Abraham. Jesus saith unto them, If ye were Abraham’s children, ye would do the works of Abraham.
40 Hata sasa mnatafuta kuniua, mtu aliyewaambia ukweli kwamba nilisikia kutoka kwa Mungu. Abrahamu hakufanya hivi.
But now ye seek to kill me, a man that hath told you the truth, which I heard from God: this did not Abraham.
41 Mnafanya kazi za baba yenu.” Wakamwambia, “Hatukuzaliwa katika uzinzi, tunaye Baba mmoja, Mungu.”
Ye do the works of your father. They said unto him, We were not born of fornication; we have one Father, [even] God.
42 Yesu akawaambia, “Ikiwa Mungu ni Baba yenu, mngenipenda mimi, kwa maana nimetoka kwa Mungu; wala sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye alinituma.
Jesus said unto them, If God were your Father, ye would love me: for I came forth and am come from God; for neither have I come of myself, but he sent me.
43 Kwa nini hamyaelewi maneno yangu? Kwa sababu hamuwezi kuvumilia kuyasikia maneno yangu.
Why do ye not understand my speech? [Even] because ye cannot hear my word.
44 Ninyi ni wa baba yenu, shetani, na mnataka kuzitenda tamaa za baba yenu. Alikuwa mwuaji tangu mwanzo na hawezi kusimama katika kweli kwa sababu kweli haimo ndani yake. Anapoongea uongo, anaongea kutoka kwenye asili yake kwa sababu ni mwongo na baba wa uongo.
Ye are of [your] father the devil, and the lusts of your father it is your will to do. He was a murderer from the beginning, and stood not in the truth, because there is no truth in him. When he speaketh a lie, he speaketh of his own: for he is a liar, and the father thereof.
45 Hata sasa, kwa sababu ninasema iliyo kweli, hamniamini.
But because I say the truth, ye believe me not.
46 Ni nani kati yenu anayenishuhudia kuwa nina dhambi? ikiwa ninasema iliyo kweli, kwa nini hamniamini?
Which of you convicteth me of sin? If I say truth, why do ye not believe me?
47 Yeye aliye wa Mungu huyasikia maneno ya Mungu; ninyi hamyasikii kwa sababu ninyi si wa Mungu.”
He that is of God heareth the words of God: for this cause ye hear [them] not, because ye are not of God.
48 Wayahudi wakamjibu na kumwambia, hatujasema kweli kuwa wewe ni Msamaria na una pepo?”
The Jews answered and said unto him, Say we not well that thou art a Samaritan, and hast a devil?
49 Yesu akajibu, sina pepo; lakini namheshimu Baba yangu, nanyi hamniheshimu.
Jesus answered, I have not a devil; but I honour my Father, and ye dishonour me.
50 Sitafuti utukufu wangu; kuna mmoja atafutaye na kuhukumu.
But I seek not mine own glory: there is one that seeketh and judgeth.
51 Amini, amini, nawaambia, iwapo yeyote atalishika neno langu, hataona mauti kamwe.” (aiōn )
Verily, verily, I say unto you, If a man keep my word, he shall never see death. (aiōn )
52 Wayahudi wakamwambia, “Sasa tumejua kuwa una pepo. Abrahamu na mabii walikufa; lakini unasema, 'Ikiwa mtu atalishika neno langu, hataonja mauti'. (aiōn )
The Jews said unto him, Now we know that thou hast a devil. Abraham is dead, and the prophets; and thou sayest, If a man keep my word, he shall never taste of death. (aiōn )
53 Wewe si mkuu kuliko baba yetu Abrahamu aliyekufa, sivyo? Manabii pia walikufa. Wewe wajifanya kuwa nani?”
Art thou greater than our father Abraham, which is dead? and the prophets are dead: whom makest thou thyself?
54 Yesu akajibu, “Ikiwa nitajitukuza mwenyewe, utukufu wangu ni bure; ni Baba yangu anayenitukuza - yule mnayemsema kuwa ni Mungu wenu.
Jesus answered, If I glorify myself, my glory is nothing: it is my Father that glorifieth me; of whom ye say, that he is your God;
55 Ninyi hamjamjua yeye, lakini mimi namjua yeye. Ikiwa nitasema, 'simjui,' nitakuwa kama nyinyi, muongo. Hata hivyo, ninamjua na maneno yake nimeyashika.
and ye have not known him: but I know him; and if I should say, I know him not, I shall be like unto you, a liar: but I know him, and keep his word.
56 Baba yenu Abrahamu alishangilia atakavyoiona siku yangu; aliiona na alifurahi.”
Your father Abraham rejoiced to see my day; and he saw it, and was glad.
57 Wayahudi wakamwambia,”Haujafikisha umri wa miaka hamsini bado, nawe umemuona Ibrahimu?”
The Jews therefore said unto him, Thou art not yet fifty years old, and hast thou seen Abraham?
58 Yesu akawaambia, “Amini, amini, nawaambia, kabla Abrahamu hajazaliwa, MIMI NIKO.”
Jesus said unto them, Verily, verily, I say unto you, Before Abraham was, I am.
59 Ndipo waliokota mawe wapate kumpiga, lakini Yesu alijificha na akatoka nje ya hekalu.
They took up stones therefore to cast at him: but Jesus hid himself, and went out of the temple.