< Yohana 7 >
1 Na baada ya mambo haya Yesu alisafiri hivi katika Galilaya, kwa sababu hakupenda kwenda Uyahudi kwa sababu wayahudi walikuwa wakifanya mipango ya kumwua.
tata. h para. m yihuudiiyalokaasta. m hantu. m samaihanta tasmaad yii"su ryihuudaaprade"se paryya. titu. m necchan gaaliil prade"se paryya. titu. m praarabhata|
2 Sasa sikukuu ya Wayahudi, sikukuu ya Vibanda, ilikuwa karibu.
kintu tasmin samaye yihuudiiyaanaa. m duu. syavaasanaamotsava upasthite
3 Ndipo ndugu zake walipomwambia, “Ondoka mahali hapa uende Uyahudi, ili kwamba wanafunzi wako vile vile wayaone matendo ufanyayo.
tasya bhraatarastam avadan yaani karmmaa. ni tvayaa kriyante taani yathaa tava "si. syaa. h pa"syanti tadartha. m tvamita. h sthaanaad yihuudiiyade"sa. m vraja|
4 Hakuna afanyaye lolote kwa siri iwapo yeye mwenyewe anataka kujulikana wazi. Iwapo unafanya mambo haya, jionyeshe mwenyewe kwa ulimwengu.”
ya. h ka"scit svaya. m pracikaa"si. sati sa kadaapi gupta. m karmma na karoti yadiid. r"sa. m karmma karo. si tarhi jagati nija. m paricaayaya|
5 Hata ndugu zake pia hawakumwamini.
yatastasya bhraataropi ta. m na vi"svasanti|
6 Ndipo Yesu alipowaambia, “Wakati wangu haujafika bado, lakini wakati wenu kila mara uko tayari.
tadaa yii"sustaan avocat mama samaya idaanii. m nopati. s.thati kintu yu. smaaka. m samaya. h satatam upati. s.thati|
7 Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, bali unanichukia mimi kwa sababu ninaushuhudia kuwa matendo yake ni maovu.
jagato lokaa yu. smaan. rtiiyitu. m na "sakruvanti kintu maameva. rtiiyante yataste. saa. m karmaa. ni du. s.taani tatra saak. syamidam aha. m dadaami|
8 Pandeni kwenda katika sikukuu; mimi siendi katika sikukuu hii kwa sababu muda wangu haujakamilika bado.”
ataeva yuuyam utsave. asmin yaata naaham idaaniim asminnutsave yaami yato mama samaya idaanii. m na sampuur. na. h|
9 Baada ya kusema mambo hayo kwao, alibaki Galilaya.
iti vaakyam ukttvaa sa gaaliili sthitavaan
10 Hata hivyo, ndugu zake walipokuwa wamekwenda katika sikukuu, ndipo naye alienda, siyo kwa wazi bali kwa siri.
kintu tasya bhraat. r.su tatra prasthite. su satsu so. apraka. ta utsavam agacchat|
11 Wayahudi walikuwa wakimtafuta katika sikukuu na kusema, “Yuko wapi?”
anantaram utsavam upasthitaa yihuudiiyaasta. m m. rgayitvaap. rcchan sa kutra?
12 Kulikuwa na majadiliano mengi miongoni mwa makutano juu yake. Wengine walisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walisema, “Hapana, huwapotosha makutano.”
tato lokaanaa. m madhye tasmin naanaavidhaa vivaadaa bhavitum aarabdhavanta. h| kecid avocan sa uttama. h puru. sa. h kecid avocan na tathaa vara. m lokaanaa. m bhrama. m janayati|
13 Hata hivyo hakuna aliyezungumza wazi juu yake kwa kuwaogopa Wayahudi.
kintu yihuudiiyaanaa. m bhayaat kopi tasya pak. se spa. s.ta. m naakathayat|
14 Wakati sikukuu ilipofika katikati, Yesu alipanda kwenda Hekaluni na kuanza kufundisha.
tata. h param utsavasya madhyasamaye yii"su rmandira. m gatvaa samupadi"sati sma|
15 Wayahudi walikuwa wakishangaa na kusema, “Kwa jinsi gani mtu huyu anajua mambo mengi? Hajasoma kamwe.”
tato yihuudiiyaa lokaa aa"scaryya. m j naatvaakathayan e. saa maanu. so naadhiityaa katham etaad. r"so vidvaanabhuut?
16 Yesu akawajibu na kuwaambia, “Mafundisho yangu siyo yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
tadaa yii"su. h pratyavocad upade"soya. m na mama kintu yo maa. m pre. sitavaan tasya|
17 Iwapo yeyote atapenda kufanya mapenzi yake yeye, atajua kuhusu mafundisho haya, kama yanatoka kwa Mungu, au kama ninazungumza kutoka kwangu mwenyewe.
yo jano nide"sa. m tasya grahii. syati mamopade"so matto bhavati kim ii"svaraad bhavati sa ganastajj naatu. m "sak. syati|
18 Kila anayezungumza yatokayo kwake mwenywe hutafuta utukufu wake, bali kila atafutaye utukufu wake yeye aliyemtuma, mtu huyo ni wa kweli, na ndani yake hakuna kutotenda haki.
yo jana. h svata. h kathayati sa sviiya. m gauravam iihate kintu ya. h prerayitu rgauravam iihate sa satyavaadii tasmin kopyadharmmo naasti|
19 Musa hakuwapa nyinyi sheria? Lakini hakuna hata mmoja kati yenu atendaye sheria. Kwa nini mnataka kuniua?
muusaa yu. smabhya. m vyavasthaagrantha. m ki. m naadadaat? kintu yu. smaaka. m kopi taa. m vyavasthaa. m na samaacarati| maa. m hantu. m kuto yatadhve?
20 Makutano wakajibu, “Una pepo. Nani anataka kukuua?”
tadaa lokaa avadan tva. m bhuutagrastastvaa. m hantu. m ko yatate?
21 Yesu akajibu na akawaambia, “Nimetenda kazi moja, nanyi nyote mmeshangazwa kwa sababu yake.
tato yii"suravocad eka. m karmma mayaakaari tasmaad yuuya. m sarvva mahaa"scaryya. m manyadhve|
22 Musa aliwapa tohara (siyo kwamba inatoka kwa Musa, bali ile inatoka kwa mababa), na katika Sabato mnamtahili mtu.
muusaa yu. smabhya. m tvakchedavidhi. m pradadau sa muusaato na jaata. h kintu pit. rpuru. sebhyo jaata. h tena vi"sraamavaare. api maanu. saa. naa. m tvakcheda. m kurutha|
23 Iwapo mtu atapokea tohara katika siku ya Sabato ili kwamba sheria ya Musa isivunjwe, kwa nini mnanikasirikia mimi kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa katika Sabato?
ataeva vi"sraamavaare manu. syaa. naa. m tvakchede k. rte yadi muusaavyavasthaama"ngana. m na bhavati tarhi mayaa vi"sraamavaare maanu. sa. h sampuur. naruupe. na svastho. akaari tatkaara. naad yuuya. m ki. m mahya. m kupyatha?
24 Msihukumu kulingana na mwonekano, bali hukumuni kwa haki.
sapak. sapaata. m vicaaramak. rtvaa nyaayya. m vicaara. m kuruta|
25 Baadhi yao kutoka Yerusalemu wakasema, “Siye huyu wanayemtafuta kumwua?
tadaa yiruu"saalam nivaasina. h katipayajanaa akathayan ime ya. m hantu. m ce. s.tante sa evaaya. m ki. m na?
26 Na tazama, anaongea wazi wazi, na hawasemi chochote juu yake. Haiwezi ikawa kwamba viongozi wanajua kweli kuwa huyu ni Kristo, inaweza kuwa?
kintu pa"syata nirbhaya. h san kathaa. m kathayati tathaapi kimapi a vadantyete ayamevaabhi. siktto bhavatiiti ni"scita. m kimadhipatayo jaananti?
27 Tunajua huyu mtu anatokea wapi. Kristo atakapokuja, hata hivyo, hakuna atakayejua wapi anakotoka.”
manujoya. m kasmaadaagamad iti vaya. m jaanoma. h kintvabhi. siktta aagate sa kasmaadaagatavaan iti kopi j naatu. m na "sak. syati|
28 Yesu alikuwa akipaza sauti yake hekaluni, akifundisha na kusema, “Ninyi nyote mnanijua mimi na mnajua nitokako. Sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye aliyenituma ni wa kweli, na hamumjui yeye.
tadaa yii"su rmadhyemandiram upadi"san uccai. hkaaram ukttavaan yuuya. m ki. m maa. m jaaniitha? kasmaaccaagatosmi tadapi ki. m jaaniitha? naaha. m svata aagatosmi kintu ya. h satyavaadii saeva maa. m pre. sitavaan yuuya. m ta. m na jaaniitha|
29 Ninamjua yeye kwa sababu nimetoka kwake na alinituma.”
tamaha. m jaane tenaaha. m prerita agatosmi|
30 Walikuwa wanajaribu kumkamata, lakini hakuna hata mmoja aliyeinua mkono wake juu yake kwa sababu saa yake ilikuwa bado haijafika.
tasmaad yihuudiiyaasta. m dharttum udyataastathaapi kopi tasya gaatre hasta. m naarpayad yato hetostadaa tasya samayo nopati. s.thati|
31 Hata hivyo, wengi katika makutano walimwamini. Walisema, “Kristo atakapokuja, atafanya ishara nyingi kuliko alizofanya mtu huyu?”
kintu bahavo lokaastasmin vi"svasya kathitavaanto. abhi. sikttapuru. sa aagatya maanu. sasyaasya kriyaabhya. h kim adhikaa aa"scaryyaa. h kriyaa. h kari. syati?
32 Mafarisayo waliwasikia makutano wakinong'onezana mambo haya kuhusu Yesu, na wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakatuma maafisa ili kumkamata.
tata. h para. m lokaastasmin ittha. m vivadante phiruu"sina. h pradhaanayaajakaa nceti "srutavantasta. m dh. rtvaa netu. m padaatiga. na. m pre. sayaamaasu. h|
33 Ndipo Yesu aliposema, “Bado kuna muda kitambo niko pamoja nanyi, na baadaye nitakwenda kwake yeye aliyenituma.
tato yii"suravadad aham alpadinaani yu. smaabhi. h saarddha. m sthitvaa matprerayitu. h samiipa. m yaasyaami|
34 Mtanitafuta wala hamtaniona; kule niendako, hamtaweza kuja.”
maa. m m. rgayi. syadhve kintuudde"sa. m na lapsyadhve ratra sthaasyaami tatra yuuya. m gantu. m na "sak. syatha|
35 Kwa hiyo Wayahudi wakasemezana wao kwa wao, “Mtu huyu atakwenda wapi kwamba tusiweze kumuona? Ataenda kwa Waliotawanyika kati ya Wayunani na kuwafundisha Wayunani?
tadaa yihuudiiyaa. h paraspara. m vakttumaarebhire asyodde"sa. m na praapsyaama etaad. r"sa. m ki. m sthaana. m yaasyati? bhinnade"se vikiir. naanaa. m yihuudiiyaanaa. m sannidhim e. sa gatvaa taan upadek. syati ki. m?
36 Ni neno gani hili alilolisema, 'Mtanitafuta wala hamtaniona; kule niendako hamtamweza kuja'?”
no cet maa. m gave. sayi. syatha kintuudde"sa. m na praapsyatha e. sa kod. r"sa. m vaakyamida. m vadati?
37 Sasa katika siku ya mwisho, siku kubwa ya sikukuu, Yesu alisimama akapaza sauti, akisema, “Ikiwa yeyote ana kiu, na aje kwangu anywe.
anantaram utsavasya carame. ahani arthaat pradhaanadine yii"surutti. s.than uccai. hkaaram aahvayan uditavaan yadi ka"scit t. r.saartto bhavati tarhi mamaantikam aagatya pivatu|
38 Yeye aniaminiye mimi, kama maandiko yalivyosema, kutoka ndani yake itatiririka mito ya maji ya uzima.”
ya. h ka"scinmayi vi"svasiti dharmmagranthasya vacanaanusaare. na tasyaabhyantarato. am. rtatoyasya srotaa. msi nirgami. syanti|
39 Lakini aliyasema haya kuhusu Roho, ambaye wao wamwaminio watampokea; Roho alikuwa bado hajatolewa kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.
ye tasmin vi"svasanti ta aatmaana. m praapsyantiityarthe sa ida. m vaakya. m vyaah. rtavaan etatkaala. m yaavad yii"su rvibhava. m na praaptastasmaat pavitra aatmaa naadiiyata|
40 Baadhi ya makutano, waliposikia maneno haya, walisema, “Kweli huyu ni nabii.”
etaa. m vaa. nii. m "srutvaa bahavo lokaa avadan ayameva ni"scita. m sa bhavi. syadvaadii|
41 Wengine walisema, “Huyu ni Kristo.” Lakini wengine walisema, “nini, Kristo aweza kutoka Galilaya?
kecid akathayan e. saeva sobhi. siktta. h kintu kecid avadan sobhi. siktta. h ki. m gaaliil prade"se jani. syate?
42 Maandiko hayajasema kuwa Kristo atatokea katika ukoo wa Daudi na kutoka Bethlehemu, kijiji ambacho Daudi alikuwa?
sobhi. siktto daayuudo va. m"se daayuudo janmasthaane baitlehami pattane jani. syate dharmmagranthe kimittha. m likhita. m naasti?
43 Hivyo, pale ukainuka mgawanyiko katikati ya makutano kwa ajili yake.
ittha. m tasmin lokaanaa. m bhinnavaakyataa jaataa|
44 Wengine kati yao wangelimkamata, lakini hakuna aliyenyoosha mikono yake juu yake.
katipayalokaasta. m dharttum aicchan tathaapi tadvapu. si kopi hasta. m naarpayat|
45 Ndipo wale maofisa wakarudi kwa wakuu wa makuhani na Mafarisayo, nao wakawaambia, “Kwa nini hamjamleta?”
anantara. m paadaatiga. ne pradhaanayaajakaanaa. m phiruu"sinaa nca samiipamaagatavati te taan ap. rcchan kuto hetosta. m naanayata?
46 Maofisa wakajibu, “Hakuna mtu aliyewahi kuzungumza kama huyu kabla.”
tadaa padaataya. h pratyavadan sa maanava iva kopi kadaapi nopaadi"sat|
47 Ndipo Mafarisayo walipowajibu, “Na nyinyi pia mmepotoshwa?
tata. h phiruu"sina. h praavocan yuuyamapi kimabhraami. s.ta?
48 Kuna yeyote kati ya watawala anayemwamini, au yeyote wa Mafarisayo?
adhipatiinaa. m phiruu"sinaa nca kopi ki. m tasmin vya"svasiit?
49 Bali hawa makutano wasiojua sheria - wamelaaniwa.”
ye "saastra. m na jaananti ta ime. adhamalokaaeva "saapagrastaa. h|
50 Nikodemo akawaambia (yeye aliyemwendea Yesu zamani, akiwa mmoja wa Mafarisayo),
tadaa nikadiimanaamaa te. saameko ya. h k. sa. nadaayaa. m yii"so. h sannidhim agaat sa ukttavaan
51 “Je sheria yetu inamhukumu mtu isipokuwa amesikilizwa kwanza na kujua anachokifanya?”
tasya vaakye na "srute karmma. ni ca na vidite. asmaaka. m vyavasthaa ki. m ka ncana manuja. m do. siikaroti?
52 Walijibu na kumwambia, “Na wewe pia unatokea Galilaya? Tafuta na uone kwamba hakuna nabii aliyetokea Galilaya.”
tataste vyaaharan tvamapi ki. m gaaliiliiyaloka. h? vivicya pa"sya galiili kopi bhavi. syadvaadii notpadyate|
53 (Zingatia: Baadhi ya maneno ya Yohana 7: 53 - 8: 11 hayamo katika nakala bora za kale). Kisha kila mtu alienda nyumbani kwake.
tata. h para. m sarvve sva. m sva. m g. rha. m gataa. h kintu yii"su rjaitunanaamaana. m "siloccaya. m gatavaan|