< Yohana 7 >
1 Na baada ya mambo haya Yesu alisafiri hivi katika Galilaya, kwa sababu hakupenda kwenda Uyahudi kwa sababu wayahudi walikuwa wakifanya mipango ya kumwua.
After these things Jesus walked in Galilee: for he would not walk in Judea, because the Jews sought to kill him.
2 Sasa sikukuu ya Wayahudi, sikukuu ya Vibanda, ilikuwa karibu.
Now the Jews' feast of tabernacles was at hand.
3 Ndipo ndugu zake walipomwambia, “Ondoka mahali hapa uende Uyahudi, ili kwamba wanafunzi wako vile vile wayaone matendo ufanyayo.
His brethren therefore said to him, Depart hence, and go into Judea, that thy disciples also may see the works that thou doest.
4 Hakuna afanyaye lolote kwa siri iwapo yeye mwenyewe anataka kujulikana wazi. Iwapo unafanya mambo haya, jionyeshe mwenyewe kwa ulimwengu.”
For [there is] no man [that] doeth any thing in secret, and he himself seeketh to be known openly. If thou doest these things, show thyself to the world.
5 Hata ndugu zake pia hawakumwamini.
(For neither did his brethren believe in him.)
6 Ndipo Yesu alipowaambia, “Wakati wangu haujafika bado, lakini wakati wenu kila mara uko tayari.
Then Jesus said to them, My time is not yet come: but your time is always ready.
7 Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, bali unanichukia mimi kwa sababu ninaushuhudia kuwa matendo yake ni maovu.
The world cannot hate you; but me it hateth, because I testify concerning it, that its works are evil.
8 Pandeni kwenda katika sikukuu; mimi siendi katika sikukuu hii kwa sababu muda wangu haujakamilika bado.”
Go ye up to this feast: I go not yet to this feast, for my time is not yet full come.
9 Baada ya kusema mambo hayo kwao, alibaki Galilaya.
When he had said these words to them, he abode [still] in Galilee.
10 Hata hivyo, ndugu zake walipokuwa wamekwenda katika sikukuu, ndipo naye alienda, siyo kwa wazi bali kwa siri.
But when his brethren had gone up, then he went also to the feast, not openly, but as it were in secret.
11 Wayahudi walikuwa wakimtafuta katika sikukuu na kusema, “Yuko wapi?”
Then the Jews sought him at the feast, and said, Where is he?
12 Kulikuwa na majadiliano mengi miongoni mwa makutano juu yake. Wengine walisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walisema, “Hapana, huwapotosha makutano.”
And there was much murmuring among the people concerning him: for some said, He is a good man: others said, No; but he deceiveth the people.
13 Hata hivyo hakuna aliyezungumza wazi juu yake kwa kuwaogopa Wayahudi.
Yet, no man spoke openly of him, for fear of the Jews.
14 Wakati sikukuu ilipofika katikati, Yesu alipanda kwenda Hekaluni na kuanza kufundisha.
Now about the midst of the feast, Jesus went up into the temple, and taught.
15 Wayahudi walikuwa wakishangaa na kusema, “Kwa jinsi gani mtu huyu anajua mambo mengi? Hajasoma kamwe.”
And the Jews marveled, saying, How knoweth this man letters, having never learned?
16 Yesu akawajibu na kuwaambia, “Mafundisho yangu siyo yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
Jesus answered them, and said, My doctrine is not mine, but his that sent me.
17 Iwapo yeyote atapenda kufanya mapenzi yake yeye, atajua kuhusu mafundisho haya, kama yanatoka kwa Mungu, au kama ninazungumza kutoka kwangu mwenyewe.
If any man will do his will, he shall know concerning the doctrine, whether it is from God, or [whether] I speak from myself.
18 Kila anayezungumza yatokayo kwake mwenywe hutafuta utukufu wake, bali kila atafutaye utukufu wake yeye aliyemtuma, mtu huyo ni wa kweli, na ndani yake hakuna kutotenda haki.
He that speaketh from himself, seeketh his own glory: but he that seeketh his glory that sent him, the same is true, and no unrighteousness is in him.
19 Musa hakuwapa nyinyi sheria? Lakini hakuna hata mmoja kati yenu atendaye sheria. Kwa nini mnataka kuniua?
Did not Moses give you the law, and [yet] none of you keepeth the law? Why go ye about to kill me?
20 Makutano wakajibu, “Una pepo. Nani anataka kukuua?”
The people answered and said, Thou hast a demon: who goeth about to kill thee?
21 Yesu akajibu na akawaambia, “Nimetenda kazi moja, nanyi nyote mmeshangazwa kwa sababu yake.
Jesus answered and said to them, I have done one work, and ye all marvel.
22 Musa aliwapa tohara (siyo kwamba inatoka kwa Musa, bali ile inatoka kwa mababa), na katika Sabato mnamtahili mtu.
Moses therefore gave to you circumcision, (not because it is from Moses, but from the fathers) and ye on the sabbath circumcise a man.
23 Iwapo mtu atapokea tohara katika siku ya Sabato ili kwamba sheria ya Musa isivunjwe, kwa nini mnanikasirikia mimi kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa katika Sabato?
If a man on the sabbath receiveth circumcision, that the law of Moses should not be broken; are ye angry at me, because I have restored a man to sound health on the sabbath?
24 Msihukumu kulingana na mwonekano, bali hukumuni kwa haki.
Judge not according to the appearance, but judge righteous judgment.
25 Baadhi yao kutoka Yerusalemu wakasema, “Siye huyu wanayemtafuta kumwua?
Then said some of them of Jerusalem, Is not this he whom they seek to kill?
26 Na tazama, anaongea wazi wazi, na hawasemi chochote juu yake. Haiwezi ikawa kwamba viongozi wanajua kweli kuwa huyu ni Kristo, inaweza kuwa?
But lo, he speaketh boldly, and they say nothing to him. Do the rulers know indeed that this is the very Christ?
27 Tunajua huyu mtu anatokea wapi. Kristo atakapokuja, hata hivyo, hakuna atakayejua wapi anakotoka.”
But we know this man, whence he is: whereas when Christ cometh, no man knoweth whence he is.
28 Yesu alikuwa akipaza sauti yake hekaluni, akifundisha na kusema, “Ninyi nyote mnanijua mimi na mnajua nitokako. Sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye aliyenituma ni wa kweli, na hamumjui yeye.
Then cried Jesus in the temple, as he taught, saying, Ye both know me, and ye know whence I am: and I am not come of myself, but he that sent me is true, whom ye know not.
29 Ninamjua yeye kwa sababu nimetoka kwake na alinituma.”
But I know him; for I am from him, and he hath sent me.
30 Walikuwa wanajaribu kumkamata, lakini hakuna hata mmoja aliyeinua mkono wake juu yake kwa sababu saa yake ilikuwa bado haijafika.
Then they sought to take him: but no man laid hands on him, because his hour was not yet come.
31 Hata hivyo, wengi katika makutano walimwamini. Walisema, “Kristo atakapokuja, atafanya ishara nyingi kuliko alizofanya mtu huyu?”
And many of the people believed on him, and said, When Christ cometh, will he do more miracles than these which this [man] hath done?
32 Mafarisayo waliwasikia makutano wakinong'onezana mambo haya kuhusu Yesu, na wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakatuma maafisa ili kumkamata.
The Pharisees heard that the people murmured such things concerning him: and the Pharisees and the chief priests sent officers to take him.
33 Ndipo Yesu aliposema, “Bado kuna muda kitambo niko pamoja nanyi, na baadaye nitakwenda kwake yeye aliyenituma.
Then said Jesus to them, Yet a little while am I with you, and [then] I go to him that sent me.
34 Mtanitafuta wala hamtaniona; kule niendako, hamtaweza kuja.”
Ye will seek me, and will not find [me]: and where I am, [thither] ye cannot come.
35 Kwa hiyo Wayahudi wakasemezana wao kwa wao, “Mtu huyu atakwenda wapi kwamba tusiweze kumuona? Ataenda kwa Waliotawanyika kati ya Wayunani na kuwafundisha Wayunani?
Then said the Jews among themselves, Whither will he go, that we shall not find him? will he go to the dispersed among the Gentiles, and teach the Gentiles?
36 Ni neno gani hili alilolisema, 'Mtanitafuta wala hamtaniona; kule niendako hamtamweza kuja'?”
What [manner of] saying is this that he said, Ye will seek me, and will not find [me]: and where I am, [thither] ye cannot come?
37 Sasa katika siku ya mwisho, siku kubwa ya sikukuu, Yesu alisimama akapaza sauti, akisema, “Ikiwa yeyote ana kiu, na aje kwangu anywe.
In the last day, that great [day] of the feast, Jesus stood and cried, saying, If any man thirsteth, let him come to me, and drink.
38 Yeye aniaminiye mimi, kama maandiko yalivyosema, kutoka ndani yake itatiririka mito ya maji ya uzima.”
He that believeth on me, as the scripture hath said, out of his belly shall flow rivers of living water.
39 Lakini aliyasema haya kuhusu Roho, ambaye wao wamwaminio watampokea; Roho alikuwa bado hajatolewa kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.
(But this he spoke of the Spirit, which they that believe on him should receive, for the Holy Spirit was not yet [given], because that Jesus was not yet glorified.)
40 Baadhi ya makutano, waliposikia maneno haya, walisema, “Kweli huyu ni nabii.”
Many of the people therefore, when they heard this saying, said, In truth this is the Prophet.
41 Wengine walisema, “Huyu ni Kristo.” Lakini wengine walisema, “nini, Kristo aweza kutoka Galilaya?
Others said, This is the Christ. But some said, Will Christ come out of Galilee?
42 Maandiko hayajasema kuwa Kristo atatokea katika ukoo wa Daudi na kutoka Bethlehemu, kijiji ambacho Daudi alikuwa?
Hath not the scripture said, That Christ cometh from the seed of David, and out of the town of Bethlehem, where David was?
43 Hivyo, pale ukainuka mgawanyiko katikati ya makutano kwa ajili yake.
So there was a division among the people because of him.
44 Wengine kati yao wangelimkamata, lakini hakuna aliyenyoosha mikono yake juu yake.
And some of them would have taken him; but no man laid hands on him.
45 Ndipo wale maofisa wakarudi kwa wakuu wa makuhani na Mafarisayo, nao wakawaambia, “Kwa nini hamjamleta?”
Then came the officers to the chief priests and Pharisees; and they said to them, Why have ye not brought him?
46 Maofisa wakajibu, “Hakuna mtu aliyewahi kuzungumza kama huyu kabla.”
The officers answered, Never man spoke like this man.
47 Ndipo Mafarisayo walipowajibu, “Na nyinyi pia mmepotoshwa?
Then the Pharisees answered them, Are ye also deceived?
48 Kuna yeyote kati ya watawala anayemwamini, au yeyote wa Mafarisayo?
Have any of the rulers, or of the Pharisees believed on him?
49 Bali hawa makutano wasiojua sheria - wamelaaniwa.”
But this people who know not the law are cursed.
50 Nikodemo akawaambia (yeye aliyemwendea Yesu zamani, akiwa mmoja wa Mafarisayo),
Nicodemus saith to them, (he that came to Jesus by night, being one of them)
51 “Je sheria yetu inamhukumu mtu isipokuwa amesikilizwa kwanza na kujua anachokifanya?”
Doth our law judge [any] man before it heareth him, and knoweth what he doeth?
52 Walijibu na kumwambia, “Na wewe pia unatokea Galilaya? Tafuta na uone kwamba hakuna nabii aliyetokea Galilaya.”
They answered and said to him, Art thou also from Galilee? Search, and look: for out of Galilee ariseth no prophet.
53 (Zingatia: Baadhi ya maneno ya Yohana 7: 53 - 8: 11 hayamo katika nakala bora za kale). Kisha kila mtu alienda nyumbani kwake.
And every man went to his own house.