< Yohana 7 >
1 Na baada ya mambo haya Yesu alisafiri hivi katika Galilaya, kwa sababu hakupenda kwenda Uyahudi kwa sababu wayahudi walikuwa wakifanya mipango ya kumwua.
And after this Jesus walked in Galilee: for he would not walk in Judea, because the Jews sought to kill him.
2 Sasa sikukuu ya Wayahudi, sikukuu ya Vibanda, ilikuwa karibu.
Now the feast of tabernacles, a feast of the Jews, was near.
3 Ndipo ndugu zake walipomwambia, “Ondoka mahali hapa uende Uyahudi, ili kwamba wanafunzi wako vile vile wayaone matendo ufanyayo.
Then his brothers said to him: Depart hence, and go into Judea, that your disciples may see your works which you do;
4 Hakuna afanyaye lolote kwa siri iwapo yeye mwenyewe anataka kujulikana wazi. Iwapo unafanya mambo haya, jionyeshe mwenyewe kwa ulimwengu.”
for no one does any thing in secret, while he himself seeks to be before the public. If you do these things, show yourself to the world.
5 Hata ndugu zake pia hawakumwamini.
For neither did his brothers believe on him.
6 Ndipo Yesu alipowaambia, “Wakati wangu haujafika bado, lakini wakati wenu kila mara uko tayari.
Then Jesus said to them: My time has not yet come; but your time is always ready.
7 Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, bali unanichukia mimi kwa sababu ninaushuhudia kuwa matendo yake ni maovu.
The world can not hate you; but me it hates, because I testify of it, that its works are evil.
8 Pandeni kwenda katika sikukuu; mimi siendi katika sikukuu hii kwa sababu muda wangu haujakamilika bado.”
Do you go up to this feast. I go not up now to this feast, because my time has not yet fully come.
9 Baada ya kusema mambo hayo kwao, alibaki Galilaya.
These things said he to them, and remained in Galilee.
10 Hata hivyo, ndugu zake walipokuwa wamekwenda katika sikukuu, ndipo naye alienda, siyo kwa wazi bali kwa siri.
But when his brothers had gone up, then he also went up to the feast, not openly, but, as it were, in secret.
11 Wayahudi walikuwa wakimtafuta katika sikukuu na kusema, “Yuko wapi?”
Then the Jews sought for him at the feast, and said: Where is he?
12 Kulikuwa na majadiliano mengi miongoni mwa makutano juu yake. Wengine walisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walisema, “Hapana, huwapotosha makutano.”
And there was much murmuring among the multitudes concerning him. Some said: He is a good man. Others said: No; but he deceives the multitude.
13 Hata hivyo hakuna aliyezungumza wazi juu yake kwa kuwaogopa Wayahudi.
However, no one spoke openly of him, for fear of the Jews.
14 Wakati sikukuu ilipofika katikati, Yesu alipanda kwenda Hekaluni na kuanza kufundisha.
Now in the middle of the feast, Jesus went up into the temple, and taught.
15 Wayahudi walikuwa wakishangaa na kusema, “Kwa jinsi gani mtu huyu anajua mambo mengi? Hajasoma kamwe.”
And the Jews were astonished, and said: How has this man a knowledge of letters, having never been taught?
16 Yesu akawajibu na kuwaambia, “Mafundisho yangu siyo yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
Then Jesus answered and said: My teaching is not mine, but his who sent me.
17 Iwapo yeyote atapenda kufanya mapenzi yake yeye, atajua kuhusu mafundisho haya, kama yanatoka kwa Mungu, au kama ninazungumza kutoka kwangu mwenyewe.
If any one will do his will, he shall know with respect to the teaching, whether it is of God, or I speak of myself.
18 Kila anayezungumza yatokayo kwake mwenywe hutafuta utukufu wake, bali kila atafutaye utukufu wake yeye aliyemtuma, mtu huyo ni wa kweli, na ndani yake hakuna kutotenda haki.
He who speaks of himself, seeks his own glory; he who seeks the glory of him that sent him, he is true, and there is no unrighteousness in him.
19 Musa hakuwapa nyinyi sheria? Lakini hakuna hata mmoja kati yenu atendaye sheria. Kwa nini mnataka kuniua?
Did not Moses give you the law? and not one of you keeps the law. Why do you seek to kill me?
20 Makutano wakajibu, “Una pepo. Nani anataka kukuua?”
The multitude answered and said: You have a demon: who seeks to kill you?
21 Yesu akajibu na akawaambia, “Nimetenda kazi moja, nanyi nyote mmeshangazwa kwa sababu yake.
Jesus answered and said to them: I have done one work, and you are all astonished on account of this.
22 Musa aliwapa tohara (siyo kwamba inatoka kwa Musa, bali ile inatoka kwa mababa), na katika Sabato mnamtahili mtu.
Moses gave you circumcision, (not that it is of Moses, but of the fathers, ) and you circumcise a man on the sabbath-day.
23 Iwapo mtu atapokea tohara katika siku ya Sabato ili kwamba sheria ya Musa isivunjwe, kwa nini mnanikasirikia mimi kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa katika Sabato?
If a man receives circumcision on the sabbath-day, that the law of Moses may not be broken, are you angry with me, because I have restored the entire man to health on the sabbath-day?
24 Msihukumu kulingana na mwonekano, bali hukumuni kwa haki.
Judge not according to appearance, but judge righteous judgment.
25 Baadhi yao kutoka Yerusalemu wakasema, “Siye huyu wanayemtafuta kumwua?
Then said some of the men of Jerusalem: Is not this he whom they seek to kill?
26 Na tazama, anaongea wazi wazi, na hawasemi chochote juu yake. Haiwezi ikawa kwamba viongozi wanajua kweli kuwa huyu ni Kristo, inaweza kuwa?
and, lo, he is speaking boldly, and they say nothing to him. Have the rulers really learned that this is the Christ?
27 Tunajua huyu mtu anatokea wapi. Kristo atakapokuja, hata hivyo, hakuna atakayejua wapi anakotoka.”
But we know this man, whence he is. But when the Christ comes, no one knows whence he is.
28 Yesu alikuwa akipaza sauti yake hekaluni, akifundisha na kusema, “Ninyi nyote mnanijua mimi na mnajua nitokako. Sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye aliyenituma ni wa kweli, na hamumjui yeye.
Then Jesus cried out in the temple, as he was teaching, and said: You both know me, and you know whence I am; and I have not come of myself, but he who sent me is true, whom you know not.
29 Ninamjua yeye kwa sababu nimetoka kwake na alinituma.”
But I know him, because I am from him, and he has sent me.
30 Walikuwa wanajaribu kumkamata, lakini hakuna hata mmoja aliyeinua mkono wake juu yake kwa sababu saa yake ilikuwa bado haijafika.
Then they sought to take him; yet no one laid his hand on him, because his hour had not yet come.
31 Hata hivyo, wengi katika makutano walimwamini. Walisema, “Kristo atakapokuja, atafanya ishara nyingi kuliko alizofanya mtu huyu?”
And many of the multitude believed on him, and said: When the Christ comes, will he do more signs than these which this man has done?
32 Mafarisayo waliwasikia makutano wakinong'onezana mambo haya kuhusu Yesu, na wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakatuma maafisa ili kumkamata.
The Pharisees heard the multitude murmuring such things concerning him; and the Pharisees and chief priests sent attendants to take him.
33 Ndipo Yesu aliposema, “Bado kuna muda kitambo niko pamoja nanyi, na baadaye nitakwenda kwake yeye aliyenituma.
Then Jesus said to them: Yet a little while I am with you, and I go away to him that sent me.
34 Mtanitafuta wala hamtaniona; kule niendako, hamtaweza kuja.”
You will seek me, and shall not find me; and where I am, you can not come.
35 Kwa hiyo Wayahudi wakasemezana wao kwa wao, “Mtu huyu atakwenda wapi kwamba tusiweze kumuona? Ataenda kwa Waliotawanyika kati ya Wayunani na kuwafundisha Wayunani?
Then the Jews said among themselves: Whither is this man about to go, that we shall not find him? Is he about to go to those who are dispersed among the Greeks, and to teach the Greeks?
36 Ni neno gani hili alilolisema, 'Mtanitafuta wala hamtaniona; kule niendako hamtamweza kuja'?”
What means this saying which he uttered, You will seek me, and will not find me; and, Where I am you can not come?
37 Sasa katika siku ya mwisho, siku kubwa ya sikukuu, Yesu alisimama akapaza sauti, akisema, “Ikiwa yeyote ana kiu, na aje kwangu anywe.
On the last day, the great day of the feast, Jesus stood and cried, saying: If any one thirst, let him come to me and drink.
38 Yeye aniaminiye mimi, kama maandiko yalivyosema, kutoka ndani yake itatiririka mito ya maji ya uzima.”
He that believes on me, as the scripture has said, from his inner self shall flow rivers of living water.
39 Lakini aliyasema haya kuhusu Roho, ambaye wao wamwaminio watampokea; Roho alikuwa bado hajatolewa kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.
But this he spoke of the Spirit, which those who believe on him were about to receive; for the Holy Spirit had not yet been given, because Jesus had not yet been glorified.
40 Baadhi ya makutano, waliposikia maneno haya, walisema, “Kweli huyu ni nabii.”
Therefore, many of the multitude, when they had heard this word, said: This is, in truth, the prophet.
41 Wengine walisema, “Huyu ni Kristo.” Lakini wengine walisema, “nini, Kristo aweza kutoka Galilaya?
Others said: This is the Christ. But others said: Does the Christ come out of Galilee?
42 Maandiko hayajasema kuwa Kristo atatokea katika ukoo wa Daudi na kutoka Bethlehemu, kijiji ambacho Daudi alikuwa?
Has not the scripture said that the Christ comes from the posterity of David, and from Bethlehem, the town where David was?
43 Hivyo, pale ukainuka mgawanyiko katikati ya makutano kwa ajili yake.
So there was a division among the multitude because of him.
44 Wengine kati yao wangelimkamata, lakini hakuna aliyenyoosha mikono yake juu yake.
And some of them desired to take him; but no one laid hands on him.
45 Ndipo wale maofisa wakarudi kwa wakuu wa makuhani na Mafarisayo, nao wakawaambia, “Kwa nini hamjamleta?”
Then came the attendants to the chief priests and the Pharisees; and they said to them: Why have you not brought him?
46 Maofisa wakajibu, “Hakuna mtu aliyewahi kuzungumza kama huyu kabla.”
The attendants answered: Never did man speak like this man.
47 Ndipo Mafarisayo walipowajibu, “Na nyinyi pia mmepotoshwa?
Then the Pharisees answered them: Are you also deceived?
48 Kuna yeyote kati ya watawala anayemwamini, au yeyote wa Mafarisayo?
Has any one of the rulers, or of the Pharisees believed on him?
49 Bali hawa makutano wasiojua sheria - wamelaaniwa.”
But this multitude that know not the law are cursed.
50 Nikodemo akawaambia (yeye aliyemwendea Yesu zamani, akiwa mmoja wa Mafarisayo),
Nicodemus said to them (he that came to Jesus by night, being one of them):
51 “Je sheria yetu inamhukumu mtu isipokuwa amesikilizwa kwanza na kujua anachokifanya?”
Does our law condemn a man unless it first hear from him, and know what he does?
52 Walijibu na kumwambia, “Na wewe pia unatokea Galilaya? Tafuta na uone kwamba hakuna nabii aliyetokea Galilaya.”
They answered and said to him: Are you also from Galilee? Search, and see that out of Galilee arises no prophet.
53 (Zingatia: Baadhi ya maneno ya Yohana 7: 53 - 8: 11 hayamo katika nakala bora za kale). Kisha kila mtu alienda nyumbani kwake.
And every one departed to his own house.