< Yohana 7 >

1 Na baada ya mambo haya Yesu alisafiri hivi katika Galilaya, kwa sababu hakupenda kwenda Uyahudi kwa sababu wayahudi walikuwa wakifanya mipango ya kumwua.
After these things, Jesus was walking in Galilee, for he would not walk in Judea, because the Jews sought to kill him.
2 Sasa sikukuu ya Wayahudi, sikukuu ya Vibanda, ilikuwa karibu.
Now the feast of the Jews, the Feast of Booths, was at hand.
3 Ndipo ndugu zake walipomwambia, “Ondoka mahali hapa uende Uyahudi, ili kwamba wanafunzi wako vile vile wayaone matendo ufanyayo.
His brothers therefore said to him, “Depart from here and go into Judea, that your disciples also may see your works which you do.
4 Hakuna afanyaye lolote kwa siri iwapo yeye mwenyewe anataka kujulikana wazi. Iwapo unafanya mambo haya, jionyeshe mwenyewe kwa ulimwengu.”
For no one does anything in secret while he seeks to be known openly. If you do these things, reveal yourself to the world.”
5 Hata ndugu zake pia hawakumwamini.
For even his brothers did not believe in him.
6 Ndipo Yesu alipowaambia, “Wakati wangu haujafika bado, lakini wakati wenu kila mara uko tayari.
Jesus therefore said to them, “My time has not yet come, but your time is always ready.
7 Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, bali unanichukia mimi kwa sababu ninaushuhudia kuwa matendo yake ni maovu.
The world cannot hate you, but it hates me, because I testify about it, that its works are evil.
8 Pandeni kwenda katika sikukuu; mimi siendi katika sikukuu hii kwa sababu muda wangu haujakamilika bado.”
You go up to the feast. I am not yet going up to this feast, because my time is not yet fulfilled.”
9 Baada ya kusema mambo hayo kwao, alibaki Galilaya.
Having said these things to them, he stayed in Galilee.
10 Hata hivyo, ndugu zake walipokuwa wamekwenda katika sikukuu, ndipo naye alienda, siyo kwa wazi bali kwa siri.
But when his brothers had gone up to the feast, then he also went up, not publicly, but as it were in secret.
11 Wayahudi walikuwa wakimtafuta katika sikukuu na kusema, “Yuko wapi?”
The Jews therefore sought him at the feast, and said, “Where is he?”
12 Kulikuwa na majadiliano mengi miongoni mwa makutano juu yake. Wengine walisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walisema, “Hapana, huwapotosha makutano.”
There was much murmuring among the multitudes concerning him. Some said, “He is a good man.” Others said, “Not so, but he leads the multitude astray.”
13 Hata hivyo hakuna aliyezungumza wazi juu yake kwa kuwaogopa Wayahudi.
Yet no one spoke openly of him for fear of the Jews.
14 Wakati sikukuu ilipofika katikati, Yesu alipanda kwenda Hekaluni na kuanza kufundisha.
But when it was now the middle of the feast, Jesus went up into the temple and taught.
15 Wayahudi walikuwa wakishangaa na kusema, “Kwa jinsi gani mtu huyu anajua mambo mengi? Hajasoma kamwe.”
The Jews therefore marveled, saying, “How does this man know letters, having never been educated?”
16 Yesu akawajibu na kuwaambia, “Mafundisho yangu siyo yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
Jesus therefore answered them, “My teaching is not mine, but his who sent me.
17 Iwapo yeyote atapenda kufanya mapenzi yake yeye, atajua kuhusu mafundisho haya, kama yanatoka kwa Mungu, au kama ninazungumza kutoka kwangu mwenyewe.
If anyone desires to do his will, he will know about the teaching, whether it is from God or if I am speaking from myself.
18 Kila anayezungumza yatokayo kwake mwenywe hutafuta utukufu wake, bali kila atafutaye utukufu wake yeye aliyemtuma, mtu huyo ni wa kweli, na ndani yake hakuna kutotenda haki.
He who speaks from himself seeks his own glory, but he who seeks the glory of him who sent him is true, and no unrighteousness is in him.
19 Musa hakuwapa nyinyi sheria? Lakini hakuna hata mmoja kati yenu atendaye sheria. Kwa nini mnataka kuniua?
Did not Moses give you the law, and yet none of you keeps the law? Why do you seek to kill me?”
20 Makutano wakajibu, “Una pepo. Nani anataka kukuua?”
The multitude answered, “You have a demon! Who seeks to kill you?”
21 Yesu akajibu na akawaambia, “Nimetenda kazi moja, nanyi nyote mmeshangazwa kwa sababu yake.
Jesus answered them, “I did one work and you all marvel because of it.
22 Musa aliwapa tohara (siyo kwamba inatoka kwa Musa, bali ile inatoka kwa mababa), na katika Sabato mnamtahili mtu.
Moses has given you circumcision (not that it is of Moses, but of the fathers), and on the Sabbath you circumcise a boy.
23 Iwapo mtu atapokea tohara katika siku ya Sabato ili kwamba sheria ya Musa isivunjwe, kwa nini mnanikasirikia mimi kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa katika Sabato?
If a boy receives circumcision on the Sabbath, that the law of Moses may not be broken, are you angry with me because I made a man completely healthy on the Sabbath?
24 Msihukumu kulingana na mwonekano, bali hukumuni kwa haki.
Do not judge according to appearance, but judge righteous judgment.”
25 Baadhi yao kutoka Yerusalemu wakasema, “Siye huyu wanayemtafuta kumwua?
Therefore some of them of Jerusalem said, “Is not this he whom they seek to kill?
26 Na tazama, anaongea wazi wazi, na hawasemi chochote juu yake. Haiwezi ikawa kwamba viongozi wanajua kweli kuwa huyu ni Kristo, inaweza kuwa?
Behold, he speaks openly, and they say nothing to him. Can it be that the rulers indeed know that this is truly the Christ?
27 Tunajua huyu mtu anatokea wapi. Kristo atakapokuja, hata hivyo, hakuna atakayejua wapi anakotoka.”
However, we know where this man comes from, but when the Christ comes, no one will know where he comes from.”
28 Yesu alikuwa akipaza sauti yake hekaluni, akifundisha na kusema, “Ninyi nyote mnanijua mimi na mnajua nitokako. Sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye aliyenituma ni wa kweli, na hamumjui yeye.
Jesus therefore cried out in the temple, teaching and saying, “You both know me, and know where I am from. I have not come of myself, but he who sent me is true, whom you do not know.
29 Ninamjua yeye kwa sababu nimetoka kwake na alinituma.”
I know him, because I am from him, and he sent me.”
30 Walikuwa wanajaribu kumkamata, lakini hakuna hata mmoja aliyeinua mkono wake juu yake kwa sababu saa yake ilikuwa bado haijafika.
They sought therefore to take him; but no one laid a hand on him, because his hour had not yet come.
31 Hata hivyo, wengi katika makutano walimwamini. Walisema, “Kristo atakapokuja, atafanya ishara nyingi kuliko alizofanya mtu huyu?”
But of the multitude, many believed in him. They said, “When the Christ comes, he will not do more signs than those which this man has done, will he?”
32 Mafarisayo waliwasikia makutano wakinong'onezana mambo haya kuhusu Yesu, na wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakatuma maafisa ili kumkamata.
The Pharisees heard the multitude murmuring these things concerning him, and the chief priests and the Pharisees sent officers to arrest him.
33 Ndipo Yesu aliposema, “Bado kuna muda kitambo niko pamoja nanyi, na baadaye nitakwenda kwake yeye aliyenituma.
Then Jesus said, “I will be with you a little while longer, then I go to him who sent me.
34 Mtanitafuta wala hamtaniona; kule niendako, hamtaweza kuja.”
You will seek me and will not find me. You cannot come where I am.”
35 Kwa hiyo Wayahudi wakasemezana wao kwa wao, “Mtu huyu atakwenda wapi kwamba tusiweze kumuona? Ataenda kwa Waliotawanyika kati ya Wayunani na kuwafundisha Wayunani?
The Jews therefore said among themselves, “Where will this man go that we will not find him? Will he go to the Dispersion among the Greeks and teach the Greeks?
36 Ni neno gani hili alilolisema, 'Mtanitafuta wala hamtaniona; kule niendako hamtamweza kuja'?”
What is this word that he said, ‘You will seek me, and will not find me;’ and ‘Where I am, you cannot come’?”
37 Sasa katika siku ya mwisho, siku kubwa ya sikukuu, Yesu alisimama akapaza sauti, akisema, “Ikiwa yeyote ana kiu, na aje kwangu anywe.
Now on the last and greatest day of the feast, Jesus stood and cried out, “If anyone is thirsty, let him come to me and drink!
38 Yeye aniaminiye mimi, kama maandiko yalivyosema, kutoka ndani yake itatiririka mito ya maji ya uzima.”
He who believes in me, as the Scripture has said, from within him will flow rivers of living water.”
39 Lakini aliyasema haya kuhusu Roho, ambaye wao wamwaminio watampokea; Roho alikuwa bado hajatolewa kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.
But he said this about the Spirit, which those believing in him were to receive. For the Holy Spirit was not yet given, because Jesus was not yet glorified.
40 Baadhi ya makutano, waliposikia maneno haya, walisema, “Kweli huyu ni nabii.”
Many of the multitude therefore, when they heard these words, said, “This is truly the prophet.”
41 Wengine walisema, “Huyu ni Kristo.” Lakini wengine walisema, “nini, Kristo aweza kutoka Galilaya?
Others said, “This is the Christ.” But some said, “What, does the Christ come out of Galilee?
42 Maandiko hayajasema kuwa Kristo atatokea katika ukoo wa Daudi na kutoka Bethlehemu, kijiji ambacho Daudi alikuwa?
Has not the Scripture said that the Christ comes of the offspring of David, and from Bethlehem, the village where David was?”
43 Hivyo, pale ukainuka mgawanyiko katikati ya makutano kwa ajili yake.
So a division arose in the multitude because of him.
44 Wengine kati yao wangelimkamata, lakini hakuna aliyenyoosha mikono yake juu yake.
Some of them would have arrested him, but no one laid hands on him.
45 Ndipo wale maofisa wakarudi kwa wakuu wa makuhani na Mafarisayo, nao wakawaambia, “Kwa nini hamjamleta?”
The officers therefore came to the chief priests and Pharisees; and they said to them, “Why did not you bring him?”
46 Maofisa wakajibu, “Hakuna mtu aliyewahi kuzungumza kama huyu kabla.”
The officers answered, “No man ever spoke like this man!”
47 Ndipo Mafarisayo walipowajibu, “Na nyinyi pia mmepotoshwa?
The Pharisees therefore answered them, “You are not also led astray, are you?
48 Kuna yeyote kati ya watawala anayemwamini, au yeyote wa Mafarisayo?
Have any of the rulers or any of the Pharisees believed in him?
49 Bali hawa makutano wasiojua sheria - wamelaaniwa.”
But this multitude that does not know the law is cursed.”
50 Nikodemo akawaambia (yeye aliyemwendea Yesu zamani, akiwa mmoja wa Mafarisayo),
Nicodemus (he who came to him by night, being one of them) said to them,
51 “Je sheria yetu inamhukumu mtu isipokuwa amesikilizwa kwanza na kujua anachokifanya?”
“Does our law judge a man unless it first hears from him personally and knows what he does?”
52 Walijibu na kumwambia, “Na wewe pia unatokea Galilaya? Tafuta na uone kwamba hakuna nabii aliyetokea Galilaya.”
They answered him, “Are you also from Galilee? Search and see that no prophet has arisen out of Galilee.”
53 (Zingatia: Baadhi ya maneno ya Yohana 7: 53 - 8: 11 hayamo katika nakala bora za kale). Kisha kila mtu alienda nyumbani kwake.
Everyone went to his own house,

< Yohana 7 >