< Yohana 7 >
1 Na baada ya mambo haya Yesu alisafiri hivi katika Galilaya, kwa sababu hakupenda kwenda Uyahudi kwa sababu wayahudi walikuwa wakifanya mipango ya kumwua.
Pak Ježíš chodil po Galileji, v Judsku mu ukládali o život.
2 Sasa sikukuu ya Wayahudi, sikukuu ya Vibanda, ilikuwa karibu.
Když se blížily židovské svátky díkůvzdání,
3 Ndipo ndugu zake walipomwambia, “Ondoka mahali hapa uende Uyahudi, ili kwamba wanafunzi wako vile vile wayaone matendo ufanyayo.
Ježíšovi bratři naléhali: „Jdi do Judska, ať lidé vidí tvoje činy!
4 Hakuna afanyaye lolote kwa siri iwapo yeye mwenyewe anataka kujulikana wazi. Iwapo unafanya mambo haya, jionyeshe mwenyewe kwa ulimwengu.”
Neskrývej se v ústraní, ale snaž se prosadit na veřejnosti.“
5 Hata ndugu zake pia hawakumwamini.
Oni ho totiž nechápali.
6 Ndipo Yesu alipowaambia, “Wakati wangu haujafika bado, lakini wakati wenu kila mara uko tayari.
Ježíš jim řekl: „Půjdu, až přijde můj čas. Vy můžete jít kdykoliv,
7 Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, bali unanichukia mimi kwa sababu ninaushuhudia kuwa matendo yake ni maovu.
protože vás lidé nebudou nenávidět tak jako mne. Neradi slyší, když je obviňuji z jejich zlých činů.
8 Pandeni kwenda katika sikukuu; mimi siendi katika sikukuu hii kwa sababu muda wangu haujakamilika bado.”
Jděte klidně sami a já přijdu, až bude vhodná chvíle.“
9 Baada ya kusema mambo hayo kwao, alibaki Galilaya.
Ježíš zůstal v Galileji, ale brzy po odchodu svých bratrů se tajně vydal na cestu. Chtěl totiž dojít do Jeruzaléma nepoznán.
10 Hata hivyo, ndugu zake walipokuwa wamekwenda katika sikukuu, ndipo naye alienda, siyo kwa wazi bali kwa siri.
11 Wayahudi walikuwa wakimtafuta katika sikukuu na kusema, “Yuko wapi?”
O svátcích ho tam lidé hledali a všude se o něm hovořilo. Někteří ho chválili, jiní zase říkali, že plete lidem hlavu.
12 Kulikuwa na majadiliano mengi miongoni mwa makutano juu yake. Wengine walisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walisema, “Hapana, huwapotosha makutano.”
13 Hata hivyo hakuna aliyezungumza wazi juu yake kwa kuwaogopa Wayahudi.
Ale to se jen šeptalo, protože mluvit o něm na veřejnosti bylo nebezpečné.
14 Wakati sikukuu ilipofika katikati, Yesu alipanda kwenda Hekaluni na kuanza kufundisha.
Uprostřed oslav se Ježíš objevil v chrámu a začal kázat.
15 Wayahudi walikuwa wakishangaa na kusema, “Kwa jinsi gani mtu huyu anajua mambo mengi? Hajasoma kamwe.”
Překvapení Židé se divili: „Jak to, že se tak vyzná v Písmu, když na to nemá školy?“
16 Yesu akawajibu na kuwaambia, “Mafundisho yangu siyo yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
Ježíš jim odpověděl: „Nepředkládám vám své vlastní názory. Tlumočím jen to, co vám chce sdělit Bůh.
17 Iwapo yeyote atapenda kufanya mapenzi yake yeye, atajua kuhusu mafundisho haya, kama yanatoka kwa Mungu, au kama ninazungumza kutoka kwangu mwenyewe.
Jste-li ochotni plnit Boží vůli, jistě poznáte, že to nejsou má vlastní slova.
18 Kila anayezungumza yatokayo kwake mwenywe hutafuta utukufu wake, bali kila atafutaye utukufu wake yeye aliyemtuma, mtu huyo ni wa kweli, na ndani yake hakuna kutotenda haki.
Kdo přináší světu jen vlastní myšlenky, ten touží po slávě a lidské chvále. Ale ten je upřímný a pravdomluvný, kdo svou řečí oslavuje Boha.
19 Musa hakuwapa nyinyi sheria? Lakini hakuna hata mmoja kati yenu atendaye sheria. Kwa nini mnataka kuniua?
Mojžíš vám dal zákon, ale nikdo z vás ho neplní. Jakým právem mne osočujete? Proč mi ukládáte o život?“
20 Makutano wakajibu, “Una pepo. Nani anataka kukuua?”
„Ty ses snad pomátl na rozumu! Copak tě chce někdo zabít?“ozvalo se z davu.
21 Yesu akajibu na akawaambia, “Nimetenda kazi moja, nanyi nyote mmeshangazwa kwa sababu yake.
Ježíš jim řekl: „Uzdravil jsem v sobotu nemocného člověka, a vyvedlo vás to z míry.
22 Musa aliwapa tohara (siyo kwamba inatoka kwa Musa, bali ile inatoka kwa mababa), na katika Sabato mnamtahili mtu.
Přitom vy sami nepovažujete za porušení, když připadne na sobotu povinnost udělat obřízku, a klidně ji vykonáte. Proč vás tedy tak rozčiluje, že jsem v sobotu vrátil člověku zdraví?
23 Iwapo mtu atapokea tohara katika siku ya Sabato ili kwamba sheria ya Musa isivunjwe, kwa nini mnanikasirikia mimi kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa katika Sabato?
24 Msihukumu kulingana na mwonekano, bali hukumuni kwa haki.
Neulpívejte na povrchu, ale pronikejte k jádru věci.“
25 Baadhi yao kutoka Yerusalemu wakasema, “Siye huyu wanayemtafuta kumwua?
Někteří z jeruzalémských občanů povstali: „Je to opravdu ten, kterého chtějí zabít?
26 Na tazama, anaongea wazi wazi, na hawasemi chochote juu yake. Haiwezi ikawa kwamba viongozi wanajua kweli kuwa huyu ni Kristo, inaweza kuwa?
Veřejně káže v chrámu, a oni ho nechají. Že by ho přece uznali za Mesiáše? To se nám nezdá. O Mesiáši prý nikdo nebude vědět, odkud přišel, ale Ježíšův původ známe.“
27 Tunajua huyu mtu anatokea wapi. Kristo atakapokuja, hata hivyo, hakuna atakayejua wapi anakotoka.”
28 Yesu alikuwa akipaza sauti yake hekaluni, akifundisha na kusema, “Ninyi nyote mnanijua mimi na mnajua nitokako. Sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye aliyenituma ni wa kweli, na hamumjui yeye.
„Znáte mne a víte, odkud pocházím, “zvolal Ježíš. „Ale neznáte toho, který mne poslal.
29 Ninamjua yeye kwa sababu nimetoka kwake na alinituma.”
Já ho znám dobře a vím, že si zaslouží naši důvěru. On za mnou stojí, neprosazuji svou vlastní věc.“
30 Walikuwa wanajaribu kumkamata, lakini hakuna hata mmoja aliyeinua mkono wake juu yake kwa sababu saa yake ilikuwa bado haijafika.
Chtěli ho zatknout, ale nikdo se k tomu neodhodlal, protože ještě nepřišla chvíle, kdy se to mělo stát. Mnozí z posluchačů v Ježíše uvěřili.
31 Hata hivyo, wengi katika makutano walimwamini. Walisema, “Kristo atakapokuja, atafanya ishara nyingi kuliko alizofanya mtu huyu?”
Řekli si: „Mesiáš by určitě nedělal více zázraků než on!“
32 Mafarisayo waliwasikia makutano wakinong'onezana mambo haya kuhusu Yesu, na wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakatuma maafisa ili kumkamata.
Když se to doneslo farizejům a velekněžím, poslali chrámovou stráž, aby ho zatkla.
33 Ndipo Yesu aliposema, “Bado kuna muda kitambo niko pamoja nanyi, na baadaye nitakwenda kwake yeye aliyenituma.
Ježíš pokračoval: „Zůstanu s vámi ještě nějaký čas a pak se vrátím k tomu, který mne poslal.
34 Mtanitafuta wala hamtaniona; kule niendako, hamtaweza kuja.”
Až odejdu, budete mne marně hledat, ale za mnou se nedostanete.“
35 Kwa hiyo Wayahudi wakasemezana wao kwa wao, “Mtu huyu atakwenda wapi kwamba tusiweze kumuona? Ataenda kwa Waliotawanyika kati ya Wayunani na kuwafundisha Wayunani?
Židé se překvapeně ptali: „Kam chce odejít, že se za ním nedostaneme? Chce snad jít mezi pohany a učit je?“
36 Ni neno gani hili alilolisema, 'Mtanitafuta wala hamtaniona; kule niendako hamtamweza kuja'?”
37 Sasa katika siku ya mwisho, siku kubwa ya sikukuu, Yesu alisimama akapaza sauti, akisema, “Ikiwa yeyote ana kiu, na aje kwangu anywe.
Poslední den svátků, když kněží v průvodu nesli vodu do chrámu, stál tam Ježíš a volal: „Kdo má žízeň, pojď se ke mně napít. Písmo říká, že nitro každého, kdo ve mne uvěří, vydá životodárný pramen.“
38 Yeye aniaminiye mimi, kama maandiko yalivyosema, kutoka ndani yake itatiririka mito ya maji ya uzima.”
39 Lakini aliyasema haya kuhusu Roho, ambaye wao wamwaminio watampokea; Roho alikuwa bado hajatolewa kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.
Mluvil o Božím Duchu, který měl být seslán až po dovršení Ježíšova díla na zemi. Měl ho dostat každý, kdo v Ježíše uvěří.
40 Baadhi ya makutano, waliposikia maneno haya, walisema, “Kweli huyu ni nabii.”
Ze zástupu se ozvaly dohady: „To je asi Mesiáš.“
41 Wengine walisema, “Huyu ni Kristo.” Lakini wengine walisema, “nini, Kristo aweza kutoka Galilaya?
Někteří však namítali: „Ne, to může být nanejvýš jeho předchůdce. Pochází přece z Galileje!
42 Maandiko hayajasema kuwa Kristo atatokea katika ukoo wa Daudi na kutoka Bethlehemu, kijiji ambacho Daudi alikuwa?
A Písmo říká, že Mesiáš se narodí v Betlémě a že bude potomkem krále Davida.“
43 Hivyo, pale ukainuka mgawanyiko katikati ya makutano kwa ajili yake.
Nakonec se pohádali.
44 Wengine kati yao wangelimkamata, lakini hakuna aliyenyoosha mikono yake juu yake.
Chrámová stráž se neodvážila Ježíše zatknout. Vrátili se ke kněžím a farizejům, kteří se na ně obořili: „Kde ho máte? Proč jste ho nepřivedli?“
45 Ndipo wale maofisa wakarudi kwa wakuu wa makuhani na Mafarisayo, nao wakawaambia, “Kwa nini hamjamleta?”
46 Maofisa wakajibu, “Hakuna mtu aliyewahi kuzungumza kama huyu kabla.”
„Nemohli jsme, takového člověka jsme ještě neslyšeli.“
47 Ndipo Mafarisayo walipowajibu, “Na nyinyi pia mmepotoshwa?
„Tak i vy jste se nechali svést?“zlobili se farizejové.
48 Kuna yeyote kati ya watawala anayemwamini, au yeyote wa Mafarisayo?
„Uvěřil mu snad někdo z velerady nebo z nás?
49 Bali hawa makutano wasiojua sheria - wamelaaniwa.”
Co se dá čekat od nevzdělaného davu! Nevyznají se v Bibli a takhle to dopadá.“
50 Nikodemo akawaambia (yeye aliyemwendea Yesu zamani, akiwa mmoja wa Mafarisayo),
Jeden z farizejů – Nikodém, který před časem Ježíše navštívil, namítl:
51 “Je sheria yetu inamhukumu mtu isipokuwa amesikilizwa kwanza na kujua anachokifanya?”
„Jak můžete odsoudit člověka, kterého jste nevyslechli? Odpovídá to našemu zákonu?“
52 Walijibu na kumwambia, “Na wewe pia unatokea Galilaya? Tafuta na uone kwamba hakuna nabii aliyetokea Galilaya.”
„Nejsi snad jeho krajan?“zeptali se ho. „Ukaž nám v Bibli, že má přijít prorok z Galileje.“
53 (Zingatia: Baadhi ya maneno ya Yohana 7: 53 - 8: 11 hayamo katika nakala bora za kale). Kisha kila mtu alienda nyumbani kwake.
A s tím se rozešli.