< Yohana 5 >
1 Baada ya hapo kulikuwa na sikukuu ya Wayahudi, na Yesu alipanda kwenda Yerusalemu.
Après cela, il y eut une fête des Juifs, et Jésus monta à Jérusalem.
2 Na kule Yerusalemu palikuwa na birika kwenye mlango wa kondoo, lililokuwa likiitwa kwa lugha ya Kiebrania Bethzatha, nalo lina matao matano.
Or, il y a à Jérusalem, près de la porte des brebis, un réservoir, appelé en hébreu Béthesda, qui est entouré de cinq portiques.
3 Idadi kubwa ya wagonjwa ilikuwemo, vipofu, viwete, au waliopooza walikuwa wamelala katika matao hayo. (Zingatia: Maneno ya mstari wa 3 hayaonekani katika nakala nzuri za kale. “Wakisubiri maji kutibuliwa.”) Kwa hakikia wakati fulani malaika alishuka ndani ya Bwana na kuyatibua maji.
Là se trouvaient couchés un grand nombre de malades, des aveugles, des impotents, des paralytiques, [qui attendaient l'agitation de l'eau;
4 Kwahiyo, yule ambaye alikuwa wa kwanza kuingia ndani ya baada ya maji kutibuliwa alifanywa mzima kutokana na chochote kilichokuwa kimemshika kwa wakati huo.
car un ange descendait de temps en temps dans le réservoir et mettait l'eau en mouvement; et le premier qui descendait dans le réservoir, après que l'eau avait été agitée, était guéri, de quelque maladie qu'il fût atteint].
5 Na mtu mmoja aliyekuwa ameugua kwa muda wa miaka thelathini na minane alikuwa ndani ya matao.
Il y avait là un homme qui était malade depuis trente-huit ans.
6 Yesu alipomwona amelala ndani ya matao na baada ya kutambua kuwa amelala pale kwa muda mrefu Yesu alimwambia, “Je unataka kuwa mzima?”
Jésus, le voyant couché et sachant qu'il était malade depuis longtemps, lui dit: Veux-tu être guéri?
7 Yule mgonjwa akamjibu, “Bwana sina mtu, wa kuniweka katika birika wakati maji yanapotibuliwa. Wakati ninapojaribu kuingia mtu mwingine hunitangulia.”
Le malade lui répondit: Seigneur, je n'ai personne pour me jeter dans le réservoir, quand l'eau est agitée; et, pendant que j'y vais, un autre y descend avant moi.
8 Yesu akamwambia, “Inuka na uchukue godoro lako na uende.”
Jésus lui dit: Lève-toi, prends ton lit et marche.
9 Mara yule mtu akaponywa, akachukua kintanda chake na akaenda. Na siku hiyo ilikuwa siku ya Sabato.
Et aussitôt cet homme fut guéri; il prit son lit et se mit à marcher. Or, c'était un jour de sabbat.
10 Hivyo Wayahudi wakamwambia yule mtu aliyeponywa, “Leo ni siku ya Sabato, na hauruhusiwi kubeba godoro lako.”
Alors les Juifs dirent à celui qui avait été guéri: C'est le jour du sabbat; il ne t'est pas permis d'emporter ton lit.
11 Akajibu, yeye aliyeniponya ndiye aliyeniambia, “Chukua godoro lako na uende.”
Il leur répondit: Celui-là même qui m'a guéri, m'a dit: Prends ton lit et marche!
12 Wakauliza, “Ni nani aliyekuambia 'Chukua godoro lako na uende?'''
Ils lui demandèrent: Qui est cet homme qui t'a dit: Prends ton lit et marche?
13 Ingawa, yule aliyeponywa hakumjua, kwa sababu Yesu alikuwa ameondoka kwa siri. Kwa kuwa kulikuwa na watu wengi katika sehemu hiyo.
Mais celui qui avait été guéri ne savait pas qui c'était; car Jésus avait disparu dans la foule qui se trouvait à cet endroit.
14 Baada ya hapo Yesu alimkuta yule mtu hekaluni na akamwambia, “Tazama, umepona! “Usitende dhambi tena usije ukapatwa na jambo baya zaidi.”
Plus tard, Jésus le trouva dans le temple et lui dit: Te voilà guéri; ne pèche plus, de peur qu'il ne t'arrive quelque chose de pire.
15 Yule mtu akaenda na kuwataarifu Wayahudi kuwa Yesu ndiye aliyemponya.
Cet homme alla dire aux Juifs que c'était Jésus qui l'avait guéri.
16 Hivyo, kwa sababu ya mambo hayo Wayahudi walimtesa Yesu, kwa sababu alifanya mambo haya siku ya Sabato.
C'est pourquoi les Juifs poursuivaient Jésus, parce qu'il faisait ces miracles le jour du sabbat.
17 Yesu akawambia, “Baba yangu anafanya kazi hata sasa nami nafanya kazi.”
Mais il leur dit: Mon Père travaille jusqu'à présent, et je travaille, moi aussi.
18 Kwa sababu hiyo Wayahudi walizidi kumtafuta ili wamuue sio tu kwa sababu ya kuivunja Sabato, bali kwa kumwita Mungu Baba yake, akijifanya kuwa sawa na Mungu.
A cause de cela, les Juifs cherchaient encore davantage à le faire mourir, non seulement parce qu'il violait le sabbat, mais encore parce qu'il disait que Dieu était son propre Père, se faisant égal à Dieu.
19 Yesu akawajibu, “Amini, amini, Mwana hawezi kufanya kitu chochote isipokuwa kile ambacho amemwona Baba yake anakifanya, kwa kuwa chochote Baba akifanyacho ndicho na Mwana atakachofanya.
Jésus prit donc la parole et leur dit: En vérité, en vérité, je vous le déclare, le Fils ne peut rien faire de lui-même: il ne fait que ce qu'il voit faire au Père; car tout ce que le Père fait, le Fils aussi le fait pareillement.
20 Kwa kuwa Baba ampenda Mwana, na amwonyesha kila kitu anachokifanya na atamwonyesha mambo makubwa kuliko haya ili kwamba mzidi kushangaa.”
Le Père aime le Fils et lui montre tout ce qu'il fait; il lui montrera des oeuvres plus grandes que celles-ci, afin que vous soyez dans l'étonnement.
21 Kwa kuwa kama vile ambavyo Baba awafufuavyo wafu na kuwapa uzima, halikadhalika Mwana pia humpa yeyote ampendaye.
En effet, de même que le Père ressuscite les morts et leur donne la vie, de même le Fils donne la vie à qui il veut.
22 Kwa kuwa Baba hamhukumu yeyote, bali amempa Mwana hukumu yote
Le Père aussi ne juge personne; mais il a remis au Fils le jugement tout entier, afin que tous honorent le Fils, comme ils honorent le Père.
23 ili kwamba wote wamuheshimu Mwana kama vile Mwana anavyomuheshimu Baba. Yeye asiyemuheshimu Mwana hamuheshimu Baba aliyemtuma.
Celui qui n'honore pas le Fils, n'honore pas le Père qui l'a envoyé.
24 Amini, amini, yeye asikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenituma anao uzima wa milele na hatahukumiwa. Badala yake, amepita kutoka mautini na kuingia uzimani. (aiōnios )
En vérité, en vérité, je vous le dis, celui qui écoute ma parole et croit en Celui qui m'a envoyé, à la vie éternelle, et il ne vient pas en jugement, mais il est passé de la mort à la vie. (aiōnios )
25 Amini, amini, nawambia wakati unakuja na sasa upo ambao wafu watasikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wote watakao sikia wataishi.
En vérité, en vérité, je vous le déclare, l'heure vient, et elle est déjà venue, où les morts entendront la voix du Fils de Dieu, et ceux qui l'auront entendue vivront.
26 Kwa kuwa kama vile Baba alivyo na uzima ndani yake mwenyewe,
Car, comme le Père a la vie en lui-même, il a aussi donné au Fils d'avoir la vie en lui-même.
27 kadhalika amempa Mwana kuwa na uzima ndani yake, na Baba amempa Mwana mamlaka ili kwamba ahukumu kwa kuwa ni Mwana wa Adamu.
Il lui a donné le pouvoir d'exercer le jugement, parce qu'il est le Fils de l'homme.
28 Msishangazwe na hili, kwa kuwa wakati unakuja ambao wafu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake
Ne soyez point étonnés de cela; car l'heure vient où tous ceux qui sont dans les sépulcres entendront sa voix et en sortiront;
29 nao watatoka nje: kwa waliotenda mema kwa ufufuo wa uzima, na walio tenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu.
ceux qui auront fait le bien ressusciteront pour la vie, et ceux qui auront fait le mal ressusciteront pour le jugement.
30 Siwezi kufanya kitu chochote kutoka kwangu mwenyewe. Kama nisikiavyo, ndivyo ninavyo hukumu na hukumu yangu ni ya haki kwa kuwa sitafuti mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenituma.
Je ne puis rien faire de moi-même; je juge d'après ce que j'entends, et mon jugement est juste, parce que je ne cherche pas ma volonté, mais la volonté de Celui qui m'a envoyé.
31 Kama nikijishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu usingelikuwa wa kweli.
Si je me rends témoignage à moi-même, mon témoignage n'est pas digne de foi.
32 Kuna mwingine anayeshuhudia kuhusu mimi na ninajua kwa hakika ushuhuda anaonishuhudia ni wa kweli.
Il y en a un autre qui me rend témoignage, et je sais que le témoignage qu'il me rend est digne de foi.
33 Mmetuma kwa Yohana naye ameishuhudia kweli.
Vous avez envoyé à Jean des messagers, et il a rendu témoignage à la vérité.
34 Hatahivyo, ushuhuda ninaoupokea hautoki kwa mwanadamu. Ninayasema haya ili kwamba mweze kuokolewa.
Pour moi, ce n'est pas le témoignage d'un homme que j'invoque; mais je parle ainsi, afin que vous soyez sauvés.
35 Yohana alikuwa ni taa iliyokuwa ikiwaka na kung'ara, na mlikuwa tayari kuifurahia kwa muda kitambo nuru yake.
Il était le flambeau allumé et brillant, et vous avez voulu, pour un peu de temps, vous réjouir à sa lumière.
36 Ushuhuda nilionao ni mkuu kuliko ule wa Yohana, kwa kazi ambazo Baba amenipa kuzikamilisha, hizo kazi nizifanyazo zashuhudia kuwa Baba amenituma.
Mais moi, j'ai un témoignage plus grand que celui de Jean; car les oeuvres que le Père m'a donné d'accomplir, ces oeuvres-là que je fais rendent à mon sujet ce témoignage, que le Père m'a envoyé.
37 Baba aliyenituma yeye mwenyewe ameshuhudia kuhusu mimi. Hamjawahi kusikia sauti yake wala kuona umbo lake wakati wowote.
Et le Père qui m'a envoyé m'a lui-même rendu témoignage. Vous n'avez jamais entendu sa voix; vous n'avez jamais vu sa face,
38 Hamna neno lake likikaa ndani yenu kwa kuwa hamumwamini yeye aliyetumwa.
et sa parole ne demeure pas en vous, puisque vous ne croyez pas celui qu'il a envoyé.
39 Mnayachunguza maandiko mkidhani ndani yake mna uzima wa milele, na hayo maandiko yanashuhudia habari zangu na (aiōnios )
Vous sondez les Écritures, parce que vous pensez avoir par elles la vie éternelle: ce sont elles qui rendent témoignage de moi. (aiōnios )
40 hamtaki kuja kwangu ili mpate uzima wa milele.
Et vous ne voulez pas venir à moi, pour avoir la vie!
41 Sipokei sifa kutoka kwa watu,
Je ne cherche point la gloire qui vient des hommes;
42 lakini ninajua kuwa hamna upendo wa Mungu ndani yenu ninyi wenyewe.
mais je sais que vous n'avez pas l'amour de Dieu en vous.
43 Nimekuja kwa jina la Baba yangu, hamukuweza kunipokea. Kama mwingine akija kwa jina lake mngempokea.
Je suis venu au nom de mon Père, et vous ne me recevez pas. Qu'un autre vienne en son propre nom, vous le recevrez.
44 Je mnawezaje kuamini ninyi ambao mnapokea sifa kutoka kwa kila mmoja wenu lakini hamtafuti sifa itokayo kwa Mungu wa pekee?
Comment pouvez-vous croire, vous qui recevez votre gloire les uns des autres, et ne recherchez pas la gloire qui vient de Dieu seul?
45 Msidhani mimi nitawashitaki mbele za Baba. Anayewashitaki ninyi ni Musa, ambaye ninyi mmeweka matumaini yenu kwake.
Ne pensez pas que ce soit moi qui doive vous accuser devant le Père; celui qui vous accusera, c'est Moïse, en qui vous avez mis votre espérance.
46 Kama mngekuwa mnamwamini Musa, mngeniamini mimi kwa sababu aliandika kuhusu habari zangu.
Car si vous croyiez Moïse, vous me croiriez aussi; en effet, c'est à mon sujet qu'il a écrit.
47 Kama hamuamini maandiko yake, mtawezaje kuamini maneno yangu?
Mais si vous ne croyez pas à ses écrits, comment croiriez-vous à mes paroles?