< Yohana 5 >
1 Baada ya hapo kulikuwa na sikukuu ya Wayahudi, na Yesu alipanda kwenda Yerusalemu.
After this, there was a feast of the Jews, and Jesus went up to Jerusalem.
2 Na kule Yerusalemu palikuwa na birika kwenye mlango wa kondoo, lililokuwa likiitwa kwa lugha ya Kiebrania Bethzatha, nalo lina matao matano.
Near the Sheep Gate in Jerusalem, there is a pool, which is called Bethesda in Hebrew. It’s surrounded by five covered colonnades.
3 Idadi kubwa ya wagonjwa ilikuwemo, vipofu, viwete, au waliopooza walikuwa wamelala katika matao hayo. (Zingatia: Maneno ya mstari wa 3 hayaonekani katika nakala nzuri za kale. “Wakisubiri maji kutibuliwa.”) Kwa hakikia wakati fulani malaika alishuka ndani ya Bwana na kuyatibua maji.
In these lay a great multitude of sick people, blind, lame, or paralyzed, waiting for the moving of the water,
4 Kwahiyo, yule ambaye alikuwa wa kwanza kuingia ndani ya baada ya maji kutibuliwa alifanywa mzima kutokana na chochote kilichokuwa kimemshika kwa wakati huo.
for an angel went down from time to time into the pool and stirred up the water. Whoever stepped in first, after the stirring of the water, was made well of whatever disease that person had.
5 Na mtu mmoja aliyekuwa ameugua kwa muda wa miaka thelathini na minane alikuwa ndani ya matao.
A certain man was there who had an infirmity thirty-eight years.
6 Yesu alipomwona amelala ndani ya matao na baada ya kutambua kuwa amelala pale kwa muda mrefu Yesu alimwambia, “Je unataka kuwa mzima?”
When Jesus saw him lying there, and knew that he had already been sick for a long time, He asked him, “Do you want to be made well?”
7 Yule mgonjwa akamjibu, “Bwana sina mtu, wa kuniweka katika birika wakati maji yanapotibuliwa. Wakati ninapojaribu kuingia mtu mwingine hunitangulia.”
The sick man answered, “Sir, I have no one to put me into the pool when the water is stirred up, but while I’m coming, another steps down before me.”
8 Yesu akamwambia, “Inuka na uchukue godoro lako na uende.”
Jesus told him, “Stand up, pick up your mat, and walk.”
9 Mara yule mtu akaponywa, akachukua kintanda chake na akaenda. Na siku hiyo ilikuwa siku ya Sabato.
Immediately, the man was made well, took up his mat, and walked. That was on the Sabbath day.
10 Hivyo Wayahudi wakamwambia yule mtu aliyeponywa, “Leo ni siku ya Sabato, na hauruhusiwi kubeba godoro lako.”
Therefore the Jews were telling him who was cured, “It’s the Sabbath, and it isn’t legal for you to carry your mat.”
11 Akajibu, yeye aliyeniponya ndiye aliyeniambia, “Chukua godoro lako na uende.”
He answered them, “He who made me well told me, ‘Take up your mat and walk.’”
12 Wakauliza, “Ni nani aliyekuambia 'Chukua godoro lako na uende?'''
Then they asked him, “Who told you to ‘Take up your mat and walk’?”
13 Ingawa, yule aliyeponywa hakumjua, kwa sababu Yesu alikuwa ameondoka kwa siri. Kwa kuwa kulikuwa na watu wengi katika sehemu hiyo.
The man who had been healed didn’t know who it was, because Jesus had disappeared into the crowd.
14 Baada ya hapo Yesu alimkuta yule mtu hekaluni na akamwambia, “Tazama, umepona! “Usitende dhambi tena usije ukapatwa na jambo baya zaidi.”
Later, Jesus found him in the temple and told him, “See, you have been made well! Don’t sin any more, so that nothing worse happens to you.”
15 Yule mtu akaenda na kuwataarifu Wayahudi kuwa Yesu ndiye aliyemponya.
The man went away, and told the Jews that it was Jesus who had made him well.
16 Hivyo, kwa sababu ya mambo hayo Wayahudi walimtesa Yesu, kwa sababu alifanya mambo haya siku ya Sabato.
For this reason, the Jews persecuted Jesus, and sought to kill Him, because He was doing these things on the Sabbath.
17 Yesu akawambia, “Baba yangu anafanya kazi hata sasa nami nafanya kazi.”
Jesus answered them, “My Father is still working, so I am working, too.”
18 Kwa sababu hiyo Wayahudi walizidi kumtafuta ili wamuue sio tu kwa sababu ya kuivunja Sabato, bali kwa kumwita Mungu Baba yake, akijifanya kuwa sawa na Mungu.
Because of this, the Jews tried all the harder to kill Him. Not only was He breaking the Sabbath, but He was even calling God His own Father, making Himself equal with God.
19 Yesu akawajibu, “Amini, amini, Mwana hawezi kufanya kitu chochote isipokuwa kile ambacho amemwona Baba yake anakifanya, kwa kuwa chochote Baba akifanyacho ndicho na Mwana atakachofanya.
Then Jesus answered, “Most assuredly, I tell you, the Son can do nothing of Himself, unless He sees the Father do it, for whatever He does, the Son does likewise.
20 Kwa kuwa Baba ampenda Mwana, na amwonyesha kila kitu anachokifanya na atamwonyesha mambo makubwa kuliko haya ili kwamba mzidi kushangaa.”
The Father loves the Son, and shows Him everything that He Himself does. He will show Him even greater works than these, that you may marvel.
21 Kwa kuwa kama vile ambavyo Baba awafufuavyo wafu na kuwapa uzima, halikadhalika Mwana pia humpa yeyote ampendaye.
As the Father raises the dead and gives life to them, even so the Son gives life to whoever He wishes.
22 Kwa kuwa Baba hamhukumu yeyote, bali amempa Mwana hukumu yote
The Father judges no one, but has committed all judgment to the Son,
23 ili kwamba wote wamuheshimu Mwana kama vile Mwana anavyomuheshimu Baba. Yeye asiyemuheshimu Mwana hamuheshimu Baba aliyemtuma.
that all may honor the Son just as they honor the Father. He who doesn’t honor the Son doesn’t honor the Father who sent Him.
24 Amini, amini, yeye asikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenituma anao uzima wa milele na hatahukumiwa. Badala yake, amepita kutoka mautini na kuingia uzimani. (aiōnios )
“Most assuredly, I tell you, the person who hears my words and believes in Him who sent me has everlasting life, and won’t come into judgment, but has passed from death into life. (aiōnios )
25 Amini, amini, nawambia wakati unakuja na sasa upo ambao wafu watasikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wote watakao sikia wataishi.
Most assuredly, I tell you, the time is coming, and now is, when the dead will hear the voice of God’s Son, and those who hear will live.
26 Kwa kuwa kama vile Baba alivyo na uzima ndani yake mwenyewe,
For just as the Father has life in Himself, so He has granted the Son to have life in Himself,
27 kadhalika amempa Mwana kuwa na uzima ndani yake, na Baba amempa Mwana mamlaka ili kwamba ahukumu kwa kuwa ni Mwana wa Adamu.
and has given Him authority to execute judgment, because He is the Son of Man.
28 Msishangazwe na hili, kwa kuwa wakati unakuja ambao wafu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake
Don’t marvel at this, for the time is coming in which all who are in the graves will hear His voice
29 nao watatoka nje: kwa waliotenda mema kwa ufufuo wa uzima, na walio tenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu.
and come out — those who have done good, to the resurrection of life, and those who have done evil, to the resurrection of condemnation.
30 Siwezi kufanya kitu chochote kutoka kwangu mwenyewe. Kama nisikiavyo, ndivyo ninavyo hukumu na hukumu yangu ni ya haki kwa kuwa sitafuti mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenituma.
I can do nothing by myself. As I hear, I judge, and my judgment is righteous, because I don’t seek my own will, but the will of the Father who sent me.
31 Kama nikijishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu usingelikuwa wa kweli.
“If I testify about myself, my testimony isn’t valid.
32 Kuna mwingine anayeshuhudia kuhusu mimi na ninajua kwa hakika ushuhuda anaonishuhudia ni wa kweli.
There is another who testifies on my behalf, and I know that his testimony about me is valid.
33 Mmetuma kwa Yohana naye ameishuhudia kweli.
You have sent to John, and he has testified to the truth.
34 Hatahivyo, ushuhuda ninaoupokea hautoki kwa mwanadamu. Ninayasema haya ili kwamba mweze kuokolewa.
Not that I accept human testimony, but I tell you this so that you may be saved.
35 Yohana alikuwa ni taa iliyokuwa ikiwaka na kung'ara, na mlikuwa tayari kuifurahia kwa muda kitambo nuru yake.
John was the burning and shining lamp, and you were willing for a time to rejoice in his light.
36 Ushuhuda nilionao ni mkuu kuliko ule wa Yohana, kwa kazi ambazo Baba amenipa kuzikamilisha, hizo kazi nizifanyazo zashuhudia kuwa Baba amenituma.
I have a greater testimony than John’s. The works that the Father has given me to finish — the very works that I do — testify about me, that the Father has sent me.
37 Baba aliyenituma yeye mwenyewe ameshuhudia kuhusu mimi. Hamjawahi kusikia sauti yake wala kuona umbo lake wakati wowote.
The Father Himself, who sent me, has testified about me. You have neither heard His voice at any time, nor seen His form.
38 Hamna neno lake likikaa ndani yenu kwa kuwa hamumwamini yeye aliyetumwa.
You don’t have His words dwelling in you, because you don’t believe the One who He sent.
39 Mnayachunguza maandiko mkidhani ndani yake mna uzima wa milele, na hayo maandiko yanashuhudia habari zangu na (aiōnios )
You search the Scriptures, for in them you think you have eternal life, and these testify about me. (aiōnios )
40 hamtaki kuja kwangu ili mpate uzima wa milele.
Yet you refuse to come to me to have life.
41 Sipokei sifa kutoka kwa watu,
“I don’t accept glory from men,
42 lakini ninajua kuwa hamna upendo wa Mungu ndani yenu ninyi wenyewe.
but I know you. I know that you don’t have God’s sincere love in you.
43 Nimekuja kwa jina la Baba yangu, hamukuweza kunipokea. Kama mwingine akija kwa jina lake mngempokea.
I have come in my Father’s name, and you don’t accept me, but if someone else comes in his own name, you will accept him.
44 Je mnawezaje kuamini ninyi ambao mnapokea sifa kutoka kwa kila mmoja wenu lakini hamtafuti sifa itokayo kwa Mungu wa pekee?
How can you believe when you accept glory from one another, and don’t seek the glory that comes from the only God?
45 Msidhani mimi nitawashitaki mbele za Baba. Anayewashitaki ninyi ni Musa, ambaye ninyi mmeweka matumaini yenu kwake.
“Don’t think that I will accuse you before the Father. Your accuser is Moses, who you have set your hope on.
46 Kama mngekuwa mnamwamini Musa, mngeniamini mimi kwa sababu aliandika kuhusu habari zangu.
If you believed Moses, you would believe me, for he wrote about me.
47 Kama hamuamini maandiko yake, mtawezaje kuamini maneno yangu?
If you don’t believe what he wrote, how will you believe what I say?”