< Yohana 5 >
1 Baada ya hapo kulikuwa na sikukuu ya Wayahudi, na Yesu alipanda kwenda Yerusalemu.
After these things was a festival day of the Jews, and Jesus went up to Jerusalem.
2 Na kule Yerusalemu palikuwa na birika kwenye mlango wa kondoo, lililokuwa likiitwa kwa lugha ya Kiebrania Bethzatha, nalo lina matao matano.
Now there is at Jerusalem a pond, called Probatica, which in Hebrew is named Bethsaida, having five porches.
3 Idadi kubwa ya wagonjwa ilikuwemo, vipofu, viwete, au waliopooza walikuwa wamelala katika matao hayo. (Zingatia: Maneno ya mstari wa 3 hayaonekani katika nakala nzuri za kale. “Wakisubiri maji kutibuliwa.”) Kwa hakikia wakati fulani malaika alishuka ndani ya Bwana na kuyatibua maji.
In these lay a great multitude of sick, of blind, of lame, of withered; waiting for the moving of the water.
4 Kwahiyo, yule ambaye alikuwa wa kwanza kuingia ndani ya baada ya maji kutibuliwa alifanywa mzima kutokana na chochote kilichokuwa kimemshika kwa wakati huo.
And an angel of the Lord descended at certain times into the pond; and the water was moved. And he that went down first into the pond after the motion of the water, was made whole, of whatsoever infirmity he lay under.
5 Na mtu mmoja aliyekuwa ameugua kwa muda wa miaka thelathini na minane alikuwa ndani ya matao.
And there was a certain man there, that had been eight and thirty years under his infirmity.
6 Yesu alipomwona amelala ndani ya matao na baada ya kutambua kuwa amelala pale kwa muda mrefu Yesu alimwambia, “Je unataka kuwa mzima?”
Him when Jesus had seen lying, and knew that he had been now a long time, he saith to him: Wilt thou be made whole?
7 Yule mgonjwa akamjibu, “Bwana sina mtu, wa kuniweka katika birika wakati maji yanapotibuliwa. Wakati ninapojaribu kuingia mtu mwingine hunitangulia.”
The infirm man answered him: Sir, I have no man, when the water is troubled, to put me into the pond. For whilst I am coming, another goeth down before me.
8 Yesu akamwambia, “Inuka na uchukue godoro lako na uende.”
Jesus saith to him: Arise, take up thy bed, and walk.
9 Mara yule mtu akaponywa, akachukua kintanda chake na akaenda. Na siku hiyo ilikuwa siku ya Sabato.
And immediately the man was made whole: and he took up his bed, and walked. And it was the sabbath that day.
10 Hivyo Wayahudi wakamwambia yule mtu aliyeponywa, “Leo ni siku ya Sabato, na hauruhusiwi kubeba godoro lako.”
The Jews therefore said to him that was healed: It is the sabbath; it is not lawful for thee to take up thy bed.
11 Akajibu, yeye aliyeniponya ndiye aliyeniambia, “Chukua godoro lako na uende.”
He answered them: He that made me whole, he said to me, Take up thy bed, and walk.
12 Wakauliza, “Ni nani aliyekuambia 'Chukua godoro lako na uende?'''
They asked him therefore: Who is that man who said to thee, Take up thy bed, and walk?
13 Ingawa, yule aliyeponywa hakumjua, kwa sababu Yesu alikuwa ameondoka kwa siri. Kwa kuwa kulikuwa na watu wengi katika sehemu hiyo.
But he who was healed, knew not who it was; for Jesus went aside from the multitude standing in the place.
14 Baada ya hapo Yesu alimkuta yule mtu hekaluni na akamwambia, “Tazama, umepona! “Usitende dhambi tena usije ukapatwa na jambo baya zaidi.”
Afterwards, Jesus findeth him in the temple, and saith to him: Behold thou art made whole: sin no more, lest some worse thing happen to thee.
15 Yule mtu akaenda na kuwataarifu Wayahudi kuwa Yesu ndiye aliyemponya.
The man went his way, and told the Jews, that it was Jesus who had made him whole.
16 Hivyo, kwa sababu ya mambo hayo Wayahudi walimtesa Yesu, kwa sababu alifanya mambo haya siku ya Sabato.
Therefore did the Jews persecute Jesus, because he did these things on the sabbath.
17 Yesu akawambia, “Baba yangu anafanya kazi hata sasa nami nafanya kazi.”
But Jesus answered them: My Father worketh until now; and I work.
18 Kwa sababu hiyo Wayahudi walizidi kumtafuta ili wamuue sio tu kwa sababu ya kuivunja Sabato, bali kwa kumwita Mungu Baba yake, akijifanya kuwa sawa na Mungu.
Hereupon therefore the Jews sought the more to kill him, because he did not only break the sabbath, but also said God was his Father, making himself equal to God.
19 Yesu akawajibu, “Amini, amini, Mwana hawezi kufanya kitu chochote isipokuwa kile ambacho amemwona Baba yake anakifanya, kwa kuwa chochote Baba akifanyacho ndicho na Mwana atakachofanya.
Then Jesus answered, and said to them: Amen, amen, I say unto you, the Son cannot do any thing of himself, but what he seeth the Father doing: for what things soever he doth, these the Son also doth in like manner.
20 Kwa kuwa Baba ampenda Mwana, na amwonyesha kila kitu anachokifanya na atamwonyesha mambo makubwa kuliko haya ili kwamba mzidi kushangaa.”
For the Father loveth the Son, and sheweth him all things which himself doth: and greater works than these will he shew him, that you may wonder.
21 Kwa kuwa kama vile ambavyo Baba awafufuavyo wafu na kuwapa uzima, halikadhalika Mwana pia humpa yeyote ampendaye.
For as the Father raiseth up the dead, and giveth life: so the Son also giveth life to whom he will.
22 Kwa kuwa Baba hamhukumu yeyote, bali amempa Mwana hukumu yote
For neither doth the Father judge any man, but hath given all judgment to the Son.
23 ili kwamba wote wamuheshimu Mwana kama vile Mwana anavyomuheshimu Baba. Yeye asiyemuheshimu Mwana hamuheshimu Baba aliyemtuma.
That all men may honour the Son, as they honour the Father. He who honoureth not the Son, honoureth not the Father, who hath sent him.
24 Amini, amini, yeye asikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenituma anao uzima wa milele na hatahukumiwa. Badala yake, amepita kutoka mautini na kuingia uzimani. (aiōnios )
Amen, amen I say unto you, that he who heareth my word, and believeth him that sent me, hath life everlasting; and cometh not into judgment, but is passed from death to life. (aiōnios )
25 Amini, amini, nawambia wakati unakuja na sasa upo ambao wafu watasikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wote watakao sikia wataishi.
Amen, amen I say unto you, that the hour cometh, and now is, when the dead shall hear the voice of the Son of God, and they that hear shall live.
26 Kwa kuwa kama vile Baba alivyo na uzima ndani yake mwenyewe,
For as the Father hath life in himself, so he hath given the Son also to have life in himself:
27 kadhalika amempa Mwana kuwa na uzima ndani yake, na Baba amempa Mwana mamlaka ili kwamba ahukumu kwa kuwa ni Mwana wa Adamu.
And he hath given him power to do judgment, because he is the Son of man.
28 Msishangazwe na hili, kwa kuwa wakati unakuja ambao wafu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake
Wonder not at this; for the hour cometh, wherein all that are in the graves shall hear the voice of the Son of God.
29 nao watatoka nje: kwa waliotenda mema kwa ufufuo wa uzima, na walio tenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu.
And they that have done good things, shall come forth unto the resurrection of life; but they that have done evil, unto the resurrection of judgment.
30 Siwezi kufanya kitu chochote kutoka kwangu mwenyewe. Kama nisikiavyo, ndivyo ninavyo hukumu na hukumu yangu ni ya haki kwa kuwa sitafuti mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenituma.
I cannot of myself do any thing. As I hear, so I judge: and my judgment is just; because I seek not my own will, but the will of him that sent me.
31 Kama nikijishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu usingelikuwa wa kweli.
If I bear witness of myself, my witness is not true.
32 Kuna mwingine anayeshuhudia kuhusu mimi na ninajua kwa hakika ushuhuda anaonishuhudia ni wa kweli.
There is another that beareth witness of me; and I know that the witness which he witnesseth of me is true.
33 Mmetuma kwa Yohana naye ameishuhudia kweli.
You sent to John, and he gave testimony to the truth.
34 Hatahivyo, ushuhuda ninaoupokea hautoki kwa mwanadamu. Ninayasema haya ili kwamba mweze kuokolewa.
But I receive not testimony from man: but I say these things, that you may be saved.
35 Yohana alikuwa ni taa iliyokuwa ikiwaka na kung'ara, na mlikuwa tayari kuifurahia kwa muda kitambo nuru yake.
He was a burning and a shining light: and you were willing for a time to rejoice in his light.
36 Ushuhuda nilionao ni mkuu kuliko ule wa Yohana, kwa kazi ambazo Baba amenipa kuzikamilisha, hizo kazi nizifanyazo zashuhudia kuwa Baba amenituma.
But I have a greater testimony than that of John: for the works which the Father hath given me to perfect; the works themselves, which I do, give testimony of me, that the Father hath sent me.
37 Baba aliyenituma yeye mwenyewe ameshuhudia kuhusu mimi. Hamjawahi kusikia sauti yake wala kuona umbo lake wakati wowote.
And the Father himself who hath sent me, hath given testimony of me: neither have you heard his voice at any time, nor seen his shape.
38 Hamna neno lake likikaa ndani yenu kwa kuwa hamumwamini yeye aliyetumwa.
And you have not his word abiding in you: for whom he hath sent, him you believe not.
39 Mnayachunguza maandiko mkidhani ndani yake mna uzima wa milele, na hayo maandiko yanashuhudia habari zangu na (aiōnios )
Search the scriptures, for you think in them to have life everlasting; and the same are they that give testimony of me. (aiōnios )
40 hamtaki kuja kwangu ili mpate uzima wa milele.
And you will not come to me that you may have life.
41 Sipokei sifa kutoka kwa watu,
I receive glory not from men.
42 lakini ninajua kuwa hamna upendo wa Mungu ndani yenu ninyi wenyewe.
But I know you, that you have not the love of God in you.
43 Nimekuja kwa jina la Baba yangu, hamukuweza kunipokea. Kama mwingine akija kwa jina lake mngempokea.
I am come in the name of my Father, and you receive me not: if another shall come in his own name, him you will receive.
44 Je mnawezaje kuamini ninyi ambao mnapokea sifa kutoka kwa kila mmoja wenu lakini hamtafuti sifa itokayo kwa Mungu wa pekee?
How can you believe, who receive glory one from another: and the glory which is from God alone, you do not seek?
45 Msidhani mimi nitawashitaki mbele za Baba. Anayewashitaki ninyi ni Musa, ambaye ninyi mmeweka matumaini yenu kwake.
Think not that I will accuse you to the Father. There is one that accuseth you, Moses, in whom you trust.
46 Kama mngekuwa mnamwamini Musa, mngeniamini mimi kwa sababu aliandika kuhusu habari zangu.
For if you did believe Moses, you would perhaps believe me also; for he wrote of me.
47 Kama hamuamini maandiko yake, mtawezaje kuamini maneno yangu?
But if you do not believe his writings, how will you believe my words?