< Yohana 4 >
1 Basi Yesu alipofahamu kuwa Mafarisayo wamesikia kuwa Yesu alikuwa anafuasa na kuwabatiza zaidi ya Yohana,
Quand le Seigneur eut appris que les pharisiens avaient entendu dire qu'il faisait et baptisait plus de disciples que Jean,
2 (ingawa Yesu mwenyewe alikuwa habatizi ila wanafunzi wake),
— toutefois ce n'était pas Jésus lui-même qui baptisait, mais c'étaient ses disciples, —
3 alitoka Judea na akaenda Galilaya.
il quitta la Judée et retourna en Galilée.
4 Hivyo ilikuwa muhimu kupitia Samaria.
Or, il fallait qu'il passât par la Samarie.
5 Na akafika kwenye mji wa Samaria, unaoitwa Sikari, karibu na eneo ambalo Yakobo alimpa mwanae Yusufu.
Il arriva donc à une ville de Samarie, nommée Sichar, près du champ que Jacob avait donné à Joseph, son fils.
6 Na kisima cha Yakobo kilikuwa hapo. Yesu alikuwa amechoka kwa ajili ya safari na akakaa karibu na kisima. Ilikuwa muda wa mchana.
Là se trouvait le puits de Jacob. Jésus, fatigué de la route, s'assit auprès du puits; c'était environ la sixième heure.
7 Mwanamke Msamaria alikuja kuteka maji, na Yesu akamwambia, “Nipe maji ninywe.”
Une femme samaritaine vint puiser de l'eau. Jésus lui dit: Donne-moi à boire.
8 Kwa sababu wanafunzi wake walikuwa wameenda zao mjini kununua chakula.
Car ses disciples étaient allés à la ville pour acheter des vivres.
9 Yule mwanamke akamwambia, “Inakuaje wewe Myahudi, kuniomba mimi mwanamke Msamaria, kitu cha kunywa?” Kwa sababu Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.
La femme samaritaine lui répondit: Comment, toi qui es Juif, me demandes-tu à boire, à moi qui suis une femme samaritaine? — Les Juifs, en effet, n'ont pas de relations avec les Samaritains. —
10 Yesu akamjibu, “Kama ungelijua karama ya Mungu, na yule anayekuambia 'Nipe maji, ' ungelimwomba, na angelikupa maji ya uzima.”
Jésus répondit et lui dit: Si tu connaissais le don de Dieu, et qui est celui qui te dit: Donne-moi à boire, — tu lui aurais demandé toi-même à boire, et il t'aurait donné une eau vive.
11 Mwanamke akajibu, “Bwana hauna ndoo ya kuchotea, na kisima ni kirefu. Utayapata wapi Maji ya Uzima?
La femme lui dit: Seigneur, tu n'as rien pour puiser, et le puits est profond; d'où aurais-tu donc cette eau vive?
12 Je wewe ni mkuu, kuliko baba yetu Yakobo, ambaye alitupa kisima hiki, na yeye mwenyewe na watoto wake pamoja na mifugo yake wakanywa maji ya kisima hiki?”
Es-tu plus grand que Jacob, notre père, qui nous a donné ce puits et qui en a bu lui-même, aussi bien que ses fils et ses troupeaux?
13 Yesu akajibu, “Yeyote anywae maji haya atapata kiu tena,
Jésus lui répondit: Quiconque boit de cette eau aura encore soif;
14 lakini yeye atakaye kunywa maji nitakayompa hatapata kiu tena. Badala yake maji nitakayompa yatakuwa chemchemi inayobubujika hata milele.” (aiōn , aiōnios )
mais celui qui boira de l'eau que je lui donnerai n'aura plus jamais soif. L'eau que je lui donnerai deviendra en lui une source d'eau qui jaillira jusque dans la vie éternelle. (aiōn , aiōnios )
15 Yule mwanamke akamwambia, “Bwana, nayaomba maji hayo ili nisipate kiu, na nisihangaike kuja hapa kuchota maji.”
La femme lui dit; Seigneur, donne-moi de cette eau, afin que je n'aie plus soif, et que je ne vienne plus ici pour puiser de l'eau.
16 Yesu akamwambia, “Nenda kamwite mumeo, kisha urudi.”
Jésus lui dit: Va, appelle ton mari, et reviens.
17 Mwanamke akamwambia, “Sina mume.” Yesu akajibu, “Umesema vyema, 'Sina mume;'
La femme répondit: Je n'ai point de mari. Jésus reprit: Tu as raison de dire: Je n'ai point de mari;
18 kwa maana umekuwa na wanaume watano, na mmoja ambaye unaye sasa sio mume wako. Katika hili umesema kweli!”
car tu as eu cinq maris, et celui que tu as maintenant n'est pas ton mari; en cela tu as dit vrai.
19 Mwanamke akamwambia, “Bwana naona yakuwa wewe ni nabii.
La femme lui dit: Seigneur, je vois que tu es un prophète!
20 Baba zetu waliabudu katika mlima huu. Lakini ninyi mwasema ya kuwa Yerusalemu ndiyo sehemu ambayo watu wanapaswa kuabudu.”
Nos pères ont adoré sur cette montagne; et vous dites, vous, que le lieu où il faut adorer est à Jérusalem.
21 Yesu akamjibu, “Mwanamke, niamini, wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba katika mlima huu au Yerusalemu.
Jésus lui répondit: Femme, crois-moi; l'heure vient où vous n'adorerez plus le Père ni sur cette montagne, ni à Jérusalem.
22 Ninyi watu mwaabudu kile msichokijua, lakini sisi twaabudu tunachokijua, kwa sababu wokovu watoka kwa Wayahudi.”
Vous adorez ce que vous ne connaissez pas. Nous, nous adorons ce que nous connaissons; car le salut vient des Juifs.
23 Hatahivyo, wakati unakuja, na sasa upo hapa, wakati waabuduo kweli watamwabudu Baba katika roho na kweli, kwa sababu Baba anawatafuta watu wa namna hiyo kuwa watu wake wanao mwabudu.
Mais l'heure vient, et elle est déjà venue, où les vrais adorateurs adoreront le Père en esprit et en vérité: ce sont là les adorateurs que le Père demande.
24 Mungu ni Roho, na wale wanaomwabudu wanapaswa kumwabudu kwa roho na kweli.”
Dieu est Esprit, et il faut que ceux qui l'adorent, l'adorent en esprit et en vérité.
25 Mwanamke akamwambia, “Ninajua kuwa Masihi anakuja, (aitwaye Kristo). Huyo atakapokuja atatwambia yote.”
La femme lui répondit: Je sais que le Messie — c'est-à-dire le Christ — doit venir; quand il sera venu, il nous annoncera toutes choses.
26 Yesu akamwambia, “Mimi unayesema nami ndiye.”
Jésus lui dit: Je le suis, moi qui te parle.
27 Wakati huo huo wanafunzi wake wakarudi. Nao walishangaa kwa nini alikuwa akizungumza na mwanamke, lakini hakuna aliyethubutu kumuuliza, “Unataka nini?” au “Kwa nini unazungumza naye?”
A ce moment, ses disciples arrivèrent, et ils furent surpris de ce qu'il parlait avec une femme. Pourtant, aucun d'eux ne lui dit: Que lui demandes-tu? ou: Pourquoi parles-tu avec elle?
28 Hivyo mwanamke akauacha mtungi wake na akaenda mjini na akawambia watu,
La femme laissa donc sa cruche et s'en alla à la ville; et elle dit aux gens de l'endroit:
29 “Njooni mwone mtu aliyeniambia mambo yangu yote niliyoyatenda, je yawezekana akawa ndiye Kristo?”
Venez voir un homme qui m'a dit tout ce que j'ai fait: ne serait-ce pas le Christ?
30 Wakatoka mjini wakaja kwake.
Alors ils sortirent de la ville et allèrent vers Jésus.
31 Wakati wa mchana wanafunzi wake walimsihi wakisema, “Rabi kula chakula.”
Cependant les disciples insistaient auprès de lui, en disant: Maître, mange.
32 lakini yeye aliwambia, “Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.”
Il leur répondit: J'ai pour me nourrir un aliment que vous ne connaissez pas.
33 Wanafunzi wakaambizana, hakuna aliyemletea kitu chochotekula,”Je walileta?”
Les disciples se disaient donc l'un à l'autre: Quelqu'un lui aurait-il apporté à manger?
34 Yesu akawambia, “Chakula changu ni kufanya mapenzi yake yeye aliyenituma na kutimiza kazi yake.
Jésus leur dit: Ma nourriture est de faire la volonté de celui qui m'a envoyé, et d'accomplir son oeuvre.
35 Je, hamsemi, 'Bado miezi mitano na mavuno yatakuwa tayari?' Ninawambieni tazameni mashamba yalivyo tayari kwa mavuno!
Ne dites-vous pas qu'il y a encore quatre mois jusqu'à la moisson? Mais moi, je vous dis: Levez les yeux et regardez les campagnes, déjà blanches pour la moisson.
36 Yeye avunaye hupokea mishahara na kukusanya matunda kwa ajili ya uzima wa milele, ili kwamba yeye apandaye naye avunaye wafurahi pamoja. (aiōnios )
Déjà le moissonneur reçoit son salaire et amasse du fruit pour la vie éternelle, afin que le semeur et le moissonneur en aient ensemble de la joie. (aiōnios )
37 Kwa kuwa msemo huu ni wa kweli, 'Mmoja apanda na mwingine avuna.'
Car c'est ici qu'on peut dire en toute vérité: Autre est le semeur, autre le moissonneur.
38 Niliwatuma kuvuna ambacho hamkukihangaikia, Wengine wamefanya kazi na ninyi mmeingia katika furaha ya kazi yao.”
Je vous ai envoyés moissonner où vous n'aviez pas travaillé; d'autres ont travaillé, et vous, vous êtes entrés dans leur travail.
39 Wasamaria wengi katika mji ule walimwani kwa sababu ya taarifa ya yule mwanamke aliyekuwa akishuhudia, “Aliyeniambia mambo yote niliyoyafanya.”
Plusieurs des Samaritains de cette ville crurent en lui, à cause de la parole de la femme qui lui avait rendu ce témoignage: Il m'a dit tout ce que j'ai fait.
40 Hivyo Wasamaria walipokuja walimsihi akae pamoja nao na akakaa kwao kwa siku mbili.
Les Samaritains, étant donc venus vers lui, le prièrent de demeurer chez eux; et il y demeura deux jours.
41 Na wengi zaidi wakamwamini kwa sababu ya neno lake.
Il y en eut beaucoup plus qui crurent en lui après avoir entendu sa parole.
42 Wakamwambia yule mwanamke, “Tunaamini sio tu kwa maneno yako, kwa sababu sisi wenyewe tumesikia, na sasa twafahamu kuwa hakika yeye ni mwokozi wa ulimwengu.”
Et ils disaient à la femme: Ce n'est plus à cause de ce que tu nous as dit, que nous croyons; car nous l'avons entendu nous-mêmes, et nous savons que c'est lui qui est véritablement le Sauveur du monde.
43 Baada ya siku hizo mbili, akaondoka na kuelekea Galilaya.
Après ces deux jours, Jésus partit de là et s'en alla en Galilée;
44 Kwa sababu yeye mwenyewe alikuwa ametangaza kuwa nabii hana heshima katika nchi yake mwenyewe.
— car il avait déclaré lui-même qu'un prophète n'est point honoré dans sa patrie. —
45 Alipokuja kutoka Galilaya, Wagalilaya walimkaribisha. Walikuwa wameona mambo yote aliyoyafanya Yerusalemu kwenye sikukuu, kwa sababu na wao pia walikuwa wamehudhuria kwenye sikukuu.
Lorsqu'il fut arrivé en Galilée, il fut bien reçu des Galiléens qui avaient vu tout ce qu'il avait fait à Jérusalem pendant la fête; car ils étaient allés, eux aussi, à la fête.
46 Alikuja tena Kana ya Galilaya huko alikoyabadilisha maji kuwa divai. Palikuwa na ofisa ambaye mwana wake alikuwa ni mgonjwa huko Kapernaumu.
Il vint donc de nouveau à Cana en Galilée, où il avait changé l'eau en vin. Or, il y avait à Capernaüm un officier royal, dont le fils était malade.
47 Aliposikia kuwa Yesu alitoka Judea na kwenda Galilaya, alienda kwa Yesu na kumsihi atelemke amponye mwanawe, ambaye alikuwa karibu kufa.
Cet officier, ayant appris que Jésus était venu de Judée en Galilée, alla le trouver et le pria de descendre pour guérir son fils, qui était mourant.
48 Ndipo Yesu akamwambia, “Ninyi msipoona ishara na maajabu hamwezi kuamini.
Jésus lui dit: Si vous ne voyez des miracles et des prodiges, vous ne croyez pas!
49 Kiongozi akasema, “Bwana shuka chini kabla mwanangu hajafa.”
L'officier royal lui répondit: Seigneur, descends, avant que mon enfant ne meure!
50 Yesu akamwambia, “Nenda mwanao ni mzima.” Yule mtu akaamini neno alilolisema Yesu na akaenda zake.
Jésus lui dit: Va, ton fils vit! Cet homme crut à la parole que Jésus lui avait dite, et il s'en alla.
51 Alipokuwa akishuka, watumishi wake walimpokea na kumwambia mwana wake alikuwa mzima.
Comme il était déjà en route, ses serviteurs vinrent à sa rencontre et lui dirent: Ton fils vit.
52 Hivyo akawauliza ni muda gani alipata nafuu. Wakajibu, “Jana muda wa saa saba homa ilipomwacha.”
Il leur demanda à quelle heure il s'était trouvé mieux. Ils lui répondirent: Hier, à la septième heure, la fièvre l'a quitté.
53 Ndipo baba yake akatambua kuwa ni muda ule ule Yesu aliosema, “Mwana wako ni mzima.” Hivyo yeye na familia yake wakaamini.
Le père reconnut que c'était à cette heure-là que Jésus lui avait dit: Ton fils vit. Et il crut, lui et toute sa maison.
54 Hii ilikuwa ni ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipotoka Yudea kwenda Galilaya.
Ce nouveau miracle fut le second que fit Jésus, à son retour de Judée en Gahlée.