< Yohana 4 >
1 Basi Yesu alipofahamu kuwa Mafarisayo wamesikia kuwa Yesu alikuwa anafuasa na kuwabatiza zaidi ya Yohana,
When therefore the Lord knew how the Pharisees had heard that Jesus made and baptized more disciples than John,
2 (ingawa Yesu mwenyewe alikuwa habatizi ila wanafunzi wake),
( Though Jesus himself baptized not, but his disciples, )
3 alitoka Judea na akaenda Galilaya.
He left Judæa, and departed again into Galilee.
4 Hivyo ilikuwa muhimu kupitia Samaria.
And he must needs go through Samaria.
5 Na akafika kwenye mji wa Samaria, unaoitwa Sikari, karibu na eneo ambalo Yakobo alimpa mwanae Yusufu.
Then cometh he to a city of Samaria, which is called Sychar, near to the parcel of ground that Jacob gave to his son Joseph.
6 Na kisima cha Yakobo kilikuwa hapo. Yesu alikuwa amechoka kwa ajili ya safari na akakaa karibu na kisima. Ilikuwa muda wa mchana.
Now Jacob’s well was there. Jesus therefore, being wearied with his journey, sat thus on the well: and it was about the sixth hour.
7 Mwanamke Msamaria alikuja kuteka maji, na Yesu akamwambia, “Nipe maji ninywe.”
There cometh a woman of Samaria to draw water: Jesus saith unto her, Give me to drink.
8 Kwa sababu wanafunzi wake walikuwa wameenda zao mjini kununua chakula.
( For his disciples were gone away unto the city to buy meat.)
9 Yule mwanamke akamwambia, “Inakuaje wewe Myahudi, kuniomba mimi mwanamke Msamaria, kitu cha kunywa?” Kwa sababu Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.
Then saith the woman of Samaria unto him, How is it that thou, being a Jew, askest drink of me, which am a woman of Samaria? for the Jews have no dealings with the Samaritans.
10 Yesu akamjibu, “Kama ungelijua karama ya Mungu, na yule anayekuambia 'Nipe maji, ' ungelimwomba, na angelikupa maji ya uzima.”
Jesus answered and said unto her, If thou knewest the gift of God, and who it is that saith to thee, Give me to drink; thou wouldest have asked of him, and he would have given thee living water.
11 Mwanamke akajibu, “Bwana hauna ndoo ya kuchotea, na kisima ni kirefu. Utayapata wapi Maji ya Uzima?
The woman saith unto him, Sir, thou hast nothing to draw with, and the well is deep: from whence then hast thou that living water?
12 Je wewe ni mkuu, kuliko baba yetu Yakobo, ambaye alitupa kisima hiki, na yeye mwenyewe na watoto wake pamoja na mifugo yake wakanywa maji ya kisima hiki?”
Art thou greater than our father Jacob, which gave us the well, and drank thereof himself, and his children, and his cattle?
13 Yesu akajibu, “Yeyote anywae maji haya atapata kiu tena,
Jesus answered and said unto her, Whosoever drinketh of this water shall thirst again:
14 lakini yeye atakaye kunywa maji nitakayompa hatapata kiu tena. Badala yake maji nitakayompa yatakuwa chemchemi inayobubujika hata milele.” (aiōn , aiōnios )
But whosoever drinketh of the water that I shall give him shall never thirst; but the water that I shall give him shall be in him a well of water springing up into everlasting life. (aiōn , aiōnios )
15 Yule mwanamke akamwambia, “Bwana, nayaomba maji hayo ili nisipate kiu, na nisihangaike kuja hapa kuchota maji.”
The woman saith unto him, Sir, give me this water, that I thirst not, neither come hither to draw.
16 Yesu akamwambia, “Nenda kamwite mumeo, kisha urudi.”
Jesus saith unto her, Go, call thy husband, and come hither.
17 Mwanamke akamwambia, “Sina mume.” Yesu akajibu, “Umesema vyema, 'Sina mume;'
The woman answered and said, I have no husband. Jesus said unto her, Thou hast well said, I have no husband:
18 kwa maana umekuwa na wanaume watano, na mmoja ambaye unaye sasa sio mume wako. Katika hili umesema kweli!”
For thou hast had five husbands; and he whom thou now hast is not thy husband: in that saidst thou truly.
19 Mwanamke akamwambia, “Bwana naona yakuwa wewe ni nabii.
The woman saith unto him, Sir, I perceive that thou art a prophet.
20 Baba zetu waliabudu katika mlima huu. Lakini ninyi mwasema ya kuwa Yerusalemu ndiyo sehemu ambayo watu wanapaswa kuabudu.”
Our fathers worshipped in this mountain; and ye say, that in Jerusalem is the place where men ought to worship.
21 Yesu akamjibu, “Mwanamke, niamini, wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba katika mlima huu au Yerusalemu.
Jesus saith unto her, Woman, believe me, the hour cometh, when ye shall neither in this mountain, nor yet at Jerusalem, worship the Father.
22 Ninyi watu mwaabudu kile msichokijua, lakini sisi twaabudu tunachokijua, kwa sababu wokovu watoka kwa Wayahudi.”
Ye worship ye know not what: we know what we worship: for salvation is of the Jews.
23 Hatahivyo, wakati unakuja, na sasa upo hapa, wakati waabuduo kweli watamwabudu Baba katika roho na kweli, kwa sababu Baba anawatafuta watu wa namna hiyo kuwa watu wake wanao mwabudu.
But the hour cometh, and now is, when the true worshippers shall worship the Father in spirit and in truth: for the Father seeketh such to worship him.
24 Mungu ni Roho, na wale wanaomwabudu wanapaswa kumwabudu kwa roho na kweli.”
God is a Spirit: and they that worship him must worship him in spirit and in truth.
25 Mwanamke akamwambia, “Ninajua kuwa Masihi anakuja, (aitwaye Kristo). Huyo atakapokuja atatwambia yote.”
The woman saith unto him, I know that Messiah cometh, which is called Christ: when he is come, he will tell us all things.
26 Yesu akamwambia, “Mimi unayesema nami ndiye.”
Jesus saith unto her, I that speak unto thee am he.
27 Wakati huo huo wanafunzi wake wakarudi. Nao walishangaa kwa nini alikuwa akizungumza na mwanamke, lakini hakuna aliyethubutu kumuuliza, “Unataka nini?” au “Kwa nini unazungumza naye?”
And upon this came his disciples, and marvelled that he talked with the woman: yet no man said, What seekest thou? or, Why talkest thou with her?
28 Hivyo mwanamke akauacha mtungi wake na akaenda mjini na akawambia watu,
The woman then left her waterpot, and went her way into the city, and saith to the men,
29 “Njooni mwone mtu aliyeniambia mambo yangu yote niliyoyatenda, je yawezekana akawa ndiye Kristo?”
Come, see a man, which told me all things that ever I did: is not this the Christ?
30 Wakatoka mjini wakaja kwake.
Then they went out of the city, and came unto him.
31 Wakati wa mchana wanafunzi wake walimsihi wakisema, “Rabi kula chakula.”
In the mean while his disciples prayed him, saying, Master, eat.
32 lakini yeye aliwambia, “Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.”
But he said unto them, I have meat to eat that ye know not of.
33 Wanafunzi wakaambizana, hakuna aliyemletea kitu chochotekula,”Je walileta?”
Therefore said the disciples one to another, Hath any man brought him ought to eat?
34 Yesu akawambia, “Chakula changu ni kufanya mapenzi yake yeye aliyenituma na kutimiza kazi yake.
Jesus saith unto them, My meat is to do the will of him that sent me, and to finish his work.
35 Je, hamsemi, 'Bado miezi mitano na mavuno yatakuwa tayari?' Ninawambieni tazameni mashamba yalivyo tayari kwa mavuno!
Say not ye, There are yet four months, and then cometh harvest? behold, I say unto you, Lift up your eyes, and look on the fields; for they are white already to harvest.
36 Yeye avunaye hupokea mishahara na kukusanya matunda kwa ajili ya uzima wa milele, ili kwamba yeye apandaye naye avunaye wafurahi pamoja. (aiōnios )
And he that reapeth receiveth wages, and gathereth fruit unto life eternal: that both he that soweth and he that reapeth may rejoice together. (aiōnios )
37 Kwa kuwa msemo huu ni wa kweli, 'Mmoja apanda na mwingine avuna.'
And herein is that saying true, One soweth, and another reapeth.
38 Niliwatuma kuvuna ambacho hamkukihangaikia, Wengine wamefanya kazi na ninyi mmeingia katika furaha ya kazi yao.”
I sent you to reap that whereon ye bestowed no labour: other men laboured, and ye are entered into their labours.
39 Wasamaria wengi katika mji ule walimwani kwa sababu ya taarifa ya yule mwanamke aliyekuwa akishuhudia, “Aliyeniambia mambo yote niliyoyafanya.”
And many of the Samaritans of that city believed on him for the saying of the woman, which testified, He told me all that ever I did.
40 Hivyo Wasamaria walipokuja walimsihi akae pamoja nao na akakaa kwao kwa siku mbili.
So when the Samaritans were come unto him, they besought him that he would tarry with them: and he abode there two days.
41 Na wengi zaidi wakamwamini kwa sababu ya neno lake.
And many more believed because of his own word;
42 Wakamwambia yule mwanamke, “Tunaamini sio tu kwa maneno yako, kwa sababu sisi wenyewe tumesikia, na sasa twafahamu kuwa hakika yeye ni mwokozi wa ulimwengu.”
And said unto the woman, Now we believe, not because of thy saying: for we have heard him ourselves, and know that this is indeed the Christ, the Saviour of the world.
43 Baada ya siku hizo mbili, akaondoka na kuelekea Galilaya.
Now after two days he departed thence, and went into Galilee.
44 Kwa sababu yeye mwenyewe alikuwa ametangaza kuwa nabii hana heshima katika nchi yake mwenyewe.
For Jesus himself testified, that a prophet hath no honour in his own country.
45 Alipokuja kutoka Galilaya, Wagalilaya walimkaribisha. Walikuwa wameona mambo yote aliyoyafanya Yerusalemu kwenye sikukuu, kwa sababu na wao pia walikuwa wamehudhuria kwenye sikukuu.
Then when he was come into Galilee, the Galilæans received him, having seen all the things that he did at Jerusalem at the feast: for they also went unto the feast.
46 Alikuja tena Kana ya Galilaya huko alikoyabadilisha maji kuwa divai. Palikuwa na ofisa ambaye mwana wake alikuwa ni mgonjwa huko Kapernaumu.
So Jesus came again into Cana of Galilee, where he made the water wine. And there was a certain nobleman, whose son was sick at Capernaum.
47 Aliposikia kuwa Yesu alitoka Judea na kwenda Galilaya, alienda kwa Yesu na kumsihi atelemke amponye mwanawe, ambaye alikuwa karibu kufa.
When he heard that Jesus was come out of Judæa into Galilee, he went unto him, and besought him that he would come down, and heal his son: for he was at the point of death.
48 Ndipo Yesu akamwambia, “Ninyi msipoona ishara na maajabu hamwezi kuamini.
Then said Jesus unto him, Except ye see signs and wonders, ye will not believe.
49 Kiongozi akasema, “Bwana shuka chini kabla mwanangu hajafa.”
The nobleman saith unto him, Sir, come down ere my child die.
50 Yesu akamwambia, “Nenda mwanao ni mzima.” Yule mtu akaamini neno alilolisema Yesu na akaenda zake.
Jesus saith unto him, Go thy way; thy son liveth. And the man believed the word that Jesus had spoken unto him, and he went his way.
51 Alipokuwa akishuka, watumishi wake walimpokea na kumwambia mwana wake alikuwa mzima.
And as he was now going down, his servants met him, and told him, saying, Thy son liveth.
52 Hivyo akawauliza ni muda gani alipata nafuu. Wakajibu, “Jana muda wa saa saba homa ilipomwacha.”
Then enquired he of them the hour when he began to amend. And they said unto him, Yesterday at the seventh hour the fever left him.
53 Ndipo baba yake akatambua kuwa ni muda ule ule Yesu aliosema, “Mwana wako ni mzima.” Hivyo yeye na familia yake wakaamini.
So the father knew that it was at the same hour, in the which Jesus said unto him, Thy son liveth: and himself believed, and his whole house.
54 Hii ilikuwa ni ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipotoka Yudea kwenda Galilaya.
This is again the second miracle that Jesus did, when he was come out of Judæa into Galilee.