< Yohana 3 >

1 Basi kulikuwa na Farisayo ambaye jina lake Nikodemo, mmoja wa wajumbe wa baraza la Wayahudi.
And there was a man of the Pharisees, Nicodemus his name, a ruler of the Jews,
2 Mtu huyu alimwendea Bwana Yesu usiku na akamwambia, “Rabi, tunajua ya kuwa u mwalimu kutoka kwa Mungu, kwa maana hakuna mtu awezaye kutenda ishara hizi zote Mungu asipokuwa pamoja naye.”
this one came unto him by night, and said to him, 'Rabbi, we have known that from God thou hast come — a teacher, for no one these signs is able to do that thou dost, if God may not be with him.'
3 Yesu akamjibu, “Amini, amini, mtu hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu asipozaliwa mara ya pili.”
Jesus answered and said to him, 'Verily, verily, I say to thee, If any one may not be born from above, he is not able to see the reign of God;'
4 Nikodemo akasema,” Mtu anawezaje kuzaliwa akiwa mzee? Hawezi kuingia tumboni mwa mama yake mara ya pili na kuzaliwa, je anaweza?”
Nicodemus saith unto him, 'How is a man able to be born, being old? is he able into the womb of his mother a second time to enter, and to be born?'
5 Yesu akajibu, “Amini, amini mtu sipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu.
Jesus answered, 'Verily, verily, I say to thee, If any one may not be born of water, and the Spirit, he is not able to enter into the reign of God;
6 Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili, na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.
that which hath been born of the flesh is flesh, and that which hath been born of the Spirit is spirit.
7 Usishangae kwa sababu nilikuwambia, 'ni lazima kuzaliwa mara ya pili.'
'Thou mayest not wonder that I said to thee, It behoveth you to be born from above;
8 Upepo huvuma popote upendapo na sauti yake mwaisikia, lakini hamjui utokako wala uendako. Ndivyo ilivyo hali ya kila aliyezaliwa na roho.
the Spirit where he willeth doth blow, and his voice thou dost hear, but thou hast not known whence he cometh, and whither he goeth; thus is every one who hath been born of the Spirit.'
9 Nikodemo akajibu, kwa kusema, “Mambo haya yawezekanaje?”
Nicodemus answered and said to him, 'How are these things able to happen?'
10 Yesu akamjibu, “Wewe u mwalimu wa Israeli, hata hauyajui mambo haya?
Jesus answered and said to him, 'Thou art the teacher of Israel — and these things thou dost not know!
11 Amini, amini, nakuambia, kile tunachokifahamu twakishuhudia kwa kile tulichokiona. Lakini hampokei ushuhuda wetu.
'Verily, verily, I say to thee — What we have known we speak, and what we have seen we testify, and our testimony ye do not receive;
12 Kama nimewambia mambo ya hapa duniani na hamuamini, mtawezaje kuamini kama nikiwambia mambo ya mbinguni?
if the earthly things I said to you, and ye do not believe, how, if I shall say to you the heavenly things, will ye believe?
13 Maana hakuna aliyepanda juu kutoka mbinguni isipokuwa yeye aliyeshuka, Mwana wa Adamu.
and no one hath gone up to the heaven, except he who out of the heaven came down — the Son of Man who is in the heaven.
14 Kama vile Musa alivyomwinua nyoka jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu lazima ainuliwe,
'And as Moses did lift up the serpent in the wilderness, so it behoveth the Son of Man to be lifted up,
15 ili kwamba wote watakaomwamini wapate uzima wa milele. (aiōnios g166)
that every one who is believing in him may not perish, but may have life age-during, (aiōnios g166)
16 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, kwamba akamtoa mwanae wa pekee, ili kwamba mtu yeyote amwaminiye asiangamie bali awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
for God did so love the world, that His Son — the only begotten — He gave, that every one who is believing in him may not perish, but may have life age-during. (aiōnios g166)
17 Kwa sababu Mungu hakumtuma mwanae duniani ili auhukumu ulimwengu, bali kwamba ulimwengu uokolewe katika yeye.
For God did not send His Son to the world that he may judge the world, but that the world may be saved through him;
18 Amwaminiye Yeye hatahukumiwa. Yeye asiyemwamini tayari ameshahukumiwa kwa sababu hajaliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.
he who is believing in him is not judged, but he who is not believing hath been judged already, because he hath not believed in the name of the only begotten Son of God.
19 Hii ndiyo sababu ya hukumu, ya kwamba nuru imekuja ulimwenguni, lakini wanadamu wakapenda giza zaidi ya nuru kwa sababu matendo yao yalikuwa maovu.
'And this is the judgment, that the light hath come to the world, and men did love the darkness rather than the light, for their works were evil;
20 kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru wala haji nuruni ili matendo yake yasije yakawekwa wazi.
for every one who is doing wicked things hateth the light, and doth not come unto the light, that his works may not be detected;
21 Lakini, yeye atendaye kweli huja kwenye nuru ili matendo yake yaonekane kwamba yametendwa kwa utiifu wa Mungu.
but he who is doing the truth doth come to the light, that his works may be manifested, that in God they are having been wrought.'
22 Baada ya haya, Yesu pamoja na wanafunzi walienda katika nchi ya Yudea. Huko alitumia muda pamoja nao na alikuwa akibatiza.
After these things came Jesus and his disciples to the land of Judea, and there he did tarry with them, and was baptizing;
23 Sasa Yohana pia alikuwa akibatiza huko Ainea karibu na Salim maana kulikuwa na maji mengi pale. Watu walikuwa wakija kwake na kubatizwa,
and John was also baptizing in Aenon, nigh to Salem, because there were many waters there, and they were coming and were being baptized —
24 kwa kuwa Yohana alikuwa hajatupwa gerezani.
for John was not yet cast into the prison —
25 Kisha palitokea mabishano kati ya wanafunzi wa Yohana na Myahudi kuhusu sikukuuu za utakaso.
there arose then a question from the disciples of John with [some] Jews about purifying,
26 Wakaenda kwa Yohana wakamwambia, “Rabi, yeye uliyekuwa naye ng'ambo ya Mto Yorodani, yeye uliyeshuhudia habari zake, tazama, anabatiza na wote wanaenda wanamfuata.”
and they came unto John, and said to him, 'Rabbi, he who was with thee beyond the Jordan, to whom thou didst testify, lo, this one is baptizing, and all are coming unto him.'
27 Yohana akajibu mtu hawezi kupokea kitu chochote isipokuwa kama amepewa kutoka mbinguni.
John answered and said, 'A man is not able to receive anything, if it may not have been given him from the heaven;
28 Ninyi wenyewe mwashuhudia kuwa nalisema kuwa, 'mimi sio Kristo', badala yake nilisema, 'nimetumwa mbele yake.'
ye yourselves do testify to me that I said, I am not the Christ, but, that I am having been sent before him;
29 Yeye aliye na bibi arusi ni bwana harusi. Sasa rafiki wa bwana arusi, asimamaye na kusikiliza hufurahia sana kwa sababu ya sauti ya bwana arusi. Hii sasa ni furaha yangu iliyotimilika.
he who is having the bride is bridegroom, and the friend of the bridegroom, who is standing and hearing him, with joy doth rejoice because of the voice of the bridegroom; this, then, my joy hath been fulfilled.
30 Anapaswa kuzidi, nami napaswa kupungua.
'Him it behoveth to increase, and me to become less;
31 Yeye atokaye juu, yu juu ya yote. Yeye aliye wa ulimwengu anatoka ulimwenguni na huongea mambo ya ki ulimwengu. Yeye atokaye mbinguni yuko juu ya yote.
he who from above is coming is above all; he who is from the earth, from the earth he is, and from the earth he speaketh; he who from the heaven is coming is above all.
32 Yeye hushuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna apokeaye ushuhuda wake.
'And what he hath seen and heard this he doth testify, and his testimony none receiveth;
33 Yeye aliye pokea ushuhuda wake amehakikisha kuwa Mungu ni mkweli.
he who is receiving his testimony did seal that God is true;
34 Kwa sababu yeye aliyetumwa na Mungu huongea maneno ya Mungu. Kwa kuwa hampi Roho kwa kipimo.
for he whom God sent, the sayings of God he speaketh; for not by measure doth God give the Spirit;
35 Baba humpenda Mwana na amempa vitu vyote mikononi mwake.
the Father doth love the Son, and all things hath given into his hand;
36 Yeye amwaminiye Mwana anao uzima wa milele, lakini kwa yeye asiye mtii Mwana hatauona uzima, bali ghadhabu ya Mungu hushikamana juu yake. (aiōnios g166)
he who is believing in the Son, hath life age-during; and he who is not believing the Son, shall not see life, but the wrath of God doth remain upon him.' (aiōnios g166)

< Yohana 3 >