< Yohana 3 >
1 Basi kulikuwa na Farisayo ambaye jina lake Nikodemo, mmoja wa wajumbe wa baraza la Wayahudi.
Now there was a man of the Pharisees, named Nicodemus, a ruler of the Jews:
2 Mtu huyu alimwendea Bwana Yesu usiku na akamwambia, “Rabi, tunajua ya kuwa u mwalimu kutoka kwa Mungu, kwa maana hakuna mtu awezaye kutenda ishara hizi zote Mungu asipokuwa pamoja naye.”
The same came unto him by night, and said to him, Rabbi, we know that thou art a teacher come from God: for no man can do these signs that thou doest, except God be with him.
3 Yesu akamjibu, “Amini, amini, mtu hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu asipozaliwa mara ya pili.”
Jesus answered and said unto him, Verily, verily, I say unto thee, Except a man be born anew, he cannot see the kingdom of God.
4 Nikodemo akasema,” Mtu anawezaje kuzaliwa akiwa mzee? Hawezi kuingia tumboni mwa mama yake mara ya pili na kuzaliwa, je anaweza?”
Nicodemus saith unto him, How can a man be born when he is old? can he enter a second time into his mother’s womb, and be born?
5 Yesu akajibu, “Amini, amini mtu sipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu.
Jesus answered, Verily, verily, I say unto thee, Except a man be born of water and the Spirit, he cannot enter into the kingdom of God.
6 Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili, na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.
That which is born of the flesh is flesh; and that which is born of the Spirit is spirit.
7 Usishangae kwa sababu nilikuwambia, 'ni lazima kuzaliwa mara ya pili.'
Marvel not that I said unto thee, Ye must be born anew.
8 Upepo huvuma popote upendapo na sauti yake mwaisikia, lakini hamjui utokako wala uendako. Ndivyo ilivyo hali ya kila aliyezaliwa na roho.
The wind bloweth where it listeth, and thou hearest the voice thereof, but knowest not whence it cometh, and whither it goeth: so is every one that is born of the Spirit.
9 Nikodemo akajibu, kwa kusema, “Mambo haya yawezekanaje?”
Nicodemus answered and said unto him, How can these things be?
10 Yesu akamjibu, “Wewe u mwalimu wa Israeli, hata hauyajui mambo haya?
Jesus answered and said unto him, Art thou the teacher of Israel, and understandest not these things?
11 Amini, amini, nakuambia, kile tunachokifahamu twakishuhudia kwa kile tulichokiona. Lakini hampokei ushuhuda wetu.
Verily, verily, I say unto thee, We speak that we do know, and bear witness of that we have seen; and ye receive not our witness.
12 Kama nimewambia mambo ya hapa duniani na hamuamini, mtawezaje kuamini kama nikiwambia mambo ya mbinguni?
If I told you earthly things, and ye believe not, how shall ye believe, if I tell you heavenly things?
13 Maana hakuna aliyepanda juu kutoka mbinguni isipokuwa yeye aliyeshuka, Mwana wa Adamu.
And no man hath ascended into heaven, but he that descended out of heaven, [even] the Son of man, which is in heaven.
14 Kama vile Musa alivyomwinua nyoka jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu lazima ainuliwe,
And as Moses lifted up the serpent in the wilderness, even so must the Son of man be lifted up:
15 ili kwamba wote watakaomwamini wapate uzima wa milele. (aiōnios )
that whosoever believeth may in him have eternal life. (aiōnios )
16 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, kwamba akamtoa mwanae wa pekee, ili kwamba mtu yeyote amwaminiye asiangamie bali awe na uzima wa milele. (aiōnios )
For God so loved the world, that he gave his only begotten Son, that whosoever believeth on him should not perish, but have eternal life. (aiōnios )
17 Kwa sababu Mungu hakumtuma mwanae duniani ili auhukumu ulimwengu, bali kwamba ulimwengu uokolewe katika yeye.
For God sent not the Son into the world to judge the world; but that the world should be saved through him.
18 Amwaminiye Yeye hatahukumiwa. Yeye asiyemwamini tayari ameshahukumiwa kwa sababu hajaliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.
He that believeth on him is not judged: he that believeth not hath been judged already, because he hath not believed on the name of the only begotten Son of God.
19 Hii ndiyo sababu ya hukumu, ya kwamba nuru imekuja ulimwenguni, lakini wanadamu wakapenda giza zaidi ya nuru kwa sababu matendo yao yalikuwa maovu.
And this is the judgment, that the light is come into the world, and men loved the darkness rather than the light; for their works were evil.
20 kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru wala haji nuruni ili matendo yake yasije yakawekwa wazi.
For every one that doeth ill hateth the light, and cometh not to the light, lest his works should be reproved.
21 Lakini, yeye atendaye kweli huja kwenye nuru ili matendo yake yaonekane kwamba yametendwa kwa utiifu wa Mungu.
But he that doeth the truth cometh to the light, that his works may be made manifest, that they have been wrought in God.
22 Baada ya haya, Yesu pamoja na wanafunzi walienda katika nchi ya Yudea. Huko alitumia muda pamoja nao na alikuwa akibatiza.
After these things came Jesus and his disciples into the land of Judaea; and there he tarried with them, and baptized.
23 Sasa Yohana pia alikuwa akibatiza huko Ainea karibu na Salim maana kulikuwa na maji mengi pale. Watu walikuwa wakija kwake na kubatizwa,
And John also was baptizing in AEnon near to Salim, because there was much water there: and they came, and were baptized.
24 kwa kuwa Yohana alikuwa hajatupwa gerezani.
For John was not yet cast into prison.
25 Kisha palitokea mabishano kati ya wanafunzi wa Yohana na Myahudi kuhusu sikukuuu za utakaso.
There arose therefore a questioning on the part of John’s disciples with a Jew about purifying.
26 Wakaenda kwa Yohana wakamwambia, “Rabi, yeye uliyekuwa naye ng'ambo ya Mto Yorodani, yeye uliyeshuhudia habari zake, tazama, anabatiza na wote wanaenda wanamfuata.”
And they came unto John, and said to him, Rabbi, he that was with thee beyond Jordan, to whom thou hast borne witness, behold, the same baptizeth, and all men come to him.
27 Yohana akajibu mtu hawezi kupokea kitu chochote isipokuwa kama amepewa kutoka mbinguni.
John answered and said, A man can receive nothing, except it have been given him from heaven.
28 Ninyi wenyewe mwashuhudia kuwa nalisema kuwa, 'mimi sio Kristo', badala yake nilisema, 'nimetumwa mbele yake.'
Ye yourselves bear me witness, that I said, I am not the Christ, but, that I am sent before him.
29 Yeye aliye na bibi arusi ni bwana harusi. Sasa rafiki wa bwana arusi, asimamaye na kusikiliza hufurahia sana kwa sababu ya sauti ya bwana arusi. Hii sasa ni furaha yangu iliyotimilika.
He that hath the bride is the bridegroom: but the friend of the bridegroom, which standeth and heareth him, rejoiceth greatly because of the bridegroom’s voice: this my joy therefore is fulfilled.
30 Anapaswa kuzidi, nami napaswa kupungua.
He must increase, but I must decrease.
31 Yeye atokaye juu, yu juu ya yote. Yeye aliye wa ulimwengu anatoka ulimwenguni na huongea mambo ya ki ulimwengu. Yeye atokaye mbinguni yuko juu ya yote.
He that cometh from above is above all: he that is of the earth is of the earth, and of the earth he speaketh: he that cometh from heaven is above all.
32 Yeye hushuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna apokeaye ushuhuda wake.
What he hath seen and heard, of that he beareth witness; and no man receiveth his witness.
33 Yeye aliye pokea ushuhuda wake amehakikisha kuwa Mungu ni mkweli.
He that hath received his witness hath set his seal to [this], that God is true.
34 Kwa sababu yeye aliyetumwa na Mungu huongea maneno ya Mungu. Kwa kuwa hampi Roho kwa kipimo.
For he whom God hath sent speaketh the words of God: for he giveth not the Spirit by measure.
35 Baba humpenda Mwana na amempa vitu vyote mikononi mwake.
The Father loveth the Son, and hath given all things into his hand.
36 Yeye amwaminiye Mwana anao uzima wa milele, lakini kwa yeye asiye mtii Mwana hatauona uzima, bali ghadhabu ya Mungu hushikamana juu yake. (aiōnios )
He that believeth on the Son hath eternal life; but he that obeyeth not the Son shall not see life, but the wrath of God abideth on him. (aiōnios )