< Yohana 21 >

1 Baada ya mambo hayo Yesu alijidhihirisha tena kwa wanafunzi katika Bahari ya Tiberia; hivi ndivyo alivyojidhihirisha mwenyewe:
Later on, Jesus showed himself again to the disciples by the Sea of Tiberias.
2 Simon Petro alikuwa pamoja na Thomaso aitwaye Didimas, Nathanaeli wa kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo na wanafunzi wengine wawili wa Yesu.
It was in this way: — Simon Peter, Thomas, who was called ‘The Twin,’ Nathanael of Cana in Galilee, Zebediah’s sons, and two other disciples of Jesus, were together, when Simon Peter said:
3 Simon Petro akawaambia, “Mimi naenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Sisi, pia tutaenda nawe.” Wakaenda wakaingia kwenye mashua, lakini usiku huo wote hawakupata chochote.
“I am going fishing.” “We will come with you,” said the others. They went out and got into the boat, but caught nothing that night.
4 Na asubuhi kulipokucha, Yesu alisimama ufukweni, nao wanafunzi hawakutambua kuwa alikuwa Yesu.
Just as day was breaking, Jesus came and stood on the beach; but the disciples did not know that it was he.
5 Kisha Yesu akawambia, “Vijana, mna chochote cha kula?” Nao wakamjibu, “Hapana.”
“My children,” he said, “have you anything to eat?” “No,” they answered.
6 Akawambia, “Shusheni wavu upande wa kuume wa mashua, nanyi mtapata kiasi.” Kwa hiyo wakashusha wavu nao hawakuweza kulivuta tena kwa sababu ya wingi wa cha samaki.
“Cast your net to the right of the boat,” he said, “and you will find fish.” So they cast the net, and now they could not haul it in on account of the quantity of fish.
7 Basi yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda akamwambia Petro, “Ni Bwana.” Naye Simon Petro aliposikia kuwa ni Bwana, akajifunga vazi lake (maana hakuwa amelivaa vizuri), kisha akajitupa baharini.
Upon this the disciple whom Jesus loved said to Peter: “It is the Master!” When Simon Peter heard that it was the Master, he fastened his coat round him (for he had taken it off), and threw himself into the Sea.
8 Wale wanafunzi wengine wakaja kwenye mashua (kwani hawakuwa mbali na pwani, yapata mita mia moja kutoka ufukweni), nao walikuwa wakivuta zile nyavu zilizokuwa zimejaa samaki.
But the rest of the disciples came in the boat (for they were only about a hundred yards from shore), dragging the net full of fish.
9 Walipofika ufukweni, waliona moto wa mkaa pale na juu yake kulikuwa na samaki pamoja na mkate.
When they had come ashore, they found a charcoal fire ready, with some fish already on it, and some bread as well.
10 Yesu akawambia, “Leteni baadhi ya samaki mliovua sasa hivi.”
“Bring some of the fish which you have just caught,” said Jesus.
11 Basi Simon Petro akapanda na kuukokota ule wavu uliokuwa umejaa samaki wakubwa, kiasi cha samaki 153; japo walikuwa wengi, ule wavu haukuchanika.
So Simon Peter got into the boat and hauled the net ashore full of large fish, a hundred and fifty-three of them; and yet, although there were so many, the net had not been torn.
12 Yesu akawaambia, “Njoni mpate kifungua kinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanfunzi aliyethubutu kumwuliza, “Wewe ni nani?” Walijua kuwa alikuwa ni Bwana.
And Jesus said to them: “Come and breakfast.” Not one of the disciples ventured to ask him who he was, knowing that it was the Master.
13 Yesu akaja, akachukua ule mkate, kisha akawapa, akafanya vivyo hivyo na kwa wale samaki.
Jesus went and took the bread and gave it to them, and the fish too.
14 Hii ilikuwa mara ya tatu kwa Yesu kujidhihirisha kwa wanafunzi wake baada ya kufufuka toka wafu.
This was the third time that Jesus showed himself to the disciples after he had risen from the dead.
15 Baada ya kuwa wamefungua kinywa, Yesu akamwambia Simon Petro, “Simon mwana wa Yohana je, wanipenda mimi kuliko hawa?” Petro akajibu, “Ndiyo, Bwana; “Wewe wajua kuwa mimi nakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha wanakondoo wangu.”
When breakfast was over, Jesus said to Simon Peter: “Simon, son of John, do you love me more than the others?” “Yes, Master,” he answered, “you know that I am your friend.” “Feed my lambs,” said Jesus.
16 Akamwambia mara ya pili, “Simon mwana wa Yona, je, wanipenda?” Petro akamwambia, “Ndiyo, Bwana; wewe wajua kuwa nakupenda. “Yesu akamwambia, “Chunga kondoo wangu.”
Then, a second time, Jesus asked: “Simon, son of John, do you love me?” “Yes, Master,” he answered, “you know that I am your friend.” “Tend my sheep,” said Jesus.
17 Akamwambia tena mara ya tatu, “Simon, mwana wa Yohana, Je wanipenda?” Naye Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, “Je Wewe wanipenda?” Naye akamwambia, “Bwana, unajua yote; unajua kuwa nakupenda.” Yesu akamwambia, Lisha kondoo wangu.
The third time, Jesus said to him: “Simon, son of John, are you my friend?” Peter was hurt at his third question being ‘Are you my friend?’; and exclaimed: “Master, you know everything! You can tell that I am your friend.” “Feed my sheep,” said Jesus.
18 Amini, amini, nakuambia, ulipokuwa kijana ulizoea kuvaa nguo mwenyewe na kwenda kokote ulikotaka; lakini utakapokuwa mzee, utanyosha mikono yako, na mwingine atakuvalisha nguo na kukupeleka usikotaka kwenda.”
“In truth I tell you,” he continued, “when you were young, you used to put on your own girdle, and walk wherever you wished; but, when you have grown old, you will have to stretch out your hands, while some one else puts on your girdle, and takes you where you do not wish.”
19 Yesu alisema haya ili kuonesha ni aina gani ya kifo ambacho Petro angemtukuza Mungu. Baada ya kuwa amesema haya, akamwambia Petro, “Nifuate.”
Jesus said this to show the death by which Peter was to honour God, and then he added: “Follow me.”
20 Petro aligeuka na kumwona yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda akawafuata- Huyu ndiye aliyekuwa amajiegemeza kwenye kifua cha Yesu wakati wa chakula cha jioni na kumwuliza, “Bwana, ni nani atakayekusaliti?”
Peter turned round, and saw the disciple whom Jesus loved following — the one who at the supper leant back on the Master’s shoulder, and asked him who it was that would betray him.
21 Petro alimwona na kisha akamwuliza Yesu, “Bwana, Huyu mtu atafanya nini?”
Seeing him, Peter said to Jesus: “Master, what about this man?”
22 Yesu akamjibu, “Kama nataka abaki mpaka nitakapokuja, hilo linakuhusu nini?” Nifuate.”
“If it is my will that he should wait till I come,” answered Jesus, “what has that to do with you? Follow me yourself.”
23 Kwa hiyo habari hii ikaenea miongoni mwa wale ndugu, kwamba mwanafunzi huyo hatakufa. Lakini Yesu hakumwambia Petro kuwa, mwanafunzi huyo hafi, “Kama nataka yeye abaki mpaka nitakapokuja yakuhusu nini?”
So the report spread among the Brethren that that disciple was not to die; yet Jesus did not say that he was not to die, but said “If it is my will that he should wait till I come, what has that to do with you?”
24 Huyu ndiye mwanafunzi atoaye ushuhuda wa mambo haya, na ndiye aliye andika mambo haya, na tunajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli.
It is this disciple who states these things, and who recorded them; and we know that his statement is true.
25 Kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu aliyafanya. Kama kila moja lingeandikwa, nadhani kwamba ulimwengu wenyewe usingetosha kuviweka vitabu ambavyo vingeandikwa.
There are many other things which Jesus did; but, if every one of them were to be recorded in detail, I suppose that even the world itself would not hold the books that would be written.

< Yohana 21 >