< Yohana 21 >
1 Baada ya mambo hayo Yesu alijidhihirisha tena kwa wanafunzi katika Bahari ya Tiberia; hivi ndivyo alivyojidhihirisha mwenyewe:
Later Jesus appeared again to the disciples by the Sea of Galilee. This is how it happened.
2 Simon Petro alikuwa pamoja na Thomaso aitwaye Didimas, Nathanaeli wa kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo na wanafunzi wengine wawili wa Yesu.
Simon Peter, Thomas the Twin, Nathanael of Cana in Galilee, and Zebedee's sons, and two other disciples were together.
3 Simon Petro akawaambia, “Mimi naenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Sisi, pia tutaenda nawe.” Wakaenda wakaingia kwenye mashua, lakini usiku huo wote hawakupata chochote.
“I'm going fishing,” Simon Peter said to them. “We'll come with you,” they replied. So they left and went out in the boat, but all night they caught nothing.
4 Na asubuhi kulipokucha, Yesu alisimama ufukweni, nao wanafunzi hawakutambua kuwa alikuwa Yesu.
When dawn came Jesus was standing on the shore, but the disciples didn't know it was him.
5 Kisha Yesu akawambia, “Vijana, mna chochote cha kula?” Nao wakamjibu, “Hapana.”
Jesus called to them, “My friends, haven't you caught anything?” “No,” they replied.
6 Akawambia, “Shusheni wavu upande wa kuume wa mashua, nanyi mtapata kiasi.” Kwa hiyo wakashusha wavu nao hawakuweza kulivuta tena kwa sababu ya wingi wa cha samaki.
“Throw the net out on the right side of the boat, and you'll find some,” he told them. So they threw out the net, and they weren't able to haul it in because it had so many fish.
7 Basi yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda akamwambia Petro, “Ni Bwana.” Naye Simon Petro aliposikia kuwa ni Bwana, akajifunga vazi lake (maana hakuwa amelivaa vizuri), kisha akajitupa baharini.
The disciple Jesus loved said to Peter, “It's the Lord.” When Peter heard it was the Lord, he put some clothes on since he was naked, and jumped into the sea.
8 Wale wanafunzi wengine wakaja kwenye mashua (kwani hawakuwa mbali na pwani, yapata mita mia moja kutoka ufukweni), nao walikuwa wakivuta zile nyavu zilizokuwa zimejaa samaki.
The other disciples followed in the boat, pulling the net full of fish, because they were not far from the shore, only about a hundred yards.
9 Walipofika ufukweni, waliona moto wa mkaa pale na juu yake kulikuwa na samaki pamoja na mkate.
Once they'd landed they saw a fire with fish cooking on it, and some bread.
10 Yesu akawambia, “Leteni baadhi ya samaki mliovua sasa hivi.”
Jesus told them, “Bring some of the fish you've just caught.”
11 Basi Simon Petro akapanda na kuukokota ule wavu uliokuwa umejaa samaki wakubwa, kiasi cha samaki 153; japo walikuwa wengi, ule wavu haukuchanika.
Simon Peter went aboard and pulled the net full of fish ashore. There were 153 large fish, yet even so the net hadn't torn.
12 Yesu akawaambia, “Njoni mpate kifungua kinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanfunzi aliyethubutu kumwuliza, “Wewe ni nani?” Walijua kuwa alikuwa ni Bwana.
“Come and eat some breakfast,” Jesus said to them. None of the disciples was brave enough to ask him, “Who are you?” They knew it was the Lord.
13 Yesu akaja, akachukua ule mkate, kisha akawapa, akafanya vivyo hivyo na kwa wale samaki.
Jesus took the bread and gave it to them and the fish as well.
14 Hii ilikuwa mara ya tatu kwa Yesu kujidhihirisha kwa wanafunzi wake baada ya kufufuka toka wafu.
This was the third time Jesus had appeared to the disciples after being raised from the dead.
15 Baada ya kuwa wamefungua kinywa, Yesu akamwambia Simon Petro, “Simon mwana wa Yohana je, wanipenda mimi kuliko hawa?” Petro akajibu, “Ndiyo, Bwana; “Wewe wajua kuwa mimi nakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha wanakondoo wangu.”
After breakfast, Jesus asked Simon Peter, “Simon, son of John, do you love me more than these?” “Yes, Lord,” he replied, “you know I love you.”
16 Akamwambia mara ya pili, “Simon mwana wa Yona, je, wanipenda?” Petro akamwambia, “Ndiyo, Bwana; wewe wajua kuwa nakupenda. “Yesu akamwambia, “Chunga kondoo wangu.”
“Take care of my lambs,” Jesus told him. “Simon, son of John, do you love me?” he asked for the second time. “Yes, Lord,” he answered, “you know I love you.”
17 Akamwambia tena mara ya tatu, “Simon, mwana wa Yohana, Je wanipenda?” Naye Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, “Je Wewe wanipenda?” Naye akamwambia, “Bwana, unajua yote; unajua kuwa nakupenda.” Yesu akamwambia, Lisha kondoo wangu.
“Look after my sheep,” Jesus said to him. “Simon, son of John, do you love me?” he asked a third time. Peter was saddened that Jesus had asked him for the third time if he loved him. “Lord, you know everything. You know I love you,” Peter told him. “Take care of my sheep,” said Jesus.
18 Amini, amini, nakuambia, ulipokuwa kijana ulizoea kuvaa nguo mwenyewe na kwenda kokote ulikotaka; lakini utakapokuwa mzee, utanyosha mikono yako, na mwingine atakuvalisha nguo na kukupeleka usikotaka kwenda.”
“I tell you the truth,” said Jesus, “when you were young, you dressed yourself and went wherever you wanted. But when you're old, you'll hold out your hands and someone will dress you and take you where you don't want to go.”
19 Yesu alisema haya ili kuonesha ni aina gani ya kifo ambacho Petro angemtukuza Mungu. Baada ya kuwa amesema haya, akamwambia Petro, “Nifuate.”
Jesus said this to explain the kind of death by which he would glorify God. Then he said to Peter, “Follow me.”
20 Petro aligeuka na kumwona yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda akawafuata- Huyu ndiye aliyekuwa amajiegemeza kwenye kifua cha Yesu wakati wa chakula cha jioni na kumwuliza, “Bwana, ni nani atakayekusaliti?”
As Peter turned round, he saw the disciple Jesus loved following them, the one who had leaned over to Jesus during the supper and asked, “Lord, who is going to betray you?”
21 Petro alimwona na kisha akamwuliza Yesu, “Bwana, Huyu mtu atafanya nini?”
Peter asked Jesus, “What about him, Lord?”
22 Yesu akamjibu, “Kama nataka abaki mpaka nitakapokuja, hilo linakuhusu nini?” Nifuate.”
Jesus told him, “If I want him to remain alive here until I return, why is that your concern? You follow me!”
23 Kwa hiyo habari hii ikaenea miongoni mwa wale ndugu, kwamba mwanafunzi huyo hatakufa. Lakini Yesu hakumwambia Petro kuwa, mwanafunzi huyo hafi, “Kama nataka yeye abaki mpaka nitakapokuja yakuhusu nini?”
This is why the saying spread among the believers that this disciple would not die. But Jesus didn't say to him that he wouldn't die, just that “If I want him to remain alive here until I return, why is that your concern?”
24 Huyu ndiye mwanafunzi atoaye ushuhuda wa mambo haya, na ndiye aliye andika mambo haya, na tunajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli.
This disciple confirms what happened and wrote all this down. We know that what he says is true.
25 Kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu aliyafanya. Kama kila moja lingeandikwa, nadhani kwamba ulimwengu wenyewe usingetosha kuviweka vitabu ambavyo vingeandikwa.
Jesus did many other things as well, and if it all was written down, I doubt the whole world could hold all the books that would be written.