< Yohana 20 >
1 Mapema siku ya kwanza ya juma, kungali bado giza, Mariamu Magdalena alikuja kaburini; akaliona lile jiwe limeondolewa kaburini.
Le premier jour de la semaine, Marie Madeleine se rendit au sépulcre, de grand matin, lorsqu'il faisait encore obscur: elle vit que la pierre en était ôtée.
2 Kwa hiyo akakimbia mbio kwenda kwa Simon Petro na kwa yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, kisha akawaambia, “wamemchukua Bwana kaburini, nasi hatujui kule walikomlaza.”
Elle courut donc trouver Simon Pierre, ainsi que l'autre disciple que Jésus aimait, et leur dit: «On a enlevé du sépulcre le Seigneur, et nous ne savons où on l’a mis.»
3 Kisha Petro na yule mwanafunzi mwingine wakatoka, kuelekea kaburini.
Pierre sortit donc, ainsi que l'autre disciple, et ils se rendirent au sépulcre.
4 Wote walipiga mbio kwa pamoja; yule mwanafunzi mwingine alikimbia kwa kasi zaidi ya Petro nakufika kaburini wa kwanza.
Ils couraient tous deux; mais l'autre disciple courut plus vite que Pierre, et arriva le premier au sépulcre;
5 Akasimama na kisha kuangalia kaburini; akaiona ile sanda ya kitani imelala, lakini hakuingia ndani.
et s'étant baissé, il vit les bandes qui étaient à terre; cependant, il n'entra point.
6 Kisha Simon Petro naye akafika akaingia ndani ya Kaburi. Akaiona ile sanda ya kitani imelala pale
Simon Pierre, qui le suivait, arriva à son tour; il entra dans le sépulcre, et vit les bandes qui étaient à terre,
7 na ile leso iliyokuwa kichwani pake haikuwa imelala pamoja na zile sanda za kitani bali ilikuwa imelala pembeni peke yake.
et le suaire, dont on avait couvert la tête de Jésus, non point avec les bandes, mais roulé à part dans un coin.
8 Ndipo yule mwanafunzi mwingine naye alipoingia ndani ya kaburi; akaona na kuamini.
Alors cet autre disciple qui était arrivé le premier au sépulcre, y entra aussi: il vit, et il crut;
9 Kwa kuwa hadi wakati huo walikuwa bado hawajayajua maandiko kwamba ilimlazimu Yesu afufuke tena katika wafu.
car ces disciples ne savaient pas encore que, d'après l'Écriture, le Messie devait ressusciter des morts.
10 Kisha wanafunzi wakaenda tena nyumbani kwao.
Là-dessus, ils s'en retournèrent chez eux.
11 Hata hivyo, Mariamu alikuwa amesimama kaburini akilia, alivyokuwa akiendelea kulia alisimama kisha akatazama kaburini.
Cependant Marie se tenait près du sépulcre, en dehors, et pleurait. Tout en pleurant, elle se baissa pour regarder dans le sépulcre,
12 Akaona malaika wawili wenye sura nyeupe wamekaa mmoja kichwani na mwingine miguuni mahali ambapo Yesu alikuwa amelala.
et elle vit deux anges, vêtus de blanc, assis au lieu où avait reposé le corps de Jésus, l'un à la tête, l'autre aux pieds.
13 Nao wakamwambia, “Mwanamke, kwa nini unalia?” Naye akawaambia, “Ni kwa sababu wamemchukua Bwana wangu, nami sijui walikomweka.”
Et ces anges lui dirent: «Femme, pourquoi pleures-tu?» Elle leur répondit: «C'est qu'on a enlevé mon Seigneur, et je ne sais où on l’a mis.»
14 Alipokwisha sema hayo, aligeuka na kumwona Yesu akiwa amesimama. Lakini hakutambua kama huyo alikuwa Yesu.
En disant ces mots, elle se retourna et vit Jésus qui était là; mais elle ne savait pas que c'était Jésus.
15 Naye Yesu akamwambia, “Mama, kwa nini unalia? Unamtafuta nani?” Naye huku akidhani kuwa ni mtunza bustani akamwambia, “Bwana, kama ni wewe uliyemchukua, niambie ulikomweka, nami nitamchukua.”
Jésus lui dit: «Femme, pourquoi pleures-tu? Qui cherches-tu?» Marie, croyant que c'était le jardinier, lui dit: «Seigneur, si c'est toi qui l'as emporté, dis-moi où tu l'as mis, et j'irai le prendre.»
16 Yesu akamwambia, “Mariamu.” Naye akageuka mwenyewe na kumwambia kwa Kiaramu, “Raboni,” yaani hii ni kusema, “Mwalimu.”
Jésus lui dit: «Marie!» Elle se retourna, et lui dit en hébreu: «Rabboni!» c’est-à-dire, Maître.
17 Yesu akamwambia, “Usiniguse, kwani bado sijapaa kwenda kwa baba; bali uende kwa ndugu zangu ukawaambie kuwa nitapaa kwenda kwa Baba yangu ambaye pia ni Baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu.”
Jésus lui dit: «Ne me touche pas, car je ne suis pas encore monté vers le Père; mais va trouver mes frères, et dis-leur que je monte vers mon Père et votre Père, vers mon Dieu et votre Dieu.»
18 Mariamu Magdalena akaja kuwaambia wanafunzi, “Nimemwona Bwana,” na kwamba amemwambia mambo haya.
Marie Madeleine alla annoncer aux disciples qu'elle avait vu le Seigneur, et qu'il lui avait dit ces choses.
19 Na ilipokuwa jioni, siku hiyo, siku ya kwanza ya juma, na milango ikiwa imefungwa mahali wanafunzi walipokuwapo kwa kuwahofia Wayahudi, Yesu alikuja na kusimama katikati yao na kuwaambia, “Amani iwe kwenu.”
Dans la soirée de ce même jour, qui était le premier de la semaine, les portes du lieu où étaient les disciples étant fermées par crainte des Juifs, Jésus vint, et, se présentant au milieu d'eux, il leur dit: «La paix soit avec vous!»
20 Alipokwisha sema haya akawaonesha mikono yake na ubavu wake. Nao wanafunzi walipomwona Bwana walifurahi.
Ayant ainsi parlé, il leur montra ses mains et son côté. Les disciples furent remplis de joie en voyant le Seigneur.
21 Kisha Yesu akawaambia tena, “Amani iwe nanyi. Kama vile Baba alivyonituma mimi, vivyo hivyo nami nawatuma ninyi.”
Jésus leur dit une seconde fois: «La paix soit avec vous! Comme le Père m'a envoyé, moi aussi je vous envoie.»
22 Yesu alipokwisha sema hayo, akawavuvia akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu.
Après ces paroles, il souffla sur eux, et leur dit: «Recevez le Saint-Esprit.
23 Yeyote mmsameheye dhambi, wamesamehewa; na wale mtakaowafungia watafungiwa.”
Ceux à qui vous pardonnerez leurs péchés, ces péchés leur seront pardonnés; ceux à qui vous retiendrez leurs péchés, ces péchés leur seront retenus.»
24 Thomaso, mmoja wa wale kumi na wawili, aliyeitwa Didimas, hakuwa na wanafunzi wenzake Yesu alipokuja.
Thomas, l'un des Douze, celui qu'on appelle Didyme, n'était pas avec eux, lorsque Jésus vint.
25 Wale wanafunzi wengine waka mwambia baadaye, “Tumemwona Bwana.” Naye akawambia, “Kama sitaona alama za misumari katika mikono yake, na kuweka vidole vyangu kwenye hizo alama, na pia kuweka mkono wangu kwenye ubavu wake sitaamini.”
Les autres disciples lui dirent donc: «Nous avons vu le Seigneur.» Mais Thomas leur dit: «Si je ne vois dans ses mains la marque des clous, si je ne mets mon doigt à la place où étaient les clous, et si je ne mets ma main dans son côté, je ne le croirai point.»
26 Baada ya siku nane wanafunzi walikuwa chumbani tena, naye Thomaso alikuwa pamoja nao. Wakati milango ilipokuwa imefungwa Yesu alisimama katikati yao. na akasema, “Amani na iwe nanyi.”
Huit jours après, les disciples se trouvaient de nouveau dans la maison, et Thomas était avec eux. Jésus vint, quoique les, portes fussent fermées, et, se présentant au milieu d'eux, leur dit: «La paix soit avec vous!»
27 Kisha akamwambia Thomaso, leta kidole chako na uone mikono yangu; leta hapa mikono yako na uweke kwenye ubavu wangu; wala usiwe asiyeamini bali aaminiye.”
Il dit ensuite à Thomas: «Approche ici ton doigt, et regarde mes mains; approche aussi ta main et la mets dans mon côté; et ne sois pas incrédule, mais crois.»
28 Naye Thomaso akajibu na kumwambia, “Bwana wangu na Mungu wangu.”
Thomas répondit et lui dit: «Mon Seigneur et mon Dieu!»
29 Yesu akamwambia, Kwa kuwa umeniona, umeamini. Wamebarikiwa wao wanaoamini, pasipokuona.”
Jésus lui dit: «Parce que tu m'as vu, tu as cru: heureux ceux qui croiront sans avoir vu!»
30 Kisha Yesu alifanya ishara nyingi mbele ya wanafunzi, ambazo hazijawahi kuandikwa katika kitabu hiki;
Jésus a fait, en présence de ses disciples, beaucoup d'autres miracles qui ne sont pas consignés dans ce livre;
31 bali hizi zimeandikwa ili kwamba muweze kuamini kwamba Yesu ndiye Kristo, mwana wa Mungu, na kwamba muaminipo muwe na uzima katika jina lake.
mais ceux-ci ont été rapportés, afin que vous croyiez que Jésus est le Messie, le Fils de Dieu, et qu'en croyant vous ayez la vie en son nom.