< Yohana 20 >
1 Mapema siku ya kwanza ya juma, kungali bado giza, Mariamu Magdalena alikuja kaburini; akaliona lile jiwe limeondolewa kaburini.
But on the first day of the week Mary the Magdalene cometh early, while it was yet dark, to the tomb, and seeth that the stone had been taken away from the tomb.
2 Kwa hiyo akakimbia mbio kwenda kwa Simon Petro na kwa yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, kisha akawaambia, “wamemchukua Bwana kaburini, nasi hatujui kule walikomlaza.”
She runneth therefore, and cometh to Simon Peter, and to the other disciple, whom Jesus loved, and saith to them, They have taken away the Lord out of the tomb, and we know not where they have laid him.
3 Kisha Petro na yule mwanafunzi mwingine wakatoka, kuelekea kaburini.
Peter therefore went forth, and the other disciple, and they set out for the tomb.
4 Wote walipiga mbio kwa pamoja; yule mwanafunzi mwingine alikimbia kwa kasi zaidi ya Petro nakufika kaburini wa kwanza.
And they ran both together; and the other disciple outran Peter, and came first to the tomb.
5 Akasimama na kisha kuangalia kaburini; akaiona ile sanda ya kitani imelala, lakini hakuingia ndani.
And stooping down, he seeth the linen cloths lying; but he did not go in.
6 Kisha Simon Petro naye akafika akaingia ndani ya Kaburi. Akaiona ile sanda ya kitani imelala pale
Then cometh also Simon Peter following him, and he went into the tomb; and he beholdeth the linen cloths lying,
7 na ile leso iliyokuwa kichwani pake haikuwa imelala pamoja na zile sanda za kitani bali ilikuwa imelala pembeni peke yake.
and the napkin that was about his head, not lying with the linen cloths, but folded up in a place by itself.
8 Ndipo yule mwanafunzi mwingine naye alipoingia ndani ya kaburi; akaona na kuamini.
Then therefore went in also the other disciple, who came first to the tomb; and he saw, and believed.
9 Kwa kuwa hadi wakati huo walikuwa bado hawajayajua maandiko kwamba ilimlazimu Yesu afufuke tena katika wafu.
For not even yet did they know the Scripture, that he must rise from the dead.
10 Kisha wanafunzi wakaenda tena nyumbani kwao.
So the disciples went away again to their home.
11 Hata hivyo, Mariamu alikuwa amesimama kaburini akilia, alivyokuwa akiendelea kulia alisimama kisha akatazama kaburini.
But Mary was standing without by the tomb weeping. And as she wept, she stooped down into the tomb,
12 Akaona malaika wawili wenye sura nyeupe wamekaa mmoja kichwani na mwingine miguuni mahali ambapo Yesu alikuwa amelala.
and beholdeth two angels in white sitting, one at the head, and one at the feet, where the body of Jesus had lain.
13 Nao wakamwambia, “Mwanamke, kwa nini unalia?” Naye akawaambia, “Ni kwa sababu wamemchukua Bwana wangu, nami sijui walikomweka.”
And they say to her, Woman, why dost thou weep? She saith to them, Because they have taken away my Lord, and I know not where they have laid him.
14 Alipokwisha sema hayo, aligeuka na kumwona Yesu akiwa amesimama. Lakini hakutambua kama huyo alikuwa Yesu.
Having said this, she turned back, and beheld Jesus standing; and knew not that it was Jesus.
15 Naye Yesu akamwambia, “Mama, kwa nini unalia? Unamtafuta nani?” Naye huku akidhani kuwa ni mtunza bustani akamwambia, “Bwana, kama ni wewe uliyemchukua, niambie ulikomweka, nami nitamchukua.”
Jesus saith to her, Woman, why dost thou weep? whom dost thou seek? She, supposing that it was the gardener, saith to him, Sir, if thou hast borne him hence, tell me where thou hast laid him, and I will take him away.
16 Yesu akamwambia, “Mariamu.” Naye akageuka mwenyewe na kumwambia kwa Kiaramu, “Raboni,” yaani hii ni kusema, “Mwalimu.”
Jesus saith to her, Mary! She turned and saith to him in Hebrew, Rabboni! Which signifieth, Teacher!
17 Yesu akamwambia, “Usiniguse, kwani bado sijapaa kwenda kwa baba; bali uende kwa ndugu zangu ukawaambie kuwa nitapaa kwenda kwa Baba yangu ambaye pia ni Baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu.”
Jesus saith to her, Touch me not; for I have not yet ascended to the Father; but go to my brethren, and say to them, I ascend to my Father and your Father, and my God and your God.
18 Mariamu Magdalena akaja kuwaambia wanafunzi, “Nimemwona Bwana,” na kwamba amemwambia mambo haya.
Mary the Magdalene cometh, bringing word to the disciples that she had seen the Lord, and that he had said these things to her.
19 Na ilipokuwa jioni, siku hiyo, siku ya kwanza ya juma, na milango ikiwa imefungwa mahali wanafunzi walipokuwapo kwa kuwahofia Wayahudi, Yesu alikuja na kusimama katikati yao na kuwaambia, “Amani iwe kwenu.”
When therefore it was evening on that day, which was the first day of the week, and the doors where the disciples were had been shut for fear of the Jews, Jesus came and stood in the midst, and said to them, Peace be to you!
20 Alipokwisha sema haya akawaonesha mikono yake na ubavu wake. Nao wanafunzi walipomwona Bwana walifurahi.
And having said this, he showed them his hands and his side. The disciples therefore were glad, when they saw the Lord.
21 Kisha Yesu akawaambia tena, “Amani iwe nanyi. Kama vile Baba alivyonituma mimi, vivyo hivyo nami nawatuma ninyi.”
Then he said to them again, Peace be to you! As the Father hath sent me, I also send you.
22 Yesu alipokwisha sema hayo, akawavuvia akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu.
And having said this, he breathed on them, and saith to them, Receive the Holy Spirit.
23 Yeyote mmsameheye dhambi, wamesamehewa; na wale mtakaowafungia watafungiwa.”
Whosever sins ye remit, they are remitted to them; whosever ye retain, they are retained.
24 Thomaso, mmoja wa wale kumi na wawili, aliyeitwa Didimas, hakuwa na wanafunzi wenzake Yesu alipokuja.
But Thomas, one of the twelve, called Didymus, was not with them when Jesus came.
25 Wale wanafunzi wengine waka mwambia baadaye, “Tumemwona Bwana.” Naye akawambia, “Kama sitaona alama za misumari katika mikono yake, na kuweka vidole vyangu kwenye hizo alama, na pia kuweka mkono wangu kwenye ubavu wake sitaamini.”
The other disciples therefore said to him, We have seen the Lord. But he said to them, Unless I see in his hands the print of the nails, and put my finger into the place of the nails, and put my hand into his side, I shall not believe.
26 Baada ya siku nane wanafunzi walikuwa chumbani tena, naye Thomaso alikuwa pamoja nao. Wakati milango ilipokuwa imefungwa Yesu alisimama katikati yao. na akasema, “Amani na iwe nanyi.”
And after eight days the disciples were again within, and Thomas with them. Jesus cometh, the doors being shut, and stood in the midst, and said, Peace be to you!
27 Kisha akamwambia Thomaso, leta kidole chako na uone mikono yangu; leta hapa mikono yako na uweke kwenye ubavu wangu; wala usiwe asiyeamini bali aaminiye.”
Then he saith to Thomas, Reach hither thy finger, and behold my hands, and reach forth thy hand, and put it into my side; and be not faithless, but believing.
28 Naye Thomaso akajibu na kumwambia, “Bwana wangu na Mungu wangu.”
Thomas answered and said to him, My Lord and my God!
29 Yesu akamwambia, Kwa kuwa umeniona, umeamini. Wamebarikiwa wao wanaoamini, pasipokuona.”
Jesus saith to him, Because thou hast seen me, thou hast believed; blessed are they who have not seen, and yet have believed.
30 Kisha Yesu alifanya ishara nyingi mbele ya wanafunzi, ambazo hazijawahi kuandikwa katika kitabu hiki;
Many other signs did Jesus in the presence of his disciples, which are not written in this book.
31 bali hizi zimeandikwa ili kwamba muweze kuamini kwamba Yesu ndiye Kristo, mwana wa Mungu, na kwamba muaminipo muwe na uzima katika jina lake.
But these have been written, that ye may believe that Jesus is the Christ the Son of God, and that believing ye may have life in his name.