< Yohana 2 >

1 Baada ya siku tatu, kulikuwa na arusi huko Kana ya Galilaya na mama yake Yesu alikuwa huko.
Two days later there was a wedding [celebration] in Cana [town], in Galilee [district]. Jesus’ mother was there.
2 Yesu na wanafunzi wake walikuwa wamealikwa katika arusi.
Jesus and [we] his disciples [were also there, because] we had been invited {someone had invited us} also.
3 Wakati walipoishiwa na divai, mama yake Yesu akamwambia, “Hawana divai.”
When the guests had drunk all the wine [that was there], Jesus’ mother said to him, “The wine is all gone; [can you do something about that]?”
4 Yesu akajibu, “Mwanamke hiyo inanihusu nini mimi? Muda wangu mimi bado haujatimia.”
Jesus said to her, “Ma’am/Woman, (do not [tell] me [what to do]!/why do you [tell] me [what to do]?) [RHQ] It is not yet time [MTY] [to show] that I am [the Messiah by working miracles].”
5 Mama yake akawambia watumishi, “Chochote atakachowambia fanyeni.”
Then Jesus’ mother said to the servants, “Do whatever he tells you!”
6 Basi kulikuwa na mitungi sita ya mawe pale iliyowekwa kwa ajili ya kunawa katika sikukuu za Wayahudi, kila moja lilikuwa na ujazo wa nzio mbili tatu.
There were six [empty] stone jars there. The Jews [habitually put water in them] to use for washing things [to make them acceptable to God]. Each jar held (20 to 30 gallons/80 to 120 liters).
7 Yesu akawambia, “Ijazeni maji mitungi ya mawe.” Wakajaza hadi juu.
Jesus said to the servants, “Fill the jars with water!” So they filled the jars to the brim.
8 Kisha akawambia wale watumishi, “Chukueni kiasi sasa na mpeleke kwa muhudumu mkuu wa meza.” Wakafanya kama walivyoagizwa.
Then he told them, “Now, ladle out some [of it] and take it (to the head waiter/to the master of ceremonies).” So the servants did that.
9 Mhudumu mkuu aliyaonja yale maji yaliyokuwa yamebadilika na kuwa divai, ila hakujua yalikotoka (lakini watumishi waliochota maji walijua yalikotoka). Kisha akamwita bwana harusi na
(The head waiter/The master of ceremonies) tasted the water, which had now become wine. He did not know where the wine had come from, but the servants who had ladled out the wine knew. [The wine was delicious]! So he called the bridegroom over,
10 kumwambia, “Kila mmoja huanza kuwahudumia watu divai nzuri na wakiishalewa huwapa divai isiyo nzuri. Lakini wewe umeitunza divai nzuri hadi sasa”
and said to him, “Everyone [else] serves the best wine first. Then when the guests have drunk so much [that they cannot tell the difference], [they serve] the cheap wine. But you [have not done what others do]. You have kept the best wine until now!”
11 Muujiza huu wa Kana ya Galilaya, ulikuwa ndio mwanzo wa ishara za miujiza aliyoifanya Yesu, akifunua utukufu wake, hivyo wanafunzi wake wakamwamini.
That was the first miracle that Jesus did. He did it in Cana [town], in Galilee [district]. By doing it he showed how awesome he is, and as a result, [we] his disciples believed that he [truly was the Messiah].
12 Baada ya hii, Yesu, mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake walienda katika mji wa Kapernaum na wakaa huko kwa siku chache.
Jesus then went down to Capernaum [city] with his mother and [younger] brothers and [us] his disciples. We stayed there several days.
13 Basi Pasaka ya Wayahudi ilikuwa imekaribia, hivyo Yesu akaenda Yerusalemu.
Later, when it was almost time for the Jewish Passover [celebration], Jesus [and we his disciples] went up to Jerusalem.
14 Akawakuta wauzaji wa ng'ombe, kondoo, na njiwa ndani ya Hekalu. Pia na wabadilisha fedha walikuwa wameketi ndani ya Hekalu.
There, in the Temple [courtyard], he saw some men who were selling cattle, sheep, and pigeons [for sacrifices]. He also saw men who were sitting at tables, [making a big profit as they] gave people [Temple tax] coins in exchange for [their Roman] coins.
15 Yesu akatengeneza mjeledi wenye vifundo, akawatoa wote walikuwemo katika hekalu, ikijumuisha ng'ombe na kondoo. Akamwaga fedha za wabadili fedha na kuzipindua meza zao.
Then Jesus made a whip from some cords and [used it to] chase out the sheep and cattle from the Temple [courtyard]. By overturning their tables he scattered the coins of the men who were exchanging them.
16 Kwa wauzaji wa njiwa akawambia, “Toeni vitu hivi mbali na mahali hapa, acheni kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa mahali pa soko.”
He said to those who were selling doves, “Take these doves away [from here]! Stop [defiling] my Father’s Temple [by] making it a market!”
17 Wanafunzi wake wakakumbuka kuwa ilikuwa imeandikwa, “Wivu wa nyumba yako utanila.”
Then [we] disciples remembered that these words had been written {that [someone/David] had written [these words]} [in the Scriptures prophesying what the Messiah would say]: “Others [PRS] will strongly oppose me because I greatly desire that [people respect] your Sacred Tent.”
18 Wakuu wa Kiyahudi wakajibu, wakamwambia, Ni ishara ipi utakayoionyesha kwa sababu unayafanya mambo haya?”
So [one of] the Jewish [leaders] [SYN] replied to him, “What miracle will you perform to show us that [you have authority from God] to do these things?”
19 Yesu akawajibu, libomoeni Hekalu hili nami nitalijenga baada ya siku tatu.”
Jesus replied to them, “If/When you destroy this temple, I will build it again within three days.”
20 Kisha wakuu wa Wayahudi wakasema, “Iligharimu miaka arobaini na sita kujenga hekalu hili nawe unasema utalijenga kwa siku tatu?”
So the Jewish [leaders] [SYN] said, “We have been building this Temple for 46 years [and it is not finished yet]! So (there is no way you will build it within three days!/how will you build it within three days?) [RHQ]”
21 Ingawa, yeye aliongea hekalu akimaanisha mwili wake.
But when Jesus said that about the temple, [he was really talking about] his own body.
22 Hivyo baadaye baada ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu, wanafunzi wake wakakumbuka kuwa alisema hivyo, wakaamini maandiko na kauli hii ambayo Yesu alikuwa amekwisha kuisema.
[Later], after Jesus had [died and had] become alive again, [we] his disciples remembered the words he had said. As a result, we believed [what had been prophesied in] the Scriptures [about the Messiah becoming alive again], and we believed that what Jesus said [was true].
23 Basi alipokuwa Yerusalemu wakati wa Pasaka, wakati wa sikukuu watu wengi waliamini jina lake, walipoona ishara ya miujiza aliyoifanya.
While Jesus was in Jerusalem at the Passover celebration, many people came to believe [that he was the Messiah] because they saw the miracles he was performing.
24 Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wanadamu wote.
But he did not let them tell him what he should do [as the Messiah], because he knew within himself what they were all [thinking].
25 Hakuhitaji mtu yeyote kumwambia kuhusu walivyo wanadamu kwa sababu alijua kilichokuwamo ndani yao.
He did not need anyone to tell him what others were thinking, because he already knew what they were [thinking and wanting].

< Yohana 2 >