< Yohana 2 >

1 Baada ya siku tatu, kulikuwa na arusi huko Kana ya Galilaya na mama yake Yesu alikuwa huko.
And the third day a wedding occurred in Cana of Galilee, and the mother of Jesus was there.
2 Yesu na wanafunzi wake walikuwa wamealikwa katika arusi.
And Jesus also was invited, and his disciples, to the wedding.
3 Wakati walipoishiwa na divai, mama yake Yesu akamwambia, “Hawana divai.”
And having lacked wine the mother of Jesus says to him, They have no wine.
4 Yesu akajibu, “Mwanamke hiyo inanihusu nini mimi? Muda wangu mimi bado haujatimia.”
And Jesus says to her, What is with me and with thee, woman? My hour is not yet here.
5 Mama yake akawambia watumishi, “Chochote atakachowambia fanyeni.”
His mother says to the helpers, Whatever he may say to you, do.
6 Basi kulikuwa na mitungi sita ya mawe pale iliyowekwa kwa ajili ya kunawa katika sikukuu za Wayahudi, kila moja lilikuwa na ujazo wa nzio mbili tatu.
Now there were six stone water pots laying there in accordance with the purification of the Jews, containing two or three measures each.
7 Yesu akawambia, “Ijazeni maji mitungi ya mawe.” Wakajaza hadi juu.
Jesus says to them, Fill the water pots with water. And they filled them until over.
8 Kisha akawambia wale watumishi, “Chukueni kiasi sasa na mpeleke kwa muhudumu mkuu wa meza.” Wakafanya kama walivyoagizwa.
And he says to them, Draw out now, and carry to the feast-ruler. And they carried.
9 Mhudumu mkuu aliyaonja yale maji yaliyokuwa yamebadilika na kuwa divai, ila hakujua yalikotoka (lakini watumishi waliochota maji walijua yalikotoka). Kisha akamwita bwana harusi na
And when the feast-ruler tasted the water that became wine, and had not known from where it was (but the helpers who drew the water had known), the feast-ruler called the bridegroom,
10 kumwambia, “Kila mmoja huanza kuwahudumia watu divai nzuri na wakiishalewa huwapa divai isiyo nzuri. Lakini wewe umeitunza divai nzuri hadi sasa”
and says to him, Every man sets out the good wine first, and when they drank much, then the lesser. Thou have kept the good wine until now.
11 Muujiza huu wa Kana ya Galilaya, ulikuwa ndio mwanzo wa ishara za miujiza aliyoifanya Yesu, akifunua utukufu wake, hivyo wanafunzi wake wakamwamini.
This is the beginning of the signs Jesus did in Cana of Galilee, and he manifested his glory. And his disciples believed in him.
12 Baada ya hii, Yesu, mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake walienda katika mji wa Kapernaum na wakaa huko kwa siku chache.
After this he went down to Capernaum, he and his mother and his brothers and his disciples. And they remained there not many days.
13 Basi Pasaka ya Wayahudi ilikuwa imekaribia, hivyo Yesu akaenda Yerusalemu.
And the Passover of the Jews was near, and Jesus went up to Jerusalem.
14 Akawakuta wauzaji wa ng'ombe, kondoo, na njiwa ndani ya Hekalu. Pia na wabadilisha fedha walikuwa wameketi ndani ya Hekalu.
And he found sitting in the temple those who sell oxen and sheep and doves, and the moneychangers.
15 Yesu akatengeneza mjeledi wenye vifundo, akawatoa wote walikuwemo katika hekalu, ikijumuisha ng'ombe na kondoo. Akamwaga fedha za wabadili fedha na kuzipindua meza zao.
And having made a whip from cords, he drove all out from the temple, both the sheep and the oxen. And he poured out the coins of the moneychangers, and turned over their tables.
16 Kwa wauzaji wa njiwa akawambia, “Toeni vitu hivi mbali na mahali hapa, acheni kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa mahali pa soko.”
And he said to those who sell the doves, Take these things from here. Make not my Father's house a house of merchandise.
17 Wanafunzi wake wakakumbuka kuwa ilikuwa imeandikwa, “Wivu wa nyumba yako utanila.”
And his disciples remembered that it is written, Zeal for thy house will consume me.
18 Wakuu wa Kiyahudi wakajibu, wakamwambia, Ni ishara ipi utakayoionyesha kwa sababu unayafanya mambo haya?”
The Jews therefore answered, and said to him, What sign do thou show us since thou do these things?
19 Yesu akawajibu, libomoeni Hekalu hili nami nitalijenga baada ya siku tatu.”
Jesus answered and said to them, Destroy this temple, and in three days I will raise it up.
20 Kisha wakuu wa Wayahudi wakasema, “Iligharimu miaka arobaini na sita kujenga hekalu hili nawe unasema utalijenga kwa siku tatu?”
The Jews therefore said, This temple was forty-six years being built, and will thou raise it up in three days?
21 Ingawa, yeye aliongea hekalu akimaanisha mwili wake.
But that man spoke about the temple of his body.
22 Hivyo baadaye baada ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu, wanafunzi wake wakakumbuka kuwa alisema hivyo, wakaamini maandiko na kauli hii ambayo Yesu alikuwa amekwisha kuisema.
When therefore he was raised from the dead his disciples remembered that he spoke this, and they believed the scripture and the word that Jesus said.
23 Basi alipokuwa Yerusalemu wakati wa Pasaka, wakati wa sikukuu watu wengi waliamini jina lake, walipoona ishara ya miujiza aliyoifanya.
Now when he was in Jerusalem at the Passover during the feast, many believed in his name seeing his signs that he did.
24 Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wanadamu wote.
But Jesus did not trust himself to them, because he knew all men,
25 Hakuhitaji mtu yeyote kumwambia kuhusu walivyo wanadamu kwa sababu alijua kilichokuwamo ndani yao.
and because he had no need that any man should testify about man, for he himself knew what was in man.

< Yohana 2 >