< Yohana 19 >
1 Basi Pilato alimchukua Yesu na kumchapa.
Tedaj Pilat Jezusa vzeme, in biča.
2 Wale maaskari wakasokota miiba na kutengeneza taji. Wakaiweka juu ya kichwa cha Yesu na kumvalisha vazi la rangi ya zambarau.
In vojaki spletó krono s trnja in mu jo denejo na glavo, in oblečejo mu škrlaten plašč,
3 Wakamjia na kusema, “Wewe mfalme wa Wayahudi! na kisha kumpiga kwa mikono yao.
In govorili so: Zdrav, kralj Judovski! in bíli so ga po licu.
4 Kisha Pilato alitoka nje na kuwaambia watu, “Tazama nawaleteeni huyu mtu kwenu ili mjue kwamba mimi sikuona hatia yoyote ndani yake.”
Pilat pa zopet izide ven, in reče jim: Glej, peljem vam ga ven, da spoznate, da ne nahajam na njem nobene krivice.
5 Kwa hiyo Yesu akatoka nje; alikuwa amevaa taji ya miiba na vazi la zambarau. Ndipo Pilato akawaambia, “Tazameni mtu huyu hapa!”
In Jezus izide ven, noseč trnjevo krono, in škrlatni plašč. In reče jim: Glej, človek!
6 Kwa hiyo wakati kuhani mkuu na wakuu walipomwona Yesu, wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe, msulubishe.” Pilato akawaambia, “Mchukueni ninyi wenyewe mkamsulubishe, kwa kuwa mimi sioni hatia ndani yake.”
Ko ga pa véliki duhovni in služabniki ogledajo, zavpijejo, govoreč: Križaj! križaj! Velí jim Pilat: Vzemite ga vi in križajte; kajti jaz ne nahajam nobene krivice na njem.
7 Wayahudi wakamjibu Pilato, “Sisi tunayo sheria, na kwa sheria hiyo inampasa kufa kwa sababu yeye alijifanya kuwa mwana wa Mungu.”
Odgovoré mu Judje: Mi imamo postavo, in po postavi našej je dolžen umreti, ker se je sina Božjega naredil.
8 Pilato aliposikia maneno haya alizidi kuogopa,
Ko je pa Pilat to besedo slišal, zbojí se bolj.
9 akaingia Praitorio tena na kumwambia Yesu, “Wewe unatoka wapi? Hata hivyo, Yesu hakumjibu.
In vnide zopet v sodnišnico, in reče Jezusu: Odkod si ti? Jezus pa mu ne dá odgovora.
10 Kisha Pilato akamwambia, “Je, wewe huongei na mimi? Je, wewe hujui kuwa mimi nina mamlaka ya kukufungua na mamlakaya kukusulubisha?”
Tedaj mu Pilat reče: Meni ne govoriš? Ne véš li, da imam oblast križati te, in da imam oblast izpustiti te?
11 Yesu akamjibu, “Usingekuwa na nguvu dhidi yangu kama usingepewa toka juu. Kwa hiyo, mtu aliyenitoa kwako ana dhambi kubwa.”
Jezus odgovorí: Ne imel bi nobene oblasti nad menoj, da ti ni dano od zgorej: za to ima tisti, kteri me je tebi izročil, veči greh.
12 Kutokana na jibu hili, Pilato akataka kumwacha huru, lakini Wayahudi wakapiga kelele wakisema, “Kama utamwacha huru basi wewe si rafiki wa Kaisari: Kila ajifanyaye kuwa mfalme hunena kinyume cah kaisari.”
Odsihmal je Pilat gledal, da bi ga izpustil. A Judje so kričali, govoreč: Če tega izpustiš, nisi prijatelj cesarju.
13 Pilato alipoyasikia maneno haya, akamleta Yesu nje kisha akakaa kwenye kiti cha hukumu mahali pale panapojulikana kama sakafu, lakini kwa Kiebrania, Gabatha.
Ko je pa Pilat to besedo slišal, pripelje ven Jezusa, in sede na sodišče, na mesto, ktero se imenuje Litostroton, Hebrejski pa Gabata.
14 Siku ya maandalizi ya pasaka ilipofika, panapo muda wa saa ya sita. Pilato akawaambia Wayahudi, “Tazameni mfalme wenu huyu hapa!”
Bilo je pa v petek pred Veliko nočjó, okoli šeste ure. In reče Judom: Glej, kralj vaš!
15 Wakapiga kelele, “Mwondoshe, mwondoshe, msulubishe!” Pilato akawaambia, “Je, nimsulubishe mfalme wenu?” Naye Kuhani mkuu akajibu, “Sisi hatuna mfalme isipokuwa Kaisari.”
Oni pa zavpijejo: Vzemi, vzemi, križaj ga! Reče jim Pilat: Kralja vašega bom križal? Véliki duhovni odgovoré: Nimamo kralja, razen cesarja.
16 Ndipo Pilato alipomtoa Yesu kwao ili asulibiwe.
Tedaj jim ga izročí, naj ga križajo. Ter vzemó Jezusa in odpeljejo.
17 Nao wakamchukua Yesu, naye akatoka, hali ameubeba msalaba wake mwenyewe mpaka kwenye eneo liitwalo fuvu la kichwa, kwa Kihebrania huitwa Golgotha.
In noseč križ svoj, izide na mesto, imenovano Črepinjek, ktero se Hebrejski imenuje Golgota.
18 Ndipo walipomsulibisha Yesu, pamoja naye wanaume wawili, mmoja upende huu na mwingine upande huu, na Yesu katikati yao.
Tu ga razpnó, in ž njim dva druga od ene in druge straní, posredi pa Jezusa.
19 Kisha Pilato akaandika alama na kuiwekwa juu ya msalaba. Hapo paliandikwa: YESU MNAZARETH, MFALME WA WAYAHUDI.
Napisal je pa Pilat, tudi napis, in del ga je na križ; bilo je pa pisano: Jezus Nazarečan kralj Judovski.
20 Wengi wa Wayahudi waliisoma alama hiyo kwani mahali pale aliposulibishwa Yesu palikuwa karibu na mji. Alama hiyo iliadikwa kwa Kiebrania, kwa Kirumi na kwa Kiyunani.
Ta napis je torej veliko Judov bralo, ker je bil kraj, kjer so Jezusa razpeli, blizu mesta; in bilo je pisano Hebrejski, Grški, Latinski.
21 Kisha wakuu wa makuhani wa Wayahudi wakamwambia Pilato, “Usiandike, 'Mfalme wa Wayahudi; bali yeye alisema mimi ni mfalme wa Wayahudi.”
Pravili so torej véliki duhovni Judovski Pilatu: Ne piši: Kralj Judovski; nego, da je sam rekel: Kralj sem Judovski.
22 Naye Pilato akawajibu, “Niliyoandika nimeandika.”
Pilat odgovorí: Kar sem pisal, pisal sem.
23 Baada ya askari kumsulibisha Yesu, walichukua mavazi yake na kuyagawa katika mafungu manne, kila askari fungu moja, vivyo hivyo na kanzo, Sasa ile kanzu haikuwa imeshonwa bali ilkuwa imefumwa yote tokea juu.
Vojaki pa, ko so bili Jezusa razpeli, vzemó obleko njegovo, (in napravijo štiri dele, vsakemu vojaku del, ) in suknjo. A suknja ni bila šivana, nego od vrha vsa iztkana.
24 Kisha wakasemezana wao kwa wao, “Tusiipasue, bali tupigeni kura ili kuona itakuwa ya nani.” Hili lilitokea ili lile andiko litimizwe, lile lisemalo waligawanya nguo zangu, na vazi langu wakalipigia kura.”
Za to rekó med seboj: Trgali je ne bomo, nego srečkajmo za njo, čegava bo; da se izpolni pismo, ktero pravi: "Razdelili so obleko mojo med seboj, in za oblačilo moje so vrgli kocko." In vojaki storé tako.
25 Askari walifanya mambo haya. Mama yake Yesu, dada wa mama yake, Mariamu mke wa Kleopa na Mariamu Magdalena - wanawake hawa walikuwa wamesimama karibu na msalaba wa Yesu.
Stale so pa pri križu Jezusovem mati njegova in sestra matere njegove Marija Kleopova, in Marija Magdalena.
26 Yesu alipomwona mama yake pamoja na yule mwanafunzi aliyempenda wakisimama karibu, akamwambia mama yake, “Mwanamke, tazama, ona mwanao huyu hapa!”
Ko pa ugleda Jezus mater, in učenca, da stojí, kterega je ljubil, reče materi svojej: Žena, glej, sin tvoj!
27 Kisha akamwambia yule mwanfunzi, “Tazama, huyu hapa mama yako. “Tokea saa hiyo yule mwanafunzi akamchukua kwenda nyumbani kwake.
Po tem reče učencu: Glej, mati tvoja! In od tega časa jo je vzel učenec k sebi.
28 Baada ya hilo, Hali Yesu akijua kuwa yote yamekwisha kumalizika ili kutimiza maandiko, akasema, “Naona kiu.”
Po tem, vedoč Jezus, da je uže vse dopolnjeno, da se izpolni pismo, reče: Žejen sem!
29 Chombo kilichokuwa kimejaa Siki kilikuwa kimewekwa pale, kwa hiyo wakaweka sifongo iliyojaa siki juu ya ufito wa hisopo, wakamwekea mdomoni mwake.
Stala je pa tam posoda polna octa; in oni napolnijo gobo z octom, in ovijejo jo okoli izopa, ter mu pritaknejo k ustom.
30 Naye Yesu alipoionja hiyo, akasema, “Imekwisha.” Kisha akainamisha kichwa chake, akaikabidhi roho yake.
Ko je pa Jezus ocet okusil, reče: Dopolnjeno je! in nakloni glavo, in izročí duha.
31 Kwa vile ilikuwa ni wakati wa maandalio, na kwa sababu miili haikutakiwa kubaki juu ya msalaba wakati wa Sabato (kwa kuwa Sabato ilikuwa siku ya muhimu), wayahudi walimwomba Pilato kuwa miguu yao wale wliokuwa wamesulibishwa ivunjwe, na kwamba miili yao ishushwe.
Judje pa, da ne ostane truplo v soboto na križu, ker je bil petek, (bil je namreč ta dan sobotni velik.) zaprosijo Pilata, naj jim goleni prebijejo, in jih snemejo.
32 Ndipo askari walipokuja na kuvunja miguu ya mtu wa kwanza na wa pili aliyekuwa amesulibiwa pamoja na Yesu.
Vojaki torej pridejo in prebijejo prvemu goleni in drugemu, kteri je bil ž njim križan.
33 Walipomfikia Yesu, walimkuta tayari alikuwa amekwisha kufa, kwa hiyo hawakuvunja miguu yake.
Ko pa pridejo do Jezusa, in vidijo, da je uže umrl, ne polomijo mu goleni:
34 Hata hivyo, mmoja wa askari alimchoma Yesu ubavuni kwa mkuki, na mara yakatoka maji na damu.
Nego eden od vojakov mu prebode s sulico rebra, in precej izide kri in voda.
35 Naye aliyeona hili ametoa ushuhuda, na ushuhuda wake ni wa kweli. Yeye anajua kuwa alichokisema ni cha kweli ili nanyi pia muamini.
In ta, ki je videl, priča, in pričanje njegovo je resnično, in on vé, da govori resnico, da boste vi verovali.
36 Mambo haya yalikuwa ili lile neno lililonenwa lipate kutimia, “Hakuna hata wake mmoja utakaovunjwa.”
Zgodilo pa se je to, da se izpolni pismo: "Kost njegova se ne bo prelomila."
37 Tena andiko lingine husema, “Watamtazama yeye waliyemchoma”
In zopet drugo pismo pravi: "Pogledali bodo, kterega so prebodli."
38 Baada ya mambo haya Yusufu wa Arimathaya, kwa vile alikuwa mwanafunzi wa Yesu, lakini kwa siri kwa kuwaogopa Wayahudi, alimwomba Pilato kwamba auchukue mwili wa Yesu. Naye Pilato akampa ruhusa. Kwa hiyo Yusufu akaja kuuondoa mwili wa Yesu.
Po tem pa zaprosi Pilata Jožef iz Arimateje, (ker je bil učenec Jezusov, to da skrivaj za voljo strahú Judovskega, ) da bi snel truplo Jezusovo: in Pilat dovoli. Ter pride in sneme truplo Jezusovo.
39 Naye Nicodemo ambaye hapo awali alimfuata Yesu usiku naye akaja. Yeye alileta mchanganyiko wa manemane na udi, yapata uzito wa ratili mia moja.
Pride pa tudi Nikodem, (kteri je bil poprej po noči prišel k Jezusu, in prinese z miro pomešane aloje kakih sto funtov.
40 Kwa hiyo wakauchukua mwili wa Yesu wakaufanga kwenye sanda ya kitani na pamoja na yale manukato, kama ilivyokuwa desturi ya wayahudi wakati wa kuzika.
In vzemeta truplo Jezusovo, in zavijeta ga v prte z dišavami vred, kakor imajo Judje navado pokopavati.
41 Mahali ambapo Yesu alisulibiwa kulikuwa na bustani; ndani ya ile bustani kulikuwa na kaburi jipya ambalo hakuna mtu alikuwa amawahi kuzikwa humo.
Bil je pa na mestu, kjer je bil križan, vrt, in na vrtu nov grob, v kterega še nikoli nobeden ni bil položen.
42 Basi, kwa kuwa ilikuwa siku ya maandalio kwa Wayahudi, na kwa vile lile kaburi lilikuwa karibu, basi wakamlaza Yesu ndani yake.
Tu torej, za voljo petka Judovskega, ker je bil grob blizu, položita Jezusa.