< Yohana 16 >

1 Nimewaambia mambo haya ili msiweze kukwazwa.
"I have told you all this so that you may not stumble.
2 Watawatoa nje ya masinagogi; hakika saa inakuja ambayo kila atakayewaua atafikiri kuwa anafanya kazi njema kwa ajili ya Mungu.
"They will excommunicate you from their synagogues; indeed the time is coming when any one who kills you will suppose that he is doing God’s service.
3 Watawatendea mambo haya kwa sababu hawamfahamu Baba wala hawanifahamu mimi.
"And they will do these things because they have not known my Father, nor me.
4 Nimewaambia mambo haya ili kwamba wakati ukifika wa haya kutokea, mnaweza kuyakumbuka na jinsi nilivyowaambia muweze wao. Sikuwaambia kuhusu mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
"But I have told you these things, that when the time comes you may remember that I told you about them, myself. I did not, however, speak of these things at first, because I was with you.
5 Japokuwa, sasa naenda kwa yule aliyenituma; lakini hakuna kati yenu anayeniuliza, “Unaenda wapi?”
"But now I go my way to Him who sent me, yet none of you asks me, ‘Where are you going?’
6 Kwa sababu nimesema maneno haya kwenu, huzuni imejaa mioyoni mwenu.
"but sorrow has filled your hearts because I have told you these things.
7 Hata hivyo, nawaambia ukweli: ni vyema kwenu nikiondoka; kwa maana nisipoondoka, mfariji hatakuja kwen; lakini nikienda ntamtuma kwenu.
"Yet - I am telling you the truth - my going is for your good. For unless I go away the Comforter will not come to you; but if I depart I will send him unto you.
8 Akija, huyo mfariji ataubitisha ulimwengu kuhusiana na dhambi, kuhusiana na haki na kuhusiana na hukumu.
"And he, when he comes, will convict the world of sins and of righteousness and of judgment;
9 Kuhusiana na dhambi, kwa sababu hawakuniamini mimi,
"of sin, because they do not believe in me;
10 kuhusiana na haki, kwa sababu naenda kwa baba, na hamtaniona tena;
11 na kuhusiana na hukumu kwa sababu mkuu wa ulimwengu huu amehukumiwa.
"because the Prince of this world has been judged.
12 Ninayo mengi ya kuwaambia, lakini hamtayaelewa sasa.
"I have yet many things to say to you, but you cannot bear them just now.
13 Lakini, yeye, Roho wa kweli, akija, atawaongoza katika kweli yote; kwa kuwa hataongea kwa ajili yake mwenyewe; lakini yoyote atakayoyasikia, atayasema mambo hayo; na atayadhihirisha kwenu mambo yatakayokuja.
"But when he is come, that Spirit of Truth, he will guide you into the whole truth. For he will not speak on his own authority, but all that he hears he will speak, and will make known to you that which is to come.
14 Yeye atanitukuza mimi, kwa sababu atayachukua mambo yangu na atayatangaza kwenu.
"He will glorify me; for he will take of what is mine and will make known to you.
15 Vitu vyote alivyonavyo Baba ni vyangu; kwa hiyo, nimesema kwamba Roho atachukua mambo yangu na atayadhihirisha kwenu.
"Everything that the Father has is mine; that is why I said that he will take of what is mine and make it known to you.
16 Bado muda mfupi, hamtaniona tena; na baada ya muda mfupi tena, mtaniona.”
"In a little while you shall behold me no more; and again in a little while you shall see me, because I am going to the Father."
17 Baadhi ya wanafunzi wake wakaambizana, “Ni nini anachotuambia, “muda mfupi, na hamtaniona tena,' na, kisha, mda mfupi mtaniona,' na, 'kwa sababu naenda kwa Baba?”
At this some of his disciples said among themselves. "What does he mean by telling us, ‘In a little while you shall behold me no more; and again in a little while you shall see me,’ and ‘because I am going to the Father’?"
18 Kwa hiyo wakasema, “Ni kitu gani anachosema, 'Bado mda mfupi'? Hatujui asemavyo.”
So they kept asking. "What does that ‘little while’ mean of which he speaks? We do not know what he is talking about."
19 Yesu aliona kuwa walitamani kumuuliza, naye akawaambia, “Mnajiuliza wenyewe kuhusu hili, nilivyosema, 'Bado muda mfupi, hamtaniona tena; na baada ya muda mfupi mtaniona'?
Jesus perceived that they wanted to ask him, and said. "Are you questioning one another about my saying, ‘A little while and you shall behold me no more, and again a little while you shall see me’?
20 Amin, amin, nawaambia, mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utashangilia, mtakuwa na huzuni lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
"I tell you solemnly that you will be weeping and wailing while the world is rejoicing; you will be grief-stricken, but your grief shall be turned into gladness.
21 Mwanamke anakuwa na huzuni wakati anapokuwa na uchungu kwa sababu wakati wa kujifungua umefika; lakini anapojifungua mtoto, hakumbuki tena maumivu kwa sababu ya furaha yake kwamba mtoto amezaliwa duniani.
"A woman in labor has grief because her hour is come; but when she has given birth to the babe she no longer remembers her anguish, because of joy that a child has been born into the world.
22 Ninyi pia mna huzuni sasa, lakini nitawaona tena; na mioyo yenu itafurahi na hakuna atakayeweza kuiondoa furaha yenu.
"So you also have sorrow now, but I will see you again and your heart will rejoice, and your joy shall no man snatch away from you.
23 Siku hiyo hamtaniuliza maswali. Amin, Amin, nawaambia, Mkiomba lolote kwa Baba, atawapa kwa jina langu.
"And in that day you will ask me no questions. Most solemnly I tell you that whatever you ask the Father in my name, he will give you.
24 Mpaka sasa hamjaomba lolote kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapokea ili kwamba furaha yenu ikamilike.
"Hitherto you have asked nothing in my name; ask, and you shall receive, that your joy may be full.
25 Nimezungumza na ninyi kwa lugha isiyoeleweka, lakini saa inakuja ambapo sitazungumza kwa lugha isiyoeleweka lakini badala yake nitawaambia waziwazi kuhusu Baba.
"I have told you these things in figures; but the time is coming when I shall no longer speak in figures, but will tell you about the Father in plain words.
26 Siku hiyo mtaomba kwa jina langu, na siwaambii kwamba nitaomba kwa Baba kwa ajili yenu;
"In that day you shall pray in my name; and I do not tell you that I will ask the Father on your behalf;
27 Kwa kuwa Baba mwenyewe anawapenda kwa sababu mmenipenda mimi na kwa sababu mmeniamini kuwa nimetoka kwa Baba.
"for the Father himself loves you, because you have loved me and believed that I came forth from the God.
28 Nilitoka kwa Baba na nimekuja ulimwenguni; tena, naondoka ulimwenguni na ninaenda kwa Baba”.
"I came forth from the Father, and am come into the world. again, I am leaving the world, and am going to the Father."
29 Wanafunzi wake wakamwambia, “Unaona, sasa unaongea wazi wazi na hautumii mafumbo.
"Ah," said the disciples, "now you are speaking plain language, and not using figures.
30 Sasa, tunajua kwamba unajua mambo yote, na hauhitaji mtu yoyote akuulize maswali. Kwa sababu hii tunaamini kuwa unatoka kwa Mungu.
Now we are sure that you know all things, and have no need for any one to question you; by this we believe that you came forth from God."
31 Yesu akawajibu, “Sasa mmeamini?”
"Do you now believe?" said Jesus;
32 Tazama, saa inakuja, ndiyo na hakika imefika, ambapo mtatawanyika kila mmoja na kwa wa kwao mtaniacha mwenyewe. Lakini siko peke yangu kwa sababu Baba yupo nami.
"behold the hour approaches and is already come when you will be scattered, each man to his home, and will leave me alone; and yet I am not alone, because the Father is with me.
33 Nawaambia mambo haya ili kwamba ndani yangu muwe na amani. Duniani mna matatizo, lakini jipeni moyo, nimeushinda ulimwengu.
"I have said all this to you that in me you might have peace. In the world you will have tribulation, but be courageous; I have overcome the world."

< Yohana 16 >