< Yohana 15 >
1 Mimi ni mzabibu wa huu kweli, na baba yangu ni mkulima wa mzabibu.
Y am a very vyne, and my fadir is an erthe tilier.
2 Kila tawi ndani yangu ambalo halizai tunda, na husafisha kila tawi ambalo huzaa tunda huliondoa ili kwamba liweze kuzaa zaidi.
Ech braunch in me that berith not fruyt, he schal take awey it; and ech that berith fruyt, he schal purge it, that it bere the more fruyt.
3 Ninyi tayari mmekuwa safi kwa sababu ya ujumbe ambao nimekwisha waambia.
Now ye ben clene, for the word that Y haue spokun to you.
4 Mkae ndani yangu, na mimi ndani yenu. Kama tawi lisivyoweza kuzaa peke yake lisipo kuwa katika mzabibu, kadhalika nayi, msipo kaa ndani yangu.
Dwelle ye in me, and Y in you; as a braunche may not make fruyt of it silf, but it dwelle in the vyne, so nether ye, but ye dwelle in me.
5 Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi. Adumuye ndani yangu na mimi ndani yake, mtu huyu huzaa matunda mengi, kwa kuwa pasipo mimi hamuwezi kufanya jambo lolote.
Y am a vyne, ye the braunchis. Who that dwellith in me, and Y in hym, this berith myche fruyt, for with outen me ye moun no thing do.
6 Ikiwa mtu yeyote hatasalia ndani yangu, atatupwa kama tawi na kukauka; watu hukusanya matawi na kuyatupa katika moto, na kuteketea.
If ony man dwellith not in me, he schal be caste out as a braunche, and schal wexe drie; and thei schulen gadere hym, and thei schulen caste hym in to the fier, and he brenneth.
7 Ikiwa mtadumu ndani yangu, na kama maneno yangu yakidumu ndani yenu, ombeni lolote mtakalo, nanyi mtafanyiwa.
If ye dwellen in me, and my wordis dwelle in you, what euer thing ye wolen, ye schulen axe, and it schal be don to you.
8 Katika hili baba yangu ametukuzwa, kwamba mnazaa matunda mengi na kwamba ni wanafunzi wangu.
In this thing my fadir is clarified, that ye brynge forth ful myche fruyt, and that ye be maad my disciplis.
9 Kama baba yangu alivyonipenda mimi, mimi pia nimewapenda ninyi; dumuni katika pendo langu.
As my fadir louede me, Y haue loued you; dwelle ye in my loue.
10 Ikiwa mtashika amri zangu, mtadumu katika pendo langu kama nilivyo shika amri za baba yangu na kudumu katika pendo lake.
If ye kepen my comaundementis, ye schulen dwelle in my loue; as Y haue kept the comaundementis of my fadir, and Y dwelle in his loue.
11 Nimesema mambo haya kwenu ili kwamba furaha yangu iwe ndani yenu na ili kwamba furaha yenu ifanyike kuwa timilifu.
These thingis Y spak to you, that my ioye be in you, and youre ioye be fulfillid.
12 Hii ndiyo amri yangu, kwamba mpendane ninyi kwa ninyi kama nilivyo wapenda ninyi.
This is my comaundement, that ye loue togidere, as Y louede you.
13 Hakuna mtu aliye na upendo mkuu kuliko huu, kwamba ayatoe maisha yake kwa ajiliya rafiki zake.
No man hath more loue than this, that a man putte his lijf for hise freendis.
14 Ninyi ni rafiki zangu ikiwa mtafanya yale niwaagizayo.
Ye ben my freendis if ye doen tho thingis, that Y comaunde to you.
15 Siwaiti watumwa, kwa kuwa mtumwa hajui kile afanyacho bwana wake. Nimewaita ninyi marafiki, kwa sababu nimewajulisheni mambo yote ambayo nimesikia kutoka kwa Baba.
Now Y schal not clepe you seruauntis, for the seruaunt woot not, what his lord schal do; but Y haue clepid you freendis, for alle thingis what euere Y herde of my fadir, Y haue maad knowun to you.
16 Hamkunichagua mimi, bali mimi niliwachagua ninyi na kuwaweka mwende mazae matunda, na tunda lenu lipate kukaa. Hii liko hivi ili kwamba chochote muombacho kwa Baba kwa jina langu, atawapeni.
Ye han not chosun me, but Y chees you; and Y haue put you, that ye go, and brynge forth fruyt, and youre fruyt dwelle; that what euere thing ye axen the fadir in my name, he yyue to you.
17 Mambo haya ninawaagiza, kwamba mpendane kila mtu na mwenzake.
These thingis Y comaunde to you, that ye loue togidere.
18 Kama ulimwengu utawachukia, mjuwe kwamba ulinichukia mimi kabla haujawachukia ninyi.
If the world hatith you, wite ye, that it hadde me in hate rather than you.
19 Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda kama wa kwao; Lakini kwa sababau ninyi sio wa ulimwengu na kwa sababu niliwachagua kutoka katika ulimwengu, ni kwa ajili hii ulimwengu huwachukia.
If ye hadden be of the world, the world schulde loue that thing that was his; but for ye ben not of the world, but Y chees you fro the world, therfor the world hatith you.
20 Kumbukeni neno ambalo niliwaambia, 'Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake.' Ikiwa walinitesa mimi, watawateseni ninyi pia; Kama walishika neno langu, wangelishika la kwenu pia.
Haue ye mynde of my word, which Y seide to you, The seruaunt is not grettere than his lord. If thei han pursued me, thei schulen pursue you also; if thei han kept my word, thei schulen kepe youre also.
21 Watawatendeeni mambo haya yote kwa ajili ya jina langu kwa sababu hawamjui yule aliyenituma.
But thei schulen do to you alle these thingis for my name, for thei knowen not hym that sente me.
22 Kama nisingekuja na kuwaambia waambia, wasingalikuwa wamefanya dhambi; lakini sasa hawana udhuru kwa dhambi yao.
If Y hadde not comun, and hadde not spokun to hem, thei schulden not haue synne; but now thei haue noon excusacioun of her synne.
23 Anichukiaye mimi humchukia Baba pia.
He that hatith me, hatith also my fadir.
24 Ikiwa sijafanya kazi miongoni mwao ambayo hapana mmoja aliyeifanya, wangelikuwa hawana dhambi; lakini sasa wamefanya yote mawili wameona na wamenichukia mimi na Baba yangu.
If Y hadde not doon werkis in hem, whiche noon other man dide, thei schulden not haue synne; but now both thei han seyn, and hatid me and my fadir.
25 Hili linatokea ili kwamba neno litimie ambalo limeandikwa katika sheria yao: 'Wananichukia mimi bila sababu.'
But that the word be fulfillid, that is writun in her lawe, For thei hadden me in hate with outen cause.
26 Wakati mfariji amekuja, ambaye nitamtuma kwenu kutoka kwa Baba, huyu ndiye, Roho wa kweli, ambaye anatokea kwa Baba, atanishuhudia.
But whanne the coumfortour schal come, which Y schal sende to you fro the fadir, a spirit of treuthe, which cometh of the fadir, he schal bere witnessyng of me;
27 Ninyi pia mnanishuhudia kwa sababu mmekuwa pamoja nami tangu mwanzo.
and ye schulen bere witnessyng, for ye ben with me fro the bigynnyng.