< Yohana 13 >
1 Sasa kabla ya sikukuu ya pasaka, kwa sababu Yesu alifahamu kuwa saa yake imefika ambayo atatoka katika dunia hii kwenda kwa baba, akiwa amewapenda watu wake ambao walikuwa duniani, aliwapenda upeo.
Avant la fête de Pâque, Jésus, sachant que son heure était venue de quitter ce monde pour aller vers le Père, témoigna souverainement aux siens, qui sont dans le monde, l'amour dont il les avait aimés.
2 Na ibilisi alikuwa amewekwa tayari katika moyo wa Yuda Isikariote, mwana wa simoni, kumsaliti Yesu.
Dans un repas, le diable ayant déjà mis dans le coeur de Judas Iscariote, fils de Simon, le dessein de livrer son Maître,
3 Yesu alifahamu kuwa baba ameweka vitu vyote katika mikono yake na kwamba ametoka kwa Mungu na alikuwa anakwenda tena kwa Mungu.
Jésus, qui savait que le Père avait remis toutes choses entre ses mains, qu'il était venu de Dieu et qu'il s'en allait vers Dieu,
4 Aliamka chakulani na akatandika chini vazi lake la nje. Kisha alichukua taulo na akajifunga mwenyewe.
se leva de table, posa son manteau, et, ayant pris un linge, il s'en ceignit;
5 Kisha akatia maji katika bakuli na akaanza kuwaosha miguu wanafunzi wake na kuwafuta na taulo ambayo alijifunga yeye mwenyewe.
puis, ayant versé de l'eau dans le bassin, il se mit à laver les pieds de ses disciples et à les essuyer avec le linge dont il était ceint.
6 Akaja kwa Simoni Petro, na Petro akamwambia, “Bwana, Unataka kuniosha miguu yangu?”
Il vint donc à Simon Pierre, qui lui dit: «Toi, Seigneur, me laver les pieds!»
7 Yesu akajibu na kumwambia, “Nifanyalo hulijui sasa, lakini utaelewa baadaye.”
Jésus lui répondit: «Ce que je fais, tu ne le sais pas en ce moment, mais tu le sauras tout à l'heure.»
8 Petro akamwambia, “Hutaniosha miguu yangu kamwe.” Yesu akamjibu, “Ikiwa sitakuosha, hutakuwa na sehemu pamoja nami.” (aiōn )
Pierre lui dit: «Non, jamais tu ne me laveras les pieds.» Jésus lui répondit: «Si je ne te lave, tu n'auras point de part avec moi.» (aiōn )
9 Simoni Petro akamwambia, “Bwana, usinioshe miguu yangu tuu, bali pia na mikono na kichwa changu.”
Simon Pierre lui dit: «Seigneur, non seulement les pieds, mais encore les mains et la tête.»
10 Yesu akamwambia, “Yeyote ambaye amekwisha kuoga haitaji kuoga isipokuwa miguu yake, na amekuwa safi mwili wake wote; ninyi mmekuwa safi, lakini si nyote.”
Jésus lui dit: «Celui qui s'est baigné, n'a besoin que de se laver les pieds, il est net dans toute sa personne; et vous êtes nets... mais non pas tous.»
11 Kwa kuwa Yesu alijua yule atakaye msaliti; hii ndiyo sababu alisema, si nyote mmekuwa safi.”
Il savait en effet qui était celui qui allait le livrer, c'est pourquoi il dit: «Vous n'êtes pas tous nets.»
12 Wakati Yesu alipokuwa amewaosha miguu yao na akiisha chukua vazi lake na kukaa tena, aliwaambia, “Je Mnaelewa kile ambacho nimewafanyia?
Après qu'il leur eut lavé les pieds, il reprit son manteau, et, s'étant remis à table, il leur dit: «Comprenez-vous ce que je vous ai fait?
13 Mnaniita mimi “Mwalimu” na Bwana hii mnasema kweli, maana ndivyo nilivyo.
Vous m'appelez Maître et Seigneur; et vous avez raison, car je le suis.
14 Ikiwa mimi Bwana na mwalimu, nimewaosha miguu yenu, ninyi pia imewapasa kuwaosha wenzenu miguu.
Si donc moi, le Seigneur et le Maître, je vous ai lavé les pieds, vous devez aussi vous laver les pieds les uns aux autres;
15 Kwa kuwa nimewapa mfano ili kwamba ninyi pia mfanye kama mimi nilivyo fanya kwenu.
car je vous ai donné un exemple, afin que, comme je vous ai fait, vous fassiez aussi vous-mêmes:
16 Amini, Amini, nawambia, mtumwa si mkuu kuliko bwana wake; wala yule ambaye ametumwa ni mkuu kuliko yule aliye mtuma.
en vérité, en vérité, je vous le dis, le serviteur n'est pas plus grand que son maître, ni l'envoyé plus grand que celui qui l'envoie.
17 Ikiwa unafahamu mambo haya, umebarikiwa ukiyatenda.
Si vous savez ces choses, vous êtes bienheureux, pourvu que vous les pratiquiez.
18 Sisemi kuhusu ninyi nyote, kwa kuwa nawajua wale ambao nimewachagua - bali nasema haya ili kwamba maandiko yaweze kutimilizwa: 'Yeye alaye mkate wangu ameniinulia kisigino chake.'
Je ne dis pas cela de vous tous; je connais ceux que j'ai choisis, mais il faut que cette parole de l'Ecriture soit accomplie: «Celui qui mange le pain avec moi, a levé le pied contre moi.»
19 Ninawambia hili sasa kabla halijatokea ili kwamba litakapotokea, muweze kuamini kuwa mimi NDIYE.
Je vous le dis dès à présent, avant que la chose arrive, afin que, lorsqu'elle sera arrivée, vous reconnaissiez qui je suis.
20 “Amini, amini, nawambia, anipokeaye mimi humpokea ambaye nina mtuma, na yule anipokeaye mimi humpokea yule aliye nituma mimi.”
En vérité, en vérité, je vous le dis, quiconque reçoit celui que j'envoie, me reçoit, et quiconque me reçoit, reçoit celui qui m'a envoyé.»
21 Wakati Yesu aliposema haya, alisumbuka rohoni, alishuhudia na kusema, “Amini, amini, nawambia kwamba mmoja wenu atanisaliti.”
Ayant ainsi parlé, Jésus fut ému profondément, et il dit ouvertement: «En vérité, en vérité, je vous dis que l'un de vous me livrera.»
22 Wanafunzi wake wakatazamana, wakishangaa ni kwa ajili ya nani alizungumza.
Ses disciples se regardaient les uns les autres, ne sachant de qui il voulait parler.
23 Kulikuwa katika meza, mmoja wa wanafunzi wake ameegama kifuani mwa Yesu yule ambaye Yesu alimpenda.
Or l'un d'eux était couché sur le sein de Jésus: c'était celui que Jésus aimait.
24 Simoni Petro alimuuliza mwanafunzi huyu na kusema, “Twambie ni yupi ambaye kwake anazungumza.”
Simon Pierre lui fit donc signe, pour lui dire: «De qui parle-t-il?»
25 Mwanafunzi yule aliye egama kifuani mwa Yesu na akamwambia, “Bwana, ni nani?”
Le disciple se penchant sur le sein de Jésus, lui dit: «Seigneur, qui est-ce?»
26 Kisha Yesu alijibu, “Ni kwake yule nitakaye chovya kipande cha mkate na kumpatia.” Hivyo alipo kuwa amechovya mkate, alimpatia Yuda mwana wa Simon Iskariote.
Jésus lui répondit: «C'est celui à qui je donnerai le morceau de pain que je vais tremper.» Alors ayant trempé le morceau, il le donna à Judas Iscariote, fils de Simon;
27 Na baada ya mkate, Shetani alimuingia. Kisha Yesu akamwambia, “Kile ambacho unataka kukifanya ukifanye haraka.”
et aussitôt que Judas l'eut pris, Satan entra en lui. Jésus lui dit: «Fais au plus tôt ce que tu as à faire; »
28 Sasa hakuna mtu katika meza alijua sababu ya Yesu kusema jambo hili kwake.
mais aucun de ceux qui étaient à table ne comprit pourquoi il lui disait cela:
29 Baadhi yao walidhani kwamba, kwa sababu Yuda alishika mfuko wa fedha, Yesu alimwambia, “Nunua vitu tunavyohitaji kwa ajili ya sikukuu,” au kwamba anapaswa kutoa kitu kwa masikini.
quelques-uns pensaient que, comme Judas avait la bourse, Jésus voulait lui dire: «Achète ce qu'il nous faut pour la fête, » ou qu'il lui commandait de donner quelque chose aux pauvres.
30 Baada ya Yuda kupokea mkate, alitoka nje harak; na ilikuwa usiku.
Judas, ayant pris le morceau de pain, sortit aussitôt. Il était nuit.
31 Wakati Yuda alipokuwa ameondoka, Yesu alisema, “Sasa mwana wa Adam ametukuzwa, na Mungu ametukuzwa katika yeye.
Lorsqu'il fut sorti, Jésus dit: «Maintenant le Fils de l'homme a été glorifié, et Dieu a été glorifié en lui.
32 Mungu atamtukuza katika yeye mwenyewe, na atamtukuza haraka.
Puisque Dieu a été glorifié en lui, Dieu aussi le glorifiera en lui-même, et il le glorifiera bientôt.
33 Watoto wadogo, niko pamoja nanyi kitambo kidogo. Mtanitafuta, na kama nilivyowambia Wayahudi, 'Niendako, hamuwezi kuja.' sasa nawambia ninyi, pia.
Mes chers enfants, je ne suis plus avec vous que pour un peu de temps; vous me chercherez; et comme j'ai dit aux Juifs qu'ils ne pouvaient venir où je vais, je vous le dis aussi à cette heure.
34 Ninawapa amri mpya, kwamba mpendane; kama mimi nilivyo wapenda ninyi, vivyo hivyo nanyi pia imewapasa kupendana ninyi kwa ninyi.
Je vous donne un commandement nouveau, c'est de vous aimer les uns les autres comme je vous ai aimés; vous aussi, aimez-vous les uns les autres.
35 Kwa ajili ya hili watu watatambua kuwa ninyi ni wanafunzi wangu, ikiwa mna upendo kwa kila mmoja na mwingine.”
C'est à ceci que tous connaîtront que vous êtes mes disciples, si vous avez de l'amour les uns pour les autres.
36 Simoni Petro alimwambia, “Bwana, unakwenda wapi?” Yesu akajibu, “Mahali ninapokwenda kwa sasa hutaweza kunifuata, lakini utanifuata baadaye.”
Simon Pierre lui dit: «Seigneur, où vas-tu?» Jésus lui répondit: «Là où je vais, tu ne peux me suivre maintenant; plus tard, tu me suivras.» —
37 Petro akamwambia, “Bwana, kwa nini nisikufuate hata sasa? Mimi nitayatoa maisha yangu kwa ajili yako.”
«Seigneur, lui dit Pierre, pourquoi ne puis-je te suivre à cette heure? Je donnerai ma vie pour toi.»
38 Yesu akajibu, “Je utayatoa maisha yako kwa ajili yangu? Amini amini nakwambia, jogoo hatawika kabla hujanikana mara tatu.”
Jésus lui répondit: «Tu donneras ta vie pour moi? En vérité, en vérité, je te le dis, le coq ne chantera pas, que tu ne m'aies renié trois fois.»