< Yohana 13 >
1 Sasa kabla ya sikukuu ya pasaka, kwa sababu Yesu alifahamu kuwa saa yake imefika ambayo atatoka katika dunia hii kwenda kwa baba, akiwa amewapenda watu wake ambao walikuwa duniani, aliwapenda upeo.
Before the Feast of the Passover, Jesus knew that His time had come that He should depart out of this world to the Father. Having sincerely loved His own who were in the world, He sincerely loved them to the end.
2 Na ibilisi alikuwa amewekwa tayari katika moyo wa Yuda Isikariote, mwana wa simoni, kumsaliti Yesu.
Supper was finished, and the Devil had already put it into the heart of Judas Iscariot, Simon’s son, to betray Jesus.
3 Yesu alifahamu kuwa baba ameweka vitu vyote katika mikono yake na kwamba ametoka kwa Mungu na alikuwa anakwenda tena kwa Mungu.
Jesus, knowing that the Father had given everything into His hands, and that He had come from God and was going to God,
4 Aliamka chakulani na akatandika chini vazi lake la nje. Kisha alichukua taulo na akajifunga mwenyewe.
got up from supper, laid aside His outer garment, and wrapped a towel around His waist.
5 Kisha akatia maji katika bakuli na akaanza kuwaosha miguu wanafunzi wake na kuwafuta na taulo ambayo alijifunga yeye mwenyewe.
Then He poured water into a basin and began to wash the disciples’ feet, and to wipe them with the towel that was wrapped around Him.
6 Akaja kwa Simoni Petro, na Petro akamwambia, “Bwana, Unataka kuniosha miguu yangu?”
Then He came to Simon Peter, and Peter asked Him, “Lord, are You washing my feet?”
7 Yesu akajibu na kumwambia, “Nifanyalo hulijui sasa, lakini utaelewa baadaye.”
Jesus answered, “You don’t understand what I am doing now, but you will know after this.”
8 Petro akamwambia, “Hutaniosha miguu yangu kamwe.” Yesu akamjibu, “Ikiwa sitakuosha, hutakuwa na sehemu pamoja nami.” (aiōn )
Peter told Him, “You will never wash my feet!” Jesus answered, “If I don’t wash you, you have no part with me.” (aiōn )
9 Simoni Petro akamwambia, “Bwana, usinioshe miguu yangu tuu, bali pia na mikono na kichwa changu.”
Simon Peter said to Him, “Lord, not just my feet, but also my hands and my head!”
10 Yesu akamwambia, “Yeyote ambaye amekwisha kuoga haitaji kuoga isipokuwa miguu yake, na amekuwa safi mwili wake wote; ninyi mmekuwa safi, lakini si nyote.”
Jesus said to him, “Someone who has bathed only needs to wash their feet, but is completely clean; and most of you are clean, but not all of you.”
11 Kwa kuwa Yesu alijua yule atakaye msaliti; hii ndiyo sababu alisema, si nyote mmekuwa safi.”
For He knew who would betray Him, therefore He said, “You aren’t all clean.”
12 Wakati Yesu alipokuwa amewaosha miguu yao na akiisha chukua vazi lake na kukaa tena, aliwaambia, “Je Mnaelewa kile ambacho nimewafanyia?
When He had washed their feet, He put on His outer garment and sat down again. He asked them, “Do you know what I have done to you?
13 Mnaniita mimi “Mwalimu” na Bwana hii mnasema kweli, maana ndivyo nilivyo.
You call me Teacher and Lord, and you are right in saying so, for so I am.
14 Ikiwa mimi Bwana na mwalimu, nimewaosha miguu yenu, ninyi pia imewapasa kuwaosha wenzenu miguu.
If I, your Lord and Teacher, have washed your feet, you also ought to wash one another’s feet.
15 Kwa kuwa nimewapa mfano ili kwamba ninyi pia mfanye kama mimi nilivyo fanya kwenu.
I have given you an example, that you should also do as I have done to you.
16 Amini, Amini, nawambia, mtumwa si mkuu kuliko bwana wake; wala yule ambaye ametumwa ni mkuu kuliko yule aliye mtuma.
Most assuredly, I tell you, a servant isn’t greater than his master, nor is he who is sent greater than he who sent him.
17 Ikiwa unafahamu mambo haya, umebarikiwa ukiyatenda.
If you know these things, you are blessed if you do them.
18 Sisemi kuhusu ninyi nyote, kwa kuwa nawajua wale ambao nimewachagua - bali nasema haya ili kwamba maandiko yaweze kutimilizwa: 'Yeye alaye mkate wangu ameniinulia kisigino chake.'
I’m not talking about all of you. I know who I have chosen; but this is to fulfill the Scripture, ‘He who eats bread with me has lifted up his heel against me.’
19 Ninawambia hili sasa kabla halijatokea ili kwamba litakapotokea, muweze kuamini kuwa mimi NDIYE.
Now I tell you before it happens, that when it does happen, you may believe that I AM.
20 “Amini, amini, nawambia, anipokeaye mimi humpokea ambaye nina mtuma, na yule anipokeaye mimi humpokea yule aliye nituma mimi.”
Most assuredly, I tell you, whoever receives anyone I send receives me; and he who receives me receives Him who sent me.”
21 Wakati Yesu aliposema haya, alisumbuka rohoni, alishuhudia na kusema, “Amini, amini, nawambia kwamba mmoja wenu atanisaliti.”
When Jesus had said these things, He was troubled in spirit, and testified and said, “Most assuredly, I tell you, one of you will betray me.”
22 Wanafunzi wake wakatazamana, wakishangaa ni kwa ajili ya nani alizungumza.
The disciples began looking at one another, perplexed about which one of them He was talking about.
23 Kulikuwa katika meza, mmoja wa wanafunzi wake ameegama kifuani mwa Yesu yule ambaye Yesu alimpenda.
One of Jesus’ disciples, who Jesus sincerely loved, was leaning against His breast.
24 Simoni Petro alimuuliza mwanafunzi huyu na kusema, “Twambie ni yupi ambaye kwake anazungumza.”
Simon Peter therefore nodded to him to ask who He spoke about.
25 Mwanafunzi yule aliye egama kifuani mwa Yesu na akamwambia, “Bwana, ni nani?”
Then, leaning back on Jesus’ breast, he asked Him, “Lord, who is it?”
26 Kisha Yesu alijibu, “Ni kwake yule nitakaye chovya kipande cha mkate na kumpatia.” Hivyo alipo kuwa amechovya mkate, alimpatia Yuda mwana wa Simon Iskariote.
Jesus answered, “It is he who I will give a morsel to when I have dipped it.” Having dipped the morsel, He gave it to Judas Iscariot, Simon’s son.
27 Na baada ya mkate, Shetani alimuingia. Kisha Yesu akamwambia, “Kile ambacho unataka kukifanya ukifanye haraka.”
After the morsel, Satan entered into him. Jesus therefore told him, “What you do, do quickly.”
28 Sasa hakuna mtu katika meza alijua sababu ya Yesu kusema jambo hili kwake.
None of those reclining at the table knew why He had said this to him.
29 Baadhi yao walidhani kwamba, kwa sababu Yuda alishika mfuko wa fedha, Yesu alimwambia, “Nunua vitu tunavyohitaji kwa ajili ya sikukuu,” au kwamba anapaswa kutoa kitu kwa masikini.
Some were supposing, because Judas had the money box, that Jesus was saying to him, “Buy the things we need for the feast”; or else, that he should give something to the poor.
30 Baada ya Yuda kupokea mkate, alitoka nje harak; na ilikuwa usiku.
Having received the morsel, he went out immediately. It was night.
31 Wakati Yuda alipokuwa ameondoka, Yesu alisema, “Sasa mwana wa Adam ametukuzwa, na Mungu ametukuzwa katika yeye.
When he had gone out, Jesus said, “Now the Son of Man is glorified, and God is glorified in Him.
32 Mungu atamtukuza katika yeye mwenyewe, na atamtukuza haraka.
If God is glorified in Him, God will also glorify Him in Himself, and will glorify Him immediately.
33 Watoto wadogo, niko pamoja nanyi kitambo kidogo. Mtanitafuta, na kama nilivyowambia Wayahudi, 'Niendako, hamuwezi kuja.' sasa nawambia ninyi, pia.
Little children, I am with you a little while longer. You will look for me, and as I told the Jews, I now tell you, also, ‘Where I am going, you can’t come.’
34 Ninawapa amri mpya, kwamba mpendane; kama mimi nilivyo wapenda ninyi, vivyo hivyo nanyi pia imewapasa kupendana ninyi kwa ninyi.
I give to you a new commandment, that you sincerely love one another, even as I have sincerely loved you, so you should also sincerely love one another.
35 Kwa ajili ya hili watu watatambua kuwa ninyi ni wanafunzi wangu, ikiwa mna upendo kwa kila mmoja na mwingine.”
By this everyone will know that you are my disciples, if you have sincere love for one another.”
36 Simoni Petro alimwambia, “Bwana, unakwenda wapi?” Yesu akajibu, “Mahali ninapokwenda kwa sasa hutaweza kunifuata, lakini utanifuata baadaye.”
Simon Peter asked Him, “Lord, where are You going?” Jesus answered, “Where I go, you aren’t able to follow me now, but you will follow later.”
37 Petro akamwambia, “Bwana, kwa nini nisikufuate hata sasa? Mimi nitayatoa maisha yangu kwa ajili yako.”
Peter asked Him, “Lord, why can’t I follow You right now? I will lay down my life for You.”
38 Yesu akajibu, “Je utayatoa maisha yako kwa ajili yangu? Amini amini nakwambia, jogoo hatawika kabla hujanikana mara tatu.”
Jesus answered, “Will you lay down your life for my sake? Most assuredly, I tell you, the rooster won’t crow until you have denied me three times.