< Yohana 13 >

1 Sasa kabla ya sikukuu ya pasaka, kwa sababu Yesu alifahamu kuwa saa yake imefika ambayo atatoka katika dunia hii kwenda kwa baba, akiwa amewapenda watu wake ambao walikuwa duniani, aliwapenda upeo.
And before the feast of the passover, Jesus knowing that the hour has come when He must depart out of this world to His Father, having loved His own who were in the world, with divine love, He loved them perfectly.
2 Na ibilisi alikuwa amewekwa tayari katika moyo wa Yuda Isikariote, mwana wa simoni, kumsaliti Yesu.
And the supper being on hand, the devil already having entered into the heart, that Judas Iscariot, the son of Simon, should betray Him,
3 Yesu alifahamu kuwa baba ameweka vitu vyote katika mikono yake na kwamba ametoka kwa Mungu na alikuwa anakwenda tena kwa Mungu.
knowing that the Father has given all things into His hands, and He came out from God, and is going away to God,
4 Aliamka chakulani na akatandika chini vazi lake la nje. Kisha alichukua taulo na akajifunga mwenyewe.
He rises from the supper, and lays aside His garments, and taking a towel, girded Himself;
5 Kisha akatia maji katika bakuli na akaanza kuwaosha miguu wanafunzi wake na kuwafuta na taulo ambayo alijifunga yeye mwenyewe.
then He pours water into a bowl, and began to wash the feet of the disciples, and to wipe them with the towel with which He was girded.
6 Akaja kwa Simoni Petro, na Petro akamwambia, “Bwana, Unataka kuniosha miguu yangu?”
Then He comes to Simon Peter; he says to Him; Lord, do you wash my feet?
7 Yesu akajibu na kumwambia, “Nifanyalo hulijui sasa, lakini utaelewa baadaye.”
Jesus responded and said to him, What I do you know not now; but shall understand hereafter.
8 Petro akamwambia, “Hutaniosha miguu yangu kamwe.” Yesu akamjibu, “Ikiwa sitakuosha, hutakuwa na sehemu pamoja nami.” (aiōn g165)
Peter says to Him, You may never wash my feet. Jesus responded to him, If I wash thee not, thou hast not part with me. (aiōn g165)
9 Simoni Petro akamwambia, “Bwana, usinioshe miguu yangu tuu, bali pia na mikono na kichwa changu.”
And Simon Peter says to Him, Lord, not only my feet, but my hands and my head.
10 Yesu akamwambia, “Yeyote ambaye amekwisha kuoga haitaji kuoga isipokuwa miguu yake, na amekuwa safi mwili wake wote; ninyi mmekuwa safi, lakini si nyote.”
Jesus says to Him, He that is bathed hath no need to wash his hands, but is altogether clean: and you are clean, but not all.
11 Kwa kuwa Yesu alijua yule atakaye msaliti; hii ndiyo sababu alisema, si nyote mmekuwa safi.”
For He knew the one betraying Him. On this account He said, You are not all clean.
12 Wakati Yesu alipokuwa amewaosha miguu yao na akiisha chukua vazi lake na kukaa tena, aliwaambia, “Je Mnaelewa kile ambacho nimewafanyia?
Then when He washed their feet, and took His garments, and sat down again, He said to them, Do you understand what I have done to you?
13 Mnaniita mimi “Mwalimu” na Bwana hii mnasema kweli, maana ndivyo nilivyo.
You call me Master and Lord, and you speak beautifully; for I am.
14 Ikiwa mimi Bwana na mwalimu, nimewaosha miguu yenu, ninyi pia imewapasa kuwaosha wenzenu miguu.
If then I, your Lord and Master, washed your feet, you ought also to wash the feet of one another.
15 Kwa kuwa nimewapa mfano ili kwamba ninyi pia mfanye kama mimi nilivyo fanya kwenu.
For I have given unto you an example, that you may also do as I have done to you.
16 Amini, Amini, nawambia, mtumwa si mkuu kuliko bwana wake; wala yule ambaye ametumwa ni mkuu kuliko yule aliye mtuma.
Truly, truly, I say unto you, The servant is not greater than his lord; nor the apostle greater than him that sent him.
17 Ikiwa unafahamu mambo haya, umebarikiwa ukiyatenda.
If you know these things, happy are ye if you may do them.
18 Sisemi kuhusu ninyi nyote, kwa kuwa nawajua wale ambao nimewachagua - bali nasema haya ili kwamba maandiko yaweze kutimilizwa: 'Yeye alaye mkate wangu ameniinulia kisigino chake.'
I do not speak concerning you all: I know whom I have chosen: but that the Scripture may be fulfilled, He that eateth bread with me has lifted up his heel against me.
19 Ninawambia hili sasa kabla halijatokea ili kwamba litakapotokea, muweze kuamini kuwa mimi NDIYE.
Now I tell you before it takes place, in order that you may believe, when it may be done, that I am He.
20 “Amini, amini, nawambia, anipokeaye mimi humpokea ambaye nina mtuma, na yule anipokeaye mimi humpokea yule aliye nituma mimi.”
Truly, truly, I say unto you, The one receiving the one whom I may send, receiveth me; and the one receiving me, receives Him that sent me.
21 Wakati Yesu aliposema haya, alisumbuka rohoni, alishuhudia na kusema, “Amini, amini, nawambia kwamba mmoja wenu atanisaliti.”
Jesus saying these things, was troubled in spirit, and testified, and said; Truly, truly, I say unto you, that one of you shall betray me.
22 Wanafunzi wake wakatazamana, wakishangaa ni kwa ajili ya nani alizungumza.
Then the disciples began to look to one another, being at a loss concerning which one He speaks.
23 Kulikuwa katika meza, mmoja wa wanafunzi wake ameegama kifuani mwa Yesu yule ambaye Yesu alimpenda.
And one of His disciples, whom Jesus loved, was leaning on the bosom of Jesus.
24 Simoni Petro alimuuliza mwanafunzi huyu na kusema, “Twambie ni yupi ambaye kwake anazungumza.”
Then Simon Peter beckons to him, to ask who he might be concerning whom He speaks.
25 Mwanafunzi yule aliye egama kifuani mwa Yesu na akamwambia, “Bwana, ni nani?”
And that one, falling toward the bosom of Jesus says to Him, Lord, who is he?
26 Kisha Yesu alijibu, “Ni kwake yule nitakaye chovya kipande cha mkate na kumpatia.” Hivyo alipo kuwa amechovya mkate, alimpatia Yuda mwana wa Simon Iskariote.
And Jesus responds, He is that one to whom, having dipped the morsel, I will give it. And having dipped the morsel, He takes it, and gives it to Judas Iscariot, the son of Simon.
27 Na baada ya mkate, Shetani alimuingia. Kisha Yesu akamwambia, “Kile ambacho unataka kukifanya ukifanye haraka.”
And after the morsel, Satan entered into him. Then Jesus says to him; What thou art doing, do more quickly.
28 Sasa hakuna mtu katika meza alijua sababu ya Yesu kusema jambo hili kwake.
And no one of those sitting with Him knew what He said to him:
29 Baadhi yao walidhani kwamba, kwa sababu Yuda alishika mfuko wa fedha, Yesu alimwambia, “Nunua vitu tunavyohitaji kwa ajili ya sikukuu,” au kwamba anapaswa kutoa kitu kwa masikini.
for some thought, as Judas had the purse, that Jesus says to him, Purchase some of those things of which we have need at the supper; or something that he might give to the poor.
30 Baada ya Yuda kupokea mkate, alitoka nje harak; na ilikuwa usiku.
Then he having taken the morsel, went out immediately: and it was night.
31 Wakati Yuda alipokuwa ameondoka, Yesu alisema, “Sasa mwana wa Adam ametukuzwa, na Mungu ametukuzwa katika yeye.
Then when he went out, Jesus says, Now is the Son of man glorified, and God is glorified in Him.
32 Mungu atamtukuza katika yeye mwenyewe, na atamtukuza haraka.
And if God is glorified in Him, God will indeed glorify Him in Himself, and will glorify Him immediately.
33 Watoto wadogo, niko pamoja nanyi kitambo kidogo. Mtanitafuta, na kama nilivyowambia Wayahudi, 'Niendako, hamuwezi kuja.' sasa nawambia ninyi, pia.
Children, I am still with you. You shall seek me, and as I said to the Jews, Whither I go, you are not able to come; and now I say to you.
34 Ninawapa amri mpya, kwamba mpendane; kama mimi nilivyo wapenda ninyi, vivyo hivyo nanyi pia imewapasa kupendana ninyi kwa ninyi.
I give unto a new commandment, That you must love one another with divine love; as I have loved you with divine love, that you must also love one another with divine love:
35 Kwa ajili ya hili watu watatambua kuwa ninyi ni wanafunzi wangu, ikiwa mna upendo kwa kila mmoja na mwingine.”
in this shall all know that you are my disciples, if you may have divine love one with another.
36 Simoni Petro alimwambia, “Bwana, unakwenda wapi?” Yesu akajibu, “Mahali ninapokwenda kwa sasa hutaweza kunifuata, lakini utanifuata baadaye.”
Simon Peter says to Him; Lord, whither do you go? Jesus responded, Whither I go you are not able to follow me now; but shall follow me hereafter.
37 Petro akamwambia, “Bwana, kwa nini nisikufuate hata sasa? Mimi nitayatoa maisha yangu kwa ajili yako.”
Peter says to Him; Lord, why am I not able to follow thee now? I will lay down my soul for thee.
38 Yesu akajibu, “Je utayatoa maisha yako kwa ajili yangu? Amini amini nakwambia, jogoo hatawika kabla hujanikana mara tatu.”
Jesus responds to him, Wilt thou lay down thy soul for me? Truly, truly, I say unto thee, that the cock shall not crow, until thou shalt thrice deny me.

< Yohana 13 >