< Yohana 12 >

1 Siku sita kabla ya Pasaka, Yesu alienda Bethania, alipokuwapo Lazaro, yeye ambaye alimfufua kutoka katika wafu.
Jesus, therefore, six days before the Passover, came to Bethany, where Lazarus was, who had died, whom He raised out of the dead;
2 Basi wakamwandalia chakula cha jioni huko, na Martha akamtumikia, wakati huo Lazaro alikuwa mmoja wapo wa wale walioketi chakulani pamoja na Yesu.
they made, therefore, a dinner to Him there, and Martha was ministering, and Lazarus was one of those reclining together with Him;
3 Kisha Mariamu akachukua ratli ya manukato yaliyotengenezwa kwa nardo safi, yenye thamani kubwa, akampaka Yesu miguuni, na kumfuta miguu kwa nywele zake; nyumba yote ilijaa harufu ya manukato.
Mary, therefore, having taken a pound of ointment of spikenard, of great price, anointed the feet of Jesus and wiped His feet with her hair, and the house was filled from the fragrance of the ointment.
4 Yuda Iskariote, mmoja wa wale wanafunzi wake, ambaye ndiye atakayemsaliti Yesu, akasema,
Therefore one of His disciples—Judas Iscariot, of Simon, who is about to deliver Him up—says,
5 “Kwanini manukato haya yasingeuzwa kwa dinari mia tatu na wakapewa maskini?”
“Why was this ointment not sold for three hundred denarii, and given to the poor?”
6 Naye aliyasema hayo, si kwa kuwahurumia maskini, bali kwa sababu alikuwa mwizi: yeye ndiye aliyeshika mfuko wa fedha na alikuwa anachukua baadhi ya vilivyowekwa humo kwa ajili yake mwenyewe.
And he said this, not because he was caring for the poor, but because he was a thief, and had the bag, and what things were put in he was carrying.
7 Yesu alisema, “Mwache aweke alicho nacho kwa ajili ya siku ya maziko yangu.
Jesus, therefore, said, “Permit her; she has kept it for the day of My embalming,
8 Maskini mtakuwa nao siku zote; lakini hamtakuwa nami siku zote.”
for you always have the poor with yourselves, and you do not always have Me.”
9 Basi umati mkubwa wa Wayahudi walipata kujua ya kuwa Yesu yuko huko, nao wakaja, si kwa ajili ya Yesu tu, ila wamwone na Lazaro ambaye Yesu alimfufua kutoka katika wafu.
Therefore, a great multitude of the Jews knew that He is there, and they came, not only because of Jesus, but that they may also see Lazarus, whom He raised out of the dead;
10 Nao wakuu wa makuhani wakafanya shauri ili wamue Lazaro;
and the chief priests took counsel, that they may also kill Lazarus,
11 maana kwa ajili yake wengi katika Wayahudi walienda zao na wakamwamini Yesu.
because on account of him many of the Jews were going away, and were believing in Jesus.
12 Na siku ya pili yake umati mkubwa walikuja kwenye sikukuu. Waliposikia ya kuwa Yesu anakuja Yerusalemu,
On the next day, a great multitude that came to the celebration, having heard that Jesus comes to Jerusalem,
13 walichukua matawi ya miti ya mitende na kutoka nje kwenda kumlaki na wakapiga kelele, “Hosana! Amebarikiwa yeye ajaye kwa jina la Bwana, Mfalme wa Israeli.”
took the branches of the palms, and went forth to meet Him, and were crying, “Hosanna! Blessed [is] He who is coming in the Name of the LORD—the King of Israel”;
14 Yesu alimpata mwana-punda akampanda; kama vile ilivyoandikwa,
and Jesus having found a young donkey sat on it, according as it is written,
15 “Usiogope, binti Sayuni; tazama, Mfalme wako anakuja, amepanda mwana-punda.”
“Do not fear, daughter of Zion, behold, your King comes, sitting on a colt of a donkey.”
16 Wanafunzi wake hawakuyaelewa mambo haya hapo kwanza; lakini Yesu alipotukuzwa, ndipo walipokumbuka ya kuwa mambo haya aliandikiwa yeye na ya kwamba wametenda mambo haya kwake.
And His disciples did not know these things at first, but when Jesus was glorified, then they remembered that these things were having been written about Him, and these things they did to Him.
17 Basi lile kundi la watu waliokuwepo pamoja na Yesu wakati alipomwita Lazaro kutoka kaburini, wakashuhudia kwa wengine.
The multitude, therefore, who are with Him, were testifying that He called Lazarus out of the tomb, and raised him out of the dead;
18 Na ilikuwa kwa sababu hii pia kwamba kundi la watu walikwenda kumlaki kwasababu walisikia ya kwamba ameifanya ishara hiyo.
because of this the multitude also met Him, because they heard of His having done this sign,
19 Mafarisayo wakasemezana wao kwa wao, “Tazama, sasa hamwezi kufanya lolote; tazama, ulimwengu umekwenda kwake.”
therefore the Pharisees said among themselves, “You see that you do not gain anything, behold, the world went after Him.”
20 Sasa baadhi ya Wayunani walikuwa miongoni mwa wale waliokuwa wakienda kuabudu kwenye sikukuu.
And there were certain Greeks out of those coming up that they may worship in the celebration,
21 Hawa walimwendea Filipo, ambaye alitoka Bethsaida ya Galilaya, wakamwomba wakisema, “Bwana, sisi tunatamani kumwona Yesu.”
these then came near to Philip, who [is] from Bethsaida of Galilee, and were asking him, saying, “Lord, we wish to see Jesus”;
22 Filipo akaenda akamwambia Andrea; Andrea na Filipo wakaenda na kumwambia Yesu.
Philip comes and tells Andrew, and again Andrew and Philip tell Jesus.
23 Yesu akawajibu akasema, “Saa imefika kwa ajili ya Mwana wa Adamu kutukuzwa.
And Jesus responded to them, saying, “The hour has come that the Son of Man may be glorified;
24 Amini, amini, nawaambia, chembe ya ngano isipoanguka katika nchi ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, itazaa matunda mengi.
truly, truly, I say to you, if the grain of the wheat, having fallen to the earth, may not die, itself remains alone; and if it may die, it bears much fruit;
25 Yeye apendaye uhai wake ataupoteza; bali yeye auchukiaye uhai wake katika ulimemngu huu atausalimisha hata uzima wa milele. (aiōnios g166)
he who is cherishing his life will lose it, and he who is hating his life in this world will keep it to continuous life; (aiōnios g166)
26 Mtu yeyote akinitumikia mimi, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Mtu yeyote akinitumikia, Baba atamheshimu.
if anyone may minister to Me, let him follow Me, and where I am, there My servant will be also; and if anyone may minister to Me—the Father will honor him.
27 Sasa roho yangu imefadhaika: nami nisemeje? 'Baba, uniokoe katika saa hii'? Lakini ni kwa kusudi hii nimeifikia saa hii.
Now My soul has been troubled; and what will I say—Father, save Me from this hour? But because of this I came to this hour;
28 Baba, ulitukuze jina lako.” Kisha sauti ikaja kutoka mbinguni na kusema, “Nimelitukuza nami nitalitukuza tena.”
Father, glorify Your Name.” Therefore there came a voice out of Heaven, “I both glorified, and again I will glorify [it]”;
29 Basi mkutano uliosimama karibu naye wakasikia, wakasema ya kwamba kumekuwa ngurumo. Wengine walisema, “Malaika amesema naye.”
the multitude, therefore, having stood and heard, were saying that there has been thunder; others said, “A messenger has spoken to Him.”
30 Yesu akajibu na kusema, “Sauti hii haikuja kwa ajili yangu, bali kwa ajili yenu.
Jesus answered and said, “This voice has not come because of Me, but because of you;
31 Sasa hukumu ya ulimwengu huu ipo: Sasa mkuu wa ulimwngu huu atatupwa nje.
now is a judgment of this world, now will the ruler of this world be cast forth;
32 Nami nikiinuliwa juu ya nchi, nitawavuta wote kwangu.”
and I, if I may be lifted up from the earth, will draw all men to Myself.”
33 Aliyanena hayo akionesha ni mauti gani atakayokufa.
And this He said signifying by what death He was about to die;
34 Mkutano wakamjibu, “Sisi tumesikia katika sheria ya kwamba Kristo atadumu hata milele. Nawe wasemaje, 'Mwana Adamu lazima ainuliwe juu'? Huyu Mwana wa Mtu ni nani?” (aiōn g165)
the multitude answered Him, “We heard that the Christ remains out of the Law—throughout the age; and how do You say that it is required that the Son of Man be lifted up? Who is this—the Son of Man?” (aiōn g165)
35 Basi Yesu akawaambia, “Nuru ingalipo pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru, ili kwamba giza lisije likawaweza. Yeye aendaye gizani hajui aendako.
Therefore Jesus said to them, “Yet a short time is the light with you; walk while you have the light, that darkness may not overtake you; and he who is walking in the darkness has not known where he goes;
36 Mngali mnayo nuru, iaminini nuru hiyo ili mpate kuwa wana wa nuru.” Yesu aliyasema haya na kisha akaenda zake akajificha wasimwone.
while you have the light, believe in the light, that you may become sons of light.” Jesus spoke these things, and having gone away, He was hid from them,
37 Ingawa Yesu alifanya ishara nyingi namna hiyo mbele yao, bado hawakumwamini
yet He, having done so many signs before them, they were not believing in Him,
38 ili litimie neno la nabii Isaya, alilosema: “Bwana, ni nani aliyezisadiki habari zetu? Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani?”
that the word of Isaiah the prophet might be fulfilled, which he said, “LORD, who gave credence to our report? And the arm of the LORD—to whom was it revealed?”
39 Ndio sababu wao hawakuamini, maana Isaya alisema tena,
Because of this they were not able to believe, that again Isaiah said,
40 “Amewapofusha macho, na ameifanya migumu mioyo yao; wasije wakaona kwa macho yao na wakafahamu kwa mioyo yao, na wakaongoka nami nikawaponya.”
“He has blinded their eyes, and hardened their heart, that they might not see with the eyes, and understand with the heart, and turn, and I might heal them”;
41 Isaya alisema maneno hayo kwa kuwa aliuona utukufu wa Yesu na akanena habari zake.
Isaiah said these things when he saw His glory, and spoke of Him.
42 Walakini, hata wakuu wengi walimwamini Yesu; lakini kwa sababu ya Mafarisayo, hawakukiri ili wasije wakatengwa na sinagogi.
Still, however, out of the rulers many also believed in Him, but because of the Pharisees they were not confessing, that they might not be put out of the synagogue,
43 Walipenda sifa za wanadamu kuliko sifa zitokazo kwa Mungu.
for they loved the glory of men more than the glory of God.
44 Yesu akapaza sauti na kusema, “Yeye aniaminiye mimi, haniamini mimi tu bali na yeye aliyenituma mimi,
And Jesus cried and said, “He who is believing in Me, does not believe in Me, but in Him who sent Me;
45 naye anionaye mimi anamuona yeye aliyenituma.
and He who is beholding Me, beholds Him who sent Me;
46 Mimi nimekuja kama nuru ulimwenguni ili kila mtu aniaminiye mimi asikae gizani.
I—light to the world—have come, that everyone who is believing in Me may not remain in the darkness;
47 Ikiwa mtu yeyote atayasikia maneno yangu lakini asiyashike, mimi simhukumu; maana sikuja ili niuhukumu ulimwengu, bali niuokoe ulimwengu.
and if anyone may hear My sayings, and not believe, I do not judge him, for I did not come that I might judge the world, but that I might save the world.
48 Yeye anikataye mimi na asiyeyakubali maneno yangu, anaye amhukumuye: neno hilo nililolinena ndilo litakalomhukumu siku ya mwisho.
He who is rejecting Me, and not receiving My sayings, has one who is judging him, the word that I spoke, that will judge him in the last day,
49 Maana mimi sikunena kwa nafsi yangu tu. Bali ni Baba aliyenipeleka, yeye mwenyewe ameniagiza nitakayonena na nitakayosema.
because I did not speak from Myself, but the Father who sent Me, He gave Me a command, what I may say, and what I may speak,
50 Nami najua ya kuwa agizo lake ni uzima wa milele; basi hayo ninenayo mimi - kama Baba alivyoniambia, ndivyo ninenavyo kwao.” (aiōnios g166)
and I have known that His command is continuous life; what, therefore, I speak, according as the Father has said to Me, so I speak.” (aiōnios g166)

< Yohana 12 >