< Yohana 12 >
1 Siku sita kabla ya Pasaka, Yesu alienda Bethania, alipokuwapo Lazaro, yeye ambaye alimfufua kutoka katika wafu.
Then Jesus, six days before the passover came into Bethany, where Lazarus, whom Jesus raised from the dead, was,
2 Basi wakamwandalia chakula cha jioni huko, na Martha akamtumikia, wakati huo Lazaro alikuwa mmoja wapo wa wale walioketi chakulani pamoja na Yesu.
Then they made a supper for Him there: and Martha was serving; and Lazarus was one of those sitting at the table with Him.
3 Kisha Mariamu akachukua ratli ya manukato yaliyotengenezwa kwa nardo safi, yenye thamani kubwa, akampaka Yesu miguuni, na kumfuta miguu kwa nywele zake; nyumba yote ilijaa harufu ya manukato.
Then Mary taking a pound of myrrh of spikenard, estimated very valuable, anointed the feet of Jesus, and wiped His feet with her hair: and the house was filled with the odor of the myrrh.
4 Yuda Iskariote, mmoja wa wale wanafunzi wake, ambaye ndiye atakayemsaliti Yesu, akasema,
Then Judas Iscariot, one of His disciples, the one about to betray Him, says:
5 “Kwanini manukato haya yasingeuzwa kwa dinari mia tatu na wakapewa maskini?”
Why was not this myrrh sold for three hundred denaria, and given to the poor?
6 Naye aliyasema hayo, si kwa kuwahurumia maskini, bali kwa sababu alikuwa mwizi: yeye ndiye aliyeshika mfuko wa fedha na alikuwa anachukua baadhi ya vilivyowekwa humo kwa ajili yake mwenyewe.
And He spoke this, not because there was a care to him for the poor; but because he was a thief, and had the purse, and was carrying those things cast in.
7 Yesu alisema, “Mwache aweke alicho nacho kwa ajili ya siku ya maziko yangu.
Then Jesus said, Let her alone; she hath reserved this unto the day of my burial;
8 Maskini mtakuwa nao siku zote; lakini hamtakuwa nami siku zote.”
for you have the poor always with you; but you have not me always.
9 Basi umati mkubwa wa Wayahudi walipata kujua ya kuwa Yesu yuko huko, nao wakaja, si kwa ajili ya Yesu tu, ila wamwone na Lazaro ambaye Yesu alimfufua kutoka katika wafu.
then a great multitude of the Jews came not only on account of Jesus, but that they might see Lazarus, whom He raised from the dead; because he was there.
10 Nao wakuu wa makuhani wakafanya shauri ili wamue Lazaro;
But the chief priest passed an edict that they would also slay Lazarus;
11 maana kwa ajili yake wengi katika Wayahudi walienda zao na wakamwamini Yesu.
because through him many of the Jews went away, and believed on Jesus.
12 Na siku ya pili yake umati mkubwa walikuja kwenye sikukuu. Waliposikia ya kuwa Yesu anakuja Yerusalemu,
On the following day a great multitude having come to the feast, hearing that Jesus comes into Jerusalem,
13 walichukua matawi ya miti ya mitende na kutoka nje kwenda kumlaki na wakapiga kelele, “Hosana! Amebarikiwa yeye ajaye kwa jina la Bwana, Mfalme wa Israeli.”
They took the branches of the palm-trees, and went out to meet Him, and continued to cry out, Hosanna: blessed is He that cometh, in the name of the Lord, the King of Israel.
14 Yesu alimpata mwana-punda akampanda; kama vile ilivyoandikwa,
And Jesus, having found a young donkey, sat upon him, as has been written,
15 “Usiogope, binti Sayuni; tazama, Mfalme wako anakuja, amepanda mwana-punda.”
Fear not, daughter of Zion: behold, thy King cometh, sitting upon the colt of a donkey.
16 Wanafunzi wake hawakuyaelewa mambo haya hapo kwanza; lakini Yesu alipotukuzwa, ndipo walipokumbuka ya kuwa mambo haya aliandikiwa yeye na ya kwamba wametenda mambo haya kwake.
But His disciples at first did not understand these things: but when Jesus was glorified, then they remembered that these things were written in reference to Him, and they did them to Him.
17 Basi lile kundi la watu waliokuwepo pamoja na Yesu wakati alipomwita Lazaro kutoka kaburini, wakashuhudia kwa wengine.
Then the multitude being with Him witnessed that He called Lazarus out of the sepulcher, and raised him from the dead.
18 Na ilikuwa kwa sababu hii pia kwamba kundi la watu walikwenda kumlaki kwasababu walisikia ya kwamba ameifanya ishara hiyo.
Therefore the multitude also went to meet Him, because they heard that He had wrought this miracle.
19 Mafarisayo wakasemezana wao kwa wao, “Tazama, sasa hamwezi kufanya lolote; tazama, ulimwengu umekwenda kwake.”
Then the Pharisees said to one another, You see, that you are prevailing as to nothing: behold, the world has gone away after Him.
20 Sasa baadhi ya Wayunani walikuwa miongoni mwa wale waliokuwa wakienda kuabudu kwenye sikukuu.
And there was certain Greeks of those having come up that they might worship at the feast:
21 Hawa walimwendea Filipo, ambaye alitoka Bethsaida ya Galilaya, wakamwomba wakisema, “Bwana, sisi tunatamani kumwona Yesu.”
then they came to Philip, who was from Bethsaida of Galilee, and requested him, saying, Sir, we wish to see Jesus.
22 Filipo akaenda akamwambia Andrea; Andrea na Filipo wakaenda na kumwambia Yesu.
Philip comes and tells Andrew: Andrew and Philip go, and speak to Jesus.
23 Yesu akawajibu akasema, “Saa imefika kwa ajili ya Mwana wa Adamu kutukuzwa.
And Jesus responds to them, saying, The hour has come, that the Son of man may be glorified.
24 Amini, amini, nawaambia, chembe ya ngano isipoanguka katika nchi ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, itazaa matunda mengi.
Truly, truly, I say unto you, Unless the grain of wheat having fallen into the ground may die, it remains alone; but if it may die, it produces much fruit.
25 Yeye apendaye uhai wake ataupoteza; bali yeye auchukiaye uhai wake katika ulimemngu huu atausalimisha hata uzima wa milele. (aiōnios )
The one loving his soul shall lose it; but the one that hateth his soul in this world will preserve it unto eternal life. (aiōnios )
26 Mtu yeyote akinitumikia mimi, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Mtu yeyote akinitumikia, Baba atamheshimu.
If any one may minister unto me, let him follow me; and where I am, there shall my minister be: if any one may minister unto me, the Father will honor him.
27 Sasa roho yangu imefadhaika: nami nisemeje? 'Baba, uniokoe katika saa hii'? Lakini ni kwa kusudi hii nimeifikia saa hii.
Now my soul is troubled; and what do I say? Father, save me from this hour. But on this account I came to this hour.
28 Baba, ulitukuze jina lako.” Kisha sauti ikaja kutoka mbinguni na kusema, “Nimelitukuza nami nitalitukuza tena.”
Father, glorify thy name. Then a voice came from heaven, I have indeed glorified thee, and will glorify thee again.
29 Basi mkutano uliosimama karibu naye wakasikia, wakasema ya kwamba kumekuwa ngurumo. Wengine walisema, “Malaika amesema naye.”
Then the multitudes standing, hearing, said, That it was thunder; others said, An angel has spoken to Him.
30 Yesu akajibu na kusema, “Sauti hii haikuja kwa ajili yangu, bali kwa ajili yenu.
Jesus responded and said, This voice was not on account of me, but on account of you.
31 Sasa hukumu ya ulimwengu huu ipo: Sasa mkuu wa ulimwngu huu atatupwa nje.
Now is the judgment of this world: now the prince of this world shall be cast out.
32 Nami nikiinuliwa juu ya nchi, nitawavuta wote kwangu.”
And if I may be lifted up from the earth, I will draw all men towards me.
33 Aliyanena hayo akionesha ni mauti gani atakayokufa.
And He spoke this, signifying by what death He was about to die.
34 Mkutano wakamjibu, “Sisi tumesikia katika sheria ya kwamba Kristo atadumu hata milele. Nawe wasemaje, 'Mwana Adamu lazima ainuliwe juu'? Huyu Mwana wa Mtu ni nani?” (aiōn )
Then the multitude responded to Him; We have heard from the law that Christ abideth forever; and how do You say, That it behooveth the Son of man to be lifted up? who is this Son of man? (aiōn )
35 Basi Yesu akawaambia, “Nuru ingalipo pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru, ili kwamba giza lisije likawaweza. Yeye aendaye gizani hajui aendako.
Then Jesus said to them, Yet a little while the light is with you. Walk about as you have the light, in order that the darkness may not overtake you: and he that walketh about in darkness does not know where he is going.
36 Mngali mnayo nuru, iaminini nuru hiyo ili mpate kuwa wana wa nuru.” Yesu aliyasema haya na kisha akaenda zake akajificha wasimwone.
While you have the light, believe in the light, in order that you may be the sons of light. And Jesus spoke these things, and having gone out was hidden from them.
37 Ingawa Yesu alifanya ishara nyingi namna hiyo mbele yao, bado hawakumwamini
And He having done so many miracles in their presence, they were not believing on Him,
38 ili litimie neno la nabii Isaya, alilosema: “Bwana, ni nani aliyezisadiki habari zetu? Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani?”
in order that the word of Isaiah the prophet might be fulfilled, which he spoke, Lord, who hath believed our report? And to whom is the arm of the Lord revealed?
39 Ndio sababu wao hawakuamini, maana Isaya alisema tena,
Wherefore were they not able to believe, because Isaiah again said,
40 “Amewapofusha macho, na ameifanya migumu mioyo yao; wasije wakaona kwa macho yao na wakafahamu kwa mioyo yao, na wakaongoka nami nikawaponya.”
He hath blinded their eyes, and hardened their heart; in order that they may not see with their eyes, nor understand with their heart, and turn, and I shall heal them.
41 Isaya alisema maneno hayo kwa kuwa aliuona utukufu wa Yesu na akanena habari zake.
Isaiah said these things, because he saw His glory; and spoke concerning Him.
42 Walakini, hata wakuu wengi walimwamini Yesu; lakini kwa sababu ya Mafarisayo, hawakukiri ili wasije wakatengwa na sinagogi.
Nevertheless indeed many of the rulers also believed on Him; but they were not confessing Him on account of the Pharisees, in order that they might not be put out of the synagogues:
43 Walipenda sifa za wanadamu kuliko sifa zitokazo kwa Mungu.
for they loved the glory of the people more than the glory of God.
44 Yesu akapaza sauti na kusema, “Yeye aniaminiye mimi, haniamini mimi tu bali na yeye aliyenituma mimi,
But Jesus cried out and said; The one believing on me, believes not on me, but on Him that sent me,
45 naye anionaye mimi anamuona yeye aliyenituma.
and the one seeing me, sees the one that sent me.
46 Mimi nimekuja kama nuru ulimwenguni ili kila mtu aniaminiye mimi asikae gizani.
I have come a light into the world, in order that every one believing on me may not abide in darkness.
47 Ikiwa mtu yeyote atayasikia maneno yangu lakini asiyashike, mimi simhukumu; maana sikuja ili niuhukumu ulimwengu, bali niuokoe ulimwengu.
And if any one may hear my words, and not keep them, I do not judge him: for I came not that I may judge the world, but that I may save the world.
48 Yeye anikataye mimi na asiyeyakubali maneno yangu, anaye amhukumuye: neno hilo nililolinena ndilo litakalomhukumu siku ya mwisho.
He that rejects me, and receiving not my words, has one judging him: the word which I have spoken, it will judge him in the last day.
49 Maana mimi sikunena kwa nafsi yangu tu. Bali ni Baba aliyenipeleka, yeye mwenyewe ameniagiza nitakayonena na nitakayosema.
Because I have not spoken of Myself; but the Father Himself having sent me, gave me commandment, what I shall speak, and what I shall say.
50 Nami najua ya kuwa agizo lake ni uzima wa milele; basi hayo ninenayo mimi - kama Baba alivyoniambia, ndivyo ninenavyo kwao.” (aiōnios )
And I know that His commandment is eternal life. Now whatsoever thing I say, as the Father has spoken unto me, so I say. (aiōnios )