< Yohana 11 >

1 Basi mtu mmoja jina lake Lazaro alikuwa mgonjwa. Alitokea Bethania, kijiji cha Mariamu na dada yake Martha.
Now a man named Lazarus was sick. He was from Bethany, the village of Mary and her sister Martha.
2 Alikuwa ni Mariamu yule yule aliyempaka Bwana Marhamu na kumfuta miguu yake kwa nywele zake, ambaye ndugu yake Lazaro alikuwa ni mgonjwa.
(Mary was the one who anointed the Lord with ointment and wiped his feet with her hair; it was her brother Lazarus who was sick.)
3 Ndipo dada hawa walituma ujumbe kwa Yesu na kusema, “Bwana, angalia yule umpendaye anaumwa.”
So the sisters sent word to Jesus, “Lord, behold, the one yoʋ love is sick.”
4 Yesu aliposikia alisema, “Ugonjwa huu si wa mauti, lakini, badala yake ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu ili kwamba Mwana wa Mungu apate kutukuzwa katika huo Ugonjwa.”
But when Jesus heard this, he said, “This sickness will not end in death but is for the glory of God, so that the Son of God may be glorified through it.”
5 Yesu alimpenda Martha na dada yake na Lazaro.
Now Jesus loved Martha, her sister Mary, and Lazarus.
6 Aliposikia kuwa Lazaro ni mgonjwa, Yesu alikaa siku mbili zaidi mahali alipokuwa.
But when he heard that Lazarus was sick, he stayed where he was for two more days.
7 Ndipo baada ya hili aliwaambia wanafunzi wake, “Twendeni Uyahudi tena.”
After that he said to the disciples, “Let us go to Judea again.”
8 Wanafunzi wakamwambia, “Rabi, Wayahudi walikuwa wakijaribu kukuponda mawe, na wewe unataka kurudi huko tena?”
The disciples said to him, “Rabbi, the Jews were just recently seeking to stone yoʋ, and yet you are going there again?”
9 Yesu akawajibu, “Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu anapotembea mchana hawezi kujikwaa, kwa sababu anaona kwa nuru ya mchana.
Jesus answered, “Are there not twelve hours in the day? If anyone walks in the day, he does not stumble, because he sees the light of this world.
10 Hata hivyo, ikiwa atatembea usiku, atajikwaa kwa sababu nuru haiko ndani yake.”
But if anyone walks in the night, he stumbles, because the light is not in him.”
11 Yesu akasema mambo haya, na baada ya mambo haya, akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini ninakwenda ili kwamba nipate kumuamsha kutoka usingizini.”
After saying this, he said to them, “Our friend Lazarus has fallen asleep, but I am going there to wake him up.”
12 Ndipo wanafunzi wakamwambia, “Bwana, kama amelala, ataamka.
His disciples said, “Lord, if he has fallen asleep, he will recover.”
13 Wakati huu Yesu alikuwa akizungumza habari za kifo cha Lazaro, lakini wao walidhani anazungumza juu ya kulala usingizi.
(They thought Jesus was speaking about natural sleep, but he was actually speaking about Lazarus' death.)
14 Ndipo Yesu akazungumza nao wazi wazi, “Lazaro amekufa.
Then Jesus told them plainly, “Lazarus has died,
15 Nina furaha kwa ajili yenu, kwamba sikuwepo kule ili kwamba mpate kuamini. Twendeni kwake.”
and I rejoice for your sake that I was not there, so that you may believe. But let us go to him.”
16 Basi Tomaso, aliyeitwa Pacha, aliwaambia wanafunzi wenzake, “Nasi twendeni pia tukafe pamoja na Yesu.”
Then Thomas (called Didymus) said to his fellow disciples, “Let us go too, so that we may die with him.”
17 Wakati Yesu alipokuja, alikuta kwamba Lazaro tayari amekwishakuwa kaburini siku nne.
When Jesus arrived, he found that Lazarus had been in the tomb for four days already.
18 Nayo Bethania ilikuwa karibu na Yerusalemu kama kilomita arobaini na tano hivi.
Now Bethany was less than two miles from Jerusalem,
19 Wengi kati ya Wayahudi wakaja kwa Martha na Mariamu kuwafariji kwa ajili ya ndugu yao.
and many of the Jews had joined the women who were with Martha and Mary, to console them about their brother.
20 Ndipo Martha aliposikia kuwa Yesu anakuja, alienda kukutana naye, lakini Mariamu aliendelea kukaa nyumbani.
When Martha heard that Jesus was coming, she went to meet him, but Mary remained seated in the house.
21 Ndipo Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungelikuwa hapa, kaka yangu asingelikufa.
Then Martha said to Jesus, “Lord, if yoʋ had been here, my brother would not have died.
22 Hata sasa, najua ya kuwa lolote utakaloomba kutoka kwa Mungu, atakupatia.”
But even now I know that God will give yoʋ whatever yoʋ ask of him.”
23 Yesu akamwambia, kaka yako atafufuka tena.”
Jesus said to her, “Yoʋr brother will rise again.”
24 Martha akamwambia, najua kwamba atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho.”
Martha said to him, “I know that he will rise again in the resurrection on the last day.”
25 Yesu akamwambia, “Mimi ni ufufuo na uzima; yeye aniaminiye, ingawa atakufa, hata hivyo atakuwa anaishi;
Jesus said to her, “I am the resurrection and the life. He who believes in me, though he may die, yet shall he live.
26 na yeye aishiye na kuniamini mimi hatakufa. Unaamini hili?” (aiōn g165)
No one who lives and believes in me will ever die. Do yoʋ believe this?” (aiōn g165)
27 Akamwambia, “Ndiyo, Bwana naamini kwamba wewe ni Kristo, Mwana wa Mungu, yeye ajaye katika ulimwengu.”
She said to him, “Yes, Lord, I have come to believe that yoʋ are the Christ, the Son of God, who is to come into the world.”
28 Alipokwisha kusema hili, alienda zake na kumwita dada yake Mariamu faraghani. Akasema, “Mwalimu yuko hapa na anakuita.”
After saying this, she went and called her sister Mary, saying in private, “The Teacher is here and is calling for yoʋ.”
29 Mariamu aliposikia haya, aliinuka kwa haraka na kwenda kwa Yesu.
When Mary heard this, she rose quickly and went to him.
30 Naye Yesu alikuwa hajaja bado ndani ya kijiji, bali alikuwa bado mahali alipokutana na Martha.
(Now Jesus had not yet come into the village, but was in the place where Martha had met him.)
31 Ndipo Wayahudi waliokuwa na Mariamu katika nyumba na wale waliokuwa wakimfariji, walipomuona akiinuka haraka na kutoka nje, walimfuata; walidhani kuwa anaenda kaburini ili akalie huko.
When the Jews who were in the house with Mary, consoling her, saw her rise quickly and go out, they followed her, saying, “She is going to the tomb to weep there.”
32 Ndipo Mariamu, alipofika pale Yesu alipokuwa alimuona na, alianguka chini ya miguu yake na kumwambia, “Bwana, kama ungelikuwa hapa, ndugu yangu asingelikufa.”
When Mary came to where Jesus was and saw him, she fell at his feet and said to him, “Lord, if yoʋ had been here, my brother would not have died.”
33 Yesu alipomuona analia, na Wayahudi waliokuja pamoja naye walikuwa wakilia pia, aliomboleza katika roho na kufadhaika;
When Jesus saw her weeping, and the Jews who had come with her also weeping, he was deeply moved in his spirit and troubled.
34 akasema, “Mmemlaza wapi? wakamwambia, Bwana, njoo utazame.”
He said, “Where have you laid him?” They said to him, “Lord, come and see.”
35 Yesu akalia.
Jesus wept.
36 Ndipo Wayahudi wakasema, “Angalia alivyompenda Lazaro!”
So the Jews said, “See how he loved him!”
37 Lakini wengine kati yao wakasema, “Siyo huyu, mtu aliyeyafumbua macho ya yule aliyekuwa kipofu, hakuweza kumfanya huyu mtu asife?”
But some of them said, “Could not he who opened the eyes of the blind man have also kept this man from dying?”
38 Ndipo Yesu, hali akiomboleza nafsini mwake tena, alienda kwenye kaburi. Sasa lilikuwa pango, na jiwe limewekwa juu yake.
Deeply moved once more, Jesus came to the tomb. (It was a cave, and a stone was lying against it.)
39 Yesu akasema, “Liondoweni jiwe.” Martha, dada yake na Lazaro, yeye aliyekufa, akamwambia Yesu, “Bwana, kwa muda huu, mwili utakuwa umeoza, kwa sababu amekwishakuwa maiti kwa siku nne.”
Jesus said, “Take away the stone.” Martha, the sister of the man who had died, said to him, “Lord, there is already a stench, for it is the fourth day.”
40 Yesu akamwambia, “Mimi sikukuwaambia ya kwamba, kama ukiamini, utauona utukufu wa Mungu?”
Jesus said to her, “Did I not tell yoʋ that if yoʋ believed yoʋ would see the glory of God?”
41 Kwa hiyo wakaliondoa jiwe. Yesu akainua macho yake juu na kusema, “Baba, nakushukuru kwa kuwa unanisikiliza.
So they took away the stone from where the dead man was lying. Then Jesus lifted up his eyes and said, “Father, I thank yoʋ that yoʋ have heard me.
42 Nilijua kwamba unanisikia mara zote, lakini ni kwa sababu ya kusanyiko ambalo limesimama kunizunguka kwamba nimesema haya, ili kwamba wapate kuamini kuwa wewe umenituma.”
I know that yoʋ always hear me, but I say this for the benefit of the crowd that is standing here, so that they may believe that yoʋ sent me.”
43 Baada ya kusema haya, alilia kwa sauti kubwa, “Lazaro, toka nje!”
After saying this, he cried out with a loud voice, “Lazarus, come out!”
44 Mfu alitoka nje amefungwa mikono na miguu kwa sanda za kuzikia, na uso wake ulifungwa na kitambaa.” Yesu akawaambia, “Mfungueni mkamwache aende.”
Then the man who had died came out, his feet and his hands bound with strips of cloth, and his face wrapped in a cloth. Jesus said to them, “Unbind him, and let him go.”
45 Ndipo Wayahudi wengi waliokuja kwa Mariamu na kuona Yesu alichofanya, walimwamini;
Therefore many of the Jews who had come to Mary, and had seen what Jesus did, believed in him.
46 lakini baadhi yao walienda kwa Mafarisayo na kuwaambia mambo aliyoyafanya Yesu.
But some of them went to the Pharisees and told them what Jesus had done.
47 Ndipo wakuu wa Makuhani na Mafarisayo wakakusanyika pamoja katika baraza na kusema, “Tutafanya nini? Mtu huyu anafanya ishara nyingi.
So the chief priests and the Pharisees convened a meeting of the Sanhedrin and said, “What are we going to do? For this man is doing many signs.
48 Ikiwa tutamwacha hivi peke yake, wote watamwamini; Warumi watakuja na kuchukua vyote mahali petu na taifa letu.”
If we allow him to continue like this, everyone will believe in him, and the Romans will come and take away our holy place and our nation.”
49 Hata hivyo, mtu mmoja kati yao, Kayafa, aliyekuwa kuhani Mkuu mwaka huo, akawaambia, “Hamjui chochote kabisa.
But one of them, Caiaphas, who was high priest that year, said to them, “You do not know anything,
50 Hamfikirii kwamba yafaa kwa ajili yenu kwamba mtu mmoja yapasa kufa kwa ajili ya watu kuliko taifa lote kuangamia.”
nor do you consider that it is better for us to have one man die for the people than to have the whole nation perish.”
51 Haya hakuyasema kwa sababu yake mwenyewe, badala yake, kwa kuwa alikuwa kuhani mkuu mwaka ule, alitabiri kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa;
(He said this not of his own accord, but as high priest that year he prophesied that Jesus was going to die for the nation,
52 na si kwa taifa peke yake, bali Yesu apate vile vile kuwakusanya watoto wa Mungu ambao wametawanyika sehemu mbali mbali.
and not only for the nation, but also to gather together and unite the children of God scattered abroad.)
53 Kwa hiyo kuanzia siku hiyo na kuendelea wakapanga namna ya kumwua Yesu.
So from that day they plotted together to kill him.
54 Yesu hakutembea tena wazi wazi kati ya Wayahudi, bali aliondoka hapo na kwenda nchi iliyo karibu na jangwa katika mji uitwao Efraimu. Hapo alikaa na wanafunzi.
Therefore Jesus no longer went around openly among the Jews. Instead, he departed from there to the region near the wilderness, to a town called Ephraim, where he spent time with his disciples.
55 Basi Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu, na wengi wakapanda kwenda Yerusalemu nje ya mji kabla ya Pasaka ili wapate kujitakasa wenyewe.
Now the Passover of the Jews was near, and many people went up to Jerusalem from the countryside to purify themselves before the Passover.
56 Walikuwa wakimtafuta Yesu, na kuzungumza kila mmoja walipokuwa wamesimama hekaluni, “Mnafikiri nini? Kwamba hatakuja katika sikukuu?”
They were looking for Jesus and saying to one another as they stood in the temple courts, “What do you think? That he will not come to the feast at all?”
57 Wakati huu wakuu wa makuhani na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba ikiwa mmoja atajua Yesu alipo, anapaswa kutoa taarifa ili kwamba wapate kumkamata.
(Now the chief priests and the Pharisees had given an order that if anyone knew where Jesus was, he should report it, so that they could arrest him.)

< Yohana 11 >