< Yohana 11 >
1 Basi mtu mmoja jina lake Lazaro alikuwa mgonjwa. Alitokea Bethania, kijiji cha Mariamu na dada yake Martha.
在伯大尼有一位名叫拉撒路的病人,与他的姐妹玛利亚和马大住在一起。
2 Alikuwa ni Mariamu yule yule aliyempaka Bwana Marhamu na kumfuta miguu yake kwa nywele zake, ambaye ndugu yake Lazaro alikuwa ni mgonjwa.
这就是那位后来在主头上抹香膏、用头发擦干主双脚的玛利亚,患病的拉撒路是她的兄弟。
3 Ndipo dada hawa walituma ujumbe kwa Yesu na kusema, “Bwana, angalia yule umpendaye anaumwa.”
姐妹二人让其他人向耶稣捎去一个口信:“主啊,你的好朋友病了。”
4 Yesu aliposikia alisema, “Ugonjwa huu si wa mauti, lakini, badala yake ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu ili kwamba Mwana wa Mungu apate kutukuzwa katika huo Ugonjwa.”
耶稣听见这个消息就说:“这病不至于死,通过他的病将显示上帝的荣光,让上帝之子获得荣耀。”
5 Yesu alimpenda Martha na dada yake na Lazaro.
尽管耶稣喜爱马大、玛利亚和拉撒路,
6 Aliposikia kuwa Lazaro ni mgonjwa, Yesu alikaa siku mbili zaidi mahali alipokuwa.
但听说拉撒路病了,他没有马上过去,而是继续在当地住了两天。
7 Ndipo baada ya hili aliwaambia wanafunzi wake, “Twendeni Uyahudi tena.”
然后他对门徒说:“我们回到犹太去吧。”
8 Wanafunzi wakamwambia, “Rabi, Wayahudi walikuwa wakijaribu kukuponda mawe, na wewe unataka kurudi huko tena?”
门徒对他说:“拉比,几天前犹太人还想用石头打你,你真的想要现在就回去吗?”
9 Yesu akawajibu, “Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu anapotembea mchana hawezi kujikwaa, kwa sababu anaona kwa nuru ya mchana.
耶稣回答:“白昼不是有十二小时吗?在白昼行走不会跌倒,因为这世界上有光。
10 Hata hivyo, ikiwa atatembea usiku, atajikwaa kwa sababu nuru haiko ndani yake.”
若在夜间行走就会跌倒,因为你没有光。”
11 Yesu akasema mambo haya, na baada ya mambo haya, akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini ninakwenda ili kwamba nipate kumuamsha kutoka usingizini.”
耶稣说完这番话,继续说:“我们的朋友拉撒路睡着了,但我要去那里唤醒他!”
12 Ndipo wanafunzi wakamwambia, “Bwana, kama amelala, ataamka.
门徒们说:“主啊,既然他睡了,就会好过来的。”
13 Wakati huu Yesu alikuwa akizungumza habari za kifo cha Lazaro, lakini wao walidhani anazungumza juu ya kulala usingizi.
其实耶稣在暗指拉撒路已死,门徒却以为他真的睡着了。
14 Ndipo Yesu akazungumza nao wazi wazi, “Lazaro amekufa.
于是,耶稣明确地告诉他们:“拉撒路死了。
15 Nina furaha kwa ajili yenu, kwamba sikuwepo kule ili kwamba mpate kuamini. Twendeni kwake.”
因为你们的原因,我很高兴我当时不在那里,因为现在你们就可以相信我了。现在我们去看看他吧。”
16 Basi Tomaso, aliyeitwa Pacha, aliwaambia wanafunzi wenzake, “Nasi twendeni pia tukafe pamoja na Yesu.”
孪生兄弟之一多马对其他门徒说:“我们也一起去吧,我们可以与他一同赴死。”
17 Wakati Yesu alipokuja, alikuta kwamba Lazaro tayari amekwishakuwa kaburini siku nne.
耶稣到了伯大尼,得知拉撒路四天前被安葬在坟墓里。
18 Nayo Bethania ilikuwa karibu na Yerusalemu kama kilomita arobaini na tano hivi.
伯大尼与耶路撒冷相距约有三公里。
19 Wengi kati ya Wayahudi wakaja kwa Martha na Mariamu kuwafariji kwa ajili ya ndugu yao.
有许多犹太人来到马大和玛利亚那里,为拉撒路的死表示哀悼。
20 Ndipo Martha aliposikia kuwa Yesu anakuja, alienda kukutana naye, lakini Mariamu aliendelea kukaa nyumbani.
马大听见耶稣来了,就去迎接他,玛利亚却仍然呆在家里。
21 Ndipo Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungelikuwa hapa, kaka yangu asingelikufa.
马大对耶稣说:“主啊,如果你早在这里,我的兄弟就不会死了。
22 Hata sasa, najua ya kuwa lolote utakaloomba kutoka kwa Mungu, atakupatia.”
就是现在,我确定无论你向上帝求什么,上帝必赐给你。”
23 Yesu akamwambia, kaka yako atafufuka tena.”
耶稣对她说:“你的兄弟将会复活。”
24 Martha akamwambia, najua kwamba atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho.”
马大回答:“我知道在末日重生之际,他必会再次站立起来。”
25 Yesu akamwambia, “Mimi ni ufufuo na uzima; yeye aniaminiye, ingawa atakufa, hata hivyo atakuwa anaishi;
耶稣说:“我就是复活,我就是生命,信我之人可死而再次站立起来。
26 na yeye aishiye na kuniamini mimi hatakufa. Unaamini hili?” (aiōn )
所有活着又相信我之人,必定永远不死,你信这话吗?” (aiōn )
27 Akamwambia, “Ndiyo, Bwana naamini kwamba wewe ni Kristo, Mwana wa Mungu, yeye ajaye katika ulimwengu.”
她说:“是的,主啊,我相信你就是基督,是上帝之子,是众人期盼降临这世界之人。”
28 Alipokwisha kusema hili, alienda zake na kumwita dada yake Mariamu faraghani. Akasema, “Mwalimu yuko hapa na anakuita.”
马大说罢,就回去叫她的姐妹玛利亚,偷偷地说:“老师来了,他要见你。”
29 Mariamu aliposikia haya, aliinuka kwa haraka na kwenda kwa Yesu.
玛利亚听言急忙站起来去见耶稣。
30 Naye Yesu alikuwa hajaja bado ndani ya kijiji, bali alikuwa bado mahali alipokutana na Martha.
当时耶稣还没有进入村子,仍然站在马大与他相见的地点。
31 Ndipo Wayahudi waliokuwa na Mariamu katika nyumba na wale waliokuwa wakimfariji, walipomuona akiinuka haraka na kutoka nje, walimfuata; walidhani kuwa anaenda kaburini ili akalie huko.
有些犹太人在房子里安慰玛利亚,见她匆忙起身出门,于是就跟着她,以为她要到坟墓那边痛哭。
32 Ndipo Mariamu, alipofika pale Yesu alipokuwa alimuona na, alianguka chini ya miguu yake na kumwambia, “Bwana, kama ungelikuwa hapa, ndugu yangu asingelikufa.”
玛利亚来到耶稣面前,见到就立刻伏倒在他脚前说:“主啊,如果你当时在这里,我的兄弟就不会死了!”
33 Yesu alipomuona analia, na Wayahudi waliokuja pamoja naye walikuwa wakilia pia, aliomboleza katika roho na kufadhaika;
见到她和跟来的犹太人在面前哭泣,耶稣心中万分悲伤难过。。
34 akasema, “Mmemlaza wapi? wakamwambia, Bwana, njoo utazame.”
他问到:“你们把他安葬在哪里?” 他们回答说:“主啊,快来看吧。”
36 Ndipo Wayahudi wakasema, “Angalia alivyompenda Lazaro!”
犹太人说:“你看,他多么爱这个人。”
37 Lakini wengine kati yao wakasema, “Siyo huyu, mtu aliyeyafumbua macho ya yule aliyekuwa kipofu, hakuweza kumfanya huyu mtu asife?”
但也有人说:“他既然能让盲人重见光明,难道不能让拉撒路不要死去吗?”
38 Ndipo Yesu, hali akiomboleza nafsini mwake tena, alienda kwenye kaburi. Sasa lilikuwa pango, na jiwe limewekwa juu yake.
耶稣分外难过地来到坟墓前面,这是一个洞穴,洞口堵着一块石头。
39 Yesu akasema, “Liondoweni jiwe.” Martha, dada yake na Lazaro, yeye aliyekufa, akamwambia Yesu, “Bwana, kwa muda huu, mwili utakuwa umeoza, kwa sababu amekwishakuwa maiti kwa siku nne.”
耶稣吩咐众人:“把这块石头挪开。” 但死者的姐妹马大说:“主啊,他已经死去四天了,味道一定特别难闻。”
40 Yesu akamwambia, “Mimi sikukuwaambia ya kwamba, kama ukiamini, utauona utukufu wa Mungu?”
耶稣说:“还记得我对你说过的吗?如果你相信我,就会看到上帝的荣耀。”
41 Kwa hiyo wakaliondoa jiwe. Yesu akainua macho yake juu na kusema, “Baba, nakushukuru kwa kuwa unanisikiliza.
于是他们挪开石头。耶稣举目望天,说:“父啊,感谢你聆听我,
42 Nilijua kwamba unanisikia mara zote, lakini ni kwa sababu ya kusanyiko ambalo limesimama kunizunguka kwamba nimesema haya, ili kwamba wapate kuamini kuwa wewe umenituma.”
我知道你总是在聆听我,但我说这番话是为了站在这里的民众,为了让他们相信,是你派我而来。”
43 Baada ya kusema haya, alilia kwa sauti kubwa, “Lazaro, toka nje!”
说罢,耶稣大喊:“拉撒路,出来吧!”
44 Mfu alitoka nje amefungwa mikono na miguu kwa sanda za kuzikia, na uso wake ulifungwa na kitambaa.” Yesu akawaambia, “Mfungueni mkamwache aende.”
那死去的人便走出来,手脚都缠着布,脸上也裹着布。 耶稣说:“解开布吧,放他自由!”
45 Ndipo Wayahudi wengi waliokuja kwa Mariamu na kuona Yesu alichofanya, walimwamini;
到玛利亚那里奔丧的犹太人看到耶稣的所为,于是信了他。
46 lakini baadhi yao walienda kwa Mafarisayo na kuwaambia mambo aliyoyafanya Yesu.
但他们中间有些人还是去了法利赛人那里,讲述了耶稣的所作所为。
47 Ndipo wakuu wa Makuhani na Mafarisayo wakakusanyika pamoja katika baraza na kusema, “Tutafanya nini? Mtu huyu anafanya ishara nyingi.
于是牧师长和法利赛人召开公议会,说:“这个人显化了许多神迹,我们该怎么办?
48 Ikiwa tutamwacha hivi peke yake, wote watamwamini; Warumi watakuja na kuchukua vyote mahali petu na taifa letu.”
如果我们任由他继续,所有人都会信他,罗马人就会过来摧毁我们的圣殿,消灭我们的民族。”
49 Hata hivyo, mtu mmoja kati yao, Kayafa, aliyekuwa kuhani Mkuu mwaka huo, akawaambia, “Hamjui chochote kabisa.
该亚法是当年的大牧师,他说:“你们什么都不知道,
50 Hamfikirii kwamba yafaa kwa ajili yenu kwamba mtu mmoja yapasa kufa kwa ajili ya watu kuliko taifa lote kuangamia.”
难道看不出来吗?让一个人代替民众而死,免得整个民族灭亡,这样做对你们更好。”
51 Haya hakuyasema kwa sababu yake mwenyewe, badala yake, kwa kuwa alikuwa kuhani mkuu mwaka ule, alitabiri kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa;
他这样说并非为了自己着想,而是因为他是那年的大牧师,所以预言耶稣要替这个民族死。
52 na si kwa taifa peke yake, bali Yesu apate vile vile kuwakusanya watoto wa Mungu ambao wametawanyika sehemu mbali mbali.
这样做不只是为了犹太民族,还是为了散落各地的上帝之子,将他们聚在一起成为一体。
53 Kwa hiyo kuanzia siku hiyo na kuendelea wakapanga namna ya kumwua Yesu.
从那天起,他们就开始密谋如何杀害耶稣。
54 Yesu hakutembea tena wazi wazi kati ya Wayahudi, bali aliondoka hapo na kwenda nchi iliyo karibu na jangwa katika mji uitwao Efraimu. Hapo alikaa na wanafunzi.
所以耶稣不再在犹太人中间公开活动,而是去了荒漠附近一个名叫以法莲的城市,与门徒一起住在那里。
55 Basi Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu, na wengi wakapanda kwenda Yerusalemu nje ya mji kabla ya Pasaka ili wapate kujitakasa wenyewe.
犹太人的逾越节快到了,许多人在节前从四乡八里来到耶路撒冷洁净自己。
56 Walikuwa wakimtafuta Yesu, na kuzungumza kila mmoja walipokuwa wamesimama hekaluni, “Mnafikiri nini? Kwamba hatakuja katika sikukuu?”
他们到处寻找耶稣,站在圣殿里彼此说:“你们觉得呢?他会来过节吗?”
57 Wakati huu wakuu wa makuhani na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba ikiwa mmoja atajua Yesu alipo, anapaswa kutoa taarifa ili kwamba wapate kumkamata.
牧师长和法利赛人早已下了命令:任何人知道耶稣在哪里,都应来此举报,他们将逮捕他。