< Yohana 10 >
1 Amin, Amini nawaambieni, yule asiyeingia kwa kupitia mlango wa zizi la kondoo, lakini anapanda kwa njia nyingine, mtu huyo ni mwizi na mnyang'anyi.
Etesheli, Etesheli embabhozya, ola wasahwinjila ashilile mundyango gwi goma lye ngole, ila azubha hwidala lya mwabho, omuntu oyo mwibha na fyozi.
2 Yeye aingiaye mlangoni ni mchungaji wa kondoo.
Omwane wa hwinjila mundyango yodimi we ngole.
3 Kwake mlinzi wa mlango humfungulia. Kondoo waisikia sauti yake na huwaita kondoo zake kwa majina yao na kuwatoa nje.
Hwa mweme olinzi we dyango ahwigulilwa. Engolezolyonvwa izu lyakwe na azikwi zya engole zyakwe hu matawa gabho na zifumye honze.
4 Atakapowatoa nje hao walio wake, huwatangulia, na kondoo humfuata, kwa sababu wanaijua sauti yake.
Naizifumya honze ezye zyazili zyakwe azitangulila ne Ngolobhe zihulondolela, afuatanaje bhalimenye izu lyakwe.
5 Hawatamfuata mgeni lakini badala yake watamuepuka, kwa sababu hawazijui sauti za wageni.”
Sezinzahumwanze ojenyu ila zinza hupemushile, afuatane sezigamenye amazu ga jenyu.”
6 Yesu alisema mfano huu kwao, lakini hawakuyaelewa mambo haya ambayo alikuwa akisema kwao.
O Yesu ayanga ofwana ogu hwabhene, ila sebhazyelewe enongo ezi zyali ayanag hwa bhene.
7 Yesu akasema nao tena, “Amini, amini, nawaambia, Mimi ni mlango wa kondoo.
O Yesu ayanga nabho nantele, “Etesheli, etesheli, embabhozya, Ane endi ndiango gwe ngole.
8 Wote walionitangulia ni wezi na wanyang'anyi, lakini kondoo hawakuwasikiliza.
Bhonti bhabhatanguliye bhibha na bhafyozi, ila engole zibhonvwa.
9 Mimi ni mlango. Yeyote aingiaye kupitia kwangu, ataokolewa; ataingia ndani na kutoka, naye atajipatia malisho.
Ane endi ndiango. Wawonti wahwinjila ashilile huline, aifyoliwa ainjila muhati na fume, wope aipata edyo.
10 Mwizi haji isipokuwa kuiba, kuua, na kuangamiza. Nimekuja ili kwamba wapate uzima na wawe nao tele.
Omwibha sahwenza ila ahwibhe, agoje, natezye, enenzele nkawepate owomi bhabhe nawo winji.
11 Mimi ni mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.
Ane endi dimi mwinza. Odimi omwinza afumya owomi wakwe huu ngole.
12 Mtumishi aliyeajiriwa, na siyo mchungaji, ambaye kondoo si mali yake, huwaona mbwa mwitu wakija na huwaacha na kuwakimbia kondoo.
Oboyi wabhehwelwe, nasio aje dimi, ola engole se vyoma vyakwe, azilola embwa zihwenza na azileha na zishembele.
13 Na mbwa mwitu huwakamata na kuwatawanya. Hukimbia kwa sababu ni mtumishi wa kuajiriwa na hawajali kondoo.
Ne mbwa zikhata na nyampanye. Zishembela afuatanaji oboyi wabhe hwelwe sazisajila engole.
14 Mimi ni mchungaji mwema, na ninawajua walio wangu, nao walio wangu wananijua mimi.
Ane endi dimi mwinza embamenye bhabhali bhahuline, wope wamenye ane.
15 Baba ananijua, nami namjua Baba, nami nautoa uhai wangu kwa ajili ya kondoo.
Odaada amenye, nane emenye Odaada, nane eufumwa owomi wane hungole.
16 Ninao kondoo wengine ambao si wa zizi hili. Hao pia, yanipasa kuwaleta, nao wataisikia sauti yangu ili kwamba pawepo na kundi moja na mchungaji mmoja.
Endi nazyo engole zimo zyasaga zya mwigoma eli ezyo zyope ehwanziwa azilete, zyope zinzahonvwe izu lyane zibheligoma limo no dimi omo.
17 Hii ndiyo sababu Baba ananipenda: Niutoe uhai wangu halafu niutwae tena.
Ene ndiyo maana Odaada angene: Eeufumye owomi wane alafu nantele aweje.
18 Hakuna auchukuaye kutoka kwangu, lakini mimi nautoa mwenyewe. Ninayo mamlaka ya kuutoa, na ninayo mamlaka ya kuutwaa pia. Nimelipokea agizo hili kutoka kwa Baba.”
Nomo wawega afume huline, ila eufumya nene. Endi waamuzi gwa ufumye na endi waamuzi ogwagwefwe nantele. Endiposheye elajizyo eli afume hwa Daada.”
19 Mgawanyiko tena ukatokea kati ya wayahudi kwa sababu ya maneno haya.
Olwaganyishe lwafuma afume hwa yahudi afuatana na maazu ega.
20 Wengi wao wakasema, “Ana pepo na ni kichaa. Kwa nini mnamsikiliza?”
Abhinji bhabho wahaga, “Ali ni pepo ndii na pelusu yenu muhumwonvwa?”
21 Wengine wakasema, “Haya siyo maneno ya mtu aliyepagawa na mapepo. Pepo linaweza kufungua macho ya kipofu?”
Bhamo bhayanga, “Ege semazu gamuntu wali ni pepo. Ipepo ligamwigula amaso ompofu?”
22 Ndipo ikaja Sikukuu ya Kuwekwa Wakfu Yerusalemu.
Nkashahenza Eshikulukulu Shabhehwe Wakifu hu Yelusalemu.
23 Ulikuwa wakati wa baridi, na Yesu alikuwa akitembea hekaluni katika ukumbi wa Selemani.
Hwali shipindi shi sasa, oYesu ali ajenda mushibhanza muukumbi wa Sulemani.
24 Ndipo Wayahudi walipomzunguka na kumwambia, “Mpaka lini utatuweka katika mashaka? kama wewe ni Kristo, tuambie wazi.
Ayahudi nkabhazyongola na hubhozye, “Paka ndii waibheha nsebho? nkashe awe we Kilisiti, tibhozye peupe.
25 Yesu akawajibu, “Nimekwisha waambia lakini hamuamini. Kazi nizifanyazo kwa jina la Baba yangu, hizo zinashuhudia juu yangu.
O Yesu ajile, “Embabhozezye ila semuhweteshela. Embombo zyenzibhomba witawa lya Daada wane, ezyo zihakikisha pamwanya yane.
26 Hata hivyo hamuamini kwa sababu ninyi si kondoo wangu.
Ata sheshi ahweteshela alenganaje amwe semuli ngole zyane.
27 Kondoo wangu waisikia sauti yangu; Nawajua, nao wanifuata mimi.
Engole zyane zihonvwa izu lyane; Enzimenye, zyope zinanza ane.
28 Nimewapa uzima wa milele; hawataangamia kamwe, na hakuna hata mmoja atakayewanyakuwa kutoka mkononi mwangu. (aiōn , aiōnios )
Embapiye owomi wewilawila sebhatega na mwaha, nomo hata weka waibhafyola afume mukhono gwane. (aiōn , aiōnios )
29 Baba yangu, aliyenipa hao, ni mkuu kuliko wengine wote, na hakuna hata mmoja aliye na uwezo wa kuwanyakua kutoka mkononi mwa Baba.
Odaada wane, wampiye ebho, yo Gosi ashile bhamwabho bhonti, na nomo hata weka wali no uwezo wa fyole mukhono gwa Daada.
30 Mimi na Baba tu mmoja.”
Ane no Daada tili hantu hamo.”
31 Wakabeba mawe ili wamponde tena.
Bhanyemla amawe aje nkabhapole nantele.
32 Yesu akawajibu, “Nimeshawaonesha kazi nyingi nzuri kutoka kwa Baba. Kwa kazi zipi kati ya hizo mnataka kuniponda mawe?”
O Yesu abhabhozya, “Embalanjile embombo enyinji enyinza afume hwa Daada. Hu mbombo zyalihu kati yezyo zyamuhwanza ampole na mawe?”
33 Wayahudi wakamjibu, “Hatukupondi mawe kwa kazi yoyote iliyo nzuri, lakini kwa kukufuru, kwa sababu wewe, uliye mtu, unajifanya kuwa Mungu.”
Ayahudi bhahaga, “Setihupola na mawe hu mbombo yayonti yeli nyinza, ila okufuru awe wo muntu ohwibheha aje oli Ngolobhe.”
34 Yesu akawajibu, “Haikuandikwa katika sheria yenu, 'Nilisema, “Ninyi ni miungu”'?”
O Yesu abhabhozya, “Seya handihwe mundajizyo zyenyu, 'Nayanjile, “'Amwe muli mangolobhe'”?”
35 Ikiwa aliwaita miungu, kwa wale ambao Neno la Mungu liliwajilia (na Maandiko hayawezi kuvunjwa),
Nkashe abhakwizizye mangolobhe, hwa bhala Izu lya Ngolobhe lya bhenzeye (na Maazu segawezi abudwe),
36 mnasema juu ya yule ambaye Baba alimtoa na kumtuma katika ulimwengu, 'Unakufuru,' kwa sababu nilisema, 'mimi ni Mwana wa Mungu'?
muyanga ahusu ola Odaada afumizye na husontezye munsi, 'Osalanya,' alengane naje nayanjile, 'ane endi Mwana wa Ngolobhe'?
37 “Ikiwa sifanyi kazi za Baba yangu, msiniamini.
“Nkashe sebhomba embombo zya Daada wane, mungaje aneteshele.
38 Hata hivyo, ikiwa ninazifanya, hata kama hamniamini, ziaminini kazi ili kwamba muweze kujua na kufahamu kwamba Baba yuko ndani yangu na mimi niko ndani ya Baba.”
Ata sheshi, nkashe ezibhomba, ata nkasemuneteshela, zyetesheli embombo aje muwezye amanye na hwelewe aje Odaada ali muhati yane nane muhati ya Daada.”
39 Wakajaribu tena kumkamata Yesu, lakini alienda zake kutoka mikononi mwao.
Bhalenga na hu khate oYesu, ahwisogoleye afume mumakhono gabho.
40 Yesu akaenda zake tena ng'ambo ya Yordani sehemu ambayo Yohana alikuwa akibatiza kwanza, na akakaa huko.
O Yesu ahwibhalila hwi syelelye Yordani esehemu hula oYohana hwahozyaga ahwande, ahakhala ohwo.
41 Watu wengi wakaja kwa Yesu. Waliendelea kusema, “Yohana kweli hakufanya ishara yoyote, lakini mambo yote aliyoyasema Yohana juu ya huyu mtu ni ya kweli.”
Abhantu abhinji bhahenza hwa Yesu. Bhahendeleye ayanje, “O Yohana lyoli sagabhombile eishara yoyonti, ila enongwa zyonti zyayanjile Yohana ahusu omuntu ono zye yoli.”
42 Watu wengi wakamwamini Yesu hapo.
Abhantu abhinji bhamweteshela oYesu epo.