< Yohana 1 >

1 Mwanzoni kulikuwako Neno, na Neno alikuwa pamoja na Mungu, na Neno alikuwa Mungu.
In the beginning was the Word, and the Word was with God, and the Word was God;
2 Huyu, Neno, Mwanzoni alikuwa pamoja na Mungu.
this one was in the beginning with God;
3 Vitu vyote vilifanyika kupitia yeye, na pasipo yeye hakuna hata kitu kimoja kilichokuwa kimefanyika.
all things through him did happen, and without him happened not even one thing that hath happened.
4 Ndani yake kulikuwa uzima, na huo uzima ulikuwa nuru ya wanadamu wote.
In him was life, and the life was the light of men,
5 Nuru yang'aa gizani, wala giza halikuizimisha.
and the light in the darkness did shine, and the darkness did not perceive it.
6 Palikuwa na mtu aliyetumwa kutoka kwa Mungu, ambaye jina lake alikuwa Yohana.
There came a man — having been sent from God — whose name [is] John,
7 Alikuja kama shahidi kushuhudia kuhusu ile nuru, ili kwamba wote waweze kuamini kupitia yeye.
this one came for testimony, that he might testify about the Light, that all might believe through him;
8 Yohana hakuwa ile nuru, bali alikuja ili ashuhudie kuhusu ile nuru
that one was not the Light, but — that he might testify about the Light.
9 Hiyo ilikuwa nuru ya kweli ambayo ilikuwa inakuja katika dunia nayo humtia nuru kila mmoja
He was the true Light, which doth enlighten every man, coming to the world;
10 Alikuwa katika dunia, na dunia iliumbwa kupitia yeye, na dunia haikumjua.
in the world he was, and the world through him was made, and the world did not know him:
11 Alikuja kwa vitu vyake, na watu wake hawakumpokea.
to his own things he came, and his own people did not receive him;
12 Bali kwa wale wengi waliompokea, ambao waliamini jina lake, kwa hao aliwapa haki ya kuwa wana wa Mungu,
but as many as did receive him to them he gave authority to become sons of God — to those believing in his name,
13 Ambao walizaliwa, sio kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili, wala kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu mwenyewe.
who — not of blood nor of a will of flesh, nor of a will of man but — of God were begotten.
14 Naye Neno alifanyika mwili na akaishi miongoni mwetu, tumeuona utukufu wake, utukufu kama wa mtu pekee wa kipekee aliyekuja kutoka kwa Baba, amejaa neema na kweli.
And the Word became flesh, and did tabernacle among us, and we beheld his glory, glory as of an only begotten of a father, full of grace and truth.
15 Yohana alishuhudia kuhusu yeye, na alipaza sauti akisema, “Huyu ndiye ambaye nilisema habari zake nikisema, “Yule ajaye baada yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa sababu amekuwako kabla yangu.”
John doth testify concerning him, and hath cried, saying, 'This was he of whom I said, He who after me is coming, hath come before me, for he was before me;'
16 Kwa kuwa kutoka katika utimilifu wake, sisi sote tumepokea bure kipawa baada ya kipawa.
and out of his fulness did we all receive, and grace over-against grace;
17 Kwa kuwa sheria ililetwa kupitia Musa. Neema na kweli vilikuja kupitia Yesu Kristo.
for the law through Moses was given, the grace and the truth through Jesus Christ did come;
18 Hakuna mwanadamu aliyemwona Mungu wakati wowote. Mtu pekee ambaye ni Mungu, aliye katika kifua cha Baba, amemfanya yeye ajulikane.
God no one hath ever seen; the only begotten Son, who is on the bosom of the Father — he did declare.
19 Na huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati makuhani na walawi waliotumwa kwake na Wayahudi kumwuliza, “Wewe ni nani?”
And this is the testimony of John, when the Jews sent out of Jerusalem priests and Levites, that they might question him, 'Who art thou?'
20 Bila kusitasita na hakukana, bali alijibu, “Mimi sio Kristo.”
and he confessed and did not deny, and confessed — 'I am not the Christ.'
21 Hivyo wakamuuliza, “kwa hiyo wewe ni nani sasa?” Wewe ni Eliya? Akasema, “Mimi siye.” Wakasema, Wewe ni nabii? Akajibu,” Hapana.”
And they questioned him, 'What then? Elijah art thou?' and he saith, 'I am not.' — 'The prophet art thou?' and he answered, 'No.'
22 Kisha wakamwambia, “Wewe ni nani, ili kwamba tuwape jibu waliotutuma”? Wajishuhudiaje wewe mwenyewe?”
They said then to him, 'Who art thou, that we may give an answer to those sending us? what dost thou say concerning thyself?'
23 Akasema, “Mimi ni sauti yake aliaye nyikani: 'Inyosheni njia ya Bwana,' kama nabii Isaya alivyosema.”
He said, 'I [am] a voice of one crying in the wilderness: Make straight the way of the Lord, as said Isaiah the prophet.'
24 Basi kulikuwa na watu wametumwa pale kutoka kwa Mafarisayo. Wakamuuliza na kusema,
And those sent were of the Pharisees,
25 “Kwa nini unabatiza basi kama wewe sio Kristo wala Eliya wala nabii?”
and they questioned him and said to him, 'Why, then, dost thou baptize, if thou art not the Christ, nor Elijah, nor the prophet?'
26 Yohana aliwajibu akisema, “Ninabatiza kwa maji. Hata hivyo, miongoni mwenu anasimama mtu msiyemtambua.
John answered them, saying, 'I baptize with water, but in midst of you he hath stood whom ye have not known, this one it is who is coming after me, who hath been before me,
27 Huyu ndiye ajaye baada yangu. Mimi sisitahili kulegeza kamba za viatu vyake.”
of whom I am not worthy that I may loose the cord of his sandal.'
28 Mambo haya yalitendeka huko Bethania, ng'ambo ya Yordani, mahali ambapo Yohana alikuwa akibatiza.
These things came to pass in Bethabara, beyond the Jordan, where John was baptizing,
29 Siku iliyofuata Yohana alimwona Yesu akija kwake akasema, “Tazama mwanakondoo wa Mungu aichukuae dhambi ya ulimwengu!
on the morrow John seeth Jesus coming unto him, and saith, 'Lo, the Lamb of God, who is taking away the sin of the world;
30 huyu ndiye niliyesema habari zake nikisema, “Yeye ajaye nyuma yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa kuwa alikuwa kabla yangu.'
this is he concerning whom I said, After me doth come a man, who hath come before me, because he was before me:
31 Sikumtambua yeye, lakini ilifanyika hivyo ili kwamba afunuliwe katika Israeli, kwamba nilikuja nikibatiza kwa maji.”
and I knew him not, but, that he might be manifested to Israel, because of this I came with the water baptizing.
32 Yohana alishuhudia, “Niliona Roho akishuka kutoka mbinguni mfano wa hua, na ilibaki juu yake.
And John testified, saying — 'I have seen the Spirit coming down, as a dove, out of heaven, and it remained on him;
33 Mimi sikumtambua lakini yeye aliyenituma ili nibatize kwa maji aliniambia, 'yule ambaye utaona Roho akishuka na kukaa juu yake, Huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu.'
and I did not know him, but he who sent me to baptize with water, He said to me, On whomsoever thou mayest see the Spirit coming down, and remaining on him, this is he who is baptizing with the Holy Spirit;
34 Nimeona na nimeshuhudia kwamba huyu ni Mwana wa Mungu.”
and I have seen, and have testified, that this is the Son of God.'
35 Tena siku iliyofuata Yohana alikuwa amesimama pamoja na wanafunzi wake wawili,
On the morrow, again, John was standing, and two of his disciples,
36 walimwona Yesu akitembea na Yohana akasema, “Tazama, Mwana kondoo wa Mungu!”
and having looked on Jesus walking, he saith, 'Lo, the Lamb of God;'
37 Wanafunzi wawili walimsikia Yohana akisema haya wakamfuata Yesu.
and the two disciples heard him speaking, and they followed Jesus.
38 Tena Yesu aligeuka na kuwaona wanafunzi wale wakimfuata, na akawambia, “Mnataka nini?” Wakajibu, “Rabbi, (maana yake 'mwalimu,' unaishi wapi?”
And Jesus having turned, and having beheld them following, saith to them, 'What seek ye?' and they said to them, 'Rabbi, (which is, being interpreted, Teacher, ) where remainest thou?'
39 Akawambia, “Njooni na mwone.”Kisha walikwenda na kuona mahali alipokuwa akiishi; walikaa pamoja naye siku hiyo, kwa kuwa ilikuwa yapata kama saa kumi hivi.
He saith to them, 'Come and see;' they came, and saw where he doth remain, and with him they remained that day and the hour was about the tenth.
40 Mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana akiongea na kisha kumfuata Yesu alikuwa ni Andrea, ndugu yake Simoni Petro.
Andrew, the brother of Simon Peter, was one of the two who heard from John, and followed him;
41 Akamwona ndugu yake Simoni na akamwambia, “Tumempata Masihi” (ambayo inatafsiriwa Kristo).
this one doth first find his own brother Simon, and saith to him, 'We have found the Messiah,' (which is, being interpreted, The Anointed, )
42 Akamleta kwa Yesu. Yesu akamtazama na akasema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana” utaitwa Kefa,” (maana yake 'Petro').
and he brought him unto Jesus: and having looked upon him, Jesus saith, 'Thou art Simon, the son of Jonas, thou shalt be called Cephas,' (which is interpreted, A rock.)
43 Siku iliyofuata wakati Yesu alipotaka kuondoka kwenda Galilaya, alimpata Filipo na akamwambia, “Nifuate mimi.”
On the morrow, he willed to go forth to Galilee, and he findeth Philip, and saith to him, 'Be following me.'
44 Filipo alikuwa ni mwenyeji wa Bethsaida, mji wa Andrea na Petro.
And Philip was from Bethsaida, of the city of Andrew and Peter;
45 Filipo alimpata Nathanaeli na kumwambia, Tumempata yule ambaye Musa aliandika habari zake katika sheria na Manabii. Yesu mwana wa Yusufu, kutoka Nazareti.
Philip findeth Nathanael, and saith to him, 'Him of whom Moses wrote in the Law, and the prophets, we have found, Jesus the son of Joseph, who [is] from Nazareth;'
46 Nathanaeli akamwambia, “Je kitu chema chaweza kutokea Nazareti?” Filipo akamwambia, Njoo na uone.”
and Nathanael said to him, 'Out of Nazareth is any good thing able to be?' Philip said to him, 'Come and see.'
47 Yesu akamwona Nathanaeli akija kwake na akasema, “Tazama, Mwisraeli kweli kweli asiye na udanganyifu ndani yake!”
Jesus saw Nathanael coming unto him, and he saith concerning him, 'Lo, truly an Israelite, in whom guile is not;'
48 Nathanaeli akamwambia, “Umenifahamuje mimi?” Yesu akajibu na akamwambia, “Kabla Filipo hajakuita ulipokuwa chini ya mtini, nalikuona.”
Nathanael saith to him, 'Whence me dost thou know?' Jesus answered and said to him, 'Before Philip's calling thee — thou being under the fig-tree — I saw thee.'
49 Nathanaeli akajibu, “Rabi wewe u Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli”!
Nathanael answered and saith to him, 'Rabbi, thou art the Son of God, thou art the king of Israel.'
50 Yesu akajibu akamwambia, Kwa sababu nilikuambia 'nilikuona chini ya mtini' je waamini? utaona matendo makubwa kuliko haya.”
Jesus answered and said to him, 'Because I said to thee, I saw thee under the fig-tree, thou dost believe; greater things than these thou shalt see;'
51 Yesu akasema, “Amini amini nawambieni mtaziona mbingu zikifunguka, na kuwaona malaika wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”
and he saith to him, 'Verily, verily, I say to you, henceforth ye shall see the heaven opened, and the messengers of God going up and coming down upon the Son of Man.'

< Yohana 1 >