< Yohana 1 >
1 Mwanzoni kulikuwako Neno, na Neno alikuwa pamoja na Mungu, na Neno alikuwa Mungu.
In the beginning was the Word, and the Word was with God, and the Word was God.
2 Huyu, Neno, Mwanzoni alikuwa pamoja na Mungu.
He was in the beginning with God.
3 Vitu vyote vilifanyika kupitia yeye, na pasipo yeye hakuna hata kitu kimoja kilichokuwa kimefanyika.
All things were made through him, and nothing that was made was made without him.
4 Ndani yake kulikuwa uzima, na huo uzima ulikuwa nuru ya wanadamu wote.
In him was life, and the life was the light of men.
5 Nuru yang'aa gizani, wala giza halikuizimisha.
The light shines in the darkness, and the darkness has not overcome it.
6 Palikuwa na mtu aliyetumwa kutoka kwa Mungu, ambaye jina lake alikuwa Yohana.
There came a man sent from God, whose name was John.
7 Alikuja kama shahidi kushuhudia kuhusu ile nuru, ili kwamba wote waweze kuamini kupitia yeye.
He came as a witness to testify about the light, so that all might believe through him.
8 Yohana hakuwa ile nuru, bali alikuja ili ashuhudie kuhusu ile nuru
He himself was not the light, but he came to testify about the light.
9 Hiyo ilikuwa nuru ya kweli ambayo ilikuwa inakuja katika dunia nayo humtia nuru kila mmoja
The true light, which gives light to everyone, was coming into the world.
10 Alikuwa katika dunia, na dunia iliumbwa kupitia yeye, na dunia haikumjua.
He was in the world, and the world was made through him, but the world did not know him.
11 Alikuja kwa vitu vyake, na watu wake hawakumpokea.
He came to his own, but his own people did not receive him.
12 Bali kwa wale wengi waliompokea, ambao waliamini jina lake, kwa hao aliwapa haki ya kuwa wana wa Mungu,
But to all who did receive him, who believed in his name, he gave the right to become children of God,
13 Ambao walizaliwa, sio kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili, wala kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu mwenyewe.
who were born not of blood, nor of the will of the flesh, nor of the will of man, but of God.
14 Naye Neno alifanyika mwili na akaishi miongoni mwetu, tumeuona utukufu wake, utukufu kama wa mtu pekee wa kipekee aliyekuja kutoka kwa Baba, amejaa neema na kweli.
The Word became flesh and dwelt among us, and we have seen his glory, the glory of the one and only Son, who came from the Father, full of grace and truth.
15 Yohana alishuhudia kuhusu yeye, na alipaza sauti akisema, “Huyu ndiye ambaye nilisema habari zake nikisema, “Yule ajaye baada yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa sababu amekuwako kabla yangu.”
John testified about him and cried out, “This is he of whom I said, ‘He who comes after me ranks ahead of me, because he existed before me.’”
16 Kwa kuwa kutoka katika utimilifu wake, sisi sote tumepokea bure kipawa baada ya kipawa.
Of his fullness we have all received, even grace upon grace.
17 Kwa kuwa sheria ililetwa kupitia Musa. Neema na kweli vilikuja kupitia Yesu Kristo.
For the law was given through Moses, but grace and truth came through Jesus Christ.
18 Hakuna mwanadamu aliyemwona Mungu wakati wowote. Mtu pekee ambaye ni Mungu, aliye katika kifua cha Baba, amemfanya yeye ajulikane.
No one has ever seen God, but the one and only Son, who is at the Father's side, has made him known.
19 Na huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati makuhani na walawi waliotumwa kwake na Wayahudi kumwuliza, “Wewe ni nani?”
This was the testimony of John when the Jews sent priests and Levites from Jerusalem to ask him, “Who are yoʋ?”
20 Bila kusitasita na hakukana, bali alijibu, “Mimi sio Kristo.”
He did not refuse to answer, but openly declared, “I am not the Christ.”
21 Hivyo wakamuuliza, “kwa hiyo wewe ni nani sasa?” Wewe ni Eliya? Akasema, “Mimi siye.” Wakasema, Wewe ni nabii? Akajibu,” Hapana.”
So they asked him, “What then? Are yoʋ Elijah?” He said, “I am not.” “Are yoʋ the Prophet?” He answered, “No.”
22 Kisha wakamwambia, “Wewe ni nani, ili kwamba tuwape jibu waliotutuma”? Wajishuhudiaje wewe mwenyewe?”
So they said to him, “Who are yoʋ? Tell us so that we may give an answer to those who sent us. What do yoʋ say about yoʋrself?”
23 Akasema, “Mimi ni sauti yake aliaye nyikani: 'Inyosheni njia ya Bwana,' kama nabii Isaya alivyosema.”
He said, “I am the voice of one crying out in the wilderness, ‘Make straight the way for the Lord,’ as the prophet Isaiah said.”
24 Basi kulikuwa na watu wametumwa pale kutoka kwa Mafarisayo. Wakamuuliza na kusema,
(Now those who had been sent were from the Pharisees.)
25 “Kwa nini unabatiza basi kama wewe sio Kristo wala Eliya wala nabii?”
Then they asked him, “Why then do yoʋ baptize if yoʋ are not the Christ, nor Elijah, nor the Prophet?”
26 Yohana aliwajibu akisema, “Ninabatiza kwa maji. Hata hivyo, miongoni mwenu anasimama mtu msiyemtambua.
John answered them, “I baptize with water, but among you stands someone you do not know.
27 Huyu ndiye ajaye baada yangu. Mimi sisitahili kulegeza kamba za viatu vyake.”
He is the one who comes after me, who ranks ahead of me, the strap of whose sandals I am not worthy to untie.”
28 Mambo haya yalitendeka huko Bethania, ng'ambo ya Yordani, mahali ambapo Yohana alikuwa akibatiza.
These things took place in Bethany beyond the Jordan, where John was baptizing.
29 Siku iliyofuata Yohana alimwona Yesu akija kwake akasema, “Tazama mwanakondoo wa Mungu aichukuae dhambi ya ulimwengu!
On the next day John saw Jesus coming to him and said, “Behold, the Lamb of God, who takes away the sin of the world!
30 huyu ndiye niliyesema habari zake nikisema, “Yeye ajaye nyuma yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa kuwa alikuwa kabla yangu.'
This is he of whom I said, ‘After me comes a man who ranks ahead of me, because he existed before me.’
31 Sikumtambua yeye, lakini ilifanyika hivyo ili kwamba afunuliwe katika Israeli, kwamba nilikuja nikibatiza kwa maji.”
I myself did not know him, but I came baptizing with water so that he might be revealed to Israel.”
32 Yohana alishuhudia, “Niliona Roho akishuka kutoka mbinguni mfano wa hua, na ilibaki juu yake.
Then John testified, “I saw the Spirit descending from heaven like a dove, and it remained upon him.
33 Mimi sikumtambua lakini yeye aliyenituma ili nibatize kwa maji aliniambia, 'yule ambaye utaona Roho akishuka na kukaa juu yake, Huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu.'
I myself did not recognize him, but he who sent me to baptize with water said to me, ‘He upon whom yoʋ see the Spirit descend and remain is the one who baptizes with the Holy Spirit.’
34 Nimeona na nimeshuhudia kwamba huyu ni Mwana wa Mungu.”
And I have seen it and can testify that this is the Son of God.”
35 Tena siku iliyofuata Yohana alikuwa amesimama pamoja na wanafunzi wake wawili,
On the next day John was again standing with two of his disciples.
36 walimwona Yesu akitembea na Yohana akasema, “Tazama, Mwana kondoo wa Mungu!”
As Jesus walked by, John looked at him and said, “Behold, the Lamb of God.”
37 Wanafunzi wawili walimsikia Yohana akisema haya wakamfuata Yesu.
When the two disciples heard him say this, they followed Jesus.
38 Tena Yesu aligeuka na kuwaona wanafunzi wale wakimfuata, na akawambia, “Mnataka nini?” Wakajibu, “Rabbi, (maana yake 'mwalimu,' unaishi wapi?”
Turning around, Jesus saw them following him and said to them, “What are you seeking?” They said to him, “Rabbi” (which means “Teacher”), “where are yoʋ staying?”
39 Akawambia, “Njooni na mwone.”Kisha walikwenda na kuona mahali alipokuwa akiishi; walikaa pamoja naye siku hiyo, kwa kuwa ilikuwa yapata kama saa kumi hivi.
He said to them, “Come and see.” So they went and saw where he was staying, and stayed with him that day; it was about the tenth hour.
40 Mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana akiongea na kisha kumfuata Yesu alikuwa ni Andrea, ndugu yake Simoni Petro.
Andrew, the brother of Simon Peter, was one of the two who heard this from John and followed Jesus.
41 Akamwona ndugu yake Simoni na akamwambia, “Tumempata Masihi” (ambayo inatafsiriwa Kristo).
Andrew first found his own brother Simon and said to him, “We have found the Messiah” (which means “Christ”),
42 Akamleta kwa Yesu. Yesu akamtazama na akasema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana” utaitwa Kefa,” (maana yake 'Petro').
and he brought Simon to Jesus. Jesus looked at him and said, “Yoʋ are Simon the son of Jonah; yoʋ shall be called Cephas” (which means “Peter”).
43 Siku iliyofuata wakati Yesu alipotaka kuondoka kwenda Galilaya, alimpata Filipo na akamwambia, “Nifuate mimi.”
On the next day Jesus decided to go to Galilee. Finding Philip, he said to him, “Follow me.”
44 Filipo alikuwa ni mwenyeji wa Bethsaida, mji wa Andrea na Petro.
(Now Philip was from Bethsaida, the city of Andrew and Peter.)
45 Filipo alimpata Nathanaeli na kumwambia, Tumempata yule ambaye Musa aliandika habari zake katika sheria na Manabii. Yesu mwana wa Yusufu, kutoka Nazareti.
Philip then found Nathanael and said to him, “We have found him of whom Moses wrote in the law, and of whom the prophets also wrote—Jesus of Nazareth, the son of Joseph.”
46 Nathanaeli akamwambia, “Je kitu chema chaweza kutokea Nazareti?” Filipo akamwambia, Njoo na uone.”
Nathanael said to him, “Can anything good come from Nazareth?” Philip said to him, “Come and see.”
47 Yesu akamwona Nathanaeli akija kwake na akasema, “Tazama, Mwisraeli kweli kweli asiye na udanganyifu ndani yake!”
When Jesus saw Nathanael coming toward him, he said of him, “Behold, an Israelite indeed, in whom there is no deceit.”
48 Nathanaeli akamwambia, “Umenifahamuje mimi?” Yesu akajibu na akamwambia, “Kabla Filipo hajakuita ulipokuwa chini ya mtini, nalikuona.”
Nathanael said to him, “How do yoʋ know me?” Jesus answered him, “Before Philip called yoʋ, when yoʋ were under the fig tree, I saw yoʋ.”
49 Nathanaeli akajibu, “Rabi wewe u Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli”!
Nathanael answered him, “Rabbi, yoʋ are the Son of God! Yoʋ are the king of Israel!”
50 Yesu akajibu akamwambia, Kwa sababu nilikuambia 'nilikuona chini ya mtini' je waamini? utaona matendo makubwa kuliko haya.”
Jesus answered him, “Do yoʋ believe because I said to yoʋ, ‘I saw yoʋ under the fig tree’? Yoʋ will see greater things than these.”
51 Yesu akasema, “Amini amini nawambieni mtaziona mbingu zikifunguka, na kuwaona malaika wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”
Then he said to him, “Truly, truly, I say to you, before long you will see heaven opened and the angels of God ascending and descending on the Son of Man.”