< Joeli 3 >
1 Tazama, katika siku hizo na wakati huo, nitakaporudi mateka wa Yuda na Yerusalemu,
For behold, in those days and at that time, When I shall bring back the captives of Judah and Jerusalem,
2 Nami nitakusanya mataifa yote, na kuwaleta mpaka bonde la Yehoshafati. Nitawahukumu huko, kwa sababu ya watu wangu na warithi wangu Israeli, ambao waliwatawanya kati ya mataifa, na kwa sababu waligawanya nchi yangu.
I will assemble all the nations, And will bring them down it to the valley of Jehoshaphat, And there will I contend with them for my people and inheritance, Israel; Because they scattered them among the nations, And divided my land among themselves.
3 Wamepiga kura kwa ajili ya watu wangu, walinunua kijana kwa ajili ya kahaba, kuuza msichana kwa divai ili waweze kunywa.
Yea, they cast lots for my people, And gave a boy for a harlot, And sold a damsel for wine to drink.
4 Sasa, kwa nini unanikasirikia, Tiro, Sidoni na mikoa yote ya Wafilisti? Je! mutanirudishia malipo? Hata kama mutanilipa, mara moja nitawarudishia malipo yenu juu ya vichwa vyenu wenyewe.
What have ye to do with me, O Tyre and Sidon, And all the borders of Philistia? Will ye retaliate on me? Or will ye do anything against me? Swiftly and speedily will I bring back your doings upon your own head.
5 Kwa maana mumechukua fedha zangu na dhahabu zangu, nanyi mukachukua hazina zangu za thamani na kuzileta katika hekalu zenu.
Ye have taken my silver and my gold, And have carried into your palaces my precious, goodly things;
6 Mumewauza watu wa Yuda na Yerusalemu kwa Wayunani, ili kuwaondoa mbali na maeneo yao.
The sons also of Judah, and the sons of Jerusalem, Ye have sold to the Grecians, That ye might remove them far from their border.
7 Tazama, nitawaamsha, watoke mahali ambako muliwauza, na nitawarudishia malipo juu ya vichwa vyenu wenyewe.
Behold, I will raise them out of the place whither ye have sold them, And I will return your injury upon your own head;
8 Nitawauza wana wako na binti zako, kwa mkono wa watu wa Yuda. Wao watawauza Sheba, kwa taifa mbali. Kwa maana Bwana amesema.
I will sell your sons and your daughters into the hand of the sons of Judah, And they shall sell them to the Sabeans, to a nation afar off; For Jehovah hath spoken it.
9 Tangaza hii kati ya mataifa, 'Jitayarisheni wenyewe kwa ajili ya vita, waamsheni mashujaa, waacheni wakaribie, mashujaa wote wa vita wapande juu.
Proclaim ye this among the nations: “Prepare war! Stir up the mighty ones! Let all the warriors draw near; let them come up!”
10 Yafueni majembe yenu kuwa panga na visu vyenu vya kuchongea kuwa mikuki. Basi wadhaifu waseme, 'Nina nguvu.'
Beat your ploughshares into swords, And your pruning-hooks into spears; Let the weak say, I am strong!
11 Haraka na mje, mataifa yote ya karibu, jikusanyeni pamoja huko. Ee Bwana, washushe mashujaa wako.
Assemble yourselves and come, all ye nations round about; Gather yourselves together! Thither, O Jehovah, bring down thy mighty ones!
12 Naam, mataifa yajihimize yenyewe kuja hadi bonde la Yehoshafati. Kwa maana nitakaa huko kuhukumu mataifa yote ya jirani.
Let the nations rise and come up to the valley of Jehoshaphat! For there will I sit to judge all the nations around.
13 Wekeni katiki mundu, kwa maana mavuno yameiva. Njoo, muponde zabibu, kwa ajiri pipa la divai limejaa. Vipuri vilivyofurika, kwa sababu uovu wao ni mkubwa sana.
Put ye in the sickle, for the harvest is ripe; Come and tread, for the wine-press is full; The vats overflow; For their wickedness is great!
14 Kuna mshtuko, mshtuko katika bonde la Hukumu. Kwa maana siku ya Bwana i karibu katika bonde la hukumu.
The multitudes, the multitudes in the valley of judgment! For the day of Jehovah is near in the valley of judgment.
15 Jua na mwezi vinakuwa giza, nyota zimeacha kuangaza.
The sun and the moon are darkened, And the stars withdraw their shining.
16 Bwana ataunguruma kutoka Sayuni, na kuinua sauti yake kutoka Yerusalemu. Mbingu na nchi zitatikisika, lakini Bwana atakuwa makao kwa ajili ya watu wake, na ngome kwa wana wa Israeli.
Jehovah also will roar from Zion, And utter his voice from Jerusalem; The heavens and the earth shall shake. But Jehovah will be a refuge to his people! A strong-hold to the sons of Israel.
17 Kwa hiyo mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu, anayeishi Sayuni, mlima wangu mtakatifu. Kisha Yerusalemu itakuwa takatifu, na hakuna jeshi litaklozunguka tena.
Then shall ye know that I am Jehovah your God, Dwelling in Zion, my holy mountain; And Jerusalem shall be holy; Strangers shall pass through her no more.
18 Katika siku hiyo, milima itatayarisha divai nzuri, milima itatiririsha maziwa, miito yote ya Yuda itapita katikati ya maji, na chemchemi zitakuja kutoka nyumba ya Bwana na maji ya bonde la Shitimu.
In that day shall the mountains drop down new wine, And the hills shall flow with milk. And all the streams of Judah shall flow with water. A fountain shall come forth from the house of Jehovah, That shall water the valley of Shittim.
19 Misri itakuwa ukiwa, na Edomu itakuwa jangwa tupu, kwa sababu ya vurugu iliyofanyika kwa watu wa Yuda, kwa sababu walimwaga damu isiyo na hatia katika nchi yao.
Egypt shall be a waste, And Edom a desolate wilderness, For their violence against the sons of Judah; For they shed innocent blood in their land.
20 Lakini Yuda utakua mwenyeji milele, na Yerusalemu itakuwa kizazi hata kizazi.
But Judah shall be inhabited for ever, And Jerusalem from generation to generation.
21 Nitawalipizia damu yao, ambayo sijajilipizia kisasi, kwa maana Bwana anaishi Sayuni.
And I will avenge their blood, which I have not avenged, And Jehovah will dwell upon Zion.