< Joeli 3 >

1 Tazama, katika siku hizo na wakati huo, nitakaporudi mateka wa Yuda na Yerusalemu,
For behold in those days, and in that time when I shall bring back the captivity of Juda and Jerusalem:
2 Nami nitakusanya mataifa yote, na kuwaleta mpaka bonde la Yehoshafati. Nitawahukumu huko, kwa sababu ya watu wangu na warithi wangu Israeli, ambao waliwatawanya kati ya mataifa, na kwa sababu waligawanya nchi yangu.
I will gather together all nations, and will bring them down into the valley of Josaphat: and I will plead with them there for my people, and for my inheritance Israel, whom they have scattered among the nations, and have parted my land.
3 Wamepiga kura kwa ajili ya watu wangu, walinunua kijana kwa ajili ya kahaba, kuuza msichana kwa divai ili waweze kunywa.
And they have cast lots upon my people: and the boy they have put in the stews, and the girl they have sold for wine, that they might drink.
4 Sasa, kwa nini unanikasirikia, Tiro, Sidoni na mikoa yote ya Wafilisti? Je! mutanirudishia malipo? Hata kama mutanilipa, mara moja nitawarudishia malipo yenu juu ya vichwa vyenu wenyewe.
But what have you to do with me, O Tyre, and Sidon, and all the coast of the Philistines? will you revenge yourselves on me? and if you revenge yourselves on me, I will very soon return you a recompense upon your own head.
5 Kwa maana mumechukua fedha zangu na dhahabu zangu, nanyi mukachukua hazina zangu za thamani na kuzileta katika hekalu zenu.
For you have taken away my silver and my gold: and my desirable and most beautiful things you have carried into your temples.
6 Mumewauza watu wa Yuda na Yerusalemu kwa Wayunani, ili kuwaondoa mbali na maeneo yao.
And the children of Juda, and the children of Jerusalem you have sold to the children of the Greeks, that you might remove them far off from their own country.
7 Tazama, nitawaamsha, watoke mahali ambako muliwauza, na nitawarudishia malipo juu ya vichwa vyenu wenyewe.
Behold, I will raise them up out of the place wherein you have sold them: and I will return your recompense upon your own heads.
8 Nitawauza wana wako na binti zako, kwa mkono wa watu wa Yuda. Wao watawauza Sheba, kwa taifa mbali. Kwa maana Bwana amesema.
And I will sell your sons, and your daughters by the hands of the children of Juda, and they shall sell them to the Sabeans, a nation far off, for the Lord hath spoken it.
9 Tangaza hii kati ya mataifa, 'Jitayarisheni wenyewe kwa ajili ya vita, waamsheni mashujaa, waacheni wakaribie, mashujaa wote wa vita wapande juu.
Proclaim ye this among the nations: prepare war, rouse up the strong: let them come, let all the men of war come up.
10 Yafueni majembe yenu kuwa panga na visu vyenu vya kuchongea kuwa mikuki. Basi wadhaifu waseme, 'Nina nguvu.'
Cut your ploughshares into swords, and your spades into spears. Let the weak say: I am strong.
11 Haraka na mje, mataifa yote ya karibu, jikusanyeni pamoja huko. Ee Bwana, washushe mashujaa wako.
Break forth, and come, all ye nations, from round about, and gather yourselves together: there will the Lord cause all thy strong ones to fall down.
12 Naam, mataifa yajihimize yenyewe kuja hadi bonde la Yehoshafati. Kwa maana nitakaa huko kuhukumu mataifa yote ya jirani.
Let them arise, and let the nations come up into the valley of Josaphat: for there I will sit to judge all nations round about.
13 Wekeni katiki mundu, kwa maana mavuno yameiva. Njoo, muponde zabibu, kwa ajiri pipa la divai limejaa. Vipuri vilivyofurika, kwa sababu uovu wao ni mkubwa sana.
Put ye in the sickles, for the harvest is ripe: come and go down, for the press is full, the fats run over: for their wickedness is multiplied.
14 Kuna mshtuko, mshtuko katika bonde la Hukumu. Kwa maana siku ya Bwana i karibu katika bonde la hukumu.
Nations, nations in the valley of destruction: for the day of the Lord is near in the valley of destruction.
15 Jua na mwezi vinakuwa giza, nyota zimeacha kuangaza.
The sun and the moon are darkened, and the stars have withdrawn their shining.
16 Bwana ataunguruma kutoka Sayuni, na kuinua sauti yake kutoka Yerusalemu. Mbingu na nchi zitatikisika, lakini Bwana atakuwa makao kwa ajili ya watu wake, na ngome kwa wana wa Israeli.
And the Lord shall roar out of Sion, and utter his voice from Jerusalem: and the heavens and the earth shall be moved, and the Lord shall be the hope of his people, and the strength of the children of Israel.
17 Kwa hiyo mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu, anayeishi Sayuni, mlima wangu mtakatifu. Kisha Yerusalemu itakuwa takatifu, na hakuna jeshi litaklozunguka tena.
And you shall know that I am the Lord your God, dwelling in Sion my holy mountain: and Jerusalem shall be holy and strangers shall pass through it no more.
18 Katika siku hiyo, milima itatayarisha divai nzuri, milima itatiririsha maziwa, miito yote ya Yuda itapita katikati ya maji, na chemchemi zitakuja kutoka nyumba ya Bwana na maji ya bonde la Shitimu.
And it shall come to pass in that day, that the mountains shall drop down sweetness, and the hills shall flow with milk: and waters shall flow through all the rivers of Juda: and a fountain shall come forth of the house of the Lord, and shall water the torrent of thorns.
19 Misri itakuwa ukiwa, na Edomu itakuwa jangwa tupu, kwa sababu ya vurugu iliyofanyika kwa watu wa Yuda, kwa sababu walimwaga damu isiyo na hatia katika nchi yao.
Egypt shall be a desolation, and Edom a wilderness destroyed: because they have done unjustly against the children of Juda, and have shed innocent blood in their land.
20 Lakini Yuda utakua mwenyeji milele, na Yerusalemu itakuwa kizazi hata kizazi.
And Judea shall be inhabited for ever, and Jerusalem to generation and generation.
21 Nitawalipizia damu yao, ambayo sijajilipizia kisasi, kwa maana Bwana anaishi Sayuni.
And I will cleanse their blood which I had not cleansed: and the Lord will dwell in Sion.

< Joeli 3 >