< Ayubu 9 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Entonces Job respondió,
2 “kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
“En verdad sé que es así, ¿pero cómo puede el hombre ser justo con Dios?
3 Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
Si se complace en contender con él, no puede responderle ni una vez entre mil.
4 Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
Dios es sabio de corazón y poderoso de fuerza. ¿Quién se ha endurecido contra él y ha prosperado?
5 ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
Él remueve las montañas, y ellos no lo saben, cuando los derriba en su cólera.
6 ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
Sacude la tierra de su lugar. Sus pilares tiemblan.
7 Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
Ordena el sol y no sale, y sella las estrellas.
8 ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
Sólo él extiende los cielos, y pisa las olas del mar.
9 ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
Él hace la Osa, Orión y las Pléyades, y las habitaciones del sur.
10 Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
Él hace grandes cosas más allá de descubrirlas; sí, cosas maravillosas sin número.
11 Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
He aquí que pasa por delante de mí y no lo veo. También pasa, pero no lo percibo.
12 Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
He aquí que él arrebata. ¿Quién puede impedirlo? ¿Quién le preguntará: “Qué estás haciendo?”?
13 Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
“Dios no retirará su ira. Los ayudantes de Rahab se inclinan bajo él.
14 Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
Cuánto menos le responderé, y elegir mis palabras para discutir con él?
15 Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
Aunque fuera justo, no le respondería. Yo haría una súplica a mi juez.
16 Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
Si yo hubiera llamado, y él me hubiera respondido, sin embargo, no creo que haya escuchado mi voz.
17 kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
Porque me rompe con una tormenta, y multiplica mis heridas sin causa.
18 Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
No me permite recuperar el aliento, pero me llena de amargura.
19 Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
Si se trata de una cuestión de fuerza, ¡he aquí que él es poderoso! Si de justicia se trata, “¿Quién — dice — me va a convocar?”.
20 Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
Aunque sea justo, mi propia boca me condenará. Aunque sea intachable, se demostrará que soy perverso.
21 Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
Soy irreprochable. No me respeto a mí mismo. Desprecio mi vida.
22 Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
“Todo es lo mismo. Por eso digo que destruye a los irreprochables y a los malvados.
23 Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
Si el azote mata de repente, se burlará en el juicio de los inocentes.
24 Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
La tierra es entregada a la mano de los malvados. Cubre los rostros de sus jueces. Si no es él, ¿quién es?
25 Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
“Ahora mis días son más rápidos que un corredor. Huyen. No ven nada bueno.
26 Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
Han pasado como las naves rápidas, como el águila que se abalanza sobre la presa.
27 Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
Si digo: ‘Olvidaré mi queja’, Voy a quitar mi cara de tristeza y a animarme”.
28 Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
Tengo miedo de todas mis penas. Sé que no me considerará inocente.
29 Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
Seré condenado. ¿Por qué entonces trabajo en vano?
30 Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
Si me lavo con nieve y limpiar mis manos con lejía,
31 Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
sin embargo, me hundirás en la zanja. Mi propia ropa me aborrecerá.
32 Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
Porque él no es un hombre como yo, para que le responda, que debemos reunirnos en el juicio.
33 Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
No hay árbitro entre nosotros, que podría poner su mano sobre nosotros dos.
34 Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
Que me quite la vara. Que su terror no me haga temer;
35 Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.
entonces hablaría y no le temería, pues no lo soy en mí mismo.

< Ayubu 9 >