< Ayubu 9 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Giobbe rispose dicendo:
2 “kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
In verità io so che è così: e come può un uomo aver ragione innanzi a Dio?
3 Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
Se uno volesse disputare con lui, non gli risponderebbe una volta su mille.
4 Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
Saggio di mente, potente per la forza, chi s'è opposto a lui ed è rimasto salvo?
5 ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
Sposta le montagne e non lo sanno, egli nella sua ira le sconvolge.
6 ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
Scuote la terra dal suo posto e le sue colonne tremano.
7 Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
Comanda al sole ed esso non sorge e alle stelle pone il suo sigillo.
8 ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
Egli da solo stende i cieli e cammina sulle onde del mare.
9 ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
Crea l'Orsa e l'Orione, le Pleiadi e i penetrali del cielo australe.
10 Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
Fa cose tanto grandi da non potersi indagare, meraviglie da non potersi contare.
11 Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
Ecco, mi passa vicino e non lo vedo, se ne va e di lui non m'accorgo.
12 Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
Se rapisce qualcosa, chi lo può impedire? Chi gli può dire: «Che fai?».
13 Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
Dio non ritira la sua collera: sotto di lui sono fiaccati i sostenitori di Raab.
14 Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
Tanto meno io potrei rispondergli, trovare parole da dirgli!
15 Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
Se avessi anche ragione, non risponderei, al mio giudice dovrei domandare pietà.
16 Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
Se io lo invocassi e mi rispondesse, non crederei che voglia ascoltare la mia voce.
17 kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
Egli con una tempesta mi schiaccia, moltiplica le mie piaghe senza ragione,
18 Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
non mi lascia riprendere il fiato, anzi mi sazia di amarezze.
19 Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
Se si tratta di forza, è lui che dà il vigore; se di giustizia, chi potrà citarlo?
20 Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
Se avessi ragione, il mio parlare mi condannerebbe; se fossi innocente, egli proverebbe che io sono reo.
21 Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
Sono innocente? Non lo so neppure io, detesto la mia vita!
22 Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
Per questo io dico: «E' la stessa cosa»: egli fa perire l'innocente e il reo!
23 Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
Se un flagello uccide all'improvviso, della sciagura degli innocenti egli ride.
24 Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
La terra è lasciata in balìa del malfattore: egli vela il volto dei suoi giudici; se non lui, chi dunque sarà?
25 Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
I miei giorni passano più veloci d'un corriere, fuggono senza godere alcun bene,
26 Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
volano come barche di giunchi, come aquila che piomba sulla preda.
27 Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
Se dico: «Voglio dimenticare il mio gemito, cambiare il mio volto ed essere lieto»,
28 Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
mi spavento per tutti i miei dolori; so bene che non mi dichiarerai innocente.
29 Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
Se sono colpevole, perché affaticarmi invano?
30 Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
Anche se mi lavassi con la neve e pulissi con la soda le mie mani,
31 Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
allora tu mi tufferesti in un pantano e in orrore mi avrebbero le mie vesti.
32 Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
Poiché non è uomo come me, che io possa rispondergli: «Presentiamoci alla pari in giudizio».
33 Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
Non c'è fra noi due un arbitro che ponga la mano su noi due.
34 Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
Allontani da me la sua verga sì che non mi spaventi il suo terrore:
35 Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.
allora io potrò parlare senza temerlo, perché così non sono in me stesso.

< Ayubu 9 >