< Ayubu 9 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Mais Job répondit, et dit:
2 “kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
Certainement je sais que cela est ainsi; et comment l'homme [mortel] se justifierait-il devant le [Dieu] Fort?
3 Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
Si [Dieu] veut plaider avec lui, de mille articles il ne saurait lui répondre sur un seul.
4 Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
[Dieu] est sage de cœur, et puissant en force. Qui est-ce qui s'est opposé à lui, et s'en est bien trouvé?
5 ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
Il transporte les montagnes, et quand il les renverse en sa fureur, elles n'en connaissent rien.
6 ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
Il remue la terre de sa place, et ses piliers sont ébranlés.
7 Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
Il parle au soleil, et le soleil ne se lève point; et c'est lui qui tient les étoiles sous son cachet.
8 ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
C'est lui seul qui étend les cieux; qui marche sur les hauteurs de la mer;
9 ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
Qui a fait le chariot, et l'Orion, et la Poussinière, et les signes qui sont au fond du Midi;
10 Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
Qui fait des choses si grandes qu'on ne les peut sonder; et tant de choses merveilleuses, qu'on ne les peut compter.
11 Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
Voici, il passera près de moi, et je ne le verrai point; et il repassera, et je ne l'apercevrai point.
12 Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
Voilà, s'il ravit, qui le lui fera rendre? et qui est-ce qui lui dira: Que fais-tu?
13 Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
Dieu ne retire point sa colère, et les hommes superbes qui viennent au secours, sont abattus sous lui.
14 Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
Combien moins lui répondrais-je, moi et arrangerais-je mes paroles contre lui?
15 Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
Moi, je ne lui répondrai point, quand même je serais juste, [mais] je demanderai grâce à mon juge.
16 Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
Si je l'invoque, et qu'il me réponde, [encore] ne croirai-je point qu'il ait écouté ma voix.
17 kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
Car il m'a écrasé du milieu d'un tourbillon, et il a ajouté plaie sur plaie, sans que je l'aie mérité.
18 Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
Il ne me permet point de reprendre haleine, mais il me remplit d'amertumes.
19 Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
S'il est question de savoir qui est le plus fort; voilà, il est fort; et [s'il est question d'aller] en justice, qui est-ce qui m'y fera comparaître?
20 Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
Si je me justifie, ma propre bouche me condamnera; [si je me fais] parfait, il me convaincra d'être coupable.
21 Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
Quand je serais parfait, je ne me soucierais pas de vivre, je dédaignerais la vie.
22 Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
Tout revient à un; c'est pourquoi j'ai dit qu'il consume l'homme juste et le méchant.
23 Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
[Au moins] si le fléau [dont il frappe] faisait mourir tout aussitôt; [mais] il se rit de l'épreuve des innocents.
24 Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
[C'est par lui que] la terre est livrée entre les mains du méchant; c'est lui qui couvre la face des juges de la [terre]; et si ce n'est pas lui, qui est-ce donc?
25 Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
Or mes jours ont été plus vite qu'un courrier; ils s'en sont fuis, et n'ont point vu de bien.
26 Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
Ils ont passé [comme] des barques de poste; comme un aigle qui vole après la proie.
27 Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
Si je dis: J'oublierai ma plainte, je renoncerai à ma colère, je me fortifierai;
28 Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
Je suis épouvanté de tous mes tourments. Je sais que tu ne me jugeras point innocent.
29 Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
Je serai [trouvé] méchant; pourquoi travaillerais-je en vain?
30 Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
Si je me lave dans de l'eau de neige, et que je nettoie mes mains dans la pureté,
31 Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
Alors tu me plongeras dans un fossé, et mes vêtements m'auront en horreur.
32 Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
Car il n'est pas comme moi un homme, pour que je lui réponde, [et] que nous allions ensemble en jugement.
33 Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
[Mais] il n'y a personne qui prît connaissance de la cause qui serait entre nous, [et] qui mît la main sur nous deux.
34 Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
Qu'il ôte [donc] sa verge de dessus moi, et que la frayeur que j'ai de lui ne me trouble plus.
35 Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.
Je parlerai, et je ne le craindrai point; mais dans l'état où je suis je ne suis point à moi-même.

< Ayubu 9 >