< Ayubu 9 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Job reprenant dit:
2 “kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
En vérité je sais qu'il en est ainsi. Comment un mortel serait-il juste aux yeux du Seigneur?
3 Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
Car si des hommes veulent aller avec Dieu en justice, il ne s'y prêtera pas; il ne voudra pas être contredit sur un seul point entre mille.
4 Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
Lui seul est sage en ses pensées; il est fort, il est grand; qui donc s'est assez endurci pour lui résister?
5 ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
Il lutte contre les montagnes et elles l'ignorent; il les bouleverse dans son courroux.
6 ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
Il ébranle dans ses fondements la terre que recouvre le ciel, et les colonnes qui la soutiennent sont chancelantes.
7 Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
Il parle au soleil, et le soleil ne se lève pas; il appose son scel sur les astres.
8 ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
C'est lui seul qui a tendu les cieux et qui marche sur la mer comme sur un sol affermi.
9 ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
Il a créé les Pléïades, et l'étoile du soir, et Arcture, et les constellations du Midi.
10 Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
Il a fait une multitude innombrable de merveilles glorieuses et incompréhensibles.
11 Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
S'il a passé au-dessus de moi, je ne l'ai point vu; s'il a marché à mes côtés, je n'en ai rien su.
12 Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
Se détourne-t-il, qui le ramènera? qui osera lui dire: Que faites-vous?
13 Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
Seul il a dompté toute fureur, il a fait plier les monstres marins sous le ciel.
14 Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
S'il m'écoutait, s'il jugeait mes arguments!
15 Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
Quand même je serais juste, il ne m'écouterait pas; je n'obtiendrais pas de lui un arrêt.
16 Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
Et si je ne l'avais invoqué et qu'il ne m'exauçât point, je ne pourrais croire qu'il eût entendu ma voix.
17 kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
Je crains qu'il ne me broie au moyen d'un tourbillon, car il amortit les ravages de mes plaies nombreuses.
18 Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
Il ne me laisse point reprendre haleine, après m'avoir rempli d'amertume,
19 Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
Et il prévaut par la force. Qui donc résisterait à la condamnation qu'il aurait prononcée?
20 Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
Juste, ma bouche se trouvera dire des impiétés; irréprochable, je passerai pour criminel.
21 Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
Car, si j'ai péché, c'est dans l'ignorance de mon âme, et néanmoins la vie m'est ôtée.
22 Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
Aussi j'ai dit: La colère détruit le riche et le grand.
23 Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
La mort qui les frappe soudain met à nu leur faiblesse; mais les justes sont tournés en dérision,
24 Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
Ils sont livrés aux mains des pervers, et le Seigneur a voilé le front des juges. Et si ce n'est pas lui qui est-ce donc?
25 Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
Ma vie est plus rapide qu'un courrier; on ne s'est point placé sur son passage et on ne l'a pas vue.
26 Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
Les navires laissent-ils une trace, ou l'aigle qui vole et cherche sa proie?
27 Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
Si je me dis: Cesse donc de parler; borne-toi à courber la tête et à gémir;
28 Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
Je tremble de tous mes membres, car je sais que vous ne me jugez point innocent.
29 Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
Ai-je donc commis quelque impiété? Mais pourquoi ne suis-je point mort?
30 Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
Lors même que je me serais lavé avec de la neige, et que des mains pures m'auraient purifié,
31 Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
Vous m'avez assez plongé dans la fange pour que ma robe m'ait souillé.
32 Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
Car vous n'êtes point comme moi un homme avec qui je puisse contester et comparaître en justice.
33 Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
Que n'existe-t-il pour nous un médiateur, qui écoute et qui prononce entre vous et moi?
34 Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
Détournez de moi votre verge; que l'effroi qu'elle m'inspire ne me trouble plus.
35 Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.
Si je cesse de craindre je parlerai, car je ne le peux en l'état où je suis.

< Ayubu 9 >